Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 211

سَلۡ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ كَمۡ ءَاتَيۡنَٰهُم مِّنۡ ءَايَةِۭ بَيِّنَةٖۗ وَمَن يُبَدِّلۡ نِعۡمَةَ ٱللَّهِ مِنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَتۡهُ فَإِنَّ ٱللَّهَ شَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ

Waulize Wana wa Israili: Ni Aya ngapi zilizo wazi tumewapa? Na yeyote atakayebadili neema za Allah baada ya kumfikia, kwa hakika Allah ni Mkali wa kuadhibu



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 212

زُيِّنَ لِلَّذِينَ كَفَرُواْ ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَا وَيَسۡخَرُونَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْۘ وَٱلَّذِينَ ٱتَّقَوۡاْ فَوۡقَهُمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۗ وَٱللَّهُ يَرۡزُقُ مَن يَشَآءُ بِغَيۡرِ حِسَابٖ

Makafiri wamepambiwa maisha ya dunia, na wanawadharau walioamini. Na Wacha Mungu watakuwa juu yao Siku ya Kiama. Na Allah anamruzuku amtakaye bila ya hesabu



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 213

كَانَ ٱلنَّاسُ أُمَّةٗ وَٰحِدَةٗ فَبَعَثَ ٱللَّهُ ٱلنَّبِيِّـۧنَ مُبَشِّرِينَ وَمُنذِرِينَ وَأَنزَلَ مَعَهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ بِٱلۡحَقِّ لِيَحۡكُمَ بَيۡنَ ٱلنَّاسِ فِيمَا ٱخۡتَلَفُواْ فِيهِۚ وَمَا ٱخۡتَلَفَ فِيهِ إِلَّا ٱلَّذِينَ أُوتُوهُ مِنۢ بَعۡدِ مَا جَآءَتۡهُمُ ٱلۡبَيِّنَٰتُ بَغۡيَۢا بَيۡنَهُمۡۖ فَهَدَى ٱللَّهُ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لِمَا ٱخۡتَلَفُواْ فِيهِ مِنَ ٱلۡحَقِّ بِإِذۡنِهِۦۗ وَٱللَّهُ يَهۡدِي مَن يَشَآءُ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٍ

Watu walikuwa umma mmoja. Allah akatuma Mitume wakitoa habari njema na wakitoa maonyo na aliteremsha vitabu pamoja nao kwa haki ili ahukumu kati ya watu katika yale ambayo wametofatiana. Na hawakutofautiana katika hayo isipokuwa wale tu waliopewa vitabu hivyo, baada ya kuwafikia hoja za waziwazi kwa sababu tu ya uovu walionao. Basi Allah akawaongoza wale ambao wameamini kwenye haki kwa idhini yake na Allah anamuongoza amtakaye kwenye njia iliyo nyooka



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 214

أَمۡ حَسِبۡتُمۡ أَن تَدۡخُلُواْ ٱلۡجَنَّةَ وَلَمَّا يَأۡتِكُم مَّثَلُ ٱلَّذِينَ خَلَوۡاْ مِن قَبۡلِكُمۖ مَّسَّتۡهُمُ ٱلۡبَأۡسَآءُ وَٱلضَّرَّآءُ وَزُلۡزِلُواْ حَتَّىٰ يَقُولَ ٱلرَّسُولُ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مَعَهُۥ مَتَىٰ نَصۡرُ ٱللَّهِۗ أَلَآ إِنَّ نَصۡرَ ٱللَّهِ قَرِيبٞ

Je, mmedhani kuwa mtaingia peponi ilhali haujakufikeni mfano wa ambao wamepita kabla yenu? Yaliwapata misukosuko na madhara na walitetemeshwa hadi akasema Mtume na walioamini pamoja naye kwamba: Ni lini itafika nusura ya Allah? Eleweni kwamba, hakika nusura ya Allah iko karibu mno



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 215

يَسۡـَٔلُونَكَ مَاذَا يُنفِقُونَۖ قُلۡ مَآ أَنفَقۡتُم مِّنۡ خَيۡرٖ فَلِلۡوَٰلِدَيۡنِ وَٱلۡأَقۡرَبِينَ وَٱلۡيَتَٰمَىٰ وَٱلۡمَسَٰكِينِ وَٱبۡنِ ٱلسَّبِيلِۗ وَمَا تَفۡعَلُواْ مِنۡ خَيۡرٖ فَإِنَّ ٱللَّهَ بِهِۦ عَلِيمٞ

Wanakuuliza: Watoe nini? Sema: Chochote cha heri mtakachotoa basi wapeni wazazi na ndugu na Mayatima na masikini na Msafiri na heri yoyote muifanyayo kwa hakika Allah anaijua mno



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 216

كُتِبَ عَلَيۡكُمُ ٱلۡقِتَالُ وَهُوَ كُرۡهٞ لَّكُمۡۖ وَعَسَىٰٓ أَن تَكۡرَهُواْ شَيۡـٔٗا وَهُوَ خَيۡرٞ لَّكُمۡۖ وَعَسَىٰٓ أَن تُحِبُّواْ شَيۡـٔٗا وَهُوَ شَرّٞ لَّكُمۡۚ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ وَأَنتُمۡ لَا تَعۡلَمُونَ

Imefaradhishiwa kwenu kupigana vita na ilihali ni jambo msilolipenda. Na huenda mkachukia kitu na ilhali ni heri kwenu. Na huenda mkapenda kitu na ilhali ni shari kwenu. Na Allah anajua na ilhali nyinyi hamjui



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 217

يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلشَّهۡرِ ٱلۡحَرَامِ قِتَالٖ فِيهِۖ قُلۡ قِتَالٞ فِيهِ كَبِيرٞۚ وَصَدٌّ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِ وَكُفۡرُۢ بِهِۦ وَٱلۡمَسۡجِدِ ٱلۡحَرَامِ وَإِخۡرَاجُ أَهۡلِهِۦ مِنۡهُ أَكۡبَرُ عِندَ ٱللَّهِۚ وَٱلۡفِتۡنَةُ أَكۡبَرُ مِنَ ٱلۡقَتۡلِۗ وَلَا يَزَالُونَ يُقَٰتِلُونَكُمۡ حَتَّىٰ يَرُدُّوكُمۡ عَن دِينِكُمۡ إِنِ ٱسۡتَطَٰعُواْۚ وَمَن يَرۡتَدِدۡ مِنكُمۡ عَن دِينِهِۦ فَيَمُتۡ وَهُوَ كَافِرٞ فَأُوْلَـٰٓئِكَ حَبِطَتۡ أَعۡمَٰلُهُمۡ فِي ٱلدُّنۡيَا وَٱلۡأٓخِرَةِۖ وَأُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ

Wanakuuliza kuhusu kupigana ndani ya mwezi mtukufu. Sema: Kupigana vita humo ni dhambi kubwa. Na kuzuia (watu) katika njia ya Allah na kumkufuru Allah na kuzuia (watu kutumia) Msikiti Mtukufu na kuwatoa humo watu wake ni dhambi kubwa zaidi mbele ya Allah na fitina ni dhambi kubwa mno kuliko kuua. Na hawataacha kukupigeni mpaka wakurudisheni muiache dini yenu kama wataweza. Na yeyote atakaye rudi nyuma akaiacha dini yake miongoni mwenu na akafa hali akiwa kafiri, basi hao amali zao zitakuwa zimebatilika duniani na akhera, na hao ndio watu wa Motoni; watakaa humo milele



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 218

إِنَّ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَٱلَّذِينَ هَاجَرُواْ وَجَٰهَدُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ أُوْلَـٰٓئِكَ يَرۡجُونَ رَحۡمَتَ ٱللَّهِۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Kwa hakika, walioamini na waliohama na wakapigana katika njia ya Allah hao wanataraji rehema za Allah, na Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa kurehemu



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 219

۞يَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلۡخَمۡرِ وَٱلۡمَيۡسِرِۖ قُلۡ فِيهِمَآ إِثۡمٞ كَبِيرٞ وَمَنَٰفِعُ لِلنَّاسِ وَإِثۡمُهُمَآ أَكۡبَرُ مِن نَّفۡعِهِمَاۗ وَيَسۡـَٔلُونَكَ مَاذَا يُنفِقُونَۖ قُلِ ٱلۡعَفۡوَۗ كَذَٰلِكَ يُبَيِّنُ ٱللَّهُ لَكُمُ ٱلۡأٓيَٰتِ لَعَلَّكُمۡ تَتَفَكَّرُونَ

Wanakuuliza kuhusu pombe na kamari. Sema: Katika viwili hivyo kuna dhambi kubwa mno na manufaa kwa watu. Na dhambi za viwili hivyo ni kubwa zaidi kuliko manufaa yake. Na wanakuuliza: Watoe nini? Sema: (Toeni) Kilichozidi mahitaji. Kama hivi Allah anakubainishieni Aya zake ili mpate kutafakari



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 220

فِي ٱلدُّنۡيَا وَٱلۡأٓخِرَةِۗ وَيَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلۡيَتَٰمَىٰۖ قُلۡ إِصۡلَاحٞ لَّهُمۡ خَيۡرٞۖ وَإِن تُخَالِطُوهُمۡ فَإِخۡوَٰنُكُمۡۚ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ ٱلۡمُفۡسِدَ مِنَ ٱلۡمُصۡلِحِۚ وَلَوۡ شَآءَ ٱللَّهُ لَأَعۡنَتَكُمۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَزِيزٌ حَكِيمٞ

(Ili mtafakari) duniani na akhera. Na wanakuuliza kuhusu Mayatima. Sema: Kuwatengenezea vizuri mambo yao ni jambo la heri, na mkijichanganya nao basi hao ni ndugu zenu. Na Allah anamjua mharibifu na mtengenezaji. Na Allah lau angetaka (kukupatisheni tabu) angekupatisheni tabu. Kwa hakika Allah ni Mwenye nguvu, Mwenye hekima mno



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 221

وَلَا تَنكِحُواْ ٱلۡمُشۡرِكَٰتِ حَتَّىٰ يُؤۡمِنَّۚ وَلَأَمَةٞ مُّؤۡمِنَةٌ خَيۡرٞ مِّن مُّشۡرِكَةٖ وَلَوۡ أَعۡجَبَتۡكُمۡۗ وَلَا تُنكِحُواْ ٱلۡمُشۡرِكِينَ حَتَّىٰ يُؤۡمِنُواْۚ وَلَعَبۡدٞ مُّؤۡمِنٌ خَيۡرٞ مِّن مُّشۡرِكٖ وَلَوۡ أَعۡجَبَكُمۡۗ أُوْلَـٰٓئِكَ يَدۡعُونَ إِلَى ٱلنَّارِۖ وَٱللَّهُ يَدۡعُوٓاْ إِلَى ٱلۡجَنَّةِ وَٱلۡمَغۡفِرَةِ بِإِذۡنِهِۦۖ وَيُبَيِّنُ ءَايَٰتِهِۦ لِلنَّاسِ لَعَلَّهُمۡ يَتَذَكَّرُونَ

Na msiwaoe wanawake washi-rikina mpaka waamini. Na kwa hakika kabisa, kijakazi Muumini ni bora kuliko mshirikina, hata kama atakupendezeni. Na msiwaozeshe wanaume washirikina (makafiri) mpaka waamini. Na kwa hakika kabisa, mtumwa Muumini ni bora kuliko mshirikina hata kama atakupendezeni. Hao (Washirikina) wanahubiri kwenda motoni, na Allah anahubiri kwenda peponi na kwenye msamaha kwa idhini yake, na anazibainisha Aya zake kwa watu ili wapate kukumbuka



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 222

وَيَسۡـَٔلُونَكَ عَنِ ٱلۡمَحِيضِۖ قُلۡ هُوَ أَذٗى فَٱعۡتَزِلُواْ ٱلنِّسَآءَ فِي ٱلۡمَحِيضِ وَلَا تَقۡرَبُوهُنَّ حَتَّىٰ يَطۡهُرۡنَۖ فَإِذَا تَطَهَّرۡنَ فَأۡتُوهُنَّ مِنۡ حَيۡثُ أَمَرَكُمُ ٱللَّهُۚ إِنَّ ٱللَّهَ يُحِبُّ ٱلتَّوَّـٰبِينَ وَيُحِبُّ ٱلۡمُتَطَهِّرِينَ

Na wanakuuliza kuhusu Hedhi. Sema: Huo ni uchafu. Basi waepukeni wanawake (wake zenu) katika kipindi cha Hedhi, na msiwasogelee (msifanye nao jimai) mpaka watoharike. Na watakapojitoharisha, basi waendeeni kwa kupitia alipokuamrisheni Allah. Hakika, Allah anawapenda wenye kujitoharisha na anawapenda wenye kutubu sana



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 223

نِسَآؤُكُمۡ حَرۡثٞ لَّكُمۡ فَأۡتُواْ حَرۡثَكُمۡ أَنَّىٰ شِئۡتُمۡۖ وَقَدِّمُواْ لِأَنفُسِكُمۡۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّكُم مُّلَٰقُوهُۗ وَبَشِّرِ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Wake zenu ni mashamba yenu. Basi yaendeeni mashamba yenu namna mtakavyo. Na jifanyieni utangulizi. Na muogopeni Allah na jueni kuwa mtakutana naye. Na wape bishara wenye kuamini



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 224

وَلَا تَجۡعَلُواْ ٱللَّهَ عُرۡضَةٗ لِّأَيۡمَٰنِكُمۡ أَن تَبَرُّواْ وَتَتَّقُواْ وَتُصۡلِحُواْ بَيۡنَ ٱلنَّاسِۚ وَٱللَّهُ سَمِيعٌ عَلِيمٞ

Msimfanye Allah kinga ya viapo vyenu mkaacha kufanya wema na kumcha (Allah) na kufanya suluhu kati ya watu. Na Allah ni Mwingi wa kusikia, Mjuzi mno



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 225

لَّا يُؤَاخِذُكُمُ ٱللَّهُ بِٱللَّغۡوِ فِيٓ أَيۡمَٰنِكُمۡ وَلَٰكِن يُؤَاخِذُكُم بِمَا كَسَبَتۡ قُلُوبُكُمۡۗ وَٱللَّهُ غَفُورٌ حَلِيمٞ

Allah hatakuchukulieni hatua kwa viapo vyenu vya kipuuzi. Lakini atakuchukulieni hatua kwa yale yaliyo nuiwa na nyoyo zenu. Na Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mpole mno



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 226

لِّلَّذِينَ يُؤۡلُونَ مِن نِّسَآئِهِمۡ تَرَبُّصُ أَرۡبَعَةِ أَشۡهُرٖۖ فَإِن فَآءُو فَإِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Kwa wanaoapa kujitenga na wake zao, basi wangoje miezi minne. Na endapo watarejea (kwa kutengua viapo vyao) basi kwa hakika Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa kurehemu



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 227

وَإِنۡ عَزَمُواْ ٱلطَّلَٰقَ فَإِنَّ ٱللَّهَ سَمِيعٌ عَلِيمٞ

Na kama wakiazimia kutoa Talaka, basi Allah ni Mwingi wa kusikia, Mjuzi mno



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 228

وَٱلۡمُطَلَّقَٰتُ يَتَرَبَّصۡنَ بِأَنفُسِهِنَّ ثَلَٰثَةَ قُرُوٓءٖۚ وَلَا يَحِلُّ لَهُنَّ أَن يَكۡتُمۡنَ مَا خَلَقَ ٱللَّهُ فِيٓ أَرۡحَامِهِنَّ إِن كُنَّ يُؤۡمِنَّ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِۚ وَبُعُولَتُهُنَّ أَحَقُّ بِرَدِّهِنَّ فِي ذَٰلِكَ إِنۡ أَرَادُوٓاْ إِصۡلَٰحٗاۚ وَلَهُنَّ مِثۡلُ ٱلَّذِي عَلَيۡهِنَّ بِٱلۡمَعۡرُوفِۚ وَلِلرِّجَالِ عَلَيۡهِنَّ دَرَجَةٞۗ وَٱللَّهُ عَزِيزٌ حَكِيمٌ

Na wanawake walioachwa wangoje Kurui tatu. Na haifai kwao kuficha alichoumba Allah kwenye mifuko yao ya uzazi ikiwa kweli wanamuamini Allah na Siku ya Mwisho. Na Waume wao wana haki zaidi ya kuwarejea katika muda huo kama wanakusudia suluhu. Na wanawake wanazo haki kwa waume wao kama walivyo na wajibu juu yao kwa wema. Na wanaume wana daraja zaidi kwa wake zao. Na Allah ni Mwenye nguvu nyingi, Mwenye hekima sana



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 229

ٱلطَّلَٰقُ مَرَّتَانِۖ فَإِمۡسَاكُۢ بِمَعۡرُوفٍ أَوۡ تَسۡرِيحُۢ بِإِحۡسَٰنٖۗ وَلَا يَحِلُّ لَكُمۡ أَن تَأۡخُذُواْ مِمَّآ ءَاتَيۡتُمُوهُنَّ شَيۡـًٔا إِلَّآ أَن يَخَافَآ أَلَّا يُقِيمَا حُدُودَ ٱللَّهِۖ فَإِنۡ خِفۡتُمۡ أَلَّا يُقِيمَا حُدُودَ ٱللَّهِ فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡهِمَا فِيمَا ٱفۡتَدَتۡ بِهِۦۗ تِلۡكَ حُدُودُ ٱللَّهِ فَلَا تَعۡتَدُوهَاۚ وَمَن يَتَعَدَّ حُدُودَ ٱللَّهِ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلظَّـٰلِمُونَ

Talaka ni mara mbili[1]. Basi (baada ya kumrejea) akae naye kwa wema au kumuacha kwa uzuri (aendelee kumaliza Eda yake). Na si halali kwenu kuchukua chochote katika vile mlivyowapa (wake zenu) isipokuwa kama wote wawili wataogopa kukiuka sharia za Allah. Basi kama mtaogopa kuwa hawatatekeleza sharia za Allah, hakuna ubaya kwa wawili (mke kurejesha mahari na mume kupokea) katika kile mwanamke alichojikombolea. Hiyo ni mipaka ya Allah, basi msiikiuke. Na watakaoikiuka mipaka ya Allah basi hao ni madhalimu hasa


1- - Ambazo mume ana haki ya kumrejea mkewe


Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 230

فَإِن طَلَّقَهَا فَلَا تَحِلُّ لَهُۥ مِنۢ بَعۡدُ حَتَّىٰ تَنكِحَ زَوۡجًا غَيۡرَهُۥۗ فَإِن طَلَّقَهَا فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡهِمَآ أَن يَتَرَاجَعَآ إِن ظَنَّآ أَن يُقِيمَا حُدُودَ ٱللَّهِۗ وَتِلۡكَ حُدُودُ ٱللَّهِ يُبَيِّنُهَا لِقَوۡمٖ يَعۡلَمُونَ

Na kama (mume) akimpa (mkewe) Talaka (ya tatu) basi si halali kwake (kumrejea au kumuoa upya) baada ya hapo mpaka afunge ndoa na mume mwingine. Na kama akimuacha (huyo mume wa pili) basi si vibaya kurejeana (kwa kufunga ndoa upya) kama wataona wanaweza kusimamisha mipaka ya Allah. Na hiyo ni mipaka ya Allah anayoibainisha kwa watu wanaojua



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 231

وَإِذَا طَلَّقۡتُمُ ٱلنِّسَآءَ فَبَلَغۡنَ أَجَلَهُنَّ فَأَمۡسِكُوهُنَّ بِمَعۡرُوفٍ أَوۡ سَرِّحُوهُنَّ بِمَعۡرُوفٖۚ وَلَا تُمۡسِكُوهُنَّ ضِرَارٗا لِّتَعۡتَدُواْۚ وَمَن يَفۡعَلۡ ذَٰلِكَ فَقَدۡ ظَلَمَ نَفۡسَهُۥۚ وَلَا تَتَّخِذُوٓاْ ءَايَٰتِ ٱللَّهِ هُزُوٗاۚ وَٱذۡكُرُواْ نِعۡمَتَ ٱللَّهِ عَلَيۡكُمۡ وَمَآ أَنزَلَ عَلَيۡكُم مِّنَ ٱلۡكِتَٰبِ وَٱلۡحِكۡمَةِ يَعِظُكُم بِهِۦۚ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٞ

Na mtakapowaacha wake na wakakaribia kumaliza muda wa Eda zao, basi ishini nao kwa wema (kwa kuwarejea) au muwaachie (wamalize Eda zao na wawe huru) kwa wema. Na msibaki nao kwa lengo la kuwadhuru ili kuwafanyia uonevu. Na yeyote atakaye fanya hivyo basi kwa hakika atakuwa amejidhulumu mwenyewe. Na msizifanyie mzaha Aya za Allah. Na kumbukeni neema za Allah kwenu, na kitabu na hekima alizokuteremshieni. Allah anakuonyeni kwa hayo, na mcheni Allah na jueni kwamba, Allah ni Mjuzi mno wa kila kitu



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 232

وَإِذَا طَلَّقۡتُمُ ٱلنِّسَآءَ فَبَلَغۡنَ أَجَلَهُنَّ فَلَا تَعۡضُلُوهُنَّ أَن يَنكِحۡنَ أَزۡوَٰجَهُنَّ إِذَا تَرَٰضَوۡاْ بَيۡنَهُم بِٱلۡمَعۡرُوفِۗ ذَٰلِكَ يُوعَظُ بِهِۦ مَن كَانَ مِنكُمۡ يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِۗ ذَٰلِكُمۡ أَزۡكَىٰ لَكُمۡ وَأَطۡهَرُۚ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ وَأَنتُمۡ لَا تَعۡلَمُونَ

Na mnapowaacha wake na wakamaliza Eda zao, basi nyinyi mawalii msiwazuie kufunga ndoa na waume zao waliowaacha iwapo wataridhiana kwa wema. Anapewa onyo hilo yule anayemuamini Allah miongoni mwenu na Siku ya Mwisho. Hayo kwenu ni bora mno na nisafi kabisa. Na Allah anajua ilihali nyinyi hamjui



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 233

۞وَٱلۡوَٰلِدَٰتُ يُرۡضِعۡنَ أَوۡلَٰدَهُنَّ حَوۡلَيۡنِ كَامِلَيۡنِۖ لِمَنۡ أَرَادَ أَن يُتِمَّ ٱلرَّضَاعَةَۚ وَعَلَى ٱلۡمَوۡلُودِ لَهُۥ رِزۡقُهُنَّ وَكِسۡوَتُهُنَّ بِٱلۡمَعۡرُوفِۚ لَا تُكَلَّفُ نَفۡسٌ إِلَّا وُسۡعَهَاۚ لَا تُضَآرَّ وَٰلِدَةُۢ بِوَلَدِهَا وَلَا مَوۡلُودٞ لَّهُۥ بِوَلَدِهِۦۚ وَعَلَى ٱلۡوَارِثِ مِثۡلُ ذَٰلِكَۗ فَإِنۡ أَرَادَا فِصَالًا عَن تَرَاضٖ مِّنۡهُمَا وَتَشَاوُرٖ فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡهِمَاۗ وَإِنۡ أَرَدتُّمۡ أَن تَسۡتَرۡضِعُوٓاْ أَوۡلَٰدَكُمۡ فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ إِذَا سَلَّمۡتُم مَّآ ءَاتَيۡتُم بِٱلۡمَعۡرُوفِۗ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرٞ

Na wazazi wanawake wan-yonyeshe watoto wao miaka miwili kamili, kwa anayetaka kutimiza kunyonyesha. Na ni juu ya baba chakula chao (mama na mtoto) na kivazi chao kwa wema. Nafsi haikalifishwi (kufanya jambo) isipokuwa lililo ndani ya uwezo wake tu. Mama asidhuriwe kwa sababu ya mwanawe, na baba asidhuriwe kwa sababu ya mwanawe. Na ni wajibu juu ya mrithi (wa mtoto kufanya hayo). Na si vibaya kwa wawili hao (baba na mama) wakitaka kumwachisha ziwa (mtoto chini ya miaka miwili) kwa kushauriana na kuridhiana. Na mkitaka kuwapatia watoto wenu mama wa kuwanyonyesha, basi hapana ubaya kwenu mkitoa kile mlichowapa kwa njia ya wema. Na mcheni Allah na jueni kwamba Allah ni mwenye kuyaona sana yote myatendayo



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 234

وَٱلَّذِينَ يُتَوَفَّوۡنَ مِنكُمۡ وَيَذَرُونَ أَزۡوَٰجٗا يَتَرَبَّصۡنَ بِأَنفُسِهِنَّ أَرۡبَعَةَ أَشۡهُرٖ وَعَشۡرٗاۖ فَإِذَا بَلَغۡنَ أَجَلَهُنَّ فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ فِيمَا فَعَلۡنَ فِيٓ أَنفُسِهِنَّ بِٱلۡمَعۡرُوفِۗ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٞ

Na wanaokufa miongoni mwenu na kuacha wake, wangoje wao wenyewe miezi minne na siku kumi. Na watakapotimiza Eda zao, basi hapana ubaya kwenu katika waliyojifanyia kwa wema. Na Allah anayajua vilivyo myafanyayo



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 235

وَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ فِيمَا عَرَّضۡتُم بِهِۦ مِنۡ خِطۡبَةِ ٱلنِّسَآءِ أَوۡ أَكۡنَنتُمۡ فِيٓ أَنفُسِكُمۡۚ عَلِمَ ٱللَّهُ أَنَّكُمۡ سَتَذۡكُرُونَهُنَّ وَلَٰكِن لَّا تُوَاعِدُوهُنَّ سِرًّا إِلَّآ أَن تَقُولُواْ قَوۡلٗا مَّعۡرُوفٗاۚ وَلَا تَعۡزِمُواْ عُقۡدَةَ ٱلنِّكَاحِ حَتَّىٰ يَبۡلُغَ ٱلۡكِتَٰبُ أَجَلَهُۥۚ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ مَا فِيٓ أَنفُسِكُمۡ فَٱحۡذَرُوهُۚ وَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ غَفُورٌ حَلِيمٞ

Na si vibaya kwenu posa za fumbo mlizowafumbia au mlicho-kificha kwenye nafsi zenu. Allah amejua kuwa nyinyi mtawakumbuka hao, Na lakini msiwaahidi (ndoa) kwa siri isipokuwa mseme maneno mema. Na msiazimie kufunga nao ndoa mpaka Eda ifike mwisho wake. Na jueni kwamba Allah anajua yaliyomo katika nafsi zenu, basi jihadharini naye, najueni kwamba Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mpole mno



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 236

لَّا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ إِن طَلَّقۡتُمُ ٱلنِّسَآءَ مَا لَمۡ تَمَسُّوهُنَّ أَوۡ تَفۡرِضُواْ لَهُنَّ فَرِيضَةٗۚ وَمَتِّعُوهُنَّ عَلَى ٱلۡمُوسِعِ قَدَرُهُۥ وَعَلَى ٱلۡمُقۡتِرِ قَدَرُهُۥ مَتَٰعَۢا بِٱلۡمَعۡرُوفِۖ حَقًّا عَلَى ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Hakuna ubaya kwenu endapo mtawaacha wake kabla ya kuwaingilia na kuwakadiria mahari yao. Na wapeni cha kuwaliwaza (kitoka nyumba). Mwenye uwezo mkubwa atoe kulingana na uwezo wake, na mwenye uwezo mdogo atoe kulingana na uwezo alionao. Niliwazo litolewalo kwa wema na ni haki kwa watendao mazuri



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 237

وَإِن طَلَّقۡتُمُوهُنَّ مِن قَبۡلِ أَن تَمَسُّوهُنَّ وَقَدۡ فَرَضۡتُمۡ لَهُنَّ فَرِيضَةٗ فَنِصۡفُ مَا فَرَضۡتُمۡ إِلَّآ أَن يَعۡفُونَ أَوۡ يَعۡفُوَاْ ٱلَّذِي بِيَدِهِۦ عُقۡدَةُ ٱلنِّكَاحِۚ وَأَن تَعۡفُوٓاْ أَقۡرَبُ لِلتَّقۡوَىٰۚ وَلَا تَنسَوُاْ ٱلۡفَضۡلَ بَيۡنَكُمۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرٌ

Na endapo mtawaacha kabla ya kuwaingilia na ilhali mmekwisha kadiria mahari, basi wapeni nusu ya mahari mliokadiria, isipokuwa kama wake wenyewe watasamehe au atasamehe yule ambaye kifungo cha ndoa kipo mikononi mwake. Na kama mtasamehe, hilo liko karibu zaidi na Ucha Mungu. Na msisahau utu kati yenu. Hakika, Allah ni Mwenye kuyaona myatendayo



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 238

حَٰفِظُواْ عَلَى ٱلصَّلَوَٰتِ وَٱلصَّلَوٰةِ ٱلۡوُسۡطَىٰ وَقُومُواْ لِلَّهِ قَٰنِتِينَ

Zichungeni swala zote (tano) na (ichungeni) swala ya kati. Na simameni kwa ajili ya Allah mkiwa wanyenyekevu



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 239

فَإِنۡ خِفۡتُمۡ فَرِجَالًا أَوۡ رُكۡبَانٗاۖ فَإِذَآ أَمِنتُمۡ فَٱذۡكُرُواْ ٱللَّهَ كَمَا عَلَّمَكُم مَّا لَمۡ تَكُونُواْ تَعۡلَمُونَ

Basi mkiwa na hofu (swalini) mkiwa mnatembea kwa miguu au mmepanda. Na mtakapokuwa katika amani basi mtajeni Allah kama alivyokufundisheni mliyokuwa hamyajui



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 240

وَٱلَّذِينَ يُتَوَفَّوۡنَ مِنكُمۡ وَيَذَرُونَ أَزۡوَٰجٗا وَصِيَّةٗ لِّأَزۡوَٰجِهِم مَّتَٰعًا إِلَى ٱلۡحَوۡلِ غَيۡرَ إِخۡرَاجٖۚ فَإِنۡ خَرَجۡنَ فَلَا جُنَاحَ عَلَيۡكُمۡ فِي مَا فَعَلۡنَ فِيٓ أَنفُسِهِنَّ مِن مَّعۡرُوفٖۗ وَٱللَّهُ عَزِيزٌ حَكِيمٞ

Na wale wanaokufa miongoni mwenu na wakaacha wake, waache Usia kwa ajili ya wake zao wapatiwe matunzo kwa mwaka mzima bila ya kuwatoa (majumbani). Na kama watatoka wenyewe, basi hakuna ubaya kwenu kwa kile walichokifanya kwenye nafsi zao. Na Allah ni Mwenye nguvu mno, Mwingi mno wa hekima