Surata: MARYAM 

O versículo : 91

أَن دَعَوۡاْ لِلرَّحۡمَٰنِ وَلَدٗا

Kwa kudai kwao kuwa (Allah) Mwingi wa Rehema ana mtoto



Surata: MARYAM 

O versículo : 92

وَمَا يَنۢبَغِي لِلرَّحۡمَٰنِ أَن يَتَّخِذَ وَلَدًا

Na haitakiwi kwa (Allah) Mwingi wa Rehema kuwa na mtoto.[1]


1- - Aya hizi tano 88, 89, 90, 91 na 92 zinakataa kwa ukali itikadi kwamba Mungu ana mtoto. Muislamu hatakiwi kabisa kuikumbatia itikadi hii au kuishabikia. Ni itikadi mbaya mno kiasi kwamba mbingu, ardhi na milima haziivumilii kuisikia.


Surata: MARYAM 

O versículo : 93

إِن كُلُّ مَن فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ إِلَّآ ءَاتِي ٱلرَّحۡمَٰنِ عَبۡدٗا

Hapana yeyote aliyomo mbinguni na ardhini ila atafika kwa Arrahmani Mwingi wa Rehema kuwa ni mtumwa wake



Surata: MARYAM 

O versículo : 94

لَّقَدۡ أَحۡصَىٰهُمۡ وَعَدَّهُمۡ عَدّٗا

Yeye hakika amewadhibiti na amewahesabu sawa sawa



Surata: MARYAM 

O versículo : 95

وَكُلُّهُمۡ ءَاتِيهِ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ فَرۡدًا

Na kila mmoja katika wao atamfikia Siku ya Kiyama peke yake



Surata: MARYAM 

O versículo : 96

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ سَيَجۡعَلُ لَهُمُ ٱلرَّحۡمَٰنُ وُدّٗا

Hakika walio amini na wakatenda mema Arrahmani Mwingi wa Rehema atawajaalia mapenzi



Surata: MARYAM 

O versículo : 97

فَإِنَّمَا يَسَّرۡنَٰهُ بِلِسَانِكَ لِتُبَشِّرَ بِهِ ٱلۡمُتَّقِينَ وَتُنذِرَ بِهِۦ قَوۡمٗا لُّدّٗا

Na hakika tumeifanya nyepesi (Qur’ani) kwa ulimi wako, ili uwabashirie kwayo wacha Mungu, na uwaonye kwayo watu wabishi



Surata: MARYAM 

O versículo : 98

وَكَمۡ أَهۡلَكۡنَا قَبۡلَهُم مِّن قَرۡنٍ هَلۡ تُحِسُّ مِنۡهُم مِّنۡ أَحَدٍ أَوۡ تَسۡمَعُ لَهُمۡ رِكۡزَۢا

Na kaumu ngapi tuziangamiza kabla yao. Je! Unawaona hata mmoja katika wao au unasikia hata mchakato wao