Surata: AL-QALAM 

O versículo : 1

نٓۚ وَٱلۡقَلَمِ وَمَا يَسۡطُرُونَ

Nuun. Nina apa kwa kalamu na yale wayoyaandika



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 2

مَآ أَنتَ بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ بِمَجۡنُونٖ

(Kwamba) Wewe (Muhammad) kwa neema ya Mola wako Mlezi (aliyokupa) sio mwendawazimu



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 3

وَإِنَّ لَكَ لَأَجۡرًا غَيۡرَ مَمۡنُونٖ

Na kwa hakika wewe una malipo (makubwa) yasiyo katika



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 4

وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٖ

Na hakika wewe uko juu ya tabia njema sana



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 5

فَسَتُبۡصِرُ وَيُبۡصِرُونَ

Basi hivi karibuni utaona, na wao wataona



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 6

بِأَييِّكُمُ ٱلۡمَفۡتُونُ

(Kwamba) Ni nani mwenye kichaa miongoni mwenu



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 7

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُهۡتَدِينَ

Hakika, Mola wako Mlezi ndiye amjuae zaidi aliyepotea njia yake, ndiye awajuae zaidi walioongoka



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 8

فَلَا تُطِعِ ٱلۡمُكَذِّبِينَ

Basi usiwatii wanao kadhibisha



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 9

وَدُّواْ لَوۡ تُدۡهِنُ فَيُدۡهِنُونَ

Wangependa uwe laini (ulegeze msimamo wako), nao wawe laini (walegeze msimamo wao na wakufuate)



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 10

وَلَا تُطِعۡ كُلَّ حَلَّافٖ مَّهِينٍ

Wala usimtii kila mwapaji sana, aliye dhalili,



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 11

هَمَّازٖ مَّشَّآءِۭ بِنَمِيمٖ

Mwingi wa kusengenya, mpitaji huku na kule kwa kufitinisha



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 12

مَّنَّاعٖ لِّلۡخَيۡرِ مُعۡتَدٍ أَثِيمٍ

Mwingi wa kuzuia ya kheri, aliyependukia katika kuwadhulumu (Watu) mwingi wa kutenda dhambi



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 13

عُتُلِّۭ بَعۡدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ

Mkavu, na juu ya hayo ni mwana haramu (kujipachika tu kabila)



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 14

أَن كَانَ ذَا مَالٖ وَبَنِينَ

Kwakuwa tu ni mwenye kumiliki mali na watoto?



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 15

إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 16

سَنَسِمُهُۥ عَلَى ٱلۡخُرۡطُومِ

Karibuni tutamtia kovu juu ya pua



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 17

إِنَّا بَلَوۡنَٰهُمۡ كَمَا بَلَوۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡجَنَّةِ إِذۡ أَقۡسَمُواْ لَيَصۡرِمُنَّهَا مُصۡبِحِينَ

Hakika sisi Tumewajaribu (Maquraysh) kama Tulivyowajaribu watu wa shamba pale walipo apa kuwa bila shaka watayavuna (matunda yake) watakapo pambaukiwa asubuhi



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 18

وَلَا يَسۡتَثۡنُونَ

Na wala hawakusema In-Shaa Allaah (Allah akipenda)!



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 19

فَطَافَ عَلَيۡهَا طَآئِفٞ مِّن رَّبِّكَ وَهُمۡ نَآئِمُونَ

Basi (shamba lao) likazungukwa na (moto) kutoka kwa mola wako ilihali wao wamelala



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 20

فَأَصۡبَحَتۡ كَٱلصَّرِيمِ

Likawa kama lilovunwa (ilion-g’olewa mimea yake)



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 21

فَتَنَادَوۡاْ مُصۡبِحِينَ

Wakaitana, pale walipopam-baukiwa asubuhi



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 22

أَنِ ٱغۡدُواْ عَلَىٰ حَرۡثِكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰرِمِينَ

Kwamba nendeni asubuhi mapema shambani mwenu, mkiwa mnataka kuvuna



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 23

فَٱنطَلَقُواْ وَهُمۡ يَتَخَٰفَتُونَ

Wakatoka na huku wanakwenda kimya kimya wakinong’onezana



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 24

أَن لَّا يَدۡخُلَنَّهَا ٱلۡيَوۡمَ عَلَيۡكُم مِّسۡكِينٞ

Wakisema kwamba:: leo Maskini asiingie humo mwenu kinyume cha utashi wenu



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 25

وَغَدَوۡاْ عَلَىٰ حَرۡدٖ قَٰدِرِينَ

Wakatoka asubuhi mapema kwa kusudio la nguvu, wakidhani wana uwezo (wa kuwazuia maskini)



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 26

فَلَمَّا رَأَوۡهَا قَالُوٓاْ إِنَّا لَضَآلُّونَ

Basi walipoliona (shamba lao) wakasema: Hakika sisi bila shaka Tumepotea



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 27

بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ

(Walivyo tanabahi!): wakasema Bali sisi tumenyimwa (mavuno yake)!



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 28

قَالَ أَوۡسَطُهُمۡ أَلَمۡ أَقُل لَّكُمۡ لَوۡلَا تُسَبِّحُونَ

Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Allah (kuiacha nia yenu mbaya)?



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 29

قَالُواْ سُبۡحَٰنَ رَبِّنَآ إِنَّا كُنَّا ظَٰلِمِينَ

Wakasema: utukufu ni wa mola wetu, hakika tulikuwa wenye kudhulumu



Surata: AL-QALAM 

O versículo : 30

فَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَلَٰوَمُونَ

Basi Wakakabiliana wenyewe kwa wenyewe wakilaumiana