Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 22

ٱلَّذِي جَعَلَ لَكُمُ ٱلۡأَرۡضَ فِرَٰشٗا وَٱلسَّمَآءَ بِنَآءٗ وَأَنزَلَ مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ فَأَخۡرَجَ بِهِۦ مِنَ ٱلثَّمَرَٰتِ رِزۡقٗا لَّكُمۡۖ فَلَا تَجۡعَلُواْ لِلَّهِ أَندَادٗا وَأَنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Ambaye amekuumbieni ardhi ikiwa imetandazwa, na mbingu ikiwa sakafu na ameteremsha kutoka mawinguni maji (mvua), akatoa kwa maji hayo riziki zenu kutoka kwenye matunda. Basi msimfanyie Allah washirika ilihali mnajua (kuwa Allah hana mshirika)



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 29

هُوَ ٱلَّذِي خَلَقَ لَكُم مَّا فِي ٱلۡأَرۡضِ جَمِيعٗا ثُمَّ ٱسۡتَوَىٰٓ إِلَى ٱلسَّمَآءِ فَسَوَّىٰهُنَّ سَبۡعَ سَمَٰوَٰتٖۚ وَهُوَ بِكُلِّ شَيۡءٍ عَلِيمٞ

Ni yeye tu aliye kuumbieni vyote vilivyomo ardhini. Kisha akakusudia mbingu na kuziumba zikiwa mbingu saba zilizo sawa. Na yeye ni mjuzi wa kila kitu



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 255

ٱللَّهُ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ ٱلۡحَيُّ ٱلۡقَيُّومُۚ لَا تَأۡخُذُهُۥ سِنَةٞ وَلَا نَوۡمٞۚ لَّهُۥ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِۗ مَن ذَا ٱلَّذِي يَشۡفَعُ عِندَهُۥٓ إِلَّا بِإِذۡنِهِۦۚ يَعۡلَمُ مَا بَيۡنَ أَيۡدِيهِمۡ وَمَا خَلۡفَهُمۡۖ وَلَا يُحِيطُونَ بِشَيۡءٖ مِّنۡ عِلۡمِهِۦٓ إِلَّا بِمَا شَآءَۚ وَسِعَ كُرۡسِيُّهُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَۖ وَلَا يَـُٔودُهُۥ حِفۡظُهُمَاۚ وَهُوَ ٱلۡعَلِيُّ ٱلۡعَظِيمُ

Allah, hakuna anayestahiki kuabudiwa isipokuwa Yeye tu. Yeye ndiye Mwenye uhai wa milele, Mwenye kusimamia kila kitu. Hapatwi na kusinzia wala kulala. Ni vyake yeye tu vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini. Ni nani awezaye kuombea mbele yake bila ya idhini yake? Anayajua yaliyo mbele yao na yaliyo nyuma yao, wala hawajui kitu katika elimu yake isipokuwa atakacho tu. Kursi yake imezienea mbingu na ardhi wala hakumchoshi kuzihifadhi (mbingu, ardhi na vilivyomo), na Yeye ndiye aliye juu na ndiye aliye Mkuu



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 75

وَكَذَٰلِكَ نُرِيٓ إِبۡرَٰهِيمَ مَلَكُوتَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَلِيَكُونَ مِنَ ٱلۡمُوقِنِينَ

Na kama hivyo tunamuonyesha Ibrahimu ufalme wa mbinguni na ardhini, na ili awe miongoni mwa wenye yakini



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 76

فَلَمَّا جَنَّ عَلَيۡهِ ٱلَّيۡلُ رَءَا كَوۡكَبٗاۖ قَالَ هَٰذَا رَبِّيۖ فَلَمَّآ أَفَلَ قَالَ لَآ أُحِبُّ ٱلۡأٓفِلِينَ

Basi (Mtume Ibrahimu) ulipomjia usiku aliona nyota (na) akasema: Huyu ni Mola wangu Mlezi. (Nyota) Ilipozama alisema: Siwapendi wanaopotea



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 77

فَلَمَّا رَءَا ٱلۡقَمَرَ بَازِغٗا قَالَ هَٰذَا رَبِّيۖ فَلَمَّآ أَفَلَ قَالَ لَئِن لَّمۡ يَهۡدِنِي رَبِّي لَأَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلضَّآلِّينَ

Na alipoona mwezi umechomoza alisema: Huyu ni Mola wangu Mlezi. Na (mwezi) ulipozama alisema: Kama Mola wangu hataniongoza, kwa hakika kabisa nitakuwa miongoni mwa watu waliopotea



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 78

فَلَمَّا رَءَا ٱلشَّمۡسَ بَازِغَةٗ قَالَ هَٰذَا رَبِّي هَٰذَآ أَكۡبَرُۖ فَلَمَّآ أَفَلَتۡ قَالَ يَٰقَوۡمِ إِنِّي بَرِيٓءٞ مِّمَّا تُشۡرِكُونَ

Na alipoliona jua limechomoza alisema: Huyu ni Mola wangu. Huyu ni mkubwa zaidi (kuliko wote). Basi (jua) lilipozama, alisema: Enyi watu wangu, mimi najitenga mbali na (Miungu yote) mnayoshirikisha (na Allah).[1]


1- - Nabii Ibrahimu katika mdahalo huu aliofanya na watu wake hakumaanisha kwamba na yeye aliamini kuwa nyota, mwezi na jua ni Miungu kama walivyoamini. Alichofanya ni maelekezo aliyopewa na Allah kama ilivyoelezwa katika Aya ya 83 ya Sura hii. Pia hiyo ni aina fulani ya mbinu za ufundishaji ya kujifanya unayemfundisha uko pamoja naye ili ufike naye kwenye ukweli na autambue kwa kutumia hoja, akili na mazingira. Nabii Ibrahimu hakuwa Mshirikishaji bali alikuwa Muumini safi anayemuamini na kumuabudu Allah tu. Rejea Aya 120-123 ya Sura Annahli (16).


Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 79

إِنِّي وَجَّهۡتُ وَجۡهِيَ لِلَّذِي فَطَرَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ حَنِيفٗاۖ وَمَآ أَنَا۠ مِنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ

Hakika, mimi nimeelekeza uso wangu kwa (Allah) aliyeumba mbingu na ardhi, nikiacha itikadi zote potofu, na mimi si miongoni mwa washirikina



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 96

فَالِقُ ٱلۡإِصۡبَاحِ وَجَعَلَ ٱلَّيۡلَ سَكَنٗا وَٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَ حُسۡبَانٗاۚ ذَٰلِكَ تَقۡدِيرُ ٱلۡعَزِيزِ ٱلۡعَلِيمِ

(Allah) Ni Mpasuaji wa mapam-bazuko ya asubuhi na ameufanya usiku mapumziko na utulivu, na (amefanya) jua na mwezi kwenda kwa hesabu. Huo ndio mpangilio wa (Allah) Mwenye nguvu nyingi, Mjuzi sana



Capítulo: AL-AN’AAM 

Verso : 97

وَهُوَ ٱلَّذِي جَعَلَ لَكُمُ ٱلنُّجُومَ لِتَهۡتَدُواْ بِهَا فِي ظُلُمَٰتِ ٱلۡبَرِّ وَٱلۡبَحۡرِۗ قَدۡ فَصَّلۡنَا ٱلۡأٓيَٰتِ لِقَوۡمٖ يَعۡلَمُونَ

Na yeye (Allah) ndiye aliye-kuwekeeni nyota ili zikuongozeni katika giza la bara na baharini. Hakika, tumezifafanua Aya (hizi) kwa watu wanaojua (wenye elimu)



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 54

إِنَّ رَبَّكُمُ ٱللَّهُ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٖ ثُمَّ ٱسۡتَوَىٰ عَلَى ٱلۡعَرۡشِۖ يُغۡشِي ٱلَّيۡلَ ٱلنَّهَارَ يَطۡلُبُهُۥ حَثِيثٗا وَٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَ وَٱلنُّجُومَ مُسَخَّرَٰتِۭ بِأَمۡرِهِۦٓۗ أَلَا لَهُ ٱلۡخَلۡقُ وَٱلۡأَمۡرُۗ تَبَارَكَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Hakika, Mola wenu Mlezi ni Allah ambaye ameziumba mbingu na ardhi katika siku sita, kisha akastawi juu ya Arshi. Anaufunika usiku kwa kuleta mchana, ukiufuata kwa haraka, na (ameumba) jua na mwezi na nyota vikiwa vimetiishwa (vimefanywa vitiifu kwa mwana-damu) kwa amri yake. Elewa (kwamba): kuumba na kuamrisha Ni kwake yeye tu. Ametukuka Allah, Mola Mlezi wa walimwengu wote



Capítulo: YUNUS 

Verso : 5

هُوَ ٱلَّذِي جَعَلَ ٱلشَّمۡسَ ضِيَآءٗ وَٱلۡقَمَرَ نُورٗا وَقَدَّرَهُۥ مَنَازِلَ لِتَعۡلَمُواْ عَدَدَ ٱلسِّنِينَ وَٱلۡحِسَابَۚ مَا خَلَقَ ٱللَّهُ ذَٰلِكَ إِلَّا بِٱلۡحَقِّۚ يُفَصِّلُ ٱلۡأٓيَٰتِ لِقَوۡمٖ يَعۡلَمُونَ

Ni yeye ambaye amelifanya jua lenye kuangaza na mwezi kuwa na nuru na ameuwekea (mwezi) vituo ili (kwa kutumia mwezi) mjue idadi ya miaka na hesabu. Allah hakuviumba hivyo isipokuwa kwa haki tu, anazifafanua Aya (zake) kwa watu wanaojua



Capítulo: AR-RA’D 

Verso : 2

ٱللَّهُ ٱلَّذِي رَفَعَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ بِغَيۡرِ عَمَدٖ تَرَوۡنَهَاۖ ثُمَّ ٱسۡتَوَىٰ عَلَى ٱلۡعَرۡشِۖ وَسَخَّرَ ٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَۖ كُلّٞ يَجۡرِي لِأَجَلٖ مُّسَمّٗىۚ يُدَبِّرُ ٱلۡأَمۡرَ يُفَصِّلُ ٱلۡأٓيَٰتِ لَعَلَّكُم بِلِقَآءِ رَبِّكُمۡ تُوقِنُونَ

Allah (pekee ndiye) aliyeziinua mbingu bila ya nguzo mnazoziona. Kisha amelingana sawa juu ya Arshi.[1] Na amelitiisha jua na mwezi[2] (kwa manufaa na maslahi ya viumbe). Kila kimoja (kati ya jua na mwezi) kinakwenda (kwenye mhimili wake) kwa muda maalumu. (Yeye Allah ndiye) Anayeendesha mambo (yote), anafafanua Aya ili mpate kuwa na yakini ya kukutana na Mola wenu Mlezi


1- - Amelingana sawa kwa namna inayowiana na Uungu wake bila ya kufananisha, kulinganisha, kukanusha au kupotosha maana.


2- - Amefanya jua na mwezi vitiifu vikifuata utaratibu na mpangilio maalum aliouweka Allah Muumba.


Capítulo: IBRAHIM 

Verso : 32

ٱللَّهُ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَأَنزَلَ مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ فَأَخۡرَجَ بِهِۦ مِنَ ٱلثَّمَرَٰتِ رِزۡقٗا لَّكُمۡۖ وَسَخَّرَ لَكُمُ ٱلۡفُلۡكَ لِتَجۡرِيَ فِي ٱلۡبَحۡرِ بِأَمۡرِهِۦۖ وَسَخَّرَ لَكُمُ ٱلۡأَنۡهَٰرَ

Allah ndiye aliyeziumba mbingu na ardhi, na akateremsha maji kutoka mawinguni. Na kwa hayo akatoa matunda kuwa ni riziki yenu. Na akayatiisha majahazi yanayopita baharini kwa amri yake, na akaitiisha mito ikutumikieni (kwa manufaa yenu mbalimbali)



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 16

وَلَقَدۡ جَعَلۡنَا فِي ٱلسَّمَآءِ بُرُوجٗا وَزَيَّنَّـٰهَا لِلنَّـٰظِرِينَ

Na kwa hakika kabisa, tumeweka katika anga vituo vya sayari, na tumeipamba mbingu (hii ya dunia) kwa ajili ya watazamao (ili wapate mazingatio)



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 17

وَحَفِظۡنَٰهَا مِن كُلِّ شَيۡطَٰنٖ رَّجِيمٍ

Na (hilo anga) tunalilinda na kila Shetani aliyelaaniwa (ili asiweze kusikia Wahyi n.k)



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 18

إِلَّا مَنِ ٱسۡتَرَقَ ٱلسَّمۡعَ فَأَتۡبَعَهُۥ شِهَابٞ مُّبِينٞ

Isipokuwa kwa (Shetani) anayesikiliza kwa kuibia, naye hufuatwa na kimondo kinachoonekana (na kuteketezwa)



Capítulo: AL-HIJRI 

Verso : 22

وَأَرۡسَلۡنَا ٱلرِّيَٰحَ لَوَٰقِحَ فَأَنزَلۡنَا مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ فَأَسۡقَيۡنَٰكُمُوهُ وَمَآ أَنتُمۡ لَهُۥ بِخَٰزِنِينَ

Na tunazipeleka pepo za kupandishia, na tunateremsha kutoka mawinguni maji, kisha tuka-kunywesheni maji hayo[1]. Wala si nyinyi mnayoyahifadhi


1- - Maji hayo ya mvua mnakunywa nyinyi, mifugo yenu, mnayatumia kwa kilimo, yanasafisha mazingira ardhi, anga, n.k


Capítulo: ANNAHLI 

Verso : 12

وَسَخَّرَ لَكُمُ ٱلَّيۡلَ وَٱلنَّهَارَ وَٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَۖ وَٱلنُّجُومُ مُسَخَّرَٰتُۢ بِأَمۡرِهِۦٓۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّقَوۡمٖ يَعۡقِلُونَ

Na amewadhalilishia usiku na mchana, na jua na mwezi, na nyota zimetiishwa kwa amri yake. Hakika katika hayo kuna ishara (juu ya uwepo wa Allah) kwa watu wenye akili



Capítulo: AL-ISRAA 

Verso : 44

تُسَبِّحُ لَهُ ٱلسَّمَٰوَٰتُ ٱلسَّبۡعُ وَٱلۡأَرۡضُ وَمَن فِيهِنَّۚ وَإِن مِّن شَيۡءٍ إِلَّا يُسَبِّحُ بِحَمۡدِهِۦ وَلَٰكِن لَّا تَفۡقَهُونَ تَسۡبِيحَهُمۡۚ إِنَّهُۥ كَانَ حَلِيمًا غَفُورٗا

Zinamtakasa zote mbingu saba na ardhi na vyote viliomo ndani yake. Na hapana kitu ila kinamtakasa kwa sifa zake. Lakini nyinyi hamfahamu kutakasa kwake. Hakika Yeye ni Mpole na Mwenye kusamehe



Capítulo: MARYAM 

Verso : 90

تَكَادُ ٱلسَّمَٰوَٰتُ يَتَفَطَّرۡنَ مِنۡهُ وَتَنشَقُّ ٱلۡأَرۡضُ وَتَخِرُّ ٱلۡجِبَالُ هَدًّا

Mbingu zinakaribia kupasuka pasuka kwa hilo, na ardhi kupasuka, na milima kuanguka vipande vipande



Capítulo: AL-ANBIYAA 

Verso : 30

أَوَلَمۡ يَرَ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ أَنَّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ كَانَتَا رَتۡقٗا فَفَتَقۡنَٰهُمَاۖ وَجَعَلۡنَا مِنَ ٱلۡمَآءِ كُلَّ شَيۡءٍ حَيٍّۚ أَفَلَا يُؤۡمِنُونَ

Je! Hao walio kufuru hawa-kuona kwamba mbingu na ardhi zilikuwa zimeambatana, kisha Sisi tukazibabadua? Na tukajaalia kutokana na maji kila kitu chenye uhai? Basi je, hawaamini?



Capítulo: AL-ANBIYAA 

Verso : 32

وَجَعَلۡنَا ٱلسَّمَآءَ سَقۡفٗا مَّحۡفُوظٗاۖ وَهُمۡ عَنۡ ءَايَٰتِهَا مُعۡرِضُونَ

Na tukaifanya mbingu kuwa dari iliyo hifadhiwa, lakini wanazipuuza Ishara zake



Capítulo: AL-ANBIYAA 

Verso : 33

وَهُوَ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلَّيۡلَ وَٱلنَّهَارَ وَٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَۖ كُلّٞ فِي فَلَكٖ يَسۡبَحُونَ

Na Yeye ndiye aliye umba usiku na mchana na jua na mwezi, vyote katika anga vinaogelea



Capítulo: ANNUUR 

Verso : 43

أَلَمۡ تَرَ أَنَّ ٱللَّهَ يُزۡجِي سَحَابٗا ثُمَّ يُؤَلِّفُ بَيۡنَهُۥ ثُمَّ يَجۡعَلُهُۥ رُكَامٗا فَتَرَى ٱلۡوَدۡقَ يَخۡرُجُ مِنۡ خِلَٰلِهِۦ وَيُنَزِّلُ مِنَ ٱلسَّمَآءِ مِن جِبَالٖ فِيهَا مِنۢ بَرَدٖ فَيُصِيبُ بِهِۦ مَن يَشَآءُ وَيَصۡرِفُهُۥ عَن مَّن يَشَآءُۖ يَكَادُ سَنَا بَرۡقِهِۦ يَذۡهَبُ بِٱلۡأَبۡصَٰرِ

Je! Huoni ya kwamba Allah huyasukuma mawingu, kisha huyaambatisha, kisha huyafanya mirundi? Basi utaona mvua ikitoka kati yake. Na huteremsha kutoka juu kwenye milima ya mawingu mvua ya mawe, ikampata amtakaye na akamuepusha nayo amtakaye. Hukurubia mmetuko wa umeme wake kupofua macho



Capítulo: ALFURQAAN 

Verso : 61

تَبَارَكَ ٱلَّذِي جَعَلَ فِي ٱلسَّمَآءِ بُرُوجٗا وَجَعَلَ فِيهَا سِرَٰجٗا وَقَمَرٗا مُّنِيرٗا

Ametukuka aliye zijaalia nyota mbinguni, na akajaalia humo taa na mwezi unao ng’ara



Capítulo: ARRUUM 

Verso : 48

ٱللَّهُ ٱلَّذِي يُرۡسِلُ ٱلرِّيَٰحَ فَتُثِيرُ سَحَابٗا فَيَبۡسُطُهُۥ فِي ٱلسَّمَآءِ كَيۡفَ يَشَآءُ وَيَجۡعَلُهُۥ كِسَفٗا فَتَرَى ٱلۡوَدۡقَ يَخۡرُجُ مِنۡ خِلَٰلِهِۦۖ فَإِذَآ أَصَابَ بِهِۦ مَن يَشَآءُ مِنۡ عِبَادِهِۦٓ إِذَا هُمۡ يَسۡتَبۡشِرُونَ

Allah ndiye anaye zituma pepo zikayatimua mawingu, kisha akayatandaza mbinguni kama apendavyo. Na akayafanya mapande mapande, basi ukaiona mvua inatoka ndani yake. Anapo wafikishia awatakao katika waja wake, mara hao huwa na furaha



Capítulo: LUQMAAN 

Verso : 10

خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ بِغَيۡرِ عَمَدٖ تَرَوۡنَهَاۖ وَأَلۡقَىٰ فِي ٱلۡأَرۡضِ رَوَٰسِيَ أَن تَمِيدَ بِكُمۡ وَبَثَّ فِيهَا مِن كُلِّ دَآبَّةٖۚ وَأَنزَلۡنَا مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗ فَأَنۢبَتۡنَا فِيهَا مِن كُلِّ زَوۡجٖ كَرِيمٍ

Ameziumba mbingu bila ya nguzo mnazo ziona; na ameweka katika ardhi milima ili ardhi isikuyumbisheni; na ametawanya humo kila namna ya wanyama; na tumeteremsha maji kutoka mbinguni, na tukaotesha katika ardhi mimea mizuri ya kila namna



Capítulo: LUQMAAN 

Verso : 29

أَلَمۡ تَرَ أَنَّ ٱللَّهَ يُولِجُ ٱلَّيۡلَ فِي ٱلنَّهَارِ وَيُولِجُ ٱلنَّهَارَ فِي ٱلَّيۡلِ وَسَخَّرَ ٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَۖ كُلّٞ يَجۡرِيٓ إِلَىٰٓ أَجَلٖ مُّسَمّٗى وَأَنَّ ٱللَّهَ بِمَا تَعۡمَلُونَ خَبِيرٞ

Kwani huoni kwamba Allah huuingiza usiku katika mchana, na huuingiza mchana katika usiku, na amedhalilisha jua na mwezi? Vyote hivyo vinakwenda mpaka wakati uliowekwa. Na Allah anazo khabari za mnayoyatenda



Capítulo: AL-AHZAAB 

Verso : 72

إِنَّا عَرَضۡنَا ٱلۡأَمَانَةَ عَلَى ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَٱلۡجِبَالِ فَأَبَيۡنَ أَن يَحۡمِلۡنَهَا وَأَشۡفَقۡنَ مِنۡهَا وَحَمَلَهَا ٱلۡإِنسَٰنُۖ إِنَّهُۥ كَانَ ظَلُومٗا جَهُولٗا

Kwa hakika Sisi tulikadimisha amana kwa mbingu na ardhi na milima; na vyote hivyo vikakataa kuichukua na vikaogopa. Lakini mwanaadamu akaichukua. Hakika yeye amekuwa dhaalimu mjinga