Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 91

إِنَّمَا يُرِيدُ ٱلشَّيۡطَٰنُ أَن يُوقِعَ بَيۡنَكُمُ ٱلۡعَدَٰوَةَ وَٱلۡبَغۡضَآءَ فِي ٱلۡخَمۡرِ وَٱلۡمَيۡسِرِ وَيَصُدَّكُمۡ عَن ذِكۡرِ ٱللَّهِ وَعَنِ ٱلصَّلَوٰةِۖ فَهَلۡ أَنتُم مُّنتَهُونَ

Ilivyo ni kwamba, Shetani anataka kuweka uadui na chuki baina yenu kwasababu ya ulevi na kamari, na kukuzuieni kumkumbuka Allah na kuswali. Basi je, mmeacha?



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 92

وَأَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُواْ ٱلرَّسُولَ وَٱحۡذَرُواْۚ فَإِن تَوَلَّيۡتُمۡ فَٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّمَا عَلَىٰ رَسُولِنَا ٱلۡبَلَٰغُ ٱلۡمُبِينُ

Na mtiini Allah na mtiini Mtume, na jihadharini (na dhambi). Na mkikengeuka basi jueni ya kuwa jukumu la Mtume wetu ni kufikisha ujumbe wenye kufafanua



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 93

لَيۡسَ عَلَى ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ جُنَاحٞ فِيمَا طَعِمُوٓاْ إِذَا مَا ٱتَّقَواْ وَّءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ ثُمَّ ٱتَّقَواْ وَّءَامَنُواْ ثُمَّ ٱتَّقَواْ وَّأَحۡسَنُواْۚ وَٱللَّهُ يُحِبُّ ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Hakuna dhambi kwa walioamini na wakatenda mema katika walivyovila madamu wakimcha Allah na wakaamini na wakatenda mema, kisha wakamcha Allah na wakaamini kisha wakamcha Allah na wakafanya mazuri. Na Allah anawapenda wafanyao mazuri



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 94

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَيَبۡلُوَنَّكُمُ ٱللَّهُ بِشَيۡءٖ مِّنَ ٱلصَّيۡدِ تَنَالُهُۥٓ أَيۡدِيكُمۡ وَرِمَاحُكُمۡ لِيَعۡلَمَ ٱللَّهُ مَن يَخَافُهُۥ بِٱلۡغَيۡبِۚ فَمَنِ ٱعۡتَدَىٰ بَعۡدَ ذَٰلِكَ فَلَهُۥ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Enyi mlioamini, Allah atawa-jaribuni kwa baadhi ya wanyamapori wafikiwao na mikono yenu na mikuki yenu, ili Allah amjue nani anayemuhofu kwa ghaibu. Basi atakayechupa mipaka baada ya hayo atapata adhabu iumizayo mno



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 95

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَقۡتُلُواْ ٱلصَّيۡدَ وَأَنتُمۡ حُرُمٞۚ وَمَن قَتَلَهُۥ مِنكُم مُّتَعَمِّدٗا فَجَزَآءٞ مِّثۡلُ مَا قَتَلَ مِنَ ٱلنَّعَمِ يَحۡكُمُ بِهِۦ ذَوَا عَدۡلٖ مِّنكُمۡ هَدۡيَۢا بَٰلِغَ ٱلۡكَعۡبَةِ أَوۡ كَفَّـٰرَةٞ طَعَامُ مَسَٰكِينَ أَوۡ عَدۡلُ ذَٰلِكَ صِيَامٗا لِّيَذُوقَ وَبَالَ أَمۡرِهِۦۗ عَفَا ٱللَّهُ عَمَّا سَلَفَۚ وَمَنۡ عَادَ فَيَنتَقِمُ ٱللَّهُ مِنۡهُۚ وَٱللَّهُ عَزِيزٞ ذُو ٱنتِقَامٍ

Enyi mlioamini, msiue wanya-mapori na hali mmeharimia (mmo ndani ya ibada ya Hija au Umra). Na yeyote miongoni mwenu atakayemuua mnyama huyo kwa makusudi, basi malipo (yake) ni (kuchinja) mnyama wa kufuga mfano wa aliyemuua. Watahukumu hayo waadilifu wawili miongoni mwenu. Mnyama (huyo) apelekwe Al-Kaaba (Makkah ili achinjwe huko na nyama yake kugaiwa sadaka kwa maskini wa huko) au kutoa kafara kwa kuwalisha masikini au badala ya hayo ni kufunga ili (aliyefanya kosa hilo la kuwinda) aonje ubaya wa jambo lake (baya alilolifanya). Allah amekwishafuta yaliyopita (lakini) atakayerudia (kufanya tena kosa hilo) Allah atamuadhibu. Na Allah ni Mwenye nguvu sana, Mwenye kutesa



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 96

أُحِلَّ لَكُمۡ صَيۡدُ ٱلۡبَحۡرِ وَطَعَامُهُۥ مَتَٰعٗا لَّكُمۡ وَلِلسَّيَّارَةِۖ وَحُرِّمَ عَلَيۡكُمۡ صَيۡدُ ٱلۡبَرِّ مَا دُمۡتُمۡ حُرُمٗاۗ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ ٱلَّذِيٓ إِلَيۡهِ تُحۡشَرُونَ

Mmehalalishiwa viwindwa vya baharini (uvuvi) na kuvila kwa faida yenu na kwa wasafiri. Na mmeharamishiwa viwindwa vya bara (nchi kavu) madhali mmehirimia (mmo ndani ya ibada ya Hija au Umra). Na mcheni Allah ambaye kwake mtakusanywa



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 97

۞جَعَلَ ٱللَّهُ ٱلۡكَعۡبَةَ ٱلۡبَيۡتَ ٱلۡحَرَامَ قِيَٰمٗا لِّلنَّاسِ وَٱلشَّهۡرَ ٱلۡحَرَامَ وَٱلۡهَدۡيَ وَٱلۡقَلَـٰٓئِدَۚ ذَٰلِكَ لِتَعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِ وَأَنَّ ٱللَّهَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٌ

Allah ameifanya Al-Kaaba, Nyumba Tukufu kuwa tegemeo la watu, na kadhalika (ameifanya) Miezi Mitukufu (tegemeo kwa kusitishwa vita) na wanyama wa hadiyi (dhabihu) waliovikwa koja. (Allah amefanya) Hayo ili mjue kwamba Allah anayajua yaliyomo mbinguni na yaliyomo ardhini, na kwamba Allah ni Mjuzi wa kila kitu



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 98

ٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ شَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ وَأَنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Jueni kwamba, Allah ni Mkali wa kuadhibu, na kwamba Allah ni Mwingi wa kusamehe, mwenye kurehemu



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 99

مَّا عَلَى ٱلرَّسُولِ إِلَّا ٱلۡبَلَٰغُۗ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ مَا تُبۡدُونَ وَمَا تَكۡتُمُونَ

Si juu ya Mtume isipokuwa kufikisha ujumbe tu. Na Allah anajua mnayoyadhihirisha na mnayoyaficha



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 100

قُل لَّا يَسۡتَوِي ٱلۡخَبِيثُ وَٱلطَّيِّبُ وَلَوۡ أَعۡجَبَكَ كَثۡرَةُ ٱلۡخَبِيثِۚ فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ يَـٰٓأُوْلِي ٱلۡأَلۡبَٰبِ لَعَلَّكُمۡ تُفۡلِحُونَ

Sema: Haliwi sawa baya na jema na hata kama wingi wa baya utakuvutia. Basi mcheni Allah, enyi wenye akili, ili mpate kufanikiwa



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 101

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَسۡـَٔلُواْ عَنۡ أَشۡيَآءَ إِن تُبۡدَ لَكُمۡ تَسُؤۡكُمۡ وَإِن تَسۡـَٔلُواْ عَنۡهَا حِينَ يُنَزَّلُ ٱلۡقُرۡءَانُ تُبۡدَ لَكُمۡ عَفَا ٱللَّهُ عَنۡهَاۗ وَٱللَّهُ غَفُورٌ حَلِيمٞ

Enyi mlioamini, msiulize mambo (ambayo) mkidhihirishiwa yanakuchukizeni. Na mkiyauliza wakati Qur’ani inateremshwa mtadhihirishiwa. (Msirudie) Allah ameshayasamehe hayo (mliyokwishauliza). Na Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mpole mno



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 102

قَدۡ سَأَلَهَا قَوۡمٞ مِّن قَبۡلِكُمۡ ثُمَّ أَصۡبَحُواْ بِهَا كَٰفِرِينَ

Hakika, waliyauliza hayo watu (waliokuwepo) kabla yenu, kisha wakawa ni wenye kuyapinga



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 103

مَا جَعَلَ ٱللَّهُ مِنۢ بَحِيرَةٖ وَلَا سَآئِبَةٖ وَلَا وَصِيلَةٖ وَلَا حَامٖ وَلَٰكِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ يَفۡتَرُونَ عَلَى ٱللَّهِ ٱلۡكَذِبَۖ وَأَكۡثَرُهُمۡ لَا يَعۡقِلُونَ

Allah hakuweka uharamu (wowote) katika Bahira[1] wala Saiba[2] wala Waswila[3] wala Hami.[4] Na lakini wale waliokufuru wanamzushia Allah uwongo, na wengi wao hawatumii akili


1- - Bahira ni jina la ngamia jike aliyetogwa masikio na kuachwa huru aende malishoni bila ya mchungaji.
Wapagani wa Kikuraishi na hasa kabila la Khuzaa walimtukuza Ngamia huyu na kumfanya maalumu kwa
ajili ya ibada za masanamu; habebeshwi kitu mgongoni kwake, ngozi yake haitiwi alama na maziwa
yake hunywewa na mgeni tu.

2- - Saiba ni ngamia aliyewekwa nadhiri kwa ajili ya masanamu pindi mtu anaposalimika na maradhi
au kupata hadhi fulani. Ngamia huyu pia aliachwa huru aende malishoni bila ya mchungaji na ilikuwa
marufuku kupandwa na yeyote, isipokuwa haikatazwi kumtumia katika kubeba majani ya malisho na utekaji maji.

3- - Waswila katika ngamia ni ngamia jike aliyeachwa huru. Na Waswila katika mbuzi au kondoo ni yule
aliyezaa majike kwa mfululizo.

4- - Hami ni fahali (dume) la ngamia lililozalisha zao nyingi na kuzeeka. Halipandwi kama chombo cha usafiri wala halibebeshwi mizigo na huachwa huru kwenda machungani bila ya mchungaji.


Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 104

وَإِذَا قِيلَ لَهُمۡ تَعَالَوۡاْ إِلَىٰ مَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ وَإِلَى ٱلرَّسُولِ قَالُواْ حَسۡبُنَا مَا وَجَدۡنَا عَلَيۡهِ ءَابَآءَنَآۚ أَوَلَوۡ كَانَ ءَابَآؤُهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ شَيۡـٔٗا وَلَا يَهۡتَدُونَ

Na wanapoambiwa: Njooni kwenye yale aliyoyateremsha Allah, na kwa Mtume, wanasema: Yanatutosha tuliyowakuta nayo baba zetu. Je, (wanafuata waliyoyakuta kwa baba zao) hata kama baba zao hao hawajui kitu na hawana muongozo?



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 105

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ عَلَيۡكُمۡ أَنفُسَكُمۡۖ لَا يَضُرُّكُم مَّن ضَلَّ إِذَا ٱهۡتَدَيۡتُمۡۚ إِلَى ٱللَّهِ مَرۡجِعُكُمۡ جَمِيعٗا فَيُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Enyi mlioamini, zijalini nafsi zenu. Hawakudhuruni waliopotea ikiwa nyinyi mmeongoka. Kwa Allah tu ndio marejeo yenu nyote; basi atakuambieni yale yote mliyokuwa mnayatenda



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 106

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ شَهَٰدَةُ بَيۡنِكُمۡ إِذَا حَضَرَ أَحَدَكُمُ ٱلۡمَوۡتُ حِينَ ٱلۡوَصِيَّةِ ٱثۡنَانِ ذَوَا عَدۡلٖ مِّنكُمۡ أَوۡ ءَاخَرَانِ مِنۡ غَيۡرِكُمۡ إِنۡ أَنتُمۡ ضَرَبۡتُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ فَأَصَٰبَتۡكُم مُّصِيبَةُ ٱلۡمَوۡتِۚ تَحۡبِسُونَهُمَا مِنۢ بَعۡدِ ٱلصَّلَوٰةِ فَيُقۡسِمَانِ بِٱللَّهِ إِنِ ٱرۡتَبۡتُمۡ لَا نَشۡتَرِي بِهِۦ ثَمَنٗا وَلَوۡ كَانَ ذَا قُرۡبَىٰ وَلَا نَكۡتُمُ شَهَٰدَةَ ٱللَّهِ إِنَّآ إِذٗا لَّمِنَ ٱلۡأٓثِمِينَ

Enyi mlioamini, ushahidi wa baina yenu kinapomfikia mmoja wenu kifo wakati wa kuusia ni (mashahidi) wawili waadilifu miongoni mwenu au wawili wengine wasiokuwa katika nyinyi, mnapokuwa safarini na ukakusibuni msiba wa kifo. Mtawazuia wawili hao baada ya Swala. Waape kwa (jina la) Allah mkiwa na shaka (wakisema): Hatununui (hatupokei) thamani yoyote kwa haya (tunayoyatolea ushahidi) hata kama (tunaowatolea ushahidi dhidi yao) wakiwa ndugu wa nasaba, na hatufichi ushahidi wa Allah. Hakika, sisi tukifanya hivyo kwa yakini kabisa tutakuwa miongoni mwa wenye dhambi



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 107

فَإِنۡ عُثِرَ عَلَىٰٓ أَنَّهُمَا ٱسۡتَحَقَّآ إِثۡمٗا فَـَٔاخَرَانِ يَقُومَانِ مَقَامَهُمَا مِنَ ٱلَّذِينَ ٱسۡتَحَقَّ عَلَيۡهِمُ ٱلۡأَوۡلَيَٰنِ فَيُقۡسِمَانِ بِٱللَّهِ لَشَهَٰدَتُنَآ أَحَقُّ مِن شَهَٰدَتِهِمَا وَمَا ٱعۡتَدَيۡنَآ إِنَّآ إِذٗا لَّمِنَ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na ikigundulika kwamba, (mashahidi) wawili hao wametenda dhambi, basi (mashahidi) wawili wengine watasimama mahali pa wale wa mwanzo; hivyo wataapa kwa (jina la) Allah (kwamba): Hakika kabisa, ushahidi wetu ni wa kweli zaidi kuliko ushahidi wa wale wawili (wa kwanza) na hatujachupa mipaka; Hakika, wakati huo (tutakapoficha Ushahidi) sisi kwa yakini kabisa tutakuwa miongoni mwa madhalimu



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 108

ذَٰلِكَ أَدۡنَىٰٓ أَن يَأۡتُواْ بِٱلشَّهَٰدَةِ عَلَىٰ وَجۡهِهَآ أَوۡ يَخَافُوٓاْ أَن تُرَدَّ أَيۡمَٰنُۢ بَعۡدَ أَيۡمَٰنِهِمۡۗ وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَٱسۡمَعُواْۗ وَٱللَّهُ لَا يَهۡدِي ٱلۡقَوۡمَ ٱلۡفَٰسِقِينَ

Hilo linaelekea karibu zaidi watoe ushahidi kwa usahihi wake au wahofie viapo kukataliwa baada ya viapo vyao. Na mcheni Allah na sikieni. Na hakika, Allah hawaongoi watu waovu



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 109

۞يَوۡمَ يَجۡمَعُ ٱللَّهُ ٱلرُّسُلَ فَيَقُولُ مَاذَآ أُجِبۡتُمۡۖ قَالُواْ لَا عِلۡمَ لَنَآۖ إِنَّكَ أَنتَ عَلَّـٰمُ ٱلۡغُيُوبِ

Siku Allah atakapowakusanya Mitume na kuwaambia: Mlijibiwa nini? Watasema: Hatujui; hakika Wewe tu ndiye Mjuzi mno wa yote yaliyofichikana



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 110

إِذۡ قَالَ ٱللَّهُ يَٰعِيسَى ٱبۡنَ مَرۡيَمَ ٱذۡكُرۡ نِعۡمَتِي عَلَيۡكَ وَعَلَىٰ وَٰلِدَتِكَ إِذۡ أَيَّدتُّكَ بِرُوحِ ٱلۡقُدُسِ تُكَلِّمُ ٱلنَّاسَ فِي ٱلۡمَهۡدِ وَكَهۡلٗاۖ وَإِذۡ عَلَّمۡتُكَ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡحِكۡمَةَ وَٱلتَّوۡرَىٰةَ وَٱلۡإِنجِيلَۖ وَإِذۡ تَخۡلُقُ مِنَ ٱلطِّينِ كَهَيۡـَٔةِ ٱلطَّيۡرِ بِإِذۡنِي فَتَنفُخُ فِيهَا فَتَكُونُ طَيۡرَۢا بِإِذۡنِيۖ وَتُبۡرِئُ ٱلۡأَكۡمَهَ وَٱلۡأَبۡرَصَ بِإِذۡنِيۖ وَإِذۡ تُخۡرِجُ ٱلۡمَوۡتَىٰ بِإِذۡنِيۖ وَإِذۡ كَفَفۡتُ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ عَنكَ إِذۡ جِئۡتَهُم بِٱلۡبَيِّنَٰتِ فَقَالَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡهُمۡ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ مُّبِينٞ

(kumbuka) Pale Allah aliposema: Ewe Issa bin Mariamu, kumbuka neema yangu kwako na kwa mama yako, nilipokutia nguvu kwa Roho Mtakatifu (Jibrili), ukazungumza na watu katika utoto na ukiwa mtumzima. Na (kumbuka) nilivyokufundisha kitabu na hekima na Taurati na Injili, na wakati unaunda kutokana na udongo mfano wa ndege kwa idhini yangu, kisha unapuliza katika mfano huo na wakawa ndege kwa idhini yangu, na (kumbuka) ulipowaponyesha vipofu na wenye mbalanga kwa idhini yangu, na (kumbuka) wakati unawafufua wafu kwa idhini yangu. Na (kumbuka) nilipowazuia Wana wa Israili wasikudhuru ulipowaendea na hoja zilizo wazi, wakasema waliokufuru miongoni mwao (kwamba): Haya (aliyoyaleta Issa) si lolote isipokuwa tu ni uchawi mtupu!



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 111

وَإِذۡ أَوۡحَيۡتُ إِلَى ٱلۡحَوَارِيِّـۧنَ أَنۡ ءَامِنُواْ بِي وَبِرَسُولِي قَالُوٓاْ ءَامَنَّا وَٱشۡهَدۡ بِأَنَّنَا مُسۡلِمُونَ

Na (kumbuka) nilipowafunulia Hawariyyina (wanafunzi wa karibu wa Nabii Issa) kwamba: Niaminini Mimi na Mtume wangu. Walisema: Tumeamini na shuhudia kuwa sisi ni Waislamu



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 112

إِذۡ قَالَ ٱلۡحَوَارِيُّونَ يَٰعِيسَى ٱبۡنَ مَرۡيَمَ هَلۡ يَسۡتَطِيعُ رَبُّكَ أَن يُنَزِّلَ عَلَيۡنَا مَآئِدَةٗ مِّنَ ٱلسَّمَآءِۖ قَالَ ٱتَّقُواْ ٱللَّهَ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ

(Kumbuka) wanafunzi waliposema: Ewe Issa bin Mariamu, Je, Mola wako Mlezi anaweza kututeremshia chakula kutoka mbinguni? Akasema: Mcheni Allah ikiwa nyinyi ni Waumini



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 113

قَالُواْ نُرِيدُ أَن نَّأۡكُلَ مِنۡهَا وَتَطۡمَئِنَّ قُلُوبُنَا وَنَعۡلَمَ أَن قَدۡ صَدَقۡتَنَا وَنَكُونَ عَلَيۡهَا مِنَ ٱلشَّـٰهِدِينَ

Wakasema: Tunataka kukila chakula hicho, na nyoyo zetu zitue (ziridhike) na tujue kwamba umetuambia kweli, na kwa ajili yake tuwe miongoni mwa mashahidi



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 114

قَالَ عِيسَى ٱبۡنُ مَرۡيَمَ ٱللَّهُمَّ رَبَّنَآ أَنزِلۡ عَلَيۡنَا مَآئِدَةٗ مِّنَ ٱلسَّمَآءِ تَكُونُ لَنَا عِيدٗا لِّأَوَّلِنَا وَءَاخِرِنَا وَءَايَةٗ مِّنكَۖ وَٱرۡزُقۡنَا وَأَنتَ خَيۡرُ ٱلرَّـٰزِقِينَ

Issa bin Mariamu akasema: Ewe Mola wangu, Ewe Mola wetu Mlezi, tuteremshie chakula kutoka mbinguni kiwe Sikukuu kwa wa mwanzo wetu na wa mwisho wetu, na kiwe Ishara itokayo kwako, na turuzuku, na Wewe ndiye mbora wa wanaoruzuku



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 115

قَالَ ٱللَّهُ إِنِّي مُنَزِّلُهَا عَلَيۡكُمۡۖ فَمَن يَكۡفُرۡ بَعۡدُ مِنكُمۡ فَإِنِّيٓ أُعَذِّبُهُۥ عَذَابٗا لَّآ أُعَذِّبُهُۥٓ أَحَدٗا مِّنَ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Allah akasema: Hakika, Mimi nitakuteremshieni. Basi yeyote katika nyinyi atakayekufuru baada ya hapo, basi hakika nitamuadhibu adhabu ambayo sijamuadhibu yeyote katika walimwengu



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 116

وَإِذۡ قَالَ ٱللَّهُ يَٰعِيسَى ٱبۡنَ مَرۡيَمَ ءَأَنتَ قُلۡتَ لِلنَّاسِ ٱتَّخِذُونِي وَأُمِّيَ إِلَٰهَيۡنِ مِن دُونِ ٱللَّهِۖ قَالَ سُبۡحَٰنَكَ مَا يَكُونُ لِيٓ أَنۡ أَقُولَ مَا لَيۡسَ لِي بِحَقٍّۚ إِن كُنتُ قُلۡتُهُۥ فَقَدۡ عَلِمۡتَهُۥۚ تَعۡلَمُ مَا فِي نَفۡسِي وَلَآ أَعۡلَمُ مَا فِي نَفۡسِكَۚ إِنَّكَ أَنتَ عَلَّـٰمُ ٱلۡغُيُوبِ

Na (kumbuka) Allah aliposema: Ewe Issa bin Mariamu, hivi wewe uliwaambia watu: Nifanyeni mimi na mama yangu Miungu badala ya Allah? (Issa) akasema: Subhanaka (utakatifu ni wako wewe tu) Haiwi kwangu mimi kusema ambayo si haki yangu (kuyasema). Ikiwa nilisema basi bila ya shaka umekwishayajua. Wewe unayajua yaliyomo ndani ya nafsi yangu, na mimi siyajui yaliyomo katika nafsi yako. Hakika, Wewe ndiye Mjuzi wa yaliyofichikana



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 117

مَا قُلۡتُ لَهُمۡ إِلَّا مَآ أَمَرۡتَنِي بِهِۦٓ أَنِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ رَبِّي وَرَبَّكُمۡۚ وَكُنتُ عَلَيۡهِمۡ شَهِيدٗا مَّا دُمۡتُ فِيهِمۡۖ فَلَمَّا تَوَفَّيۡتَنِي كُنتَ أَنتَ ٱلرَّقِيبَ عَلَيۡهِمۡۚ وَأَنتَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ شَهِيدٌ

Sikuwaambia isipokuwa tu yale uliyoniamrisha, kwamba: Muabuduni Allah, Mola wangu Mlezi na Mola wenu Mlezi. Na mimi nilikuwa shahidi juu yao nilipokuwa nao. Na uliponifisha[1] ukawa Wewe ndiye Muangalizi juu yao. Na Wewe ni shahidi wa kila kitu


1- - Rejea maelezo yaliyopo katika Aya ya 55 ya Sura Aal-imran (3).


Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 118

إِن تُعَذِّبۡهُمۡ فَإِنَّهُمۡ عِبَادُكَۖ وَإِن تَغۡفِرۡ لَهُمۡ فَإِنَّكَ أَنتَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡحَكِيمُ

Ukiwaadhibu basi hao ni waja wako. Na ukiwasamehe basi Wewe ndiye Mwenye nguvu, Mwenye hekima nyingi



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 119

قَالَ ٱللَّهُ هَٰذَا يَوۡمُ يَنفَعُ ٱلصَّـٰدِقِينَ صِدۡقُهُمۡۚ لَهُمۡ جَنَّـٰتٞ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهَا ٱلۡأَنۡهَٰرُ خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدٗاۖ رَّضِيَ ٱللَّهُ عَنۡهُمۡ وَرَضُواْ عَنۡهُۚ ذَٰلِكَ ٱلۡفَوۡزُ ٱلۡعَظِيمُ

Allah atasema: Hii ndiyo Siku ambayo wasemao kweli utawafaa ukweli wao. Wao watapata Pepo zipitazo mito mbele yake, watadumu humo milele. Allah amewawia radhi, nao wamemuwia radhi. Huko ndiko kufuzu kukubwa sana



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 120

لِلَّهِ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا فِيهِنَّۚ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرُۢ

Ni wa Allah tu ufalme wa mbinguni na ardhini na vilivyomo ndani yake. Na yeye ni Muweza wa kila kitu