Capítulo: ATTAUBA 

Verso : 86

وَإِذَآ أُنزِلَتۡ سُورَةٌ أَنۡ ءَامِنُواْ بِٱللَّهِ وَجَٰهِدُواْ مَعَ رَسُولِهِ ٱسۡتَـٔۡذَنَكَ أُوْلُواْ ٱلطَّوۡلِ مِنۡهُمۡ وَقَالُواْ ذَرۡنَا نَكُن مَّعَ ٱلۡقَٰعِدِينَ

Na inapoteremshwa Sura (inayowaamrisha) kwamba: Muaminini Allah na piganeni Jihadi pamoja na Mtume wake, wale wenye uwezo (wa mali na nguvu) miongoni mwao wanakuomba ruhusa na kusema: Tuache tuwe pamoja na wanaokaa nyuma



Capítulo: ATTAUBA 

Verso : 87

رَضُواْ بِأَن يَكُونُواْ مَعَ ٱلۡخَوَالِفِ وَطُبِعَ عَلَىٰ قُلُوبِهِمۡ فَهُمۡ لَا يَفۡقَهُونَ

Wameridhia kuwa pamoja na wabakiao nyuma (wenye nyudhuru), na nyoyo zao zikapigwa chapa kwa hivyo hawafahamu



Capítulo: ATTAUBA 

Verso : 88

لَٰكِنِ ٱلرَّسُولُ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مَعَهُۥ جَٰهَدُواْ بِأَمۡوَٰلِهِمۡ وَأَنفُسِهِمۡۚ وَأُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمُ ٱلۡخَيۡرَٰتُۖ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ

Lakini Mtume na wale walioamini pamoja naye walipigana Jihadi kwa mali zao na nafsi zao. Na hao ndio watakaopata heri nyingi na hao ndio hasa wenye kufaulu



Capítulo: ATTAUBA 

Verso : 89

أَعَدَّ ٱللَّهُ لَهُمۡ جَنَّـٰتٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَاۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ

Allah amewaandalia Pepo zipitazo mito mbele yake wadumu humo. Huko ndiko kufuzu kukubwa hasa



Capítulo: ATTAUBA 

Verso : 90

وَجَآءَ ٱلۡمُعَذِّرُونَ مِنَ ٱلۡأَعۡرَابِ لِيُؤۡذَنَ لَهُمۡ وَقَعَدَ ٱلَّذِينَ كَذَبُواْ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥۚ سَيُصِيبُ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Na walikuja wenye kujitia udhuru katika Mabedui ili wapewe ruhusa (ya kutokwenda vitani), na walikaa wale (wanafiki) waliomwambia uwongo Allah na Mtume wake. Itawafika (wale) waliokufuru katika wao (na kusema uongo) adhabu iumizayo sana



Capítulo: ATTAUBA 

Verso : 91

لَّيۡسَ عَلَى ٱلضُّعَفَآءِ وَلَا عَلَى ٱلۡمَرۡضَىٰ وَلَا عَلَى ٱلَّذِينَ لَا يَجِدُونَ مَا يُنفِقُونَ حَرَجٌ إِذَا نَصَحُواْ لِلَّهِ وَرَسُولِهِۦۚ مَا عَلَى ٱلۡمُحۡسِنِينَ مِن سَبِيلٖۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Hakuna dhambi kwa wanyonge na wagonjwa na wasiokuwa na cha kutoa, iwapo wanamsafia nia Allah na Mtume wake. Hakuna njia ya kuwalaumu wanaofanya mazuri. Na Allah ni Mwenye kusamehe, mwenye Rehemu



Capítulo: ATTAUBA 

Verso : 92

وَلَا عَلَى ٱلَّذِينَ إِذَا مَآ أَتَوۡكَ لِتَحۡمِلَهُمۡ قُلۡتَ لَآ أَجِدُ مَآ أَحۡمِلُكُمۡ عَلَيۡهِ تَوَلَّواْ وَّأَعۡيُنُهُمۡ تَفِيضُ مِنَ ٱلدَّمۡعِ حَزَنًا أَلَّا يَجِدُواْ مَا يُنفِقُونَ

Na wala (hawana dhambi) wale (Answari) ambao walipokujia ili uwachukue (uwawezeshe na uwape vipando vya kwendea jihadi) ulisema: Sina kipando cha kukuchukueni (cha kukupeni) waliondoka na ilhali macho yao yanatiririka machozi kwa huzuni ya kukosa cha kutoa