Capítulo: QAAF 

Verso : 1

قٓۚ وَٱلۡقُرۡءَانِ ٱلۡمَجِيدِ

Qaaf. Nina apa kwa Qur’ani Tukufu



Capítulo: QAAF 

Verso : 2

بَلۡ عَجِبُوٓاْ أَن جَآءَهُم مُّنذِرٞ مِّنۡهُمۡ فَقَالَ ٱلۡكَٰفِرُونَ هَٰذَا شَيۡءٌ عَجِيبٌ

Bali wamestaajabu kwamba amewajia muonyaji miongoni mwao, na kwa sababu hiyo makafiri wakasema: “Hili ni jambo la ajabu sana!



Capítulo: QAAF 

Verso : 3

أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗاۖ ذَٰلِكَ رَجۡعُۢ بَعِيدٞ

Je, hivi tukifa na tukawa udongo (tutafufuliwa)? Kurejea huko kuko mbali sana”



Capítulo: QAAF 

Verso : 4

قَدۡ عَلِمۡنَا مَا تَنقُصُ ٱلۡأَرۡضُ مِنۡهُمۡۖ وَعِندَنَا كِتَٰبٌ حَفِيظُۢ

Hakika, sisi tumejua kila ambacho ardhi inakipunguza kwao[1] na tunacho Kitabu kinachohifadhi barabara


1- - Kinachokusudiwa hap ani kwamba, kwa Allah hakipotei kitu. Pamoja na kwamba, makafifiri katika Aya iliyopita kabla ya hii wanaona kwamba wakifa na kuzikwa miili yao inaoza ardhini na kwamba si jambo linalowezekana kurejea tena kwenye hali yao ya zamani, Allah anasema hilo kwake ni jepesi na hakuna kitakachopotea.


Capítulo: QAAF 

Verso : 5

بَلۡ كَذَّبُواْ بِٱلۡحَقِّ لَمَّا جَآءَهُمۡ فَهُمۡ فِيٓ أَمۡرٖ مَّرِيجٍ

Bali wameikadhibisha (wamei-pinga) haki ilipowajia. Basi wao wamo katika jambo la mkorogeko



Capítulo: QAAF 

Verso : 6

أَفَلَمۡ يَنظُرُوٓاْ إِلَى ٱلسَّمَآءِ فَوۡقَهُمۡ كَيۡفَ بَنَيۡنَٰهَا وَزَيَّنَّـٰهَا وَمَا لَهَا مِن فُرُوجٖ

Je, hawatazami mbingu juu yao, vipi Tumezijenga na Tumezipamba, na wala hazina mipasuko yoyote



Capítulo: QAAF 

Verso : 7

وَٱلۡأَرۡضَ مَدَدۡنَٰهَا وَأَلۡقَيۡنَا فِيهَا رَوَٰسِيَ وَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوۡجِۭ بَهِيجٖ

Na ardhi Tumeitandaza na Tukaiwekea milima thabiti, na Tukaotesha humo kila aina ya mimea ya kupendeza



Capítulo: QAAF 

Verso : 8

تَبۡصِرَةٗ وَذِكۡرَىٰ لِكُلِّ عَبۡدٖ مُّنِيبٖ

Ni ufumbuzi wa macho na ukumbusho kwa kila mja mwenye kuelekea kwa Allah



Capítulo: QAAF 

Verso : 9

وَنَزَّلۡنَا مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ مُّبَٰرَكٗا فَأَنۢبَتۡنَا بِهِۦ جَنَّـٰتٖ وَحَبَّ ٱلۡحَصِيدِ

Na Tukateremsha kutoka mbinguni maji yaliyobarikiwa, kisha Tukaotesha kwayo mabustani na nafaka za kuvunwa



Capítulo: QAAF 

Verso : 10

وَٱلنَّخۡلَ بَاسِقَٰتٖ لَّهَا طَلۡعٞ نَّضِيدٞ

Na mitende mirefu yenye mashada (makole) ya matunda yenye kuzaa kwa wingi



Capítulo: QAAF 

Verso : 11

رِّزۡقٗا لِّلۡعِبَادِۖ وَأَحۡيَيۡنَا بِهِۦ بَلۡدَةٗ مَّيۡتٗاۚ كَذَٰلِكَ ٱلۡخُرُوجُ

Ili iwe ni riziki kwa waja wangu. Na Tukahuisha kwayo nchi iliyokufa, kama hivyo ndivyo utakavyokuwa ufufuaji



Capítulo: QAAF 

Verso : 12

كَذَّبَتۡ قَبۡلَهُمۡ قَوۡمُ نُوحٖ وَأَصۡحَٰبُ ٱلرَّسِّ وَثَمُودُ

Walikadhibisha kabla yao watu wa Nuhu na wakazi wa Ar-Rass na kina Thamud



Capítulo: QAAF 

Verso : 13

وَعَادٞ وَفِرۡعَوۡنُ وَإِخۡوَٰنُ لُوطٖ

Na kina Aad na Firaun na ndugu wa Lutwi



Capítulo: QAAF 

Verso : 14

وَأَصۡحَٰبُ ٱلۡأَيۡكَةِ وَقَوۡمُ تُبَّعٖۚ كُلّٞ كَذَّبَ ٱلرُّسُلَ فَحَقَّ وَعِيدِ

Na wakaazi wa Machakani na watu wa Tubbaa, wote walikadhibisha Mitume. Basi onyo likathibitika juu yao



Capítulo: QAAF 

Verso : 15

أَفَعَيِينَا بِٱلۡخَلۡقِ ٱلۡأَوَّلِۚ بَلۡ هُمۡ فِي لَبۡسٖ مِّنۡ خَلۡقٖ جَدِيدٖ

Je, kwani Tulichoka kwa uumbaji wa kwanza? Bali wao wamo katika shaka juu ya uumbaji upya (kufufuliwa)



Capítulo: QAAF 

Verso : 16

وَلَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ وَنَعۡلَمُ مَا تُوَسۡوِسُ بِهِۦ نَفۡسُهُۥۖ وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنۡ حَبۡلِ ٱلۡوَرِيدِ

Na kwa yakini Tumemuumba Mtu na Tunajua yale inayowaza nafsi yake, na Sisi Tuko karibu naye kuliko mshipa wa shingoni mwake



Capítulo: QAAF 

Verso : 17

إِذۡ يَتَلَقَّى ٱلۡمُتَلَقِّيَانِ عَنِ ٱلۡيَمِينِ وَعَنِ ٱلشِّمَالِ قَعِيدٞ

Pale wanapopokea wapokeaji wawili (Malaika) wanaokaa kuliani na kushotoni



Capítulo: QAAF 

Verso : 18

مَّا يَلۡفِظُ مِن قَوۡلٍ إِلَّا لَدَيۡهِ رَقِيبٌ عَتِيدٞ

Hatamki kauli yoyote isipokuwa anaye mchungaji aliyejitayarisha (kurekodi)



Capítulo: QAAF 

Verso : 19

وَجَآءَتۡ سَكۡرَةُ ٱلۡمَوۡتِ بِٱلۡحَقِّۖ ذَٰلِكَ مَا كُنتَ مِنۡهُ تَحِيدُ

Na uchungu wa mauti (wa kutoka roho) utakapomjia kwa haki. (Itasemwa): Hayo ndiyo yale uliyokuwa ukiyakimbia



Capítulo: QAAF 

Verso : 20

وَنُفِخَ فِي ٱلصُّورِۚ ذَٰلِكَ يَوۡمُ ٱلۡوَعِيدِ

Na litapulizwa baragumu. Hiyo ndio Siku ya miadi. (makamiano)



Capítulo: QAAF 

Verso : 21

وَجَآءَتۡ كُلُّ نَفۡسٖ مَّعَهَا سَآئِقٞ وَشَهِيدٞ

Na kila nafsi itakuja pamoja nayo mcungaji na shahidi



Capítulo: QAAF 

Verso : 22

لَّقَدۡ كُنتَ فِي غَفۡلَةٖ مِّنۡ هَٰذَا فَكَشَفۡنَا عَنكَ غِطَآءَكَ فَبَصَرُكَ ٱلۡيَوۡمَ حَدِيدٞ

(Aambiwe): Kwa yakini ulikuwa umeghafilika na haya! Basi Tumekuondoshea kifuniko chako (pazia lako), basi kuona kwako leo ni kukali



Capítulo: QAAF 

Verso : 23

وَقَالَ قَرِينُهُۥ هَٰذَا مَا لَدَيَّ عَتِيدٌ

Na Malaika wake aliyepewa jukumu atasema: Hii (rekodi) iliyoko kwangu imeshatayarishwa



Capítulo: QAAF 

Verso : 24

أَلۡقِيَا فِي جَهَنَّمَ كُلَّ كَفَّارٍ عَنِيدٖ

(Allaah Atasema): Mtupeni katika Jahannam kila kafiri, mkaidi!



Capítulo: QAAF 

Verso : 25

مَّنَّاعٖ لِّلۡخَيۡرِ مُعۡتَدٖ مُّرِيبٍ

Mzuiaji wa kheri, mwenye kuruka mipaka, mwenye kutia shaka



Capítulo: QAAF 

Verso : 26

ٱلَّذِي جَعَلَ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ فَأَلۡقِيَاهُ فِي ٱلۡعَذَابِ ٱلشَّدِيدِ

Ambaye amefanya mwabudiwa mwengine pamoja na Allah, basi mtupeni katika adhabu kali



Capítulo: QAAF 

Verso : 27

۞قَالَ قَرِينُهُۥ رَبَّنَا مَآ أَطۡغَيۡتُهُۥ وَلَٰكِن كَانَ فِي ضَلَٰلِۭ بَعِيدٖ

Shatani mwenzake atasema: Ee Mola wetu mlezi! Sikumpoteza mimi, bali yeye mwenyewe alikuwa katika upotofu wa mbali. (na haki)



Capítulo: QAAF 

Verso : 28

قَالَ لَا تَخۡتَصِمُواْ لَدَيَّ وَقَدۡ قَدَّمۡتُ إِلَيۡكُم بِٱلۡوَعِيدِ

(Allah) Atasema: Msigombane mbele yangu, na hali Nilikuleteeni onyo Langu!



Capítulo: QAAF 

Verso : 29

مَا يُبَدَّلُ ٱلۡقَوۡلُ لَدَيَّ وَمَآ أَنَا۠ بِظَلَّـٰمٖ لِّلۡعَبِيدِ

Haibadilishwi kauli Kwangu, Nami si mwenye kudhulumu waja wangu



Capítulo: QAAF 

Verso : 30

يَوۡمَ نَقُولُ لِجَهَنَّمَ هَلِ ٱمۡتَلَأۡتِ وَتَقُولُ هَلۡ مِن مَّزِيدٖ

Siku Tutakapoiambia Jahannam: Je, umeshajaa? Nayo itasema: Je, kuna ziada yoyote?