Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 1

إِذَا وَقَعَتِ ٱلۡوَاقِعَةُ

Wakati kitakapotokea Kiyama



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 2

لَيۡسَ لِوَقۡعَتِهَا كَاذِبَةٌ

Hakuna mpingaji wa kutokea kwake



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 3

خَافِضَةٞ رَّافِعَةٌ

Ni chenye kuwashusha hadhi (makafiri) na kuwanyanyua hadhi (waumini)



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 4

إِذَا رُجَّتِ ٱلۡأَرۡضُ رَجّٗا

Wakati ardhi itakapotikiswa mtikiso mkubwa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 5

وَبُسَّتِ ٱلۡجِبَالُ بَسّٗا

Na milima ikapondwa pondwa upondwaji mkubwa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 6

فَكَانَتۡ هَبَآءٗ مُّنۢبَثّٗا

(Kwa sababu ya kupondwa pondwa huko, milima) ikawa vumbi lenye kutawanyika



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 7

وَكُنتُمۡ أَزۡوَٰجٗا ثَلَٰثَةٗ

Na nyinyi (watu) mtakuwa namna tatu



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 8

فَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ

Basi watakuwepo watu wa kuliani. Je, ni kina nani watu wa kuliani?



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 9

وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ

Na (watakuwepo) watu wa kushotoni. Je, ni kina nani watu wa kushotoni?



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 10

وَٱلسَّـٰبِقُونَ ٱلسَّـٰبِقُونَ

Na (watakuwepo) waliotangulia mbele, (basi) watakua mbele.[1]


1- - Hawa ni wale ambao walitangulia mbele katika mambo ya kheri duniani ndio watakuwa mbele katika vyeo vya akhera.


Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 11

أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلۡمُقَرَّبُونَ

Hao ndio watakao kurubishwa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 12

فِي جَنَّـٰتِ ٱلنَّعِيمِ

katika pepo zenye neema



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 13

ثُلَّةٞ مِّنَ ٱلۡأَوَّلِينَ

Kundi kubwa katika wa mwanzo



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 14

وَقَلِيلٞ مِّنَ ٱلۡأٓخِرِينَ

Na wachache katika wa mwishoni.[1]


1- - Hawa walio karibishwa mbele ni kundi la wengi katika mataifa yalio tangulia na Manabii wao, na wachache katika Umma wa Muhammad rehma na amani ziwe juu yake ukilinganishwa na hao.


Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 15

عَلَىٰ سُرُرٖ مَّوۡضُونَةٖ

watakua juu ya vitanda vilivyofumwa vizuri



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 16

مُّتَّكِـِٔينَ عَلَيۡهَا مُتَقَٰبِلِينَ

hali wakiwa wameviegemea huku wakitazamana



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 17

يَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ وِلۡدَٰنٞ مُّخَلَّدُونَ

Watazungukiwa na vijana wenye kudumu



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 18

بِأَكۡوَابٖ وَأَبَارِيقَ وَكَأۡسٖ مِّن مَّعِينٖ

Kwa bilauri na mabirika na vikombe vya mvinyo kutoka kwenye chemchemu



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 19

لَّا يُصَدَّعُونَ عَنۡهَا وَلَا يُنزِفُونَ

Hawatapata maumivu ya kichwa kwa vinywaji hivyo wala hawa-tatokwa na akili



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 20

وَفَٰكِهَةٖ مِّمَّا يَتَخَيَّرُونَ

Na matunda watakayo pendelea wao



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 21

وَلَحۡمِ طَيۡرٖ مِّمَّا يَشۡتَهُونَ

Na nyama za ndege katika wata-kazozitamani



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 22

وَحُورٌ عِينٞ

Na wanawake wenye macho makubwa yaliyo meupe sana na weusi sana



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 23

كَأَمۡثَٰلِ ٱللُّؤۡلُوِٕ ٱلۡمَكۡنُونِ

Kama mfano wa lulu zilizohi-fadhiwa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 24

جَزَآءَۢ بِمَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Ikiwa ni malipo kwa ambayo walikuwa wanatenda (duniani)



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 25

لَا يَسۡمَعُونَ فِيهَا لَغۡوٗا وَلَا تَأۡثِيمًا

Hawatasikia humo maneno ya upuuzi wala yanayopelekea kupata madhambi



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 26

إِلَّا قِيلٗا سَلَٰمٗا سَلَٰمٗا

Isipokuwa itasemwa: Salama, na Amani!



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 27

وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلۡيَمِينِ

Na watu wa kuliani, ni wepi hao watu wa kuliani?



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 28

فِي سِدۡرٖ مَّخۡضُودٖ

Watakuwa kwenye mikunazi isiyo na miba



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 29

وَطَلۡحٖ مَّنضُودٖ

Na migomba iliyopangiliwa



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 30

وَظِلّٖ مَّمۡدُودٖ

Na kivuli kilichotandazwa