Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 1

وَٱلۡفَجۡرِ

Naapa kwa alfajiri,



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 2

وَلَيَالٍ عَشۡرٖ

Na kwa masiku kumi,



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 3

وَٱلشَّفۡعِ وَٱلۡوَتۡرِ

Na kwa viwili viwili na kimoja kimoja,



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 4

وَٱلَّيۡلِ إِذَا يَسۡرِ

Na kwa usiku unapo pita,



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 5

هَلۡ فِي ذَٰلِكَ قَسَمٞ لِّذِي حِجۡرٍ

Je! Hapana katika haya kiapo kwa mwenye akili?



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 6

أَلَمۡ تَرَ كَيۡفَ فَعَلَ رَبُّكَ بِعَادٍ

Kwani hukuona jinsi Mola wako Mlezi alivyo wafanya kina A’di?



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 7

إِرَمَ ذَاتِ ٱلۡعِمَادِ

Wa Iram, wenye majumba marefu?



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 8

ٱلَّتِي لَمۡ يُخۡلَقۡ مِثۡلُهَا فِي ٱلۡبِلَٰدِ

Ambao haukuumbwa mfano wake katika nchi?



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 9

وَثَمُودَ ٱلَّذِينَ جَابُواْ ٱلصَّخۡرَ بِٱلۡوَادِ

Na Thamudi walio chonga majabali huko bondeni?



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 10

وَفِرۡعَوۡنَ ذِي ٱلۡأَوۡتَادِ

Na Firauni mwenye vigingi??



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 11

ٱلَّذِينَ طَغَوۡاْ فِي ٱلۡبِلَٰدِ

Ambao walifanya jeuri katika nchi



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 12

فَأَكۡثَرُواْ فِيهَا ٱلۡفَسَادَ

Wakakithirisha humo ufisadi?



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 13

فَصَبَّ عَلَيۡهِمۡ رَبُّكَ سَوۡطَ عَذَابٍ

Basi Mola wako Mlezi aliwapiga mjeledi wa adhabu



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 14

إِنَّ رَبَّكَ لَبِٱلۡمِرۡصَادِ

Hakika Mola wako Mlezi yupo kwenye mavizio anawavizia



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 15

فَأَمَّا ٱلۡإِنسَٰنُ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ رَبُّهُۥ فَأَكۡرَمَهُۥ وَنَعَّمَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَكۡرَمَنِ

Ama mtu anapo jaribiwa na Mola wake Mlezi, akamkirimu na akamneemesha, husema: Mola wangu Mlezi amenikirimu



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 16

وَأَمَّآ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ فَقَدَرَ عَلَيۡهِ رِزۡقَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَهَٰنَنِ

Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 17

كَلَّاۖ بَل لَّا تُكۡرِمُونَ ٱلۡيَتِيمَ

Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 18

وَلَا تَحَـٰٓضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ

Wala hamhimizani kulisha masikini;



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 19

وَتَأۡكُلُونَ ٱلتُّرَاثَ أَكۡلٗا لَّمّٗا

Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 20

وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبّٗا جَمّٗا

Na mnapenda mali mapenzi ya kupita kiasi



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 21

كَلَّآۖ إِذَا دُكَّتِ ٱلۡأَرۡضُ دَكّٗا دَكّٗا

Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 22

وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلۡمَلَكُ صَفّٗا صَفّٗا

Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 23

وَجِاْيٓءَ يَوۡمَئِذِۭ بِجَهَنَّمَۚ يَوۡمَئِذٖ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ وَأَنَّىٰ لَهُ ٱلذِّكۡرَىٰ

Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 24

يَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي قَدَّمۡتُ لِحَيَاتِي

Atasema: Laiti ningeli jitangulizia (mema) katika uhai wangu!



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 25

فَيَوۡمَئِذٖ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُۥٓ أَحَدٞ

Basi siku hiyo hataadhibu yeyote kama kuadhibu kwake



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 26

وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُۥٓ أَحَدٞ

Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 27

يَـٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَئِنَّةُ

Ewe nafsi iliyo tua!



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 28

ٱرۡجِعِيٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةٗ مَّرۡضِيَّةٗ

Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 29

فَٱدۡخُلِي فِي عِبَٰدِي

Basi ingia miongoni mwa waja wangu,



Capítulo: AL-FAJRI 

Verso : 30

وَٱدۡخُلِي جَنَّتِي

Na ingia katika Pepo yangu