Surata: ATTUR 

O versículo : 1

وَٱلطُّورِ

Nina apa kwa mlima wa Tur



Surata: ATTUR 

O versículo : 2

وَكِتَٰبٖ مَّسۡطُورٖ

Na kwa kitabu kilichoandikwa



Surata: ATTUR 

O versículo : 3

فِي رَقّٖ مَّنشُورٖ

Katika karatasi ya ngozi nyembamba iliyokunjuliwa



Surata: ATTUR 

O versículo : 4

وَٱلۡبَيۡتِ ٱلۡمَعۡمُورِ

Na (nina apa) kwa Nyumba iliyoimarishwa (iliyojengwa imara)



Surata: ATTUR 

O versículo : 5

وَٱلسَّقۡفِ ٱلۡمَرۡفُوعِ

Na (nina apa) kwa sakafu (za mbingu) zilizonyanyuliwa



Surata: ATTUR 

O versículo : 6

وَٱلۡبَحۡرِ ٱلۡمَسۡجُورِ

Na (nina apa) kwa bahari yenye kuwashwa moto)



Surata: ATTUR 

O versículo : 7

إِنَّ عَذَابَ رَبِّكَ لَوَٰقِعٞ

(Nina apa kwamba) Hakika, adhabu ya Mola wako Mlezi bila ya shaka yoyote itatokea



Surata: ATTUR 

O versículo : 8

مَّا لَهُۥ مِن دَافِعٖ

Hapana wa kuizuia



Surata: ATTUR 

O versículo : 9

يَوۡمَ تَمُورُ ٱلسَّمَآءُ مَوۡرٗا

Siku hiyo mbingu itatikisika kutikisika kikweli



Surata: ATTUR 

O versículo : 10

وَتَسِيرُ ٱلۡجِبَالُ سَيۡرٗا

Na majabali yatatembea mwendo wa kasi



Surata: ATTUR 

O versículo : 11

فَوَيۡلٞ يَوۡمَئِذٖ لِّلۡمُكَذِّبِينَ

Basi ole wao Siku hiyo kwa wakadhibishao



Surata: ATTUR 

O versículo : 12

ٱلَّذِينَ هُمۡ فِي خَوۡضٖ يَلۡعَبُونَ

Ambao wamo katika kushughulika na upuuzi wakicheza



Surata: ATTUR 

O versículo : 13

يَوۡمَ يُدَعُّونَ إِلَىٰ نَارِ جَهَنَّمَ دَعًّا

Siku watasukumwa katika Moto wa Jahannam kwa msukumo wa nguvu



Surata: ATTUR 

O versículo : 14

هَٰذِهِ ٱلنَّارُ ٱلَّتِي كُنتُم بِهَا تُكَذِّبُونَ

Huu ndio ule moto ambao mlikuwa mkiukadhibisha



Surata: ATTUR 

O versículo : 15

أَفَسِحۡرٌ هَٰذَآ أَمۡ أَنتُمۡ لَا تُبۡصِرُونَ

Je, hivi ni uchawi huu au nyinyi hamuoni?



Surata: ATTUR 

O versículo : 16

ٱصۡلَوۡهَا فَٱصۡبِرُوٓاْ أَوۡ لَا تَصۡبِرُواْ سَوَآءٌ عَلَيۡكُمۡۖ إِنَّمَا تُجۡزَوۡنَ مَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Ingieni muungue humo kwenye Jahannam, mkistahamili au msistahamili ni sawasawa kwenu, hakika hapana ila mnalipwa yale mliyokuwa mkiyatenda



Surata: ATTUR 

O versículo : 17

إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّـٰتٖ وَنَعِيمٖ

Hakika ya wacha mungu watakua katika bustani na neema



Surata: ATTUR 

O versículo : 18

فَٰكِهِينَ بِمَآ ءَاتَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ وَوَقَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ عَذَابَ ٱلۡجَحِيمِ

Wakifurahia kwa ambayo Amewapa Mola wao, na Akawaokoa na adhabu ya moto uwakao vikali mno



Surata: ATTUR 

O versículo : 19

كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ هَنِيٓـَٔۢا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Kuleni na kunyweni kwa raha kwa sababu ya mliyokuwa mnatenda



Surata: ATTUR 

O versículo : 20

مُتَّكِـِٔينَ عَلَىٰ سُرُرٖ مَّصۡفُوفَةٖۖ وَزَوَّجۡنَٰهُم بِحُورٍ عِينٖ

Hali ya kuegemea juu ya makochi ya fakhari yaliyopangwa safu safu, na Tutawaozesha huwr ‘ayn, (wanawake weupe) wazuri wenye macho makubwa ya kupendeza



Surata: ATTUR 

O versículo : 21

وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَٱتَّبَعَتۡهُمۡ ذُرِّيَّتُهُم بِإِيمَٰنٍ أَلۡحَقۡنَا بِهِمۡ ذُرِّيَّتَهُمۡ وَمَآ أَلَتۡنَٰهُم مِّنۡ عَمَلِهِم مِّن شَيۡءٖۚ كُلُّ ٱمۡرِيِٕۭ بِمَا كَسَبَ رَهِينٞ

Na wale walioamini na wakafuatwa na dhuriya wao kwa Imani Tutawakutanisha nao dhuriya wao na Hatutawapunguzia katika ‘amali zao kitu chochote. Kila mtu lazima atapata alicho kichuma



Surata: ATTUR 

O versículo : 22

وَأَمۡدَدۡنَٰهُم بِفَٰكِهَةٖ وَلَحۡمٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ

Na Tutawapa matunda na nyama katika ambavyo wanatamani



Surata: ATTUR 

O versículo : 23

يَتَنَٰزَعُونَ فِيهَا كَأۡسٗا لَّا لَغۡوٞ فِيهَا وَلَا تَأۡثِيمٞ

Watabadilishana humo gilasi za mvinyo usiosababisha maneno ya upuuzi na wala ya dhambi



Surata: ATTUR 

O versículo : 24

۞وَيَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ غِلۡمَانٞ لَّهُمۡ كَأَنَّهُمۡ لُؤۡلُؤٞ مَّكۡنُونٞ

Na watawazungukia watumishi vijana kwa ajili yao kana kwamba ni lulu zilizohifadhiwa



Surata: ATTUR 

O versículo : 25

وَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ

Na watakabiliana baadhi yao kwa wengine wakiulizana



Surata: ATTUR 

O versículo : 26

قَالُوٓاْ إِنَّا كُنَّا قَبۡلُ فِيٓ أَهۡلِنَا مُشۡفِقِينَ

Watasema hakika sisi tulikua kabla ya hapa kwa watu wetu wenye kuwafanyia upole



Surata: ATTUR 

O versículo : 27

فَمَنَّ ٱللَّهُ عَلَيۡنَا وَوَقَىٰنَا عَذَابَ ٱلسَّمُومِ

Basi Allah Akatufadhilisha, na Akatuokoa na adhabu ya mvuke wa moto (unaobabua)



Surata: ATTUR 

O versículo : 28

إِنَّا كُنَّا مِن قَبۡلُ نَدۡعُوهُۖ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلۡبَرُّ ٱلرَّحِيمُ

Hakika sisi tulikuwa tunamuabudu kabla ya hapa hakika yeye ni mwema mwingi wa rehma



Surata: ATTUR 

O versículo : 29

فَذَكِّرۡ فَمَآ أَنتَ بِنِعۡمَتِ رَبِّكَ بِكَاهِنٖ وَلَا مَجۡنُونٍ

Basi kumbusha (Ewe Muhammad) na haukua wewe kwa neema ya mola wako mlezi kuhani wala mwendawazimu



Surata: ATTUR 

O versículo : 30

أَمۡ يَقُولُونَ شَاعِرٞ نَّتَرَبَّصُ بِهِۦ رَيۡبَ ٱلۡمَنُونِ

Au wanasema (huyu Muhammad þ ni) mshairi, tunamtarajia kupatikana maafa ya dahari