Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 61

فَلَمَّا جَآءَ ءَالَ لُوطٍ ٱلۡمُرۡسَلُونَ

Basi wale wajumbe (waliotumwa) walipofika kwa Lutwi



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 62

قَالَ إِنَّكُمۡ قَوۡمٞ مُّنكَرُونَ

(Lutwi) Alisema: Hakika nyinyi ni watu msiojulikana (hapa kwetu)



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 63

قَالُواْ بَلۡ جِئۡنَٰكَ بِمَا كَانُواْ فِيهِ يَمۡتَرُونَ

(Malaika) Walisema: Bali sisi tumekuletea (adhabu ya) yale waliyokuwa wakiyatilia shaka



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 64

وَأَتَيۡنَٰكَ بِٱلۡحَقِّ وَإِنَّا لَصَٰدِقُونَ

Na tumefika kwako kwa Haki, na hakika sisi tunasema kweli



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 65

فَأَسۡرِ بِأَهۡلِكَ بِقِطۡعٖ مِّنَ ٱلَّيۡلِ وَٱتَّبِعۡ أَدۡبَٰرَهُمۡ وَلَا يَلۡتَفِتۡ مِنكُمۡ أَحَدٞ وَٱمۡضُواْ حَيۡثُ تُؤۡمَرُونَ

Basi ondoka na ahli zako kwenye sehemu ya usiku, nawe ufuate nyuma yao (huku ukiwahimiza ili waharakishe kuondoka), wala yeyote kati yenu asigeuke nyuma. Na mwende mlikoamrishwa



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 66

وَقَضَيۡنَآ إِلَيۡهِ ذَٰلِكَ ٱلۡأَمۡرَ أَنَّ دَابِرَ هَـٰٓؤُلَآءِ مَقۡطُوعٞ مُّصۡبِحِينَ

Na tukamfunulia Lutwi wahyi huo kwamba, mwisho wa watu hawa ikifika (mapambazuko ya) asubuhi watakuwa wameshakatiliwa mbali



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 67

وَجَآءَ أَهۡلُ ٱلۡمَدِينَةِ يَسۡتَبۡشِرُونَ

Na walikuja watu wa mji ule (baada ya kusikia kwa Lutu kuna wageni wazuri) huku wakifurahi



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 68

قَالَ إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ ضَيۡفِي فَلَا تَفۡضَحُونِ

(Lutwi) Alisema (kuwaambia): Hakika hawa wageni wangu (wanahitaji kuenziwa), tafadhalini msinifedheheshe



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 69

وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَلَا تُخۡزُونِ

Na mcheni Allah, wala msinidhalilishe (mbele ya wageni)



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 70

قَالُوٓاْ أَوَلَمۡ نَنۡهَكَ عَنِ ٱلۡعَٰلَمِينَ

(Watu wa Lutwi) Walisema: Sisi situlikukataza usitie (neno tunapomtaka) yeyote katika walimwengu?



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 71

قَالَ هَـٰٓؤُلَآءِ بَنَاتِيٓ إِن كُنتُمۡ فَٰعِلِينَ

(Lutwi) Alisema (kuwaambia msinivunjie heshima): Hawa (hapa) binti zangu (waoeni), ikiwa nyinyi ni wafanyaji (mnaotaka kukata hamu zenu)



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 72

لَعَمۡرُكَ إِنَّهُمۡ لَفِي سَكۡرَتِهِمۡ يَعۡمَهُونَ

(Allah alisema) Naapia kwa umri wako! Hakika hao (watu wa Lutwi) wamepagawa katika ulevi wao, wanahangaika



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 73

فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّيۡحَةُ مُشۡرِقِينَ

Basi (ghafla) Ukelele mkali uliwachukua kipindi cha mapam-bazuko



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 74

فَجَعَلۡنَا عَٰلِيَهَا سَافِلَهَا وَأَمۡطَرۡنَا عَلَيۡهِمۡ حِجَارَةٗ مِّن سِجِّيلٍ

Na tukaigeuza nchi (yao) juu chini chini juu, na tukawanyeshea (mvua ya) mawe ya udongo wa Motoni



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 75

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّلۡمُتَوَسِّمِينَ

Hakika katika hiyo (adhabu iliyowapata watu wa Lutwi) zipo ishara kwa wanaozingatia



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 76

وَإِنَّهَا لَبِسَبِيلٖ مُّقِيمٍ

Na (kitongoji cha watu wa Lutwi) kipo kwenye barabara ipitwayo (na watu wanaokwenda Sham)



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 77

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗ لِّلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika katika hiyo (adhabu) ipo ishara (na mazingatio) kwa Waumini



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 78

وَإِن كَانَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡأَيۡكَةِ لَظَٰلِمِينَ

Japokuwa watu wa mji uliozingirwa na msitu (nao) walikuwa madhalimu[1]


1- - Hawa ni watu wa Nabii Shuaib, nao pia walikuwa wanamkufuru Allah.


Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 79

فَٱنتَقَمۡنَا مِنۡهُمۡ وَإِنَّهُمَا لَبِإِمَامٖ مُّبِينٖ

Kwa hivyo tuliwaadhibu. Na miji miwili hiyo ipo kwenye barabara iliyo wazi



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 80

وَلَقَدۡ كَذَّبَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡحِجۡرِ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na bila ya shaka wakazi wa Hijr[1] waliwapinga Mitume


1- - Hijri ni bonde linalopatikana kati ya mji wa Madina na ardhi ya Shamu


Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 81

وَءَاتَيۡنَٰهُمۡ ءَايَٰتِنَا فَكَانُواْ عَنۡهَا مُعۡرِضِينَ

Na tuliwapa (watu wa Thamud) ishara zetu, nao walizipuuza



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 82

وَكَانُواْ يَنۡحِتُونَ مِنَ ٱلۡجِبَالِ بُيُوتًا ءَامِنِينَ

Nao walikuwa wakichonga katika milima (na kuyafanya majumba) kwa amani



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 83

فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّيۡحَةُ مُصۡبِحِينَ

Basi ukelele ukawatwaa asubuhi



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 84

فَمَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ

Basi hayakuwafaa waliyokuwa wanayachuma



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 85

وَمَا خَلَقۡنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَآ إِلَّا بِٱلۡحَقِّۗ وَإِنَّ ٱلسَّاعَةَ لَأٓتِيَةٞۖ فَٱصۡفَحِ ٱلصَّفۡحَ ٱلۡجَمِيلَ

Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ila kwa ajili ya Haki. Na hakika Kiyama kitafika tu (wala hilo halina shaka). Basi (Ewe Mtume) samehe (watu wako) msamaha mzuri



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 86

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ ٱلۡخَلَّـٰقُ ٱلۡعَلِيمُ

Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji (wa kila kitu tena) Mjuzi sana



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 87

وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَٰكَ سَبۡعٗا مِّنَ ٱلۡمَثَانِي وَٱلۡقُرۡءَانَ ٱلۡعَظِيمَ

Na tumekupa Aya saba (za Sura Al-fatiha) zisomwazo mara kwa mara, na Qur’ani Tukufu



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 88

لَا تَمُدَّنَّ عَيۡنَيۡكَ إِلَىٰ مَا مَتَّعۡنَا بِهِۦٓ أَزۡوَٰجٗا مِّنۡهُمۡ وَلَا تَحۡزَنۡ عَلَيۡهِمۡ وَٱخۡفِضۡ جَنَاحَكَ لِلۡمُؤۡمِنِينَ

Usivikodolee macho yako vitu tulivyo waneemesha makundi fulani kati yao (hao makafiri), wala usiwahuzunikie (wasipoamaini). Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 89

وَقُلۡ إِنِّيٓ أَنَا ٱلنَّذِيرُ ٱلۡمُبِينُ

Na sema: Hakika mimi ni muonyaji mwenye kubainisha



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 90

كَمَآ أَنزَلۡنَا عَلَى ٱلۡمُقۡتَسِمِينَ

(Tumekuteremshia hii Qur’an) Kama tulivyowateremshia (Kitabu Mayahudi na Manaswara) walikigawanya (kwa kuamini baadhi na kukataa baadhi)