Capítulo: SWAAD 

Verso : 59

هَٰذَا فَوۡجٞ مُّقۡتَحِمٞ مَّعَكُمۡ لَا مَرۡحَبَۢا بِهِمۡۚ إِنَّهُمۡ صَالُواْ ٱلنَّارِ

Hili ndilo kundi litakalo ingia pamoja nanyi. Hapana makaribisho mema kwao. Hakika hao wanaingia Motoni



Capítulo: SWAAD 

Verso : 60

قَالُواْ بَلۡ أَنتُمۡ لَا مَرۡحَبَۢا بِكُمۡۖ أَنتُمۡ قَدَّمۡتُمُوهُ لَنَاۖ فَبِئۡسَ ٱلۡقَرَارُ

Waseme: Lakini nyinyi! Hamna mapokezi mazuri! Nyinyi ndio mlio tusababishia haya, napo ni pahala pabaya kabisa!



Capítulo: SWAAD 

Verso : 61

قَالُواْ رَبَّنَا مَن قَدَّمَ لَنَا هَٰذَا فَزِدۡهُ عَذَابٗا ضِعۡفٗا فِي ٱلنَّارِ

Waseme: Mola wetu Mlezi! Aliye tusababishia haya mzidishie adhabu mara mbili Motoni



Capítulo: SWAAD 

Verso : 62

وَقَالُواْ مَا لَنَا لَا نَرَىٰ رِجَالٗا كُنَّا نَعُدُّهُم مِّنَ ٱلۡأَشۡرَارِ

Watasema: Tuna nini hata hatuwaoni wale watu ambao tukiwahesabu ndio katika waovu?



Capítulo: SWAAD 

Verso : 63

أَتَّخَذۡنَٰهُمۡ سِخۡرِيًّا أَمۡ زَاغَتۡ عَنۡهُمُ ٱلۡأَبۡصَٰرُ

Tulikosea tulipo wafanyia mas-khara, au macho yetu tu hayawaoni?



Capítulo: SWAAD 

Verso : 64

إِنَّ ذَٰلِكَ لَحَقّٞ تَخَاصُمُ أَهۡلِ ٱلنَّارِ

Hakika hayo bila ya shaka ndiyo makhasimiano ya watu wa Motoni



Capítulo: GHAAFIR 

Verso : 6

وَكَذَٰلِكَ حَقَّتۡ كَلِمَتُ رَبِّكَ عَلَى ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ أَنَّهُمۡ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِ

Namna hivi limewathibitikia makafiri neno la Mola wako Mlezi ya kwamba wao ni watu wa Motoni



Capítulo: GHAAFIR 

Verso : 46

ٱلنَّارُ يُعۡرَضُونَ عَلَيۡهَا غُدُوّٗا وَعَشِيّٗاۚ وَيَوۡمَ تَقُومُ ٱلسَّاعَةُ أَدۡخِلُوٓاْ ءَالَ فِرۡعَوۡنَ أَشَدَّ ٱلۡعَذَابِ

Wanaonyeshwa Moto asubuhi na jioni. Na itakapofika Saa ya Kiyama patasemwa: Waingizeni watu wa Firauni katika adhabu kali kabisa!



Capítulo: GHAAFIR 

Verso : 47

وَإِذۡ يَتَحَآجُّونَ فِي ٱلنَّارِ فَيَقُولُ ٱلضُّعَفَـٰٓؤُاْ لِلَّذِينَ ٱسۡتَكۡبَرُوٓاْ إِنَّا كُنَّا لَكُمۡ تَبَعٗا فَهَلۡ أَنتُم مُّغۡنُونَ عَنَّا نَصِيبٗا مِّنَ ٱلنَّارِ

Na watakapo hojiana huko Motoni, wanyonge watawaambia walio jitukuza: Hakika sisi tulikuwa wafuasi wenu, basi je, hamtuondolei sehemu ya huu Moto?



Capítulo: GHAAFIR 

Verso : 48

قَالَ ٱلَّذِينَ ٱسۡتَكۡبَرُوٓاْ إِنَّا كُلّٞ فِيهَآ إِنَّ ٱللَّهَ قَدۡ حَكَمَ بَيۡنَ ٱلۡعِبَادِ

Watasema walio jitukuza: Hakika sote sisi tumo humo humo! Kwani Allah ameshahukumu baina ya waja!



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 74

إِنَّ ٱلۡمُجۡرِمِينَ فِي عَذَابِ جَهَنَّمَ خَٰلِدُونَ

Kwa hakika wakosefu watakaa katika adhabu ya Jahannamu



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 75

لَا يُفَتَّرُ عَنۡهُمۡ وَهُمۡ فِيهِ مُبۡلِسُونَ

Hawatapumzishwa nayo, na humo watakata tamaa



Capítulo: AZZUKHRUF 

Verso : 76

وَمَا ظَلَمۡنَٰهُمۡ وَلَٰكِن كَانُواْ هُمُ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Wala Sisi hatukuwadhulumu, bali wao ndio walio kuwa madhalimu



Capítulo: QAAF 

Verso : 24

أَلۡقِيَا فِي جَهَنَّمَ كُلَّ كَفَّارٍ عَنِيدٖ

(Allaah Atasema): Mtupeni katika Jahannam kila kafiri, mkaidi!



Capítulo: QAAF 

Verso : 25

مَّنَّاعٖ لِّلۡخَيۡرِ مُعۡتَدٖ مُّرِيبٍ

Mzuiaji wa kheri, mwenye kuruka mipaka, mwenye kutia shaka



Capítulo: QAAF 

Verso : 26

ٱلَّذِي جَعَلَ مَعَ ٱللَّهِ إِلَٰهًا ءَاخَرَ فَأَلۡقِيَاهُ فِي ٱلۡعَذَابِ ٱلشَّدِيدِ

Ambaye amefanya mwabudiwa mwengine pamoja na Allah, basi mtupeni katika adhabu kali



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 47

إِنَّ ٱلۡمُجۡرِمِينَ فِي ضَلَٰلٖ وَسُعُرٖ

Hakika wahalifu wamo katika upotofu na wazimu



Capítulo: AL-QAMAR

Verso : 48

يَوۡمَ يُسۡحَبُونَ فِي ٱلنَّارِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمۡ ذُوقُواْ مَسَّ سَقَرَ

Siku watakayoburutwa motoni kifudi fudi, Waambiwe: Onjeni mguso wa moto mkali mno



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 41

وَأَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ مَآ أَصۡحَٰبُ ٱلشِّمَالِ

Na watu wa kushotoni, je, ni wepi watu wa kushotoni?



Capítulo: AL-WAAQIA’H 

Verso : 42

فِي سَمُومٖ وَحَمِيمٖ

(Watakuwa) Kwenye moto ubabuao na maji yachemkayo



Capítulo: ALJINN 

Verso : 15

وَأَمَّا ٱلۡقَٰسِطُونَ فَكَانُواْ لِجَهَنَّمَ حَطَبٗا

Na ama wanaoacha haki, hao watakuwa kuni za Moto wa Jahannamu



Capítulo: ALJINN 

Verso : 23

إِلَّا بَلَٰغٗا مِّنَ ٱللَّهِ وَرِسَٰلَٰتِهِۦۚ وَمَن يَعۡصِ ٱللَّهَ وَرَسُولَهُۥ فَإِنَّ لَهُۥ نَارَ جَهَنَّمَ خَٰلِدِينَ فِيهَآ أَبَدًا

Isipokuwa nifikishe Ujumbe utokao kwa Allah, na ujumbe wake. Na wenye kumuasi Allah na Mtume wake, basi hakika hao watapata Moto wa Jahannamu wadumu humo milele



Capítulo: ANNAAZIAAT 

Verso : 37

فَأَمَّا مَن طَغَىٰ

Basi yule aliyepindukia mipaka na kuasi



Capítulo: ANNAAZIAAT 

Verso : 38

وَءَاثَرَ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا

Na akapenda zaidi maisha ya dunia



Capítulo: ANNAAZIAAT 

Verso : 39

فَإِنَّ ٱلۡجَحِيمَ هِيَ ٱلۡمَأۡوَىٰ

Kwa hakika Jahannamu ndiyo makaazi yake!



Capítulo: AL-BURUJI 

Verso : 10

إِنَّ ٱلَّذِينَ فَتَنُواْ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتِ ثُمَّ لَمۡ يَتُوبُواْ فَلَهُمۡ عَذَابُ جَهَنَّمَ وَلَهُمۡ عَذَابُ ٱلۡحَرِيقِ

Hakika walio wafitini Waumini wanaume na Waumini wanawake, kisha hawakutubu, basi watapata adhabu ya Jahannamu na watapata adhabu ya kuungua



Capítulo: AL-BAYYINAH 

Verso : 6

إِنَّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ وَٱلۡمُشۡرِكِينَ فِي نَارِ جَهَنَّمَ خَٰلِدِينَ فِيهَآۚ أُوْلَـٰٓئِكَ هُمۡ شَرُّ ٱلۡبَرِيَّةِ

Hakika walio kufuru miongoni mwa Watu wa Kitabu na washirikina wataingia katika Moto wa Jahannamu wadumu milele humo. Hao ndio viumbe waovu kabisa



Capítulo: AL-QAARIAH 

Verso : 8

وَأَمَّا مَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ

Na yule ambaye mizani yake itakuwa khafifu,



Capítulo: AL-QAARIAH 

Verso : 9

فَأُمُّهُۥ هَاوِيَةٞ

Huyo maskani yake yatakuwa Moto wa Hawiya!



Capítulo: AL-QAARIAH 

Verso : 10

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا هِيَهۡ

Na nini kitacho kujuilisha nini hiyo?