Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 1

نٓۚ وَٱلۡقَلَمِ وَمَا يَسۡطُرُونَ

Nuun. Nina apa kwa kalamu na yale wayoyaandika



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 2

مَآ أَنتَ بِنِعۡمَةِ رَبِّكَ بِمَجۡنُونٖ

(Kwamba) Wewe (Muhammad) kwa neema ya Mola wako Mlezi (aliyokupa) sio mwendawazimu



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 3

وَإِنَّ لَكَ لَأَجۡرًا غَيۡرَ مَمۡنُونٖ

Na kwa hakika wewe una malipo (makubwa) yasiyo katika



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 4

وَإِنَّكَ لَعَلَىٰ خُلُقٍ عَظِيمٖ

Na hakika wewe uko juu ya tabia njema sana



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 5

فَسَتُبۡصِرُ وَيُبۡصِرُونَ

Basi hivi karibuni utaona, na wao wataona



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 6

بِأَييِّكُمُ ٱلۡمَفۡتُونُ

(Kwamba) Ni nani mwenye kichaa miongoni mwenu



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 7

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُهۡتَدِينَ

Hakika, Mola wako Mlezi ndiye amjuae zaidi aliyepotea njia yake, ndiye awajuae zaidi walioongoka



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 8

فَلَا تُطِعِ ٱلۡمُكَذِّبِينَ

Basi usiwatii wanao kadhibisha



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 9

وَدُّواْ لَوۡ تُدۡهِنُ فَيُدۡهِنُونَ

Wangependa uwe laini (ulegeze msimamo wako), nao wawe laini (walegeze msimamo wao na wakufuate)



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 10

وَلَا تُطِعۡ كُلَّ حَلَّافٖ مَّهِينٍ

Wala usimtii kila mwapaji sana, aliye dhalili,



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 11

هَمَّازٖ مَّشَّآءِۭ بِنَمِيمٖ

Mwingi wa kusengenya, mpitaji huku na kule kwa kufitinisha



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 12

مَّنَّاعٖ لِّلۡخَيۡرِ مُعۡتَدٍ أَثِيمٍ

Mwingi wa kuzuia ya kheri, aliyependukia katika kuwadhulumu (Watu) mwingi wa kutenda dhambi



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 13

عُتُلِّۭ بَعۡدَ ذَٰلِكَ زَنِيمٍ

Mkavu, na juu ya hayo ni mwana haramu (kujipachika tu kabila)



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 14

أَن كَانَ ذَا مَالٖ وَبَنِينَ

Kwakuwa tu ni mwenye kumiliki mali na watoto?



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 15

إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِ ءَايَٰتُنَا قَالَ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Anapo somewa Aya zetu, husema: Hizi ni simulizi za uwongo za watu wa zamani!



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 16

سَنَسِمُهُۥ عَلَى ٱلۡخُرۡطُومِ

Karibuni tutamtia kovu juu ya pua



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 17

إِنَّا بَلَوۡنَٰهُمۡ كَمَا بَلَوۡنَآ أَصۡحَٰبَ ٱلۡجَنَّةِ إِذۡ أَقۡسَمُواْ لَيَصۡرِمُنَّهَا مُصۡبِحِينَ

Hakika sisi Tumewajaribu (Maquraysh) kama Tulivyowajaribu watu wa shamba pale walipo apa kuwa bila shaka watayavuna (matunda yake) watakapo pambaukiwa asubuhi



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 18

وَلَا يَسۡتَثۡنُونَ

Na wala hawakusema In-Shaa Allaah (Allah akipenda)!



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 19

فَطَافَ عَلَيۡهَا طَآئِفٞ مِّن رَّبِّكَ وَهُمۡ نَآئِمُونَ

Basi (shamba lao) likazungukwa na (moto) kutoka kwa mola wako ilihali wao wamelala



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 20

فَأَصۡبَحَتۡ كَٱلصَّرِيمِ

Likawa kama lilovunwa (ilion-g’olewa mimea yake)



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 21

فَتَنَادَوۡاْ مُصۡبِحِينَ

Wakaitana, pale walipopam-baukiwa asubuhi



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 22

أَنِ ٱغۡدُواْ عَلَىٰ حَرۡثِكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰرِمِينَ

Kwamba nendeni asubuhi mapema shambani mwenu, mkiwa mnataka kuvuna



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 23

فَٱنطَلَقُواْ وَهُمۡ يَتَخَٰفَتُونَ

Wakatoka na huku wanakwenda kimya kimya wakinong’onezana



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 24

أَن لَّا يَدۡخُلَنَّهَا ٱلۡيَوۡمَ عَلَيۡكُم مِّسۡكِينٞ

Wakisema kwamba:: leo Maskini asiingie humo mwenu kinyume cha utashi wenu



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 25

وَغَدَوۡاْ عَلَىٰ حَرۡدٖ قَٰدِرِينَ

Wakatoka asubuhi mapema kwa kusudio la nguvu, wakidhani wana uwezo (wa kuwazuia maskini)



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 26

فَلَمَّا رَأَوۡهَا قَالُوٓاْ إِنَّا لَضَآلُّونَ

Basi walipoliona (shamba lao) wakasema: Hakika sisi bila shaka Tumepotea



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 27

بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ

(Walivyo tanabahi!): wakasema Bali sisi tumenyimwa (mavuno yake)!



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 28

قَالَ أَوۡسَطُهُمۡ أَلَمۡ أَقُل لَّكُمۡ لَوۡلَا تُسَبِّحُونَ

Mbora wao akasema: Sikukwambieni, kwa nini hamumtakasi Allah (kuiacha nia yenu mbaya)?



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 29

قَالُواْ سُبۡحَٰنَ رَبِّنَآ إِنَّا كُنَّا ظَٰلِمِينَ

Wakasema: utukufu ni wa mola wetu, hakika tulikuwa wenye kudhulumu



Capítulo: AL-QALAM 

Verso : 30

فَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَلَٰوَمُونَ

Basi Wakakabiliana wenyewe kwa wenyewe wakilaumiana