Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 80

تَرَىٰ كَثِيرٗا مِّنۡهُمۡ يَتَوَلَّوۡنَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْۚ لَبِئۡسَ مَا قَدَّمَتۡ لَهُمۡ أَنفُسُهُمۡ أَن سَخِطَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِمۡ وَفِي ٱلۡعَذَابِ هُمۡ خَٰلِدُونَ

Utawaona wengi wao wana-wafanya makafiri marafiki (wao) wa ndani. Kwa yakini kabisa, ni maovu sana hayo yaliyotangulia kufanywa na nafsi zao hadi Allah amewakasirikia, na watadumu milele katika adhabu



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 91

إِنَّمَا يُرِيدُ ٱلشَّيۡطَٰنُ أَن يُوقِعَ بَيۡنَكُمُ ٱلۡعَدَٰوَةَ وَٱلۡبَغۡضَآءَ فِي ٱلۡخَمۡرِ وَٱلۡمَيۡسِرِ وَيَصُدَّكُمۡ عَن ذِكۡرِ ٱللَّهِ وَعَنِ ٱلصَّلَوٰةِۖ فَهَلۡ أَنتُم مُّنتَهُونَ

Ilivyo ni kwamba, Shetani anataka kuweka uadui na chuki baina yenu kwasababu ya ulevi na kamari, na kukuzuieni kumkumbuka Allah na kuswali. Basi je, mmeacha?



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 95

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَقۡتُلُواْ ٱلصَّيۡدَ وَأَنتُمۡ حُرُمٞۚ وَمَن قَتَلَهُۥ مِنكُم مُّتَعَمِّدٗا فَجَزَآءٞ مِّثۡلُ مَا قَتَلَ مِنَ ٱلنَّعَمِ يَحۡكُمُ بِهِۦ ذَوَا عَدۡلٖ مِّنكُمۡ هَدۡيَۢا بَٰلِغَ ٱلۡكَعۡبَةِ أَوۡ كَفَّـٰرَةٞ طَعَامُ مَسَٰكِينَ أَوۡ عَدۡلُ ذَٰلِكَ صِيَامٗا لِّيَذُوقَ وَبَالَ أَمۡرِهِۦۗ عَفَا ٱللَّهُ عَمَّا سَلَفَۚ وَمَنۡ عَادَ فَيَنتَقِمُ ٱللَّهُ مِنۡهُۚ وَٱللَّهُ عَزِيزٞ ذُو ٱنتِقَامٍ

Enyi mlioamini, msiue wanya-mapori na hali mmeharimia (mmo ndani ya ibada ya Hija au Umra). Na yeyote miongoni mwenu atakayemuua mnyama huyo kwa makusudi, basi malipo (yake) ni (kuchinja) mnyama wa kufuga mfano wa aliyemuua. Watahukumu hayo waadilifu wawili miongoni mwenu. Mnyama (huyo) apelekwe Al-Kaaba (Makkah ili achinjwe huko na nyama yake kugaiwa sadaka kwa maskini wa huko) au kutoa kafara kwa kuwalisha masikini au badala ya hayo ni kufunga ili (aliyefanya kosa hilo la kuwinda) aonje ubaya wa jambo lake (baya alilolifanya). Allah amekwishafuta yaliyopita (lakini) atakayerudia (kufanya tena kosa hilo) Allah atamuadhibu. Na Allah ni Mwenye nguvu sana, Mwenye kutesa



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 97

۞جَعَلَ ٱللَّهُ ٱلۡكَعۡبَةَ ٱلۡبَيۡتَ ٱلۡحَرَامَ قِيَٰمٗا لِّلنَّاسِ وَٱلشَّهۡرَ ٱلۡحَرَامَ وَٱلۡهَدۡيَ وَٱلۡقَلَـٰٓئِدَۚ ذَٰلِكَ لِتَعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِ وَأَنَّ ٱللَّهَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٌ

Allah ameifanya Al-Kaaba, Nyumba Tukufu kuwa tegemeo la watu, na kadhalika (ameifanya) Miezi Mitukufu (tegemeo kwa kusitishwa vita) na wanyama wa hadiyi (dhabihu) waliovikwa koja. (Allah amefanya) Hayo ili mjue kwamba Allah anayajua yaliyomo mbinguni na yaliyomo ardhini, na kwamba Allah ni Mjuzi wa kila kitu



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 98

ٱعۡلَمُوٓاْ أَنَّ ٱللَّهَ شَدِيدُ ٱلۡعِقَابِ وَأَنَّ ٱللَّهَ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Jueni kwamba, Allah ni Mkali wa kuadhibu, na kwamba Allah ni Mwingi wa kusamehe, mwenye kurehemu



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 99

مَّا عَلَى ٱلرَّسُولِ إِلَّا ٱلۡبَلَٰغُۗ وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ مَا تُبۡدُونَ وَمَا تَكۡتُمُونَ

Si juu ya Mtume isipokuwa kufikisha ujumbe tu. Na Allah anajua mnayoyadhihirisha na mnayoyaficha



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 101

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَسۡـَٔلُواْ عَنۡ أَشۡيَآءَ إِن تُبۡدَ لَكُمۡ تَسُؤۡكُمۡ وَإِن تَسۡـَٔلُواْ عَنۡهَا حِينَ يُنَزَّلُ ٱلۡقُرۡءَانُ تُبۡدَ لَكُمۡ عَفَا ٱللَّهُ عَنۡهَاۗ وَٱللَّهُ غَفُورٌ حَلِيمٞ

Enyi mlioamini, msiulize mambo (ambayo) mkidhihirishiwa yanakuchukizeni. Na mkiyauliza wakati Qur’ani inateremshwa mtadhihirishiwa. (Msirudie) Allah ameshayasamehe hayo (mliyokwishauliza). Na Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mpole mno



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 109

۞يَوۡمَ يَجۡمَعُ ٱللَّهُ ٱلرُّسُلَ فَيَقُولُ مَاذَآ أُجِبۡتُمۡۖ قَالُواْ لَا عِلۡمَ لَنَآۖ إِنَّكَ أَنتَ عَلَّـٰمُ ٱلۡغُيُوبِ

Siku Allah atakapowakusanya Mitume na kuwaambia: Mlijibiwa nini? Watasema: Hatujui; hakika Wewe tu ndiye Mjuzi mno wa yote yaliyofichikana



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 116

وَإِذۡ قَالَ ٱللَّهُ يَٰعِيسَى ٱبۡنَ مَرۡيَمَ ءَأَنتَ قُلۡتَ لِلنَّاسِ ٱتَّخِذُونِي وَأُمِّيَ إِلَٰهَيۡنِ مِن دُونِ ٱللَّهِۖ قَالَ سُبۡحَٰنَكَ مَا يَكُونُ لِيٓ أَنۡ أَقُولَ مَا لَيۡسَ لِي بِحَقٍّۚ إِن كُنتُ قُلۡتُهُۥ فَقَدۡ عَلِمۡتَهُۥۚ تَعۡلَمُ مَا فِي نَفۡسِي وَلَآ أَعۡلَمُ مَا فِي نَفۡسِكَۚ إِنَّكَ أَنتَ عَلَّـٰمُ ٱلۡغُيُوبِ

Na (kumbuka) Allah aliposema: Ewe Issa bin Mariamu, hivi wewe uliwaambia watu: Nifanyeni mimi na mama yangu Miungu badala ya Allah? (Issa) akasema: Subhanaka (utakatifu ni wako wewe tu) Haiwi kwangu mimi kusema ambayo si haki yangu (kuyasema). Ikiwa nilisema basi bila ya shaka umekwishayajua. Wewe unayajua yaliyomo ndani ya nafsi yangu, na mimi siyajui yaliyomo katika nafsi yako. Hakika, Wewe ndiye Mjuzi wa yaliyofichikana



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 120

لِلَّهِ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا فِيهِنَّۚ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرُۢ

Ni wa Allah tu ufalme wa mbinguni na ardhini na vilivyomo ndani yake. Na yeye ni Muweza wa kila kitu



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 3

وَهُوَ ٱللَّهُ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَفِي ٱلۡأَرۡضِ يَعۡلَمُ سِرَّكُمۡ وَجَهۡرَكُمۡ وَيَعۡلَمُ مَا تَكۡسِبُونَ

Na yeye ndiye Allah (mwenye haki ya kuabudiwa) mbinguni na ardhini. Anajua mambo yenu ya siri na ya dhahiri na anayajua mnayoyachuma (mnayoyafanya)



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 12

قُل لِّمَن مَّا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۖ قُل لِّلَّهِۚ كَتَبَ عَلَىٰ نَفۡسِهِ ٱلرَّحۡمَةَۚ لَيَجۡمَعَنَّكُمۡ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ لَا رَيۡبَ فِيهِۚ ٱلَّذِينَ خَسِرُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ فَهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ

Sema: Ni vya nani vilivyomo mbinguni na ardhini? Sema: Ni vya Allah. Amejithibitishia rehema. Kwa yakini kabisa, atakukusanyeni Siku ya Kiama isiyokuwa na shaka. Waliozitia hasara nafsi zao, hawaamini



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 13

۞وَلَهُۥ مَا سَكَنَ فِي ٱلَّيۡلِ وَٱلنَّهَارِۚ وَهُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ

Na ni milki yake (Allah) tu vyote vilivyotulia usiku na mchana, na yeye ni Mwenye kusikia, Mjuzi sana



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 18

وَهُوَ ٱلۡقَاهِرُ فَوۡقَ عِبَادِهِۦۚ وَهُوَ ٱلۡحَكِيمُ ٱلۡخَبِيرُ

Na yeye ni Mwenye nguvu juu ya waja wake, na yeye ni Mwenye hekima nyingi, Mwenye habari zote (za kila jambo)



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 19

قُلۡ أَيُّ شَيۡءٍ أَكۡبَرُ شَهَٰدَةٗۖ قُلِ ٱللَّهُۖ شَهِيدُۢ بَيۡنِي وَبَيۡنَكُمۡۚ وَأُوحِيَ إِلَيَّ هَٰذَا ٱلۡقُرۡءَانُ لِأُنذِرَكُم بِهِۦ وَمَنۢ بَلَغَۚ أَئِنَّكُمۡ لَتَشۡهَدُونَ أَنَّ مَعَ ٱللَّهِ ءَالِهَةً أُخۡرَىٰۚ قُل لَّآ أَشۡهَدُۚ قُلۡ إِنَّمَا هُوَ إِلَٰهٞ وَٰحِدٞ وَإِنَّنِي بَرِيٓءٞ مِّمَّا تُشۡرِكُونَ

Sema: Ni kitu gani kikubwa zaidi kwa ushahidi? Sema: Allah ni Shahidi sana baina yangu na baina yenu. Na nimeletewa Wahyi wa hii Qur’ani ili nikuonyeni kwayo na yeyote itakayomfikia. Je, hivi nyinyi, kwa hakika kabisa, mnashuhudia kwamba pamoja na Allah kuna Miungu wengine? Sema: Mimi sishuhudii (hilo). Sema: Hakika ni kwamba, yeye ni Mungu Mmoja tu na mimi simo kwenye yote mnayomshirikisha (nayo Allah)



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 36

۞إِنَّمَا يَسۡتَجِيبُ ٱلَّذِينَ يَسۡمَعُونَۘ وَٱلۡمَوۡتَىٰ يَبۡعَثُهُمُ ٱللَّهُ ثُمَّ إِلَيۡهِ يُرۡجَعُونَ

Ilivyo ni kwamba, wanaoitika (wito) ni wale tu wanaosikia (usikivu wa mazingatio). Na wafu (wa nyoyo ambao ni makafiri) Allah atawafufua, kisha kwake tu watarudishwa



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 37

وَقَالُواْ لَوۡلَا نُزِّلَ عَلَيۡهِ ءَايَةٞ مِّن رَّبِّهِۦۚ قُلۡ إِنَّ ٱللَّهَ قَادِرٌ عَلَىٰٓ أَن يُنَزِّلَ ءَايَةٗ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Na walisema: (ingekuwa vizuri) lau kama (Mtume Muhammad) angeteremshiwa Aya (Muujiza) kutoka kwa Mola wake. Sema: Hakika, Allah ni mwenye uwezo wa kuteremsha Aya (Muujiza wanaoutaka) lakini wengi wao hawajui (kitakachowakuta kama wakiteremshiwa muujiza na wasiamini)



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 54

وَإِذَا جَآءَكَ ٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِـَٔايَٰتِنَا فَقُلۡ سَلَٰمٌ عَلَيۡكُمۡۖ كَتَبَ رَبُّكُمۡ عَلَىٰ نَفۡسِهِ ٱلرَّحۡمَةَ أَنَّهُۥ مَنۡ عَمِلَ مِنكُمۡ سُوٓءَۢا بِجَهَٰلَةٖ ثُمَّ تَابَ مِنۢ بَعۡدِهِۦ وَأَصۡلَحَ فَأَنَّهُۥ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Na watakapokujia wale wanao-ziamini Aya zetu sema (uwaambie): Amani iwe kwenu. Mola wenu mwenyewe rehema amejithibitishia kwamba, yeyote miongoni mwenu atakayefanya jambo ovu kwa kutojua, kisha baada yake akatubu na kurekebisha (tabia yake) basi hakika yeye (Allah) ni Msamehevu sana, Mwenye kurehemu



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 59

۞وَعِندَهُۥ مَفَاتِحُ ٱلۡغَيۡبِ لَا يَعۡلَمُهَآ إِلَّا هُوَۚ وَيَعۡلَمُ مَا فِي ٱلۡبَرِّ وَٱلۡبَحۡرِۚ وَمَا تَسۡقُطُ مِن وَرَقَةٍ إِلَّا يَعۡلَمُهَا وَلَا حَبَّةٖ فِي ظُلُمَٰتِ ٱلۡأَرۡضِ وَلَا رَطۡبٖ وَلَا يَابِسٍ إِلَّا فِي كِتَٰبٖ مُّبِينٖ

Na ziko kwake yeye (Allah) tu funguo (hazina) za Ghaibu; hakuna azijuaye isipokuwa yeye tu. Na anajua kilichopo nchi kavu na baharini. Na halidondoki jani lolote ila analijua. Na (haidondoka) punje yoyote katika giza la ardhini na kibichi na kikavu isipokuwa kipo katika kitabu kinachobainisha (kila kitu)



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 60

وَهُوَ ٱلَّذِي يَتَوَفَّىٰكُم بِٱلَّيۡلِ وَيَعۡلَمُ مَا جَرَحۡتُم بِٱلنَّهَارِ ثُمَّ يَبۡعَثُكُمۡ فِيهِ لِيُقۡضَىٰٓ أَجَلٞ مُّسَمّٗىۖ ثُمَّ إِلَيۡهِ مَرۡجِعُكُمۡ ثُمَّ يُنَبِّئُكُم بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Na yeye (Allah) ndiye ambaye anakufisheni usiku (anakutieni katika usingizi) na anajua mliyoyafanya mchana. Kisha atakufufueni humo (katika mchana) ili utimizwe muda uliowekwa. Kisha kwake tu ndio marejeo yenu, kisha atakupeni habari ya yote mliyokuwa mnayafanya



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 61

وَهُوَ ٱلۡقَاهِرُ فَوۡقَ عِبَادِهِۦۖ وَيُرۡسِلُ عَلَيۡكُمۡ حَفَظَةً حَتَّىٰٓ إِذَا جَآءَ أَحَدَكُمُ ٱلۡمَوۡتُ تَوَفَّتۡهُ رُسُلُنَا وَهُمۡ لَا يُفَرِّطُونَ

Na yeye tu ndiye Mwenye nguvu kubwa juu ya waja wake, na anatuma kwenu (Malaika) waangalizi (wanaowalinda binadamu na kutunza kumbukumbu za matendo yao)[1], mpaka kinapomfikia mmoja wenu kifo wajumbe wetu wanamfisha, na hawafanyi uzembe


1- - Rejea Aya ya 11, Sura Arraad (13).


Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 65

قُلۡ هُوَ ٱلۡقَادِرُ عَلَىٰٓ أَن يَبۡعَثَ عَلَيۡكُمۡ عَذَابٗا مِّن فَوۡقِكُمۡ أَوۡ مِن تَحۡتِ أَرۡجُلِكُمۡ أَوۡ يَلۡبِسَكُمۡ شِيَعٗا وَيُذِيقَ بَعۡضَكُم بَأۡسَ بَعۡضٍۗ ٱنظُرۡ كَيۡفَ نُصَرِّفُ ٱلۡأٓيَٰتِ لَعَلَّهُمۡ يَفۡقَهُونَ

Sema: Yeye tu ndiye Muweza wa kuleta kwenu adhabu itokayo juu yenu au chini ya miguu yenu, au kukuvalisheni nguo ya mfarakano wa makundi na kukuonjesheni mkong’oto wa (nguvu za) wengine. Ona, namna tunavyozifafanua Aya (hoja) ili wapate kufahamu



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 71

قُلۡ أَنَدۡعُواْ مِن دُونِ ٱللَّهِ مَا لَا يَنفَعُنَا وَلَا يَضُرُّنَا وَنُرَدُّ عَلَىٰٓ أَعۡقَابِنَا بَعۡدَ إِذۡ هَدَىٰنَا ٱللَّهُ كَٱلَّذِي ٱسۡتَهۡوَتۡهُ ٱلشَّيَٰطِينُ فِي ٱلۡأَرۡضِ حَيۡرَانَ لَهُۥٓ أَصۡحَٰبٞ يَدۡعُونَهُۥٓ إِلَى ٱلۡهُدَى ٱئۡتِنَاۗ قُلۡ إِنَّ هُدَى ٱللَّهِ هُوَ ٱلۡهُدَىٰۖ وَأُمِرۡنَا لِنُسۡلِمَ لِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Sema: Hivi tuwaombe (tuwaa-budu) badala ya Allah (Miungu) ambao hawatunufaishi na hawatudhuru na turudishwe nyuma (kwenye itikadi potofu tulizokwisha ziacha) baada ya Allah kutuongoa kama yule ambaye mashetani wamempagawisha katika ardhi, akiduwaa, akiwa na marafiki wanaomuita aende katika uongofu (wakimwambia): Njoo kwetu?[1] Sema: Hakika, muongozo wa Allah ndio uongofu, na tumeamrishwa tujisalimishe kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote


1- - Aya hapa inamtaka Muumini kuwa na msimamo imara na thabiti katika Imani na itikadi yake. Hatakiwi kuyumba au kuyumbishwa. Sio kila analolisikia au kuliona au kushawishiwa alifuate.


Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 73

وَهُوَ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ بِٱلۡحَقِّۖ وَيَوۡمَ يَقُولُ كُن فَيَكُونُۚ قَوۡلُهُ ٱلۡحَقُّۚ وَلَهُ ٱلۡمُلۡكُ يَوۡمَ يُنفَخُ فِي ٱلصُّورِۚ عَٰلِمُ ٱلۡغَيۡبِ وَٱلشَّهَٰدَةِۚ وَهُوَ ٱلۡحَكِيمُ ٱلۡخَبِيرُ

Na yeye ndiye aliyeumba mbingu na ardhi kwa haki. Na (kumbuka) siku (Allah) anaposema (kuliambia jambo): Kuwa, basi linakuwa. Kauli yake ni haki. Ni wake yeye tu ufalme siku litakapopulizwa baragumu. Ni mjuzi wa Ghaibu (yaliyofichika) na yaliyo bayana. Na yeye ni Mwenye hekima, Mjuzi wa habari (zote)



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 80

وَحَآجَّهُۥ قَوۡمُهُۥۚ قَالَ أَتُحَـٰٓجُّوٓنِّي فِي ٱللَّهِ وَقَدۡ هَدَىٰنِۚ وَلَآ أَخَافُ مَا تُشۡرِكُونَ بِهِۦٓ إِلَّآ أَن يَشَآءَ رَبِّي شَيۡـٔٗاۚ وَسِعَ رَبِّي كُلَّ شَيۡءٍ عِلۡمًاۚ أَفَلَا تَتَذَكَّرُونَ

Na watu wake wakamuwekea mdahalo. Alisema: Hivi, mnanihoji kuhusu Allah, na ilhali ameniongoa? Na siwaogopi hao mnaowashirikisha naye, isipokuwa kama Mola wangu atapenda jambo lolote (linipate). Mola wangu anajua kila kitu kwa mapana na marefu. Hivi hamuonyeki (na haya ninayokuambieni)?



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 102

ذَٰلِكُمُ ٱللَّهُ رَبُّكُمۡۖ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۖ خَٰلِقُ كُلِّ شَيۡءٖ فَٱعۡبُدُوهُۚ وَهُوَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ وَكِيلٞ

Huyo Ndiye Allah, Mola wenu Mlezi. Hakuna mwenye haki ya kuabudiwa ila yeye tu, Muumba wa kila kitu. Basi muabudini. Na yeye ni Msimamizi mzuri sana wa kila kitu



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 103

لَّا تُدۡرِكُهُ ٱلۡأَبۡصَٰرُ وَهُوَ يُدۡرِكُ ٱلۡأَبۡصَٰرَۖ وَهُوَ ٱللَّطِيفُ ٱلۡخَبِيرُ

Macho hayamuoni (hapa duniani) na yeye anayaona macho[1]. Na yeye ni Mpole sana, Mwenye habari (za kila kitu)


1- - Itikadi ya Watu wa Suna na Jamaa (Suni) ni kwamba, Allah haonekani hapa duniani kwa mujibu wa Aya hii na pia kwa mujibu wa: 1) Nukuu ya Mama Aisha mke wa Mtume aliyenukuliwa akisema kuwa: “Anayedai kuwa Muhammad alimuona Mola wake hakika amesema uongo”. 2) Aya ya 143 ya Sura Al-aaraaf (7) ambapo Mtume Musa alimuomba Mola wake amuwezeshe kumuona na ikashindikana. Ama Akhera Allah ataonekana kwa mujibu wa: 1) Aya ya 23 ya Sura Alqiyama (75). 2) Aya ya 15 ya Sura Almutwaffifiin (83) inayoeleza kuwa makafiri Siku ya Kiama watazuiwa kumuona Mola wao. Amesema Imamu Shaafii katika kuitafsiri Aya hii kwamba, hii inaonesha kuwa Waumini hawatazuiwa kumuona Mola wao.


Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 106

ٱتَّبِعۡ مَآ أُوحِيَ إِلَيۡكَ مِن رَّبِّكَۖ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَۖ وَأَعۡرِضۡ عَنِ ٱلۡمُشۡرِكِينَ

Fuata yale yote uliyoletewa Wahyi kutoka kwa Mola wako. Hakuna mwenye haki ya kuabudiwa isipokuwa yeye tu, na wapuuze washirikina[1]


1- - Hukumu ya Aya hii imefutwa na Aya 5 ya Sura Attauba (9).


Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 117

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ مَن يَضِلُّ عَن سَبِيلِهِۦۖ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُهۡتَدِينَ

Kwa hakika, Mola wako Mlezi ndiye tu amjuae zaidi aliyepotea katika njia yake, na yeye ndiye awajuae zaidi wenye kuongoka



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 119

وَمَا لَكُمۡ أَلَّا تَأۡكُلُواْ مِمَّا ذُكِرَ ٱسۡمُ ٱللَّهِ عَلَيۡهِ وَقَدۡ فَصَّلَ لَكُم مَّا حَرَّمَ عَلَيۡكُمۡ إِلَّا مَا ٱضۡطُرِرۡتُمۡ إِلَيۡهِۗ وَإِنَّ كَثِيرٗا لَّيُضِلُّونَ بِأَهۡوَآئِهِم بِغَيۡرِ عِلۡمٍۚ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِٱلۡمُعۡتَدِينَ

Na mna kikwazo gani nyinyi hamli miongoni mwa vilivyotajiwa jina la Allah na ilhali amekufafanulieni vile alivyokuharamishieni[1], isipokuwa vile mlivyolazimika kwa dharura? Na kwa hakika, wengi wanapotea kwa sababu ya utashi wa nafsi zao bila ya elimu. Kwa hakika, Mola wako Mlezi anawajua zaidi wanaovuka mipaka


1- - Rejea Aya ya 3 ya Sura Almaida (5).