Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 31

وَلِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِ لِيَجۡزِيَ ٱلَّذِينَ أَسَـٰٓـُٔواْ بِمَا عَمِلُواْ وَيَجۡزِيَ ٱلَّذِينَ أَحۡسَنُواْ بِٱلۡحُسۡنَى

Na ni vya Allah Pekee vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini, ili Awalipe wale waliofanya uovu kwa yale waliyoyatenda, na Awalipe wale waliofanya mema kwa mema zaidi



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 32

ٱلَّذِينَ يَجۡتَنِبُونَ كَبَـٰٓئِرَ ٱلۡإِثۡمِ وَٱلۡفَوَٰحِشَ إِلَّا ٱللَّمَمَۚ إِنَّ رَبَّكَ وَٰسِعُ ٱلۡمَغۡفِرَةِۚ هُوَ أَعۡلَمُ بِكُمۡ إِذۡ أَنشَأَكُم مِّنَ ٱلۡأَرۡضِ وَإِذۡ أَنتُمۡ أَجِنَّةٞ فِي بُطُونِ أُمَّهَٰتِكُمۡۖ فَلَا تُزَكُّوٓاْ أَنفُسَكُمۡۖ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَنِ ٱتَّقَىٰٓ

Wale wanaojiepusha na madhambi makubwa na machafu isipokuwa makosa madogo-madogo. Hakika Bwana wako ni Mwingi wa msamaha. Yeye Anakujueni vyema, tangu Alipokuanzisheni kutoka katika ardhi, na pale mlipokuwa mimba changa matumboni mwa mama zenu. Basi msizitakase nafsi zenu. Yeye Anamjua zaidi aliyekuwa na taqwa



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 33

أَفَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي تَوَلَّىٰ

Hivi umemuona yule ambaye amekengeuka



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 34

وَأَعۡطَىٰ قَلِيلٗا وَأَكۡدَىٰٓ

Na Akatoa kidogo, kisha akazuia.?



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 35

أَعِندَهُۥ عِلۡمُ ٱلۡغَيۡبِ فَهُوَ يَرَىٰٓ

hivi yeye ana elimu ya ghaibu basi kwa elimu hiyo yeye anaona?



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 36

أَمۡ لَمۡ يُنَبَّأۡ بِمَا فِي صُحُفِ مُوسَىٰ

Au hawajaambiwa kwa ambayo yamo kwenye kitabu cha Mussa?



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 37

وَإِبۡرَٰهِيمَ ٱلَّذِي وَفَّىٰٓ

Na Ibraahim aliyetimiza (ahadi)



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 38

أَلَّا تَزِرُ وَازِرَةٞ وِزۡرَ أُخۡرَىٰ

Na kwamba mbebaji dhambi hatobeba mzigo wa mwengine



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 39

وَأَن لَّيۡسَ لِلۡإِنسَٰنِ إِلَّا مَا سَعَىٰ

Na kwamba Mtu hatopata malipo isipokuwa yale aliyoyafanyia juhudi



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 40

وَأَنَّ سَعۡيَهُۥ سَوۡفَ يُرَىٰ

Na kwamba juhudi yake itakuja kuonekana



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 41

ثُمَّ يُجۡزَىٰهُ ٱلۡجَزَآءَ ٱلۡأَوۡفَىٰ

Kisha atalipwa malipo yake kamilifu



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 42

وَأَنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلۡمُنتَهَىٰ

Na hakika kwa bwana wako ndio marejeo



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 43

وَأَنَّهُۥ هُوَ أَضۡحَكَ وَأَبۡكَىٰ

Na kwamba Yeye Ndiye Anayesababisha kwa Mtu kicheko (furaha) na kilio



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 44

وَأَنَّهُۥ هُوَ أَمَاتَ وَأَحۡيَا

Na hakika yeye ndiye anafisha na ndiye anayehuisha



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 45

وَأَنَّهُۥ خَلَقَ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰ

Na hakika yeye ameumba aina mbili ya viumbe Dume Na Jike



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 46

مِن نُّطۡفَةٍ إِذَا تُمۡنَىٰ

Kutokana na tone la manii linapomiminwa



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 47

وَأَنَّ عَلَيۡهِ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأُخۡرَىٰ

Na kwamba ni juu Yake uanzishaji mwengine (kufufua)



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 48

وَأَنَّهُۥ هُوَ أَغۡنَىٰ وَأَقۡنَىٰ

Na kwamba Yeye Ndiye Atoshelezaye na Akinaishaye



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 49

وَأَنَّهُۥ هُوَ رَبُّ ٱلشِّعۡرَىٰ

Na kwamba Yeye ndiye Mola wa nyota ya Ash-Shi’-raa (inayoabudiwa).[1]


1- - Ash-Shi’-raa:- Hii ni Nyota maarufu, na Allah ameihusisha kuitaja hapa, ijapokuwa yeye ni Mola wa kila kitu kwasababu hii Nyota ni katika zilizokuwa zikiabudiwa katika zama za Kijaahiliyya, kwahiyo Allah akabainisha kila chochote wanacho kiabudu Washirikina basi hicho kimeumbwa na Allah, na hakistahiki kuabudiwa.


Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 50

وَأَنَّهُۥٓ أَهۡلَكَ عَادًا ٱلۡأُولَىٰ

Na kwamba Yeye Ndiye Aliyeangamiza kina ‘Aad Mwanzo



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 51

وَثَمُودَاْ فَمَآ أَبۡقَىٰ

Na Watu wa Thamuwd kisha Hakuwabakisha



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 52

وَقَوۡمَ نُوحٖ مِّن قَبۡلُۖ إِنَّهُمۡ كَانُواْ هُمۡ أَظۡلَمَ وَأَطۡغَىٰ

Na Watu wa Nuwh hapo kabla, hakika wao walikuwa madhalimu zaidi na wapindukaji mipaka zaidi wa kuasi



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 53

وَٱلۡمُؤۡتَفِكَةَ أَهۡوَىٰ

Na miji iliyopinduliwa ni yeye Allah aliyeipindulia mbali



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 54

فَغَشَّىٰهَا مَا غَشَّىٰ

Na ikawafunika ambacho kimewafunika



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 55

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكَ تَتَمَارَىٰ

Basi neema gani za Bwana wako unazitilia shaka?



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 56

هَٰذَا نَذِيرٞ مِّنَ ٱلنُّذُرِ ٱلۡأُولَىٰٓ

Huyu (Mtume þ) ni muonyaji miongoni mwa waonyaji wa awali



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 57

أَزِفَتِ ٱلۡأٓزِفَةُ

Kimekaribia kinachokaribia



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 58

لَيۡسَ لَهَا مِن دُونِ ٱللَّهِ كَاشِفَةٌ

Hakuna asiyekuwa Allah mwenye uwezo wa kukibainisha



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 59

أَفَمِنۡ هَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ تَعۡجَبُونَ

Je, mnastaajabu kwa Mazungumzo haya (ya Qur-aan)?



Capítulo: ANNAJMI 

Verso : 60

وَتَضۡحَكُونَ وَلَا تَبۡكُونَ

Na mnacheka na wala hamlii?