يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ كُلُواْ مِن طَيِّبَٰتِ مَا رَزَقۡنَٰكُمۡ وَٱشۡكُرُواْ لِلَّهِ إِن كُنتُمۡ إِيَّاهُ تَعۡبُدُونَ
Enyi mlioamini, kuleni vizuri tulivyokuruzukuni, na mshukuruni Allah ikiwa mnamuabudu yeye tu
إِنَّمَا حَرَّمَ عَلَيۡكُمُ ٱلۡمَيۡتَةَ وَٱلدَّمَ وَلَحۡمَ ٱلۡخِنزِيرِ وَمَآ أُهِلَّ بِهِۦ لِغَيۡرِ ٱللَّهِۖ فَمَنِ ٱضۡطُرَّ غَيۡرَ بَاغٖ وَلَا عَادٖ فَلَآ إِثۡمَ عَلَيۡهِۚ إِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٌ
Yeye tu amekuharamishieni mzoga na damu na nyama ya nguruwe na kilichochinjwa kwa kutaja jina lisiliokuwa la Allah. Lakini, aliyefikwa na dharura bila ya kutamani wala kupitiliza kiasi, hana dhambi[1]. Hakika, Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa kurehemu
1- - Kula katika hivyo vilivyo haramishwa.
إِنَّ ٱلَّذِينَ يَكۡتُمُونَ مَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ مِنَ ٱلۡكِتَٰبِ وَيَشۡتَرُونَ بِهِۦ ثَمَنٗا قَلِيلًا أُوْلَـٰٓئِكَ مَا يَأۡكُلُونَ فِي بُطُونِهِمۡ إِلَّا ٱلنَّارَ وَلَا يُكَلِّمُهُمُ ٱللَّهُ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ وَلَا يُزَكِّيهِمۡ وَلَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٌ
Hakika, wale wanaoficha yaliyoteremshwa na Allah katika kitabu, na kufadhilisha kwayo thamani ndogo, hao hawali matumboni mwao isipokuwa moto tu, wala Allah hatawasemeza Siku ya Kiyama wala hatawatakasa; na watapata adhabu iumizayo
أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ ٱشۡتَرَوُاْ ٱلضَّلَٰلَةَ بِٱلۡهُدَىٰ وَٱلۡعَذَابَ بِٱلۡمَغۡفِرَةِۚ فَمَآ أَصۡبَرَهُمۡ عَلَى ٱلنَّارِ
Hao ndio walionunua upotevu badala ya uongofu, na adhabu badala ya msamaha. Ni wakushangaza sana uvumilivu wao wa kuuvumilia Moto!
ذَٰلِكَ بِأَنَّ ٱللَّهَ نَزَّلَ ٱلۡكِتَٰبَ بِٱلۡحَقِّۗ وَإِنَّ ٱلَّذِينَ ٱخۡتَلَفُواْ فِي ٱلۡكِتَٰبِ لَفِي شِقَاقِۭ بَعِيدٖ
Hayo ni kwa sababu Allah ameteremsha kitabu kwa haki, na wale waliotafautiana katika kitabu wamo katika mpasuko ulio mbali
۞لَّيۡسَ ٱلۡبِرَّ أَن تُوَلُّواْ وُجُوهَكُمۡ قِبَلَ ٱلۡمَشۡرِقِ وَٱلۡمَغۡرِبِ وَلَٰكِنَّ ٱلۡبِرَّ مَنۡ ءَامَنَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ وَٱلۡمَلَـٰٓئِكَةِ وَٱلۡكِتَٰبِ وَٱلنَّبِيِّـۧنَ وَءَاتَى ٱلۡمَالَ عَلَىٰ حُبِّهِۦ ذَوِي ٱلۡقُرۡبَىٰ وَٱلۡيَتَٰمَىٰ وَٱلۡمَسَٰكِينَ وَٱبۡنَ ٱلسَّبِيلِ وَٱلسَّآئِلِينَ وَفِي ٱلرِّقَابِ وَأَقَامَ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتَى ٱلزَّكَوٰةَ وَٱلۡمُوفُونَ بِعَهۡدِهِمۡ إِذَا عَٰهَدُواْۖ وَٱلصَّـٰبِرِينَ فِي ٱلۡبَأۡسَآءِ وَٱلضَّرَّآءِ وَحِينَ ٱلۡبَأۡسِۗ أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ صَدَقُواْۖ وَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُتَّقُونَ
Sio wema peke yake kuwa mnaelekeza nyuso zenu upande wa mashariki na magharibi. Bali wema ni (wa) wanaomuamini Allah na Siku ya Mwisho na Malaika na Vitabu na Manabii, na wanatoa mali pamoja na kuwa wanaipenda wakawapa ndugu na mayatima na maskini na wasafiri na waombao na katika (kuwakomboa) watumwa, na wakawa wanasimamisha swala na kutoa zaka, na watekelezao ahadi zao wanapoahidi, na wavumiliao katika shida na madhara na (katika) wakati wa vita. Hao ndio wa kweli na hao ndio wa mchao Allah
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ كُتِبَ عَلَيۡكُمُ ٱلۡقِصَاصُ فِي ٱلۡقَتۡلَىۖ ٱلۡحُرُّ بِٱلۡحُرِّ وَٱلۡعَبۡدُ بِٱلۡعَبۡدِ وَٱلۡأُنثَىٰ بِٱلۡأُنثَىٰۚ فَمَنۡ عُفِيَ لَهُۥ مِنۡ أَخِيهِ شَيۡءٞ فَٱتِّبَاعُۢ بِٱلۡمَعۡرُوفِ وَأَدَآءٌ إِلَيۡهِ بِإِحۡسَٰنٖۗ ذَٰلِكَ تَخۡفِيفٞ مِّن رَّبِّكُمۡ وَرَحۡمَةٞۗ فَمَنِ ٱعۡتَدَىٰ بَعۡدَ ذَٰلِكَ فَلَهُۥ عَذَابٌ أَلِيمٞ
Enyi mlioamini, mmeandikiwa kulipa kisasi katika waliouawa; muungwana kwa muungwana na mtumwa kwa mtumwa na mwanamke kwa mwanamke. Na aliyesamehewa jambo na ndugu yake (mtendewa jinai) basi fidia ifuatiliwe kwa wema na atekelezewe kwa uzuri. Hiyo ni tahafifu itokayo kwa Mola wenu na ni rehema. Na atakayekiuka baada ya hayo, basi yeye atapata adhabu iumizayo
وَلَكُمۡ فِي ٱلۡقِصَاصِ حَيَوٰةٞ يَـٰٓأُوْلِي ٱلۡأَلۡبَٰبِ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ
Na mtakuwa na uhai (ulio bora) katika kulipiza kisasi enyi wenye akili, ili muogope (msalimike)
كُتِبَ عَلَيۡكُمۡ إِذَا حَضَرَ أَحَدَكُمُ ٱلۡمَوۡتُ إِن تَرَكَ خَيۡرًا ٱلۡوَصِيَّةُ لِلۡوَٰلِدَيۡنِ وَٱلۡأَقۡرَبِينَ بِٱلۡمَعۡرُوفِۖ حَقًّا عَلَى ٱلۡمُتَّقِينَ
Mmeandikiwa mmoja wenu kutoa wasia kwa wazazi na ndugu kwa namna nzuri anapofikwa na mauti kama akiacha mali, ikiwa ni haki kwa wa mchao Allah
فَمَنۢ بَدَّلَهُۥ بَعۡدَ مَا سَمِعَهُۥ فَإِنَّمَآ إِثۡمُهُۥ عَلَى ٱلَّذِينَ يُبَدِّلُونَهُۥٓۚ إِنَّ ٱللَّهَ سَمِيعٌ عَلِيمٞ
Na atakayeubadilisha wasia huo baada ya kuusikia, basi ilivyo ni kwamba dhambi yake ipo kwa wale watakaoubadilisha. Hakika, Allah ni Msikiaji mno[1], Mjuzi mno[2]
1- - Wa kauli ya mtoa wasia.
2- - Wa kitendo chake na atamlipa.
فَمَنۡ خَافَ مِن مُّوصٖ جَنَفًا أَوۡ إِثۡمٗا فَأَصۡلَحَ بَيۡنَهُمۡ فَلَآ إِثۡمَ عَلَيۡهِۚ إِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Na mwenye kuchelea kwa mtoa wasia kupotoka au dhambi akarekebisha baina yao, basi hatakuwa na dhambi. Hakika, Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa kurehemu
يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ كُتِبَ عَلَيۡكُمُ ٱلصِّيَامُ كَمَا كُتِبَ عَلَى ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِكُمۡ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ
Enyi mlioamini, mmeandikiwa funga kama walivyoandikiwa waliokuwepo kabla yenu ili mpate kumcha Allah
أَيَّامٗا مَّعۡدُودَٰتٖۚ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوۡ عَلَىٰ سَفَرٖ فَعِدَّةٞ مِّنۡ أَيَّامٍ أُخَرَۚ وَعَلَى ٱلَّذِينَ يُطِيقُونَهُۥ فِدۡيَةٞ طَعَامُ مِسۡكِينٖۖ فَمَن تَطَوَّعَ خَيۡرٗا فَهُوَ خَيۡرٞ لَّهُۥۚ وَأَن تَصُومُواْ خَيۡرٞ لَّكُمۡ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ
Ni siku chache za kuhesabika tu. Na atakayekuwa mgonjwa miongoni mwenu au safarini, basi[1] atimize hesabu katika siku nyingine. Na wale wasioiweza (funga), watoe fidia kwa kumlisha maskini. Na atakayefanya wema kwa ridhaa ya nafsi yake, basi ni bora kwake, na kufunga ni bora kwenu, ikiwa mnajua
1- - Anaruhusiwa kuacha kufunga na atimize.
شَهۡرُ رَمَضَانَ ٱلَّذِيٓ أُنزِلَ فِيهِ ٱلۡقُرۡءَانُ هُدٗى لِّلنَّاسِ وَبَيِّنَٰتٖ مِّنَ ٱلۡهُدَىٰ وَٱلۡفُرۡقَانِۚ فَمَن شَهِدَ مِنكُمُ ٱلشَّهۡرَ فَلۡيَصُمۡهُۖ وَمَن كَانَ مَرِيضًا أَوۡ عَلَىٰ سَفَرٖ فَعِدَّةٞ مِّنۡ أَيَّامٍ أُخَرَۗ يُرِيدُ ٱللَّهُ بِكُمُ ٱلۡيُسۡرَ وَلَا يُرِيدُ بِكُمُ ٱلۡعُسۡرَ وَلِتُكۡمِلُواْ ٱلۡعِدَّةَ وَلِتُكَبِّرُواْ ٱللَّهَ عَلَىٰ مَا هَدَىٰكُمۡ وَلَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ
Ni mwezi wa Ramadhani ambao ndani yake imeteremshwa Qur’aniwe muongozo kwa watu, na hoja zilizo wazi za uongozi na upambanuzi. Basi atakayeshuhudia mwezi (huo) miongoni mwenu afunge. Na mwenye kuwa mgonjwa au safarini, basi[1] atimize hesabu katika siku nyingine[2]. Allah anakutakieni wepesi na hakutakieni uzito, na ili mumtukuze Allah kwa kukuongozeni na ili mpate kushukuru
1- - Anaruhusiwa kutofunga na kutimiza.
2- - Kwa kufunga zile siku ambazo hakufunga.
وَإِذَا سَأَلَكَ عِبَادِي عَنِّي فَإِنِّي قَرِيبٌۖ أُجِيبُ دَعۡوَةَ ٱلدَّاعِ إِذَا دَعَانِۖ فَلۡيَسۡتَجِيبُواْ لِي وَلۡيُؤۡمِنُواْ بِي لَعَلَّهُمۡ يَرۡشُدُونَ
Na waja wangu wakikuuliza kuhusu mimi, kwa yakini kabisa mimi nipo karibu; naitikia ombi la muombaji anaponiomba. Basi nawaniitikie na waniamini ili wapate kuongoka
أُحِلَّ لَكُمۡ لَيۡلَةَ ٱلصِّيَامِ ٱلرَّفَثُ إِلَىٰ نِسَآئِكُمۡۚ هُنَّ لِبَاسٞ لَّكُمۡ وَأَنتُمۡ لِبَاسٞ لَّهُنَّۗ عَلِمَ ٱللَّهُ أَنَّكُمۡ كُنتُمۡ تَخۡتَانُونَ أَنفُسَكُمۡ فَتَابَ عَلَيۡكُمۡ وَعَفَا عَنكُمۡۖ فَٱلۡـَٰٔنَ بَٰشِرُوهُنَّ وَٱبۡتَغُواْ مَا كَتَبَ ٱللَّهُ لَكُمۡۚ وَكُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ حَتَّىٰ يَتَبَيَّنَ لَكُمُ ٱلۡخَيۡطُ ٱلۡأَبۡيَضُ مِنَ ٱلۡخَيۡطِ ٱلۡأَسۡوَدِ مِنَ ٱلۡفَجۡرِۖ ثُمَّ أَتِمُّواْ ٱلصِّيَامَ إِلَى ٱلَّيۡلِۚ وَلَا تُبَٰشِرُوهُنَّ وَأَنتُمۡ عَٰكِفُونَ فِي ٱلۡمَسَٰجِدِۗ تِلۡكَ حُدُودُ ٱللَّهِ فَلَا تَقۡرَبُوهَاۗ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ ٱللَّهُ ءَايَٰتِهِۦ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمۡ يَتَّقُونَ
Mmehalalishiwa usiku wafunga kukutana kimwili na wake zenu. Wao ni vazi lenu, na nyinyi ni vazi lao. Allah amejua kwamba mlikuwa mkizihini nafsi zenu. Kwa hivyo, amekukubalieni toba yenu na amekusameheni. Basi sasa kutaneni nao kimwili natakeni aliyokuandikieni Allah. Na kuleni na kunyweni mpaka ubainike kwenu weupe wa Alfajiri dhidi ya weusi wa usiku. Kisha timizeni funga mpaka usiku. Wala msikutane nao kimwili, na hali mmekaa Itikafu misikitini. Hiyo ni mipaka ya Allah, basi msiisogelee. Hivi ndivyo Allah anavyobainisha hoja zake kwa watu ili wapate kumcha
وَلَا تَأۡكُلُوٓاْ أَمۡوَٰلَكُم بَيۡنَكُم بِٱلۡبَٰطِلِ وَتُدۡلُواْ بِهَآ إِلَى ٱلۡحُكَّامِ لِتَأۡكُلُواْ فَرِيقٗا مِّنۡ أَمۡوَٰلِ ٱلنَّاسِ بِٱلۡإِثۡمِ وَأَنتُمۡ تَعۡلَمُونَ
Na msile mali zenu baina yenu kwa batili na kuzipeleka kwa mahakimu ili mpate kula sehemu ya mali ya watu kwa dhambi na ilhali mnajua
۞يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلۡأَهِلَّةِۖ قُلۡ هِيَ مَوَٰقِيتُ لِلنَّاسِ وَٱلۡحَجِّۗ وَلَيۡسَ ٱلۡبِرُّ بِأَن تَأۡتُواْ ٱلۡبُيُوتَ مِن ظُهُورِهَا وَلَٰكِنَّ ٱلۡبِرَّ مَنِ ٱتَّقَىٰۗ وَأۡتُواْ ٱلۡبُيُوتَ مِنۡ أَبۡوَٰبِهَاۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ لَعَلَّكُمۡ تُفۡلِحُونَ
Wanakuuliza kuhusu miezi miandamo. Sema (uwaambie): Hiyo (miezi miandamo) ni vipimo vya nyakati kwa watu na Hija. Na si katika wema kuingia (katika) nyumba kwa nyuma lakini wema ni kumcha Allah. Na ingieni majumbani kupitia kwenye milango yake, na mcheni Allah ili mpate kufaulu
وَقَٰتِلُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ ٱلَّذِينَ يُقَٰتِلُونَكُمۡ وَلَا تَعۡتَدُوٓاْۚ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ ٱلۡمُعۡتَدِينَ
Na piganeni na wanaokupigeni katika njia ya Allah, na msivuke mipaka (mkawashambulia wasiohusika), kwa sababu Allah hawapendi wavukao mipaka
وَٱقۡتُلُوهُمۡ حَيۡثُ ثَقِفۡتُمُوهُمۡ وَأَخۡرِجُوهُم مِّنۡ حَيۡثُ أَخۡرَجُوكُمۡۚ وَٱلۡفِتۡنَةُ أَشَدُّ مِنَ ٱلۡقَتۡلِۚ وَلَا تُقَٰتِلُوهُمۡ عِندَ ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِ حَتَّىٰ يُقَٰتِلُوكُمۡ فِيهِۖ فَإِن قَٰتَلُوكُمۡ فَٱقۡتُلُوهُمۡۗ كَذَٰلِكَ جَزَآءُ ٱلۡكَٰفِرِينَ
Na waueni popote mtaka-powakuta, na wafukuzeni popote watakapo kufukuzeni. Na fitina ni mbaya zaidi kuliko kuua. Na msipigane nao mbele ya Msikiti Mtukufu mpaka wao wapigane nanyi humo. Wakipigana nanyi humo, basi waueni. Hivyo ndivyo yatakiwavyo kuwa malipo ya makafiri
فَإِنِ ٱنتَهَوۡاْ فَإِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Ikiwa wataacha[1] basi Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa kurehemu
1- - Kukuchokozeni au kupambana nanyi
وَقَٰتِلُوهُمۡ حَتَّىٰ لَا تَكُونَ فِتۡنَةٞ وَيَكُونَ ٱلدِّينُ لِلَّهِۖ فَإِنِ ٱنتَهَوۡاْ فَلَا عُدۡوَٰنَ إِلَّا عَلَى ٱلظَّـٰلِمِينَ
Na piganeni nao mpaka pasiwepo na fitina na dini iwe ya Allah tu. Ikiwa wataacha (kukufanyieni uadui) basi hapatakiwi kuwepo na uadui isipokuwa kwa madhalimu tu
ٱلشَّهۡرُ ٱلۡحَرَامُ بِٱلشَّهۡرِ ٱلۡحَرَامِ وَٱلۡحُرُمَٰتُ قِصَاصٞۚ فَمَنِ ٱعۡتَدَىٰ عَلَيۡكُمۡ فَٱعۡتَدُواْ عَلَيۡهِ بِمِثۡلِ مَا ٱعۡتَدَىٰ عَلَيۡكُمۡۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ مَعَ ٱلۡمُتَّقِينَ
Mwezi mtukufu kwa mwezi mtukufu. Na kila kilicho kitukufu kitalipiwa kisasi. Na yeyote atakaye fanya uadui juu yenu, basi mlipeni sawa na uadui alioufanya kwenu. Na mcheni Allah na jueni kwamba Allah yupamoja na wamchao
وَأَنفِقُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ وَلَا تُلۡقُواْ بِأَيۡدِيكُمۡ إِلَى ٱلتَّهۡلُكَةِ وَأَحۡسِنُوٓاْۚ إِنَّ ٱللَّهَ يُحِبُّ ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Na toeni katika njia ya Allah, na msijiingize kwenye maangamizi kwa mikono yenu. Na fanyeni mazuri, hakika Allah anawapenda wafanyao mazuri
وَأَتِمُّواْ ٱلۡحَجَّ وَٱلۡعُمۡرَةَ لِلَّهِۚ فَإِنۡ أُحۡصِرۡتُمۡ فَمَا ٱسۡتَيۡسَرَ مِنَ ٱلۡهَدۡيِۖ وَلَا تَحۡلِقُواْ رُءُوسَكُمۡ حَتَّىٰ يَبۡلُغَ ٱلۡهَدۡيُ مَحِلَّهُۥۚ فَمَن كَانَ مِنكُم مَّرِيضًا أَوۡ بِهِۦٓ أَذٗى مِّن رَّأۡسِهِۦ فَفِدۡيَةٞ مِّن صِيَامٍ أَوۡ صَدَقَةٍ أَوۡ نُسُكٖۚ فَإِذَآ أَمِنتُمۡ فَمَن تَمَتَّعَ بِٱلۡعُمۡرَةِ إِلَى ٱلۡحَجِّ فَمَا ٱسۡتَيۡسَرَ مِنَ ٱلۡهَدۡيِۚ فَمَن لَّمۡ يَجِدۡ فَصِيَامُ ثَلَٰثَةِ أَيَّامٖ فِي ٱلۡحَجِّ وَسَبۡعَةٍ إِذَا رَجَعۡتُمۡۗ تِلۡكَ عَشَرَةٞ كَامِلَةٞۗ ذَٰلِكَ لِمَن لَّمۡ يَكُنۡ أَهۡلُهُۥ حَاضِرِي ٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ شَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ
Na timizeni Hija na Umra kwa ajili ya Allah. Na ikiwa mmezuiwa[1], basi chinjeni wanyama watakaokuwa rahisi kupatikana. Na wala msinyoe vichwa vyenu, hadi mnyama afike mahali pake. Basi ambaye atakuwa mgonjwa miongoni mwenu, au ana tatizo kichwani kwake, basi atoe fidia ya kufunga au sadaka au mnyama. Na mtakapokuwa katika hali ya amani, atakayefanya Umra kabla ya Hija[2] basi afunge siku tatu katika Hija na siku saba mtakaporejea kwenu. Hizo ni siku kumi kamili. Hilo ni kwa ambaye familia yake sio wakazi wa (mji wa) Msikiti Mtukufu (wa Makka). Na mcheni Allah, na jueni kwamba, Allah ni mkali wa kuadhibu
1- - Kutimiza ibada hizo
2- - Bila kuunganisha Umra na Hija
ٱلۡحَجُّ أَشۡهُرٞ مَّعۡلُومَٰتٞۚ فَمَن فَرَضَ فِيهِنَّ ٱلۡحَجَّ فَلَا رَفَثَ وَلَا فُسُوقَ وَلَا جِدَالَ فِي ٱلۡحَجِّۗ وَمَا تَفۡعَلُواْ مِنۡ خَيۡرٖ يَعۡلَمۡهُ ٱللَّهُۗ وَتَزَوَّدُواْ فَإِنَّ خَيۡرَ ٱلزَّادِ ٱلتَّقۡوَىٰۖ وَٱتَّقُونِ يَـٰٓأُوْلِي ٱلۡأَلۡبَٰبِ
Hija ina miezi maalumu. Basi yeyote atakayeingia katika wajibu wa kutekeleza Hija katika miezi hiyo asiseme maneno yaliyokatazwa wala vitendo vilivyokatazwa wala asifanye mabishano katika Hija. Na wema wowote mnaoufanya Allah anaujua. Na jiandaeni, hakika maandalizi bora ni Ucha Mungu. Basi niogopeni enyi wenye akili
لَيۡسَ عَلَيۡكُمۡ جُنَاحٌ أَن تَبۡتَغُواْ فَضۡلٗا مِّن رَّبِّكُمۡۚ فَإِذَآ أَفَضۡتُم مِّنۡ عَرَفَٰتٖ فَٱذۡكُرُواْ ٱللَّهَ عِندَ ٱلۡمَشۡعَرِ ٱلۡحَرَامِۖ وَٱذۡكُرُوهُ كَمَا هَدَىٰكُمۡ وَإِن كُنتُم مِّن قَبۡلِهِۦ لَمِنَ ٱلضَّآلِّينَ
Hakuna ubaya wowote kwenu kutafuta fadhila za Mola wenu. Basi mtakapomiminika kutoka Arafa, mtajeni Allah kwenye eneo la Mash-arilharam. Na mtajeni kama alivyokupeni muongozo. Na hakika, kabla yake mlikuwa katika watu waliopotea
ثُمَّ أَفِيضُواْ مِنۡ حَيۡثُ أَفَاضَ ٱلنَّاسُ وَٱسۡتَغۡفِرُواْ ٱللَّهَۚ إِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ
Kisha miminikeni kutokea pale walipomiminika watu, naombeni msamaha kwa Allah, hakika Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mpole mno
فَإِذَا قَضَيۡتُم مَّنَٰسِكَكُمۡ فَٱذۡكُرُواْ ٱللَّهَ كَذِكۡرِكُمۡ ءَابَآءَكُمۡ أَوۡ أَشَدَّ ذِكۡرٗاۗ فَمِنَ ٱلنَّاسِ مَن يَقُولُ رَبَّنَآ ءَاتِنَا فِي ٱلدُّنۡيَا وَمَا لَهُۥ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ مِنۡ خَلَٰقٖ
Mtakapomaliza ibada zenu, basi mtajeni Allah, kama mnavyowataja baba zenu au zaidi. Na miongoni mwa watu wapo wanaosema: “Ewe Mola wetu tupe katika dunia, na hawatakuwa na fungu lolote Akhera
وَمِنۡهُم مَّن يَقُولُ رَبَّنَآ ءَاتِنَا فِي ٱلدُّنۡيَا حَسَنَةٗ وَفِي ٱلۡأٓخِرَةِ حَسَنَةٗ وَقِنَا عَذَابَ ٱلنَّارِ
Na baadhi yao wapo wanaosema: Ewe Mola wetu, tupe katika dunia wema, na Akhera wema na utukinge na adhabu ya Moto