Capítulo: ATTUR 

Verso : 31

قُلۡ تَرَبَّصُواْ فَإِنِّي مَعَكُم مِّنَ ٱلۡمُتَرَبِّصِينَ

Sema subirini basi hakika mimi pamoja nanyi ni miongoni mwa wenye kusubiri



Capítulo: ATTUR 

Verso : 32

أَمۡ تَأۡمُرُهُمۡ أَحۡلَٰمُهُم بِهَٰذَآۚ أَمۡ هُمۡ قَوۡمٞ طَاغُونَ

Au zinawaamuru wao ndoto zao kwa hili au wao ni watu waovu



Capítulo: ATTUR 

Verso : 33

أَمۡ يَقُولُونَ تَقَوَّلَهُۥۚ بَل لَّا يُؤۡمِنُونَ

Au wanasema ameizua hiyo qurani bali hawaamini



Capítulo: ATTUR 

Verso : 34

فَلۡيَأۡتُواْ بِحَدِيثٖ مِّثۡلِهِۦٓ إِن كَانُواْ صَٰدِقِينَ

Basi walete mazungumzo (Quran) mfano wake kama watakua wakweli



Capítulo: ATTUR 

Verso : 35

أَمۡ خُلِقُواْ مِنۡ غَيۡرِ شَيۡءٍ أَمۡ هُمُ ٱلۡخَٰلِقُونَ

Au wameumbwa pasipo na kitu chochote (bila ya muumba) au wao ndio waumbaji?



Capítulo: ATTUR 

Verso : 36

أَمۡ خَلَقُواْ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَۚ بَل لَّا يُوقِنُونَ

Au wameumba mbingu na ardhi? Bali hawana yakini



Capítulo: ATTUR 

Verso : 37

أَمۡ عِندَهُمۡ خَزَآئِنُ رَبِّكَ أَمۡ هُمُ ٱلۡمُصَۜيۡطِرُونَ

Au wanazo hazina za Mola wako mlezi, au wao ndio wenye madaraka? (wenye kudhibiti)?



Capítulo: ATTUR 

Verso : 38

أَمۡ لَهُمۡ سُلَّمٞ يَسۡتَمِعُونَ فِيهِۖ فَلۡيَأۡتِ مُسۡتَمِعُهُم بِسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٍ

Au wanazo ngazi wanasikilizia kwa makini humo? Basi msikilizaji wao alete dalili bayana



Capítulo: ATTUR 

Verso : 39

أَمۡ لَهُ ٱلۡبَنَٰتُ وَلَكُمُ ٱلۡبَنُونَ

Au (Allah) Ana watoto wa kike, nanyi mna watoto wa kiume?



Capítulo: ATTUR 

Verso : 40

أَمۡ تَسۡـَٔلُهُمۡ أَجۡرٗا فَهُم مِّن مَّغۡرَمٖ مُّثۡقَلُونَ

Au unawaomba ujira kwa hiyo wameelemewa na uzito wa gharama?



Capítulo: ATTUR 

Verso : 41

أَمۡ عِندَهُمُ ٱلۡغَيۡبُ فَهُمۡ يَكۡتُبُونَ

Au wanayo elimu ya ghayb kisha wao wanaandika?



Capítulo: ATTUR 

Verso : 42

أَمۡ يُرِيدُونَ كَيۡدٗاۖ فَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ هُمُ ٱلۡمَكِيدُونَ

Au wanakusudia hila (shari)? Basi wale waliokufuru wao ndio watakaopangiwa hila



Capítulo: ATTUR 

Verso : 43

أَمۡ لَهُمۡ إِلَٰهٌ غَيۡرُ ٱللَّهِۚ سُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يُشۡرِكُونَ

Au wana wao mungu asiye Allah utakasifu ni wake allah na yote wanayomshirikisha nayo



Capítulo: ATTUR 

Verso : 44

وَإِن يَرَوۡاْ كِسۡفٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ سَاقِطٗا يَقُولُواْ سَحَابٞ مَّرۡكُومٞ

Na hata wangeliona pande la moto kutoka mbinguni linaanguka wangelisema: Mawingu tu yamerundikana



Capítulo: ATTUR 

Verso : 45

فَذَرۡهُمۡ حَتَّىٰ يُلَٰقُواْ يَوۡمَهُمُ ٱلَّذِي فِيهِ يُصۡعَقُونَ

Basi waachilie mbali mpaka wakutane na Siku yao ambayo humo wataangamizwa



Capítulo: ATTUR 

Verso : 46

يَوۡمَ لَا يُغۡنِي عَنۡهُمۡ كَيۡدُهُمۡ شَيۡـٔٗا وَلَا هُمۡ يُنصَرُونَ

Siku ambayo njama zao hazitowafaa kitu chochote, na wala wao hawatonusuriwa



Capítulo: ATTUR 

Verso : 47

وَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُواْ عَذَابٗا دُونَ ذَٰلِكَ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Na hakika wale waliodhulumu watapata adhabu nyingine isiyokuwa hiyo, lakini wengi wao hawajui



Capítulo: ATTUR 

Verso : 48

وَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ فَإِنَّكَ بِأَعۡيُنِنَاۖ وَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ حِينَ تَقُومُ

Na subiri hukumu ya mola wako mlezi na hakika wewe uko machoni kwetu (uangalizi wetu) na msabihi Mola wako mlezi pamoja na kusifu wakati unapoamka



Capítulo: ATTUR 

Verso : 49

وَمِنَ ٱلَّيۡلِ فَسَبِّحۡهُ وَإِدۡبَٰرَ ٱلنُّجُومِ

Na katika usiku Msabbih na zinapokuchwa nyota