Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 1

حمٓ

Haamiim



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 2

وَٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُبِينِ

Nina apa kwa Kitabu kinacho-bainisha



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 3

إِنَّا جَعَلۡنَٰهُ قُرۡءَٰنًا عَرَبِيّٗا لَّعَلَّكُمۡ تَعۡقِلُونَ

Hakika, Sisi tumekifanya (hicho kitabu) Qur’ani ya Kiarabu ili mfahamu



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 4

وَإِنَّهُۥ فِيٓ أُمِّ ٱلۡكِتَٰبِ لَدَيۡنَا لَعَلِيٌّ حَكِيمٌ

Na hakika kitabu hicho katika Kitabu Mama kilichopo kwetu, kwa yakini kabisa, ni kitukufu, chenye hekima nyingi



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 5

أَفَنَضۡرِبُ عَنكُمُ ٱلذِّكۡرَ صَفۡحًا أَن كُنتُمۡ قَوۡمٗا مُّسۡرِفِينَ

Je! Tuache kukukumbusheni kabisa kwa kuwa nyinyi ni watu mliovuka mipaka (kwa ukafiri)?



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 6

وَكَمۡ أَرۡسَلۡنَا مِن نَّبِيّٖ فِي ٱلۡأَوَّلِينَ

Na Manabii wangapi tuliwatuma kwa watu wa zamani? (Ni wengi tu)



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 7

وَمَا يَأۡتِيهِم مِّن نَّبِيٍّ إِلَّا كَانُواْ بِهِۦ يَسۡتَهۡزِءُونَ

Na hawaendei Nabii yeyote ila walikuwa wakimkejeli



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 8

فَأَهۡلَكۡنَآ أَشَدَّ مِنۡهُم بَطۡشٗا وَمَضَىٰ مَثَلُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Basi tuliwaangamiza waliokuwa na nguvu sana kushinda wao. Na mfano wa watu wa zamani umekwisha pita



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 9

وَلَئِن سَأَلۡتَهُم مَّنۡ خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ لَيَقُولُنَّ خَلَقَهُنَّ ٱلۡعَزِيزُ ٱلۡعَلِيمُ

Na ukiwauliza: Nani aliye ziumba mbingu na ardhi? Bila ya shaka watasema: Kaziumba Mwenye nguvu, Mjuzi,



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 10

ٱلَّذِي جَعَلَ لَكُمُ ٱلۡأَرۡضَ مَهۡدٗا وَجَعَلَ لَكُمۡ فِيهَا سُبُلٗا لَّعَلَّكُمۡ تَهۡتَدُونَ

Ambaye amekufanyieni ardhi kama tandiko, na akakufanyieni ndani yake njia mpate kuongoka



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 11

وَٱلَّذِي نَزَّلَ مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءَۢ بِقَدَرٖ فَأَنشَرۡنَا بِهِۦ بَلۡدَةٗ مَّيۡتٗاۚ كَذَٰلِكَ تُخۡرَجُونَ

Na ambaye ndiye aliye teremsha kutoka mbinguni maji kwa kiasi, na kwa hayo tukaifufua nchi iliyo kufa. Na namna hivi ndivyo mtakavyo tolewa



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 12

وَٱلَّذِي خَلَقَ ٱلۡأَزۡوَٰجَ كُلَّهَا وَجَعَلَ لَكُم مِّنَ ٱلۡفُلۡكِ وَٱلۡأَنۡعَٰمِ مَا تَرۡكَبُونَ

Na ambaye ndiye aliyeumba katika kila kitu jike na dume, na akakufanyieni marikebu na wanyama mnao wapanda



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 13

لِتَسۡتَوُۥاْ عَلَىٰ ظُهُورِهِۦ ثُمَّ تَذۡكُرُواْ نِعۡمَةَ رَبِّكُمۡ إِذَا ٱسۡتَوَيۡتُمۡ عَلَيۡهِ وَتَقُولُواْ سُبۡحَٰنَ ٱلَّذِي سَخَّرَ لَنَا هَٰذَا وَمَا كُنَّا لَهُۥ مُقۡرِنِينَ

Ili mkae vizuri migongoni mwao, kisha mkumbuke neema za Mola wenu Mlezi mnapokaa sawa sawa juu yao na mseme: Ametakasika aliye mfanya huyu atutumikie, na tusingeliweza kufanya haya wenyewe



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 14

وَإِنَّآ إِلَىٰ رَبِّنَا لَمُنقَلِبُونَ

Na hakika sisi tutarudi kwa Mola wetu Mlezi



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 15

وَجَعَلُواْ لَهُۥ مِنۡ عِبَادِهِۦ جُزۡءًاۚ إِنَّ ٱلۡإِنسَٰنَ لَكَفُورٞ مُّبِينٌ

Na wanamfanyia katika waja wake fungu. Kwa hakika mwanaa-damu ni mtovu wa fadhila aliye dhaahiri



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 16

أَمِ ٱتَّخَذَ مِمَّا يَخۡلُقُ بَنَاتٖ وَأَصۡفَىٰكُم بِٱلۡبَنِينَ

Au amejichukulia watoto wanawake katika vile alivyo viumba, na akakuteulieni nyinyi watoto wanaume?



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 17

وَإِذَا بُشِّرَ أَحَدُهُم بِمَا ضَرَبَ لِلرَّحۡمَٰنِ مَثَلٗا ظَلَّ وَجۡهُهُۥ مُسۡوَدّٗا وَهُوَ كَظِيمٌ

Na anapo bashiriwa mmoja wao kwa yale aliyo mpigia mfano Allah, uso wake husawijika na hujaa hasira



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 18

أَوَمَن يُنَشَّؤُاْ فِي ٱلۡحِلۡيَةِ وَهُوَ فِي ٱلۡخِصَامِ غَيۡرُ مُبِينٖ

Ati aliyelelewa katika mapambo, na katika mabishano hawezi kusema kwa bayana...?



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 19

وَجَعَلُواْ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةَ ٱلَّذِينَ هُمۡ عِبَٰدُ ٱلرَّحۡمَٰنِ إِنَٰثًاۚ أَشَهِدُواْ خَلۡقَهُمۡۚ سَتُكۡتَبُ شَهَٰدَتُهُمۡ وَيُسۡـَٔلُونَ

Na wakawafanya Malaika, ambao ni waja wa Mwingi wa Rehema, kuwa ni wanawake! Kwani wameshuhudia kuumbwa kwao? Ushahidi wao utaandikwa na wao watahojiwa!



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 20

وَقَالُواْ لَوۡ شَآءَ ٱلرَّحۡمَٰنُ مَا عَبَدۡنَٰهُمۗ مَّا لَهُم بِذَٰلِكَ مِنۡ عِلۡمٍۖ إِنۡ هُمۡ إِلَّا يَخۡرُصُونَ

Nao husema: Angeli penda Mwingi wa Rehema tusingeliwaabudu. Hawana ujuzi wowote wa hayo! Hawana ila kusema uongo tu!



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 21

أَمۡ ءَاتَيۡنَٰهُمۡ كِتَٰبٗا مِّن قَبۡلِهِۦ فَهُم بِهِۦ مُسۡتَمۡسِكُونَ

Kwani tuliwapa Kitabu kabla ya hiki, na ikawa wao wanakishikilia hicho?



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 22

بَلۡ قَالُوٓاْ إِنَّا وَجَدۡنَآ ءَابَآءَنَا عَلَىٰٓ أُمَّةٖ وَإِنَّا عَلَىٰٓ ءَاثَٰرِهِم مُّهۡتَدُونَ

Bali wanasema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu wanashika dini makhsusi, basi na sisi tunaongoza (tukafuata) nyayo zao



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 23

وَكَذَٰلِكَ مَآ أَرۡسَلۡنَا مِن قَبۡلِكَ فِي قَرۡيَةٖ مِّن نَّذِيرٍ إِلَّا قَالَ مُتۡرَفُوهَآ إِنَّا وَجَدۡنَآ ءَابَآءَنَا عَلَىٰٓ أُمَّةٖ وَإِنَّا عَلَىٰٓ ءَاثَٰرِهِم مُّقۡتَدُونَ

Na kadhalika hatukumtuma mwonyaji kwenye mji wowote ila watu wake walio deka kwa starehe walisema: Hakika sisi tuliwakuta baba zetu wanashika dini makhsusi, na sisi tunafuata nyayo zao



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 24

۞قَٰلَ أَوَلَوۡ جِئۡتُكُم بِأَهۡدَىٰ مِمَّا وَجَدتُّمۡ عَلَيۡهِ ءَابَآءَكُمۡۖ قَالُوٓاْ إِنَّا بِمَآ أُرۡسِلۡتُم بِهِۦ كَٰفِرُونَ

Akasema (Mwonyaji): Hata nikikuleteeni yenye uongofu bora kuliko mlio wakuta nao baba zenu? Wakasema: Sisi tunayakataa tu hayo mliyo tumwa



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 25

فَٱنتَقَمۡنَا مِنۡهُمۡۖ فَٱنظُرۡ كَيۡفَ كَانَ عَٰقِبَةُ ٱلۡمُكَذِّبِينَ

Basi tukawalipizia. Angalia ulikuwaje mwisho wa walio kadhi-bisha!



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 26

وَإِذۡ قَالَ إِبۡرَٰهِيمُ لِأَبِيهِ وَقَوۡمِهِۦٓ إِنَّنِي بَرَآءٞ مِّمَّا تَعۡبُدُونَ

Na pale Ibrahim alipo mwambia baba yake na watu wake: Hakika mimi ninajitenga mbali na hayo mnayo yaabudu



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 27

إِلَّا ٱلَّذِي فَطَرَنِي فَإِنَّهُۥ سَيَهۡدِينِ

Isipo kuwa yule aliye niumba, kwani Yeye ataniongoa



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 28

وَجَعَلَهَا كَلِمَةَۢ بَاقِيَةٗ فِي عَقِبِهِۦ لَعَلَّهُمۡ يَرۡجِعُونَ

Na akalifanya hili liwe neno lenye kubaki katika vizazi vyake ili warejee



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 29

بَلۡ مَتَّعۡتُ هَـٰٓؤُلَآءِ وَءَابَآءَهُمۡ حَتَّىٰ جَآءَهُمُ ٱلۡحَقُّ وَرَسُولٞ مُّبِينٞ

Bali tuliwastarehesha hawa na baba zao mpaka ikawafikia Haki na Mtume aliye bainisha



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 30

وَلَمَّا جَآءَهُمُ ٱلۡحَقُّ قَالُواْ هَٰذَا سِحۡرٞ وَإِنَّا بِهِۦ كَٰفِرُونَ

Na ilipowafikia Haki wakasema: Huu ni uchawi, na sisi hakika tunaukataa