Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 247

وَقَالَ لَهُمۡ نَبِيُّهُمۡ إِنَّ ٱللَّهَ قَدۡ بَعَثَ لَكُمۡ طَالُوتَ مَلِكٗاۚ قَالُوٓاْ أَنَّىٰ يَكُونُ لَهُ ٱلۡمُلۡكُ عَلَيۡنَا وَنَحۡنُ أَحَقُّ بِٱلۡمُلۡكِ مِنۡهُ وَلَمۡ يُؤۡتَ سَعَةٗ مِّنَ ٱلۡمَالِۚ قَالَ إِنَّ ٱللَّهَ ٱصۡطَفَىٰهُ عَلَيۡكُمۡ وَزَادَهُۥ بَسۡطَةٗ فِي ٱلۡعِلۡمِ وَٱلۡجِسۡمِۖ وَٱللَّهُ يُؤۡتِي مُلۡكَهُۥ مَن يَشَآءُۚ وَٱللَّهُ وَٰسِعٌ عَلِيمٞ

Na Nabii wao akawaambia: Hakika Allah ameshakuteulieni Twaluti kuwa Mfalme. Wakasema: Anawezaje kuwa Mfalme wetu, na ilhali sisi tuna haki zaidi ya Ufalme kuliko yeye, na wala hakupewa wasaa wa mali? Akasema: Hakika Allah ameshakuteulieni na amemzidishia wasaa wa elimu na mwili. Na Allah humpa Ufalme wake amtakaye na Allah ni Mwenye wasaa, Mjuzi mno



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 248

وَقَالَ لَهُمۡ نَبِيُّهُمۡ إِنَّ ءَايَةَ مُلۡكِهِۦٓ أَن يَأۡتِيَكُمُ ٱلتَّابُوتُ فِيهِ سَكِينَةٞ مِّن رَّبِّكُمۡ وَبَقِيَّةٞ مِّمَّا تَرَكَ ءَالُ مُوسَىٰ وَءَالُ هَٰرُونَ تَحۡمِلُهُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗ لَّكُمۡ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ

Na Nabii wao akawaambia: “Hakika alama ya ufalme wake nikukuleteeni sanduku ambalo ndani yake kuna kitulizacho nyoyo zenu kitokacho kwa Mola wenu na mabaki ya yale waliyoyaacha watu wa Musa na watu wa Haruni linalobebwa na Malaika. Bila shaka katika hayo mna dalili kwenu ikiwa ninyi ni waumini



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 249

فَلَمَّا فَصَلَ طَالُوتُ بِٱلۡجُنُودِ قَالَ إِنَّ ٱللَّهَ مُبۡتَلِيكُم بِنَهَرٖ فَمَن شَرِبَ مِنۡهُ فَلَيۡسَ مِنِّي وَمَن لَّمۡ يَطۡعَمۡهُ فَإِنَّهُۥ مِنِّيٓ إِلَّا مَنِ ٱغۡتَرَفَ غُرۡفَةَۢ بِيَدِهِۦۚ فَشَرِبُواْ مِنۡهُ إِلَّا قَلِيلٗا مِّنۡهُمۡۚ فَلَمَّا جَاوَزَهُۥ هُوَ وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ مَعَهُۥ قَالُواْ لَا طَاقَةَ لَنَا ٱلۡيَوۡمَ بِجَالُوتَ وَجُنُودِهِۦۚ قَالَ ٱلَّذِينَ يَظُنُّونَ أَنَّهُم مُّلَٰقُواْ ٱللَّهِ كَم مِّن فِئَةٖ قَلِيلَةٍ غَلَبَتۡ فِئَةٗ كَثِيرَةَۢ بِإِذۡنِ ٱللَّهِۗ وَٱللَّهُ مَعَ ٱلصَّـٰبِرِينَ

Basi Twaluti alipoondoka na majeshi alisema: Hakika Allah atakufanyieni mtihani kwa mto, basi atakayekunywa humo si pamoja nami, na asiye yanywa bila shaka yupo pamoja nami, ila atakayeteka kiasi cha kiganja cha mkono wake. Basi walikunywa humo isipokuwa wachache miongoni mwao. Basi alipovuka yeye na walioamini pamoja naye, walisema: Leo hatumuwezi Jaluti na majeshi yake. Wakasema: wale ambao wana yakini ya kukutana na Allah: Makundi mangapi machache yameyashinda makundi mengi kwa idhini ya Allah? Na Allah yupo pamoja na wafanyao subira