Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 54

وَإِذۡ قَالَ مُوسَىٰ لِقَوۡمِهِۦ يَٰقَوۡمِ إِنَّكُمۡ ظَلَمۡتُمۡ أَنفُسَكُم بِٱتِّخَاذِكُمُ ٱلۡعِجۡلَ فَتُوبُوٓاْ إِلَىٰ بَارِئِكُمۡ فَٱقۡتُلُوٓاْ أَنفُسَكُمۡ ذَٰلِكُمۡ خَيۡرٞ لَّكُمۡ عِندَ بَارِئِكُمۡ فَتَابَ عَلَيۡكُمۡۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلتَّوَّابُ ٱلرَّحِيمُ

Na (kumbukeni) Musa alip-owaambia watu wake (kuwa): Enyi watu wangu, kwa hakika nyinyi mmezidhulumu nafsi zenu kwa kumfanya kwenu ndama Mungu. Basi tubieni kwa Mola wenu na uaneni. Hilo ni bora kwenu mbeleya Muumba wenu. Allah akakubali toba yenu. Kwa hakika, yeye ni Mwingi wa kukubali toba, Mwingi wa rehema



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 55

وَإِذۡ قُلۡتُمۡ يَٰمُوسَىٰ لَن نُّؤۡمِنَ لَكَ حَتَّىٰ نَرَى ٱللَّهَ جَهۡرَةٗ فَأَخَذَتۡكُمُ ٱلصَّـٰعِقَةُ وَأَنتُمۡ تَنظُرُونَ

Na (kumbukeni) mliposema (kumwambia Mtume Musa kuwa): Ewe Musa, hatutakuamini mpaka tumuone Allah waziwazi. Basi ukakuchukueni (ukakuteketezeni) moto wa radi na hali mnatazama



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 56

ثُمَّ بَعَثۡنَٰكُم مِّنۢ بَعۡدِ مَوۡتِكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ

Kisha tukakufufueni baada ya kufa kwenu ili mpate kushukuru



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 57

وَظَلَّلۡنَا عَلَيۡكُمُ ٱلۡغَمَامَ وَأَنزَلۡنَا عَلَيۡكُمُ ٱلۡمَنَّ وَٱلسَّلۡوَىٰۖ كُلُواْ مِن طَيِّبَٰتِ مَا رَزَقۡنَٰكُمۡۚ وَمَا ظَلَمُونَا وَلَٰكِن كَانُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ يَظۡلِمُونَ

Na tukakufunikeni kivuli cha mawingu na tukakuteremshieni Mana na Salwa, (na kukuambieni): Kuleni katika vitu vizuri tulivyokuruzukuni, na hawakutudhulumu sisi, lakini walikuwa wanajidhulumu wenyewe



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 58

وَإِذۡ قُلۡنَا ٱدۡخُلُواْ هَٰذِهِ ٱلۡقَرۡيَةَ فَكُلُواْ مِنۡهَا حَيۡثُ شِئۡتُمۡ رَغَدٗا وَٱدۡخُلُواْ ٱلۡبَابَ سُجَّدٗا وَقُولُواْ حِطَّةٞ نَّغۡفِرۡ لَكُمۡ خَطَٰيَٰكُمۡۚ وَسَنَزِيدُ ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Na (kumbuka) tuliposema (kuwaambia Wana wa Israili kuwa): Ingieni katika mji huu. Kuleni humo mtakavyo (na) kwa wasaa, naingieni katika lango mkiwa mmesujudu, na sememeni: “Ombi letu ni kusamehewa dhambi”, tutakusameheni makosa yenu. Na tutawazidishia watendao mazuri



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 59

فَبَدَّلَ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ قَوۡلًا غَيۡرَ ٱلَّذِي قِيلَ لَهُمۡ فَأَنزَلۡنَا عَلَى ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ رِجۡزٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ بِمَا كَانُواْ يَفۡسُقُونَ

Basi waliodhulumu walibadilisha kauli (nyingine) sio ile waliyoambiwa. Kwa sababu hiyo, tuliwateremshia waliodhulumu adhabu kutoka mbinguni kwa sababu ya uovu waliokuwa wakiufanya



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 60

۞وَإِذِ ٱسۡتَسۡقَىٰ مُوسَىٰ لِقَوۡمِهِۦ فَقُلۡنَا ٱضۡرِب بِّعَصَاكَ ٱلۡحَجَرَۖ فَٱنفَجَرَتۡ مِنۡهُ ٱثۡنَتَا عَشۡرَةَ عَيۡنٗاۖ قَدۡ عَلِمَ كُلُّ أُنَاسٖ مَّشۡرَبَهُمۡۖ كُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ مِن رِّزۡقِ ٱللَّهِ وَلَا تَعۡثَوۡاْ فِي ٱلۡأَرۡضِ مُفۡسِدِينَ

Na kumbuka Musa alipo-waombea maji watu wake tukam-wambia: Lipige jiwe kwa fimbo yako. (Alipolipiga) Zikabubujika kutoka katika jiwe hilo chemchemi kumi na mbili. Kila watu walijua mahali pao pa (kuchota maji ya) kunywa. (Tuliwaambia:) Kuleni na kunyweni katika riziki za Allah, na msifanye uovu katika ardhi



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 61

وَإِذۡ قُلۡتُمۡ يَٰمُوسَىٰ لَن نَّصۡبِرَ عَلَىٰ طَعَامٖ وَٰحِدٖ فَٱدۡعُ لَنَا رَبَّكَ يُخۡرِجۡ لَنَا مِمَّا تُنۢبِتُ ٱلۡأَرۡضُ مِنۢ بَقۡلِهَا وَقِثَّآئِهَا وَفُومِهَا وَعَدَسِهَا وَبَصَلِهَاۖ قَالَ أَتَسۡتَبۡدِلُونَ ٱلَّذِي هُوَ أَدۡنَىٰ بِٱلَّذِي هُوَ خَيۡرٌۚ ٱهۡبِطُواْ مِصۡرٗا فَإِنَّ لَكُم مَّا سَأَلۡتُمۡۗ وَضُرِبَتۡ عَلَيۡهِمُ ٱلذِّلَّةُ وَٱلۡمَسۡكَنَةُ وَبَآءُو بِغَضَبٖ مِّنَ ٱللَّهِۚ ذَٰلِكَ بِأَنَّهُمۡ كَانُواْ يَكۡفُرُونَ بِـَٔايَٰتِ ٱللَّهِ وَيَقۡتُلُونَ ٱلنَّبِيِّـۧنَ بِغَيۡرِ ٱلۡحَقِّۚ ذَٰلِكَ بِمَا عَصَواْ وَّكَانُواْ يَعۡتَدُونَ

Na (kumbukeni) mliposema: Ewe Musa, hatutaweza kuvumilia (kula) chakula cha aina moja tu. Basi tuombee kwa Mola wako atutolee katika vile ambavyo ardhi inaotesha, ikiwa ni pamoja na mboga mboga zake na matango yake na vitunguu saumu vyake na dengu zake na vitunguu maji vyake. Musa akasema: Hivi, mnataka kubadilisha ambacho ni duni sana kwa ambacho ni bora zaidi? Shukeni mjini. Huko mtapata hivyo mlivyovitaka. Na wakapigwa chapa ya udhalili na umaskini na wakastahiki ghadhabu za Allah. Hayo ni kwa sababu walikuwa wakizikufuru Aya za Allah na wakiwaua Mitume pasina haki yoyote. Hayo ni kwa sababu ya kuasi kwao, na walikuwa wakichupa mipaka



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 62

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَٱلَّذِينَ هَادُواْ وَٱلنَّصَٰرَىٰ وَٱلصَّـٰبِـِٔينَ مَنۡ ءَامَنَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ وَعَمِلَ صَٰلِحٗا فَلَهُمۡ أَجۡرُهُمۡ عِندَ رَبِّهِمۡ وَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ

Hakika, Walioamini na Waya-hudi na Wanasara na Wasabai; waliomuamini Allah na Siku ya Mwisho na wakatenda matendo mema basi hao wanamalipo mbele ya Mola wao, na hawatakuwa na hofu yoyote na hawatahuzunika



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 63

وَإِذۡ أَخَذۡنَا مِيثَٰقَكُمۡ وَرَفَعۡنَا فَوۡقَكُمُ ٱلطُّورَ خُذُواْ مَآ ءَاتَيۡنَٰكُم بِقُوَّةٖ وَٱذۡكُرُواْ مَا فِيهِ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ

Na (kumbukeni) tulipochukua ahadi zenu na tukanyanyua (mlima) Turi juu yenu (tukakuambieni kuwa): Kichukueni kwanguvu tulichokupeni na yakumbukeni yaliyomo ndani yake ili mpate kuwa Wacha Mungu



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 64

ثُمَّ تَوَلَّيۡتُم مِّنۢ بَعۡدِ ذَٰلِكَۖ فَلَوۡلَا فَضۡلُ ٱللَّهِ عَلَيۡكُمۡ وَرَحۡمَتُهُۥ لَكُنتُم مِّنَ ٱلۡخَٰسِرِينَ

Kisha mkageuka baada ya hayo. Na lau kama sio fadhila za Allah na rehema zake kwenu mngekuwa miongoni mwa wenye hasara



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 65

وَلَقَدۡ عَلِمۡتُمُ ٱلَّذِينَ ٱعۡتَدَوۡاْ مِنكُمۡ فِي ٱلسَّبۡتِ فَقُلۡنَا لَهُمۡ كُونُواْ قِرَدَةً خَٰسِـِٔينَ

Na, kwa hakika kabisa, mmewajua waliovuka mipaka miongoni mwenu katika (siku ya) Jumamosi, tukawaambia: Kuweni nyani dhalili



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 66

فَجَعَلۡنَٰهَا نَكَٰلٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهَا وَمَا خَلۡفَهَا وَمَوۡعِظَةٗ لِّلۡمُتَّقِينَ

Tukalifanya tukio hilo onyo kwa waliopo na wajao baada yake, na ni mazingatio kwa Wacha Mungu



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 67

وَإِذۡ قَالَ مُوسَىٰ لِقَوۡمِهِۦٓ إِنَّ ٱللَّهَ يَأۡمُرُكُمۡ أَن تَذۡبَحُواْ بَقَرَةٗۖ قَالُوٓاْ أَتَتَّخِذُنَا هُزُوٗاۖ قَالَ أَعُوذُ بِٱللَّهِ أَنۡ أَكُونَ مِنَ ٱلۡجَٰهِلِينَ

Na (wakumbushe watu wako) pale Musa alipowaambia watu wake kuwa: Hakika, Allah anakuamrisheni kuchinja ng’ombe. Wakasema: Je, unatufanyia mzaha? Akasema: Naomba kinga kwa Allah anilinde nisiwe miongoni mwa wajinga



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 68

قَالُواْ ٱدۡعُ لَنَا رَبَّكَ يُبَيِّن لَّنَا مَا هِيَۚ قَالَ إِنَّهُۥ يَقُولُ إِنَّهَا بَقَرَةٞ لَّا فَارِضٞ وَلَا بِكۡرٌ عَوَانُۢ بَيۡنَ ذَٰلِكَۖ فَٱفۡعَلُواْ مَا تُؤۡمَرُونَ

Wakasema: Tuombee (kwa) Mola wako atubainishie ni ng’ombe gani? Akasema: Hakika yeye (Allah) anasema: Ni ng’ombe ambaye sio mpevu sana wala sio mchanga sana. Ni wakati baina ya sifa hizo. Basi tekelezeni mnayoamriwa



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 69

قَالُواْ ٱدۡعُ لَنَا رَبَّكَ يُبَيِّن لَّنَا مَا لَوۡنُهَاۚ قَالَ إِنَّهُۥ يَقُولُ إِنَّهَا بَقَرَةٞ صَفۡرَآءُ فَاقِعٞ لَّوۡنُهَا تَسُرُّ ٱلنَّـٰظِرِينَ

Wakasema: Tuulizie (kwa) Mola wako atubainishie ni warangi gani? Akasema: Hakika yeye (Allah) anasema: Ni ng’ombe wa rangi ya manjano iliyokoza anayewafurahisha wanaomtazama



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 70

قَالُواْ ٱدۡعُ لَنَا رَبَّكَ يُبَيِّن لَّنَا مَا هِيَ إِنَّ ٱلۡبَقَرَ تَشَٰبَهَ عَلَيۡنَا وَإِنَّآ إِن شَآءَ ٱللَّهُ لَمُهۡتَدُونَ

Wakasema: Tuulizie (kwa) Mola wako atubainishie kuwa yuko vipi? Hakika ng’ombe wametuchanganya (kwa kufanana), nasi Allah akipenda tutaongoka



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 71

قَالَ إِنَّهُۥ يَقُولُ إِنَّهَا بَقَرَةٞ لَّا ذَلُولٞ تُثِيرُ ٱلۡأَرۡضَ وَلَا تَسۡقِي ٱلۡحَرۡثَ مُسَلَّمَةٞ لَّا شِيَةَ فِيهَاۚ قَالُواْ ٱلۡـَٰٔنَ جِئۡتَ بِٱلۡحَقِّۚ فَذَبَحُوهَا وَمَا كَادُواْ يَفۡعَلُونَ

Akasema: Allah anasema kuwa ni ng’ombe asiyetumikishwa kwa kazi ya kulima wala kumwagilia mashamba. Awe salama; asiwe na kasoro katika mwili wake. Wakasema: Sasa umekuja na haki. Basi wakamchinja na walikaribia kutotekeleza



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 72

وَإِذۡ قَتَلۡتُمۡ نَفۡسٗا فَٱدَّـٰرَٰٔتُمۡ فِيهَاۖ وَٱللَّهُ مُخۡرِجٞ مَّا كُنتُمۡ تَكۡتُمُونَ

Na (kumbukeni enyi Wana wa Israeli) mlipoua nafsi (mtu) kisha mkatafautiana katika hilo, na Allah ni mwenye kuyatoa hayo mliyokuwa mkiyaficha



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 73

فَقُلۡنَا ٱضۡرِبُوهُ بِبَعۡضِهَاۚ كَذَٰلِكَ يُحۡيِ ٱللَّهُ ٱلۡمَوۡتَىٰ وَيُرِيكُمۡ ءَايَٰتِهِۦ لَعَلَّكُمۡ تَعۡقِلُونَ

Tukasema: Mpigeni huyo ng’ombe kwa sehemu yake. Ni kama hivyo Allah anawafufua waliokufa, na anakuonesheni aya zake ili mpate kuweka mambo akilini



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 74

ثُمَّ قَسَتۡ قُلُوبُكُم مِّنۢ بَعۡدِ ذَٰلِكَ فَهِيَ كَٱلۡحِجَارَةِ أَوۡ أَشَدُّ قَسۡوَةٗۚ وَإِنَّ مِنَ ٱلۡحِجَارَةِ لَمَا يَتَفَجَّرُ مِنۡهُ ٱلۡأَنۡهَٰرُۚ وَإِنَّ مِنۡهَا لَمَا يَشَّقَّقُ فَيَخۡرُجُ مِنۡهُ ٱلۡمَآءُۚ وَإِنَّ مِنۡهَا لَمَا يَهۡبِطُ مِنۡ خَشۡيَةِ ٱللَّهِۗ وَمَا ٱللَّهُ بِغَٰفِلٍ عَمَّا تَعۡمَلُونَ

Kisha mioyo yenu ikawa migumu; ikawa kama jiwe au migumu zaidi (yajiwe). Kwa hakika, katika mawe yapo ambayo mito hububujika kutokea humo, na pia katika hayo mawe yapo ambayo hupasuka na maji yakatoka humo, na pia katika mawe yapo ambayo huporomoka kutokana na kumuogopa Allah. Na Allah si mwenye kughafilika na hayo mnayoyafanya



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 75

۞أَفَتَطۡمَعُونَ أَن يُؤۡمِنُواْ لَكُمۡ وَقَدۡ كَانَ فَرِيقٞ مِّنۡهُمۡ يَسۡمَعُونَ كَلَٰمَ ٱللَّهِ ثُمَّ يُحَرِّفُونَهُۥ مِنۢ بَعۡدِ مَا عَقَلُوهُ وَهُمۡ يَعۡلَمُونَ

“Je, hivi mnatumai kuwa watakufuateni katika imani na ilhali baadhi yao walikuwa wakisikia maneno ya Allah, kisha wanayapotosha baada yakuwa wameyafahamu vizuri, na ilhali wanajua.[1]


1- - Kuwa wanachofanya ni upotoshaji?


Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 76

وَإِذَا لَقُواْ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ قَالُوٓاْ ءَامَنَّا وَإِذَا خَلَا بَعۡضُهُمۡ إِلَىٰ بَعۡضٖ قَالُوٓاْ أَتُحَدِّثُونَهُم بِمَا فَتَحَ ٱللَّهُ عَلَيۡكُمۡ لِيُحَآجُّوكُم بِهِۦ عِندَ رَبِّكُمۡۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ

Na wakikutana na walioamini wanasema: Nasi pia tumeamini. Na wanapokuwa peke yao husema wakiambizana kuwa: Hivi mnawaambia yale aliyoyafunua Allah kwenu ili wapate kukuhojini kwayo mbele ya Mola wenu? Hivi nyinyi hamna akili?



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 77

أَوَلَا يَعۡلَمُونَ أَنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ مَا يُسِرُّونَ وَمَا يُعۡلِنُونَ

Hivi hawajui kwamba Allah anayajua wanayoyaficha na wanayoyadhihirisha?



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 78

وَمِنۡهُمۡ أُمِّيُّونَ لَا يَعۡلَمُونَ ٱلۡكِتَٰبَ إِلَّآ أَمَانِيَّ وَإِنۡ هُمۡ إِلَّا يَظُنُّونَ

Na miongoni mwao wapo wajinga wasiojua (kusoma) kitabu isipokuwa (wanachojua ni) matumaini tu, na hawakuwa wao ila ni watu wanao-fuata dhana tu



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 79

فَوَيۡلٞ لِّلَّذِينَ يَكۡتُبُونَ ٱلۡكِتَٰبَ بِأَيۡدِيهِمۡ ثُمَّ يَقُولُونَ هَٰذَا مِنۡ عِندِ ٱللَّهِ لِيَشۡتَرُواْ بِهِۦ ثَمَنٗا قَلِيلٗاۖ فَوَيۡلٞ لَّهُم مِّمَّا كَتَبَتۡ أَيۡدِيهِمۡ وَوَيۡلٞ لَّهُم مِّمَّا يَكۡسِبُونَ

Basi ole wao wanaoandika maandishi kwa mikono yao kisha wanasema kuwa (maandishi) hayo yanatoka kwa Allah, ili kwa kufanya hivyo wabadilishe kwa lengo la kupata pato dogo. Basi ole wao kwa kile kinachoandikwa kwa mikono yao, na ole wao kwa yale wanayoyafanya



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 80

وَقَالُواْ لَن تَمَسَّنَا ٱلنَّارُ إِلَّآ أَيَّامٗا مَّعۡدُودَةٗۚ قُلۡ أَتَّخَذۡتُمۡ عِندَ ٱللَّهِ عَهۡدٗا فَلَن يُخۡلِفَ ٱللَّهُ عَهۡدَهُۥٓۖ أَمۡ تَقُولُونَ عَلَى ٱللَّهِ مَا لَا تَعۡلَمُونَ

Na walisema: Moto (wa Jaha-namu) hautatugusa (hautatuunguza) isipokuwa (kwa) siku chache tu zenye kuhesabika. Sema (uwaulize): Je, mna ahadi kwa Allah juu ya hilo na kwamba Allah hatavunja ahadi yake? Au mnamsingizia Allah mambo msiyoyajua?



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 81

بَلَىٰۚ مَن كَسَبَ سَيِّئَةٗ وَأَحَٰطَتۡ بِهِۦ خَطِيٓـَٔتُهُۥ فَأُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ

Hali si kama wanavyodai. (Hali iko hivi): Wote watendao dhambi na dhambi zao zikawazunguka[1] hao ndio watu wa Motoni; wataishi humo milele


1- - Wakabobea katika kutenda dhambi.


Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 82

وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡجَنَّةِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ

Na walioamini na wakatenda yaliyo mema hao ndio watu wa Peponi; wataishi humo milele



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 83

وَإِذۡ أَخَذۡنَا مِيثَٰقَ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ لَا تَعۡبُدُونَ إِلَّا ٱللَّهَ وَبِٱلۡوَٰلِدَيۡنِ إِحۡسَانٗا وَذِي ٱلۡقُرۡبَىٰ وَٱلۡيَتَٰمَىٰ وَٱلۡمَسَٰكِينِ وَقُولُواْ لِلنَّاسِ حُسۡنٗا وَأَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتُواْ ٱلزَّكَوٰةَ ثُمَّ تَوَلَّيۡتُمۡ إِلَّا قَلِيلٗا مِّنكُمۡ وَأَنتُم مُّعۡرِضُونَ

Na (kumbukeni) Tulipochukua ahadi kwa Wana wa Israeli kwamba, hamtamuabudu yeyote Ila Allah tu, na mtawatendea wema wazazi, na ndugu na yatima na maskini, na mseme na watu kwa maneno mazuri. Na simamisheni Swala na toeni Zaka, kisha mkakengeuka isipokuwa wachache tu kati yenu, na ilhali nyinyi mnapuuza