Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 114

يُؤۡمِنُونَ بِٱللَّهِ وَٱلۡيَوۡمِ ٱلۡأٓخِرِ وَيَأۡمُرُونَ بِٱلۡمَعۡرُوفِ وَيَنۡهَوۡنَ عَنِ ٱلۡمُنكَرِ وَيُسَٰرِعُونَ فِي ٱلۡخَيۡرَٰتِۖ وَأُوْلَـٰٓئِكَ مِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Wanamuamini Allah na Siku ya Mwisho na wanaamrisha mema na kukataza maovu na wanayaendea haraka mambo ya kheri, na hao ni katika watu wema



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 115

وَمَا يَفۡعَلُواْ مِنۡ خَيۡرٖ فَلَن يُكۡفَرُوهُۗ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِٱلۡمُتَّقِينَ

Na chochote cha kheri wanachokifanya hawatonyimwa malipo yake, na Allah anawajua mno wamchao (Yeye)



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 56

وَلَا تُفۡسِدُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ بَعۡدَ إِصۡلَٰحِهَا وَٱدۡعُوهُ خَوۡفٗا وَطَمَعًاۚ إِنَّ رَحۡمَتَ ٱللَّهِ قَرِيبٞ مِّنَ ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Na msifanye uharibifu katika ardhi baada ya (ya Allah) kutengeneza na muombeni yeye (tu) kwa kuogopa (adhabu yake) na kutumai (rehema zake). Hakika, rehema za Allah zipo karibu na wenye kufanya mazuri



Capítulo: YUNUS 

Verso : 26

۞لِّلَّذِينَ أَحۡسَنُواْ ٱلۡحُسۡنَىٰ وَزِيَادَةٞۖ وَلَا يَرۡهَقُ وُجُوهَهُمۡ قَتَرٞ وَلَا ذِلَّةٌۚ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡجَنَّةِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ

Wale waliofanya mazuri (hapa duniani), watapata mazuri (Akhera) na ziada[1] na wala nyuso zao hazitafunikwa na vumbi na madhila. Hao ndio watu wa Peponi; humo watakaa milele


1- - Swahaba wengi, Allah awawie radhi, wametafsiri “mazuri” kwamba ni Pepo na “ziada” kwamba ni kumuona Allah Mtukufu.


Capítulo: YUSUF 

Verso : 56

وَكَذَٰلِكَ مَكَّنَّا لِيُوسُفَ فِي ٱلۡأَرۡضِ يَتَبَوَّأُ مِنۡهَا حَيۡثُ يَشَآءُۚ نُصِيبُ بِرَحۡمَتِنَا مَن نَّشَآءُۖ وَلَا نُضِيعُ أَجۡرَ ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Na kama hivyo tulimmakinisha Yusuf (na kumpa cheo katika nchi); akawa anakaa humo popote anapopenda. Tunamfikishia rehema zetu tumtakaye, na hatupotezi malipo ya wafanyao mazuri



Capítulo: ANNAHLI 

Verso : 128

إِنَّ ٱللَّهَ مَعَ ٱلَّذِينَ ٱتَّقَواْ وَّٱلَّذِينَ هُم مُّحۡسِنُونَ

Kwa hakika Allah yupo pamoja na wale wanaomcha (Allah), na wale wafanyao wema



Capítulo: ALMUUMINUUN 

Verso : 61

أُوْلَـٰٓئِكَ يُسَٰرِعُونَ فِي ٱلۡخَيۡرَٰتِ وَهُمۡ لَهَا سَٰبِقُونَ

Basi wote hao ndio wanao kimbilia katika mambo ya kheri, na ndio watakao tangulia kuyafikia