Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 22

وَيَوۡمَ نَحۡشُرُهُمۡ جَمِيعٗا ثُمَّ نَقُولُ لِلَّذِينَ أَشۡرَكُوٓاْ أَيۡنَ شُرَكَآؤُكُمُ ٱلَّذِينَ كُنتُمۡ تَزۡعُمُونَ

Na (kumbuka) siku tutakapowa-kusanya wote kisha tuwaambie wale washirikina (kwamba): Wako wapi washirika wenu ambao mlikuwa mnadai (kuwa ni washirika wa Allah)?



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 23

ثُمَّ لَمۡ تَكُن فِتۡنَتُهُمۡ إِلَّآ أَن قَالُواْ وَٱللَّهِ رَبِّنَا مَا كُنَّا مُشۡرِكِينَ

Kisha haukuwa mtihani wao isipokuwa kwamba walisema tu: Ewe Mola wetu tunaapa; sisi hatukuwa Washirikina



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 24

ٱنظُرۡ كَيۡفَ كَذَبُواْ عَلَىٰٓ أَنفُسِهِمۡۚ وَضَلَّ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَفۡتَرُونَ

Ona namna walivyozidanganya nafsi zao na yakawapotea yote waliyokuwa wanayazua



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 25

وَمِنۡهُم مَّن يَسۡتَمِعُ إِلَيۡكَۖ وَجَعَلۡنَا عَلَىٰ قُلُوبِهِمۡ أَكِنَّةً أَن يَفۡقَهُوهُ وَفِيٓ ءَاذَانِهِمۡ وَقۡرٗاۚ وَإِن يَرَوۡاْ كُلَّ ءَايَةٖ لَّا يُؤۡمِنُواْ بِهَاۖ حَتَّىٰٓ إِذَا جَآءُوكَ يُجَٰدِلُونَكَ يَقُولُ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّآ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Na miongni mwao wapo wanaokusikiliza na tumeweka juu ya nyoyo zao vifuniko wasiyafahamu (hayo wanayoyasikia) na katika masikio yao (tumeweka) uziwi. Na wanapoona kila Aya (inayoteremka kusadikisha Utume wako) hawaiamini mpaka wanapokujia wanakufanyia mjadala wakisema wale waliokufuru kwamba: (Haya anayoyasema) sio chochote isipokuwa tu ni hadithi za kale



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 26

وَهُمۡ يَنۡهَوۡنَ عَنۡهُ وَيَنۡـَٔوۡنَ عَنۡهُۖ وَإِن يُهۡلِكُونَ إِلَّآ أَنفُسَهُمۡ وَمَا يَشۡعُرُونَ

Na wanakataza (watu kuiamini Qur’ani) na (wao wenyewe) wanajitenga nayo. Na hawaangamizi isipokuwa nafsi zao tu, na hawatambui



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 27

وَلَوۡ تَرَىٰٓ إِذۡ وُقِفُواْ عَلَى ٱلنَّارِ فَقَالُواْ يَٰلَيۡتَنَا نُرَدُّ وَلَا نُكَذِّبَ بِـَٔايَٰتِ رَبِّنَا وَنَكُونَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Na lau ungeona wakati watakaposimamishwa motoni na kusema (kwa majuto): Eee! Laiti tungerudishwa (duniani) na tusizikanushe Aya za Mola wetu Mlezi na tuwe miongoni mwa Waumini



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 28

بَلۡ بَدَا لَهُم مَّا كَانُواْ يُخۡفُونَ مِن قَبۡلُۖ وَلَوۡ رُدُّواْ لَعَادُواْ لِمَا نُهُواْ عَنۡهُ وَإِنَّهُمۡ لَكَٰذِبُونَ

Bali yamewadhihirikia yale waliyokuwa wanayaficha kabla ya hapo. Na lau kama wangerudishwa, kwa yakini kabisa wangerudia yale waliyokatazwa. Na kwa hakika kabisa wao ni waongo



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 29

وَقَالُوٓاْ إِنۡ هِيَ إِلَّا حَيَاتُنَا ٱلدُّنۡيَا وَمَا نَحۡنُ بِمَبۡعُوثِينَ

Na walisema: Hayakuwa haya (maisha) isipokuwa tu ni maisha yetu ya duniani, na sisi si wenye kufufuliwa



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 30

وَلَوۡ تَرَىٰٓ إِذۡ وُقِفُواْ عَلَىٰ رَبِّهِمۡۚ قَالَ أَلَيۡسَ هَٰذَا بِٱلۡحَقِّۚ قَالُواْ بَلَىٰ وَرَبِّنَاۚ قَالَ فَذُوقُواْ ٱلۡعَذَابَ بِمَا كُنتُمۡ تَكۡفُرُونَ

Na lau kama utawaona wakati watakaposimamishwa kwa Mola wao atasema Allah na kuwaambia): Hivi hili (la kufufuliwa) sio kweli? Watasema: Tunaapa kwa Mola wetu (kwamba ni kweli). (Allah) Atasema: Basi onjeni adhabu kwa sababu ya yale mliyokuwa mnayapinga



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 31

قَدۡ خَسِرَ ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِلِقَآءِ ٱللَّهِۖ حَتَّىٰٓ إِذَا جَآءَتۡهُمُ ٱلسَّاعَةُ بَغۡتَةٗ قَالُواْ يَٰحَسۡرَتَنَا عَلَىٰ مَا فَرَّطۡنَا فِيهَا وَهُمۡ يَحۡمِلُونَ أَوۡزَارَهُمۡ عَلَىٰ ظُهُورِهِمۡۚ أَلَا سَآءَ مَا يَزِرُونَ

Hakika, wamepata hasara wale waliopinga kukutana na Allah, hadi kitakapowajia Kiyama ghafla watasema: Eee! Majuto ni yetu kwa (sababu ya) yale tuliyoyafanyia uzembe humo (duniani), na huku wanabeba mizigo (makosa) yao migongoni mwao. Elewa kwamba, ni mabaya mno hayo (madhambi) wanayoyabeba



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 32

وَمَا ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَآ إِلَّا لَعِبٞ وَلَهۡوٞۖ وَلَلدَّارُ ٱلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لِّلَّذِينَ يَتَّقُونَۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ

Na maisha ya duniani si chochote isipokuwa tu ni mchezo na pumbao. Na kwa yakini kabisa, nyumba ya Akhera ndio bora zaidi kwa wanaomcha Allah. Je, hamtumii akili?



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 33

قَدۡ نَعۡلَمُ إِنَّهُۥ لَيَحۡزُنُكَ ٱلَّذِي يَقُولُونَۖ فَإِنَّهُمۡ لَا يُكَذِّبُونَكَ وَلَٰكِنَّ ٱلظَّـٰلِمِينَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ يَجۡحَدُونَ

Hakika, tunajua kuwa kwa yakini kabisa, yanakuhuzunisha mno yale wanayosema. Kwa hakika hawakupingi wewe, lakini madhalimu wanazipinga Aya za Allah



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 34

وَلَقَدۡ كُذِّبَتۡ رُسُلٞ مِّن قَبۡلِكَ فَصَبَرُواْ عَلَىٰ مَا كُذِّبُواْ وَأُوذُواْ حَتَّىٰٓ أَتَىٰهُمۡ نَصۡرُنَاۚ وَلَا مُبَدِّلَ لِكَلِمَٰتِ ٱللَّهِۚ وَلَقَدۡ جَآءَكَ مِن نَّبَإِيْ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na kwa hakika kabisa, walipingwa Mitume wengi kabla yako, wakasubiri juu ya yale waliopingwa, na walifanyiwa maudhi hadi ulipowajia msaada wetu. Na hakuna wa kubadilisha maneno ya Allah. Na kwa hakika kabisa, zimekujia baadhi ya habari za Mitume



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 35

وَإِن كَانَ كَبُرَ عَلَيۡكَ إِعۡرَاضُهُمۡ فَإِنِ ٱسۡتَطَعۡتَ أَن تَبۡتَغِيَ نَفَقٗا فِي ٱلۡأَرۡضِ أَوۡ سُلَّمٗا فِي ٱلسَّمَآءِ فَتَأۡتِيَهُم بِـَٔايَةٖۚ وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ لَجَمَعَهُمۡ عَلَى ٱلۡهُدَىٰۚ فَلَا تَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡجَٰهِلِينَ

Na kama umekwazwa sana na upinzani wao, basi kama utaweza kupata njia ya chini ya ardhi au ngazi upande mbinguni ili uwaletee Aya (zisizo kuwa hizi basi fanya). Na lau kama Allah angetaka, basi kwa hakika kabisa angewakusanya wote (wakawa) katika uongofu. Basi (acha kabisa) usiwe miongoni mwa wajinga



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 36

۞إِنَّمَا يَسۡتَجِيبُ ٱلَّذِينَ يَسۡمَعُونَۘ وَٱلۡمَوۡتَىٰ يَبۡعَثُهُمُ ٱللَّهُ ثُمَّ إِلَيۡهِ يُرۡجَعُونَ

Ilivyo ni kwamba, wanaoitika (wito) ni wale tu wanaosikia (usikivu wa mazingatio). Na wafu (wa nyoyo ambao ni makafiri) Allah atawafufua, kisha kwake tu watarudishwa



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 37

وَقَالُواْ لَوۡلَا نُزِّلَ عَلَيۡهِ ءَايَةٞ مِّن رَّبِّهِۦۚ قُلۡ إِنَّ ٱللَّهَ قَادِرٌ عَلَىٰٓ أَن يُنَزِّلَ ءَايَةٗ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Na walisema: (ingekuwa vizuri) lau kama (Mtume Muhammad) angeteremshiwa Aya (Muujiza) kutoka kwa Mola wake. Sema: Hakika, Allah ni mwenye uwezo wa kuteremsha Aya (Muujiza wanaoutaka) lakini wengi wao hawajui (kitakachowakuta kama wakiteremshiwa muujiza na wasiamini)



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 38

وَمَا مِن دَآبَّةٖ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَلَا طَـٰٓئِرٖ يَطِيرُ بِجَنَاحَيۡهِ إِلَّآ أُمَمٌ أَمۡثَالُكُمۚ مَّا فَرَّطۡنَا فِي ٱلۡكِتَٰبِ مِن شَيۡءٖۚ ثُمَّ إِلَىٰ رَبِّهِمۡ يُحۡشَرُونَ

Na hakuna kiumbe yeyote anayetembea ardhini wala ndege anayeruka kwa mbawa zake, isipokuwa tu ni mataifa mfano wenu. Hatukuzembea (hatukuacha) kitu chochote katika (hiki) Kitabu (cha Qur’ani). Kisha watakusanywa kwa Mola wao tu (Siku ya Kiyama)



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 39

وَٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا صُمّٞ وَبُكۡمٞ فِي ٱلظُّلُمَٰتِۗ مَن يَشَإِ ٱللَّهُ يُضۡلِلۡهُ وَمَن يَشَأۡ يَجۡعَلۡهُ عَلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ

Na wale waliozipinga Aya zetu ni viziwi na mabubu (wamo) katika giza. Allah akitaka yeyote (apotee) atampoteza, na mwenye kumtaka (aongoke) anamuweka katika njia iliyonyooka (Uislamu)



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 40

قُلۡ أَرَءَيۡتَكُمۡ إِنۡ أَتَىٰكُمۡ عَذَابُ ٱللَّهِ أَوۡ أَتَتۡكُمُ ٱلسَّاعَةُ أَغَيۡرَ ٱللَّهِ تَدۡعُونَ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Sema: Hivi mnaonaje itakapokujieni adhabu ya Allah (hapa duniani) au kitakapokujieni Kiyama, hivi mtawaomba (Miungu wengine) badala ya Allah kama kweli nyinyi ni wakweli?



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 41

بَلۡ إِيَّاهُ تَدۡعُونَ فَيَكۡشِفُ مَا تَدۡعُونَ إِلَيۡهِ إِن شَآءَ وَتَنسَوۡنَ مَا تُشۡرِكُونَ

Bali ni yeye tu ndiye mnayemuomba na (kwa sababu ya maombi yenu) anatatua matatizo mnayo omba (yatatuliwe) akitaka, na (wakati huo) mnawasahau wale (Miungu) mnaowashirikisha (na Allah)



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 42

وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَآ إِلَىٰٓ أُمَمٖ مِّن قَبۡلِكَ فَأَخَذۡنَٰهُم بِٱلۡبَأۡسَآءِ وَٱلضَّرَّآءِ لَعَلَّهُمۡ يَتَضَرَّعُونَ

Na kwa hakika kabisa, tulituma (Mitume) katika mataifa mengi kabla yako (wakawapinga) tukawachukulia hatua (ya kuwaadhibu) kwa shida na madhara ili wawe wanyenyekevu



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 43

فَلَوۡلَآ إِذۡ جَآءَهُم بَأۡسُنَا تَضَرَّعُواْ وَلَٰكِن قَسَتۡ قُلُوبُهُمۡ وَزَيَّنَ لَهُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ مَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Basi walau ilipowajia adhabu yetu wangekuwa wanyenyekevu, lakini nyoyo zao zilikuwa ngumu, na shetani aliwapambia yale waliyokuwa wanayatenda



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 44

فَلَمَّا نَسُواْ مَا ذُكِّرُواْ بِهِۦ فَتَحۡنَا عَلَيۡهِمۡ أَبۡوَٰبَ كُلِّ شَيۡءٍ حَتَّىٰٓ إِذَا فَرِحُواْ بِمَآ أُوتُوٓاْ أَخَذۡنَٰهُم بَغۡتَةٗ فَإِذَا هُم مُّبۡلِسُونَ

Basi walipoyasahau (na kuacha kuyafanyia kazi) yale waliyokumbushwa, tuliwafungulia milango ya kila kitu, hadi walipofurahia yale waliyopewa tuliwachukulia hatua (na kuwaadhibu) ghafla, mara moja wakawa wamekata tamaa (ya kuokoka)



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 45

فَقُطِعَ دَابِرُ ٱلۡقَوۡمِ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْۚ وَٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ رَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Basi mzizi wa watu walio-dhulumu (waliomfanyia ushirika Allah) ukakatwa (wakaangamizwa wote), na kila sifa njema anaistahiki Allah Mola Mlezi wa viumbe wote



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 46

قُلۡ أَرَءَيۡتُمۡ إِنۡ أَخَذَ ٱللَّهُ سَمۡعَكُمۡ وَأَبۡصَٰرَكُمۡ وَخَتَمَ عَلَىٰ قُلُوبِكُم مَّنۡ إِلَٰهٌ غَيۡرُ ٱللَّهِ يَأۡتِيكُم بِهِۗ ٱنظُرۡ كَيۡفَ نُصَرِّفُ ٱلۡأٓيَٰتِ ثُمَّ هُمۡ يَصۡدِفُونَ

Sema: Je, mnaonaje kama Allah atachukua usikivu wenu na macho yenu na akaziziba nyoyo zenu, ni Mungu gani asiyekuwa Allah atakayewaletea hayo? Angalia namna tunavyobainisha Aya (hoja) kisha wao wanapinga!



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 47

قُلۡ أَرَءَيۡتَكُمۡ إِنۡ أَتَىٰكُمۡ عَذَابُ ٱللَّهِ بَغۡتَةً أَوۡ جَهۡرَةً هَلۡ يُهۡلَكُ إِلَّا ٱلۡقَوۡمُ ٱلظَّـٰلِمُونَ

Sema: Hivi mwaonaje kama itakujieni adhabu ya Allah ghafla au (ikikujieni) wazi wazi (ilhali mnaiona), si hawataangamizwa isipokuwa tu watu madhalimu (wanaomfanyia ushirika Allah)?



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 48

وَمَا نُرۡسِلُ ٱلۡمُرۡسَلِينَ إِلَّا مُبَشِّرِينَ وَمُنذِرِينَۖ فَمَنۡ ءَامَنَ وَأَصۡلَحَ فَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ

Na hatutumi Mitume isipokuwa (kazi yao ni) kutoa bishara (habari njema kwa wenye kutenda mema) na kutoa maonyo (kwa watendao maovu). Basi watakaoamini na wakatenda mema, hawatakuwa na hofu na hawatahuzunika



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 49

وَٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا يَمَسُّهُمُ ٱلۡعَذَابُ بِمَا كَانُواْ يَفۡسُقُونَ

Na wale waliozipinga Aya zetu itawashika (itawapata) adhabu kwasababu ya uovu waliokuwa wanaufanya



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 50

قُل لَّآ أَقُولُ لَكُمۡ عِندِي خَزَآئِنُ ٱللَّهِ وَلَآ أَعۡلَمُ ٱلۡغَيۡبَ وَلَآ أَقُولُ لَكُمۡ إِنِّي مَلَكٌۖ إِنۡ أَتَّبِعُ إِلَّا مَا يُوحَىٰٓ إِلَيَّۚ قُلۡ هَلۡ يَسۡتَوِي ٱلۡأَعۡمَىٰ وَٱلۡبَصِيرُۚ أَفَلَا تَتَفَكَّرُونَ

Sema (uwaambie): Mimi sikuambieni kuwa ninamiliki hazina za Allah, na wala sijui Ghaibu na wala sikuambieni kuwa mimi ni Malaika. Mimi sifuati isipokuwa tu wahyi (ufunuo) ninaoletewa. Sema: Hivi yuko sawa kipofu na anayeona? Hivi hamtafakari?



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 51

وَأَنذِرۡ بِهِ ٱلَّذِينَ يَخَافُونَ أَن يُحۡشَرُوٓاْ إِلَىٰ رَبِّهِمۡ لَيۡسَ لَهُم مِّن دُونِهِۦ وَلِيّٞ وَلَا شَفِيعٞ لَّعَلَّهُمۡ يَتَّقُونَ

Na waonye kwayo (Qur’ani) wale wanao ogopa kukusanywa kwa Mola wao wakiwa hawana msimamizi wala muombezi isipokuwa yeye (Allah), ili wamche Allah