Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 115

إِنۡ أَنَا۠ إِلَّا نَذِيرٞ مُّبِينٞ

Mimi si chochote ila ni Muonyaji wa dhahiri



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 116

قَالُواْ لَئِن لَّمۡ تَنتَهِ يَٰنُوحُ لَتَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡمَرۡجُومِينَ

Wakasema: Ikiwa huachi, ewe Nuhu, bila ya shaka utapigwa mawe



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 117

قَالَ رَبِّ إِنَّ قَوۡمِي كَذَّبُونِ

Akasema: Mola wangu Mlezi! Hakika watu wangu wamenikanusha



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 118

فَٱفۡتَحۡ بَيۡنِي وَبَيۡنَهُمۡ فَتۡحٗا وَنَجِّنِي وَمَن مَّعِيَ مِنَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Basi hukumu baina yangu na wao kwa hukumu yako, na uniokoe mimi na walio pamoja nami, Waumini



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 119

فَأَنجَيۡنَٰهُ وَمَن مَّعَهُۥ فِي ٱلۡفُلۡكِ ٱلۡمَشۡحُونِ

Kwahivyo tukamwokoa yeye na walio kuwa pamoja naye katika marikebu iliyo sheheni



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 120

ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا بَعۡدُ ٱلۡبَاقِينَ

Kisha tukawazamisha baadaye walio bakia



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 121

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Hakika katika hayo ipo ishara, lakini si wengi wao waliokuwa waumini



Capítulo: ASH-SHUARAA 

Verso : 122

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Na hakika Mola wako Mlezi ndiye Yeye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu



Capítulo: AL-ANKABUUT 

Verso : 14

وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوۡمِهِۦ فَلَبِثَ فِيهِمۡ أَلۡفَ سَنَةٍ إِلَّا خَمۡسِينَ عَامٗا فَأَخَذَهُمُ ٱلطُّوفَانُ وَهُمۡ ظَٰلِمُونَ

Na hakika tulimtuma Nuhu kwa watu wake, na akakaa nao miaka elfu kasoro miaka khamsini. Basi tufani liliwachukua, nao ni madhaalimu



Capítulo: AL-ANKABUUT 

Verso : 15

فَأَنجَيۡنَٰهُ وَأَصۡحَٰبَ ٱلسَّفِينَةِ وَجَعَلۡنَٰهَآ ءَايَةٗ لِّلۡعَٰلَمِينَ

Nasi tukamwokoa yeye na wenzie katika safina, na tukaifanya kuwa ni Ishara kwa walimwengu wote



Capítulo: AL-AHZAAB 

Verso : 7

وَإِذۡ أَخَذۡنَا مِنَ ٱلنَّبِيِّـۧنَ مِيثَٰقَهُمۡ وَمِنكَ وَمِن نُّوحٖ وَإِبۡرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ وَعِيسَى ٱبۡنِ مَرۡيَمَۖ وَأَخَذۡنَا مِنۡهُم مِّيثَٰقًا غَلِيظٗا

Na tulipo chukua ahadi kwa Manabii na kwako wewe, na Nuhu na Ibrahim na Isa mwana wa Mariamu, na tulichukua kwao ahadi ngumu,



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 75

وَلَقَدۡ نَادَىٰنَا نُوحٞ فَلَنِعۡمَ ٱلۡمُجِيبُونَ

Na hakika Nuhu alituita, na Sisi ni bora wa waitikiaji



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 76

وَنَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥ مِنَ ٱلۡكَرۡبِ ٱلۡعَظِيمِ

Na tulimwokoa yeye na watu wake kutokana na msiba mkubwa



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 77

وَجَعَلۡنَا ذُرِّيَّتَهُۥ هُمُ ٱلۡبَاقِينَ

Na tuliwajaalia dhuriya zake (watoto wake) ndio wenye kubakia



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 78

وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ

Na tukamwachia (sifa njema) kwa walio kuja baadaye



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 79

سَلَٰمٌ عَلَىٰ نُوحٖ فِي ٱلۡعَٰلَمِينَ

Iwe salama kwa Nuhu ulimwenguni kote!



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 80

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Kwa hakika hivi ndivyo tunavyo walipa wanao fanya mema



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 81

إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini



Capítulo: ASSWAAFFAAT 

Verso : 82

ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ

Kisha tukawazamisha wale wengine



Capítulo: ASH-SHUURAA 

Verso : 13

۞شَرَعَ لَكُم مِّنَ ٱلدِّينِ مَا وَصَّىٰ بِهِۦ نُوحٗا وَٱلَّذِيٓ أَوۡحَيۡنَآ إِلَيۡكَ وَمَا وَصَّيۡنَا بِهِۦٓ إِبۡرَٰهِيمَ وَمُوسَىٰ وَعِيسَىٰٓۖ أَنۡ أَقِيمُواْ ٱلدِّينَ وَلَا تَتَفَرَّقُواْ فِيهِۚ كَبُرَ عَلَى ٱلۡمُشۡرِكِينَ مَا تَدۡعُوهُمۡ إِلَيۡهِۚ ٱللَّهُ يَجۡتَبِيٓ إِلَيۡهِ مَن يَشَآءُ وَيَهۡدِيٓ إِلَيۡهِ مَن يُنِيبُ

Amekuamrisheni Dini ile ile aliyo muusia Nuhu na tuliyo kufunulia wewe, na tuliyo wausia Ibrahim na Mussa na Issa, kwamba shikeni Dini wala msifarakane kwayo. Ni magumu kwa washirikina hayo unayo waitia. Allah humteua amtakaye, na humwongoa aelekeaye



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 9

۞كَذَّبَتۡ قَبۡلَهُمۡ قَوۡمُ نُوحٖ فَكَذَّبُواْ عَبۡدَنَا وَقَالُواْ مَجۡنُونٞ وَٱزۡدُجِرَ

Walikadhibisha kabla yao watu wa nuhu na wakamkadhibisha mja wetu wakasema mwendawazimu na akafanyiwa maudhi



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 10

فَدَعَا رَبَّهُۥٓ أَنِّي مَغۡلُوبٞ فَٱنتَصِرۡ

Basi akamwita Mola wake mlezi kwamba: Hakika mimi nimeshindwa (nimezidiwa nguvu) basi ni Nusuru



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 11

فَفَتَحۡنَآ أَبۡوَٰبَ ٱلسَّمَآءِ بِمَآءٖ مُّنۡهَمِرٖ

Tukafungua milango ya mbingu kwa maji yanayofoka na kumiminika kwa nguvu



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 12

وَفَجَّرۡنَا ٱلۡأَرۡضَ عُيُونٗا فَٱلۡتَقَى ٱلۡمَآءُ عَلَىٰٓ أَمۡرٖ قَدۡ قُدِرَ

Na tukaipasua ardhi yote kwa chemchem, na yakakutana maji kwa pamoja kwa jambo lililokadiriwa



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 13

وَحَمَلۡنَٰهُ عَلَىٰ ذَاتِ أَلۡوَٰحٖ وَدُسُرٖ

Na Tukambeba kwenye ile (jahazi) yenye mbao na misumari



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 14

تَجۡرِي بِأَعۡيُنِنَا جَزَآءٗ لِّمَن كَانَ كُفِرَ

Kikienda haraka tukikitazama kwa macho yetu ikiwa ni malipo kwa ambaye alikuwa amekufuru



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 15

وَلَقَد تَّرَكۡنَٰهَآ ءَايَةٗ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ

Na kwa yakini Tumeiacha iwe ni mazingatio, Je, basi yuko yeyote mwenye kuwaidhika?



Capítulo: AL-HADIID

Verso : 26

وَلَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا نُوحٗا وَإِبۡرَٰهِيمَ وَجَعَلۡنَا فِي ذُرِّيَّتِهِمَا ٱلنُّبُوَّةَ وَٱلۡكِتَٰبَۖ فَمِنۡهُم مُّهۡتَدٖۖ وَكَثِيرٞ مِّنۡهُمۡ فَٰسِقُونَ

Na hakika tulimpeleka Nuhu na Ibrahim na tukajaalia kwenye kizazi chao Mitume na Vitabu. Basi miongoni mwao kuna waliyoongoka na wengi kati yao mafasiki



Capítulo: NUUH 

Verso : 1

إِنَّآ أَرۡسَلۡنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوۡمِهِۦٓ أَنۡ أَنذِرۡ قَوۡمَكَ مِن قَبۡلِ أَن يَأۡتِيَهُمۡ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Hakika, Sisi Tulimtuma Nuhu kwa watu wake (tukamwambia) kwamba: Waonye watu wako kabla haijawafikia adhabu iumizayo sana



Capítulo: NUUH 

Verso : 2

قَالَ يَٰقَوۡمِ إِنِّي لَكُمۡ نَذِيرٞ مُّبِينٌ

(Nuhu) Akasema: Enyi watu wangu, hakika mimi kwenu ni muonyaji wa dhahiri (wa wazi) kwenu