Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 31

وَعَلَّمَ ءَادَمَ ٱلۡأَسۡمَآءَ كُلَّهَا ثُمَّ عَرَضَهُمۡ عَلَى ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةِ فَقَالَ أَنۢبِـُٔونِي بِأَسۡمَآءِ هَـٰٓؤُلَآءِ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Na akamfundisha Adamu majina yote, kisha akawaleta wenye majina hayo mbele ya malaika. Akawaambia: Nitajieni majina ya hawa kama ninyi ni wa kweli



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 33

قَالَ يَـٰٓـَٔادَمُ أَنۢبِئۡهُم بِأَسۡمَآئِهِمۡۖ فَلَمَّآ أَنۢبَأَهُم بِأَسۡمَآئِهِمۡ قَالَ أَلَمۡ أَقُل لَّكُمۡ إِنِّيٓ أَعۡلَمُ غَيۡبَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَأَعۡلَمُ مَا تُبۡدُونَ وَمَا كُنتُمۡ تَكۡتُمُونَ

Akasema: Ewe Adamu, waambie majina yao. Basi alipowaambia majina yao, (Allah) akasema: Je, si nilikuambieni kuwa mimi ninajua visivyoonekana mbinguni na ardhini? Na ninayajua mno mnayo yadhihirisha na mnayoyaficha



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 34

وَإِذۡ قُلۡنَا لِلۡمَلَـٰٓئِكَةِ ٱسۡجُدُواْ لِأٓدَمَ فَسَجَدُوٓاْ إِلَّآ إِبۡلِيسَ أَبَىٰ وَٱسۡتَكۡبَرَ وَكَانَ مِنَ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Na (kumbuka) tulipowaambia Malaika (kuwa): Msujudieni Adamu. Wakasujudu, isipokuwa Ibilisi alikataa na kuleta kiburi na akawa miongoni mwa makafiri



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 35

وَقُلۡنَا يَـٰٓـَٔادَمُ ٱسۡكُنۡ أَنتَ وَزَوۡجُكَ ٱلۡجَنَّةَ وَكُلَا مِنۡهَا رَغَدًا حَيۡثُ شِئۡتُمَا وَلَا تَقۡرَبَا هَٰذِهِ ٱلشَّجَرَةَ فَتَكُونَا مِنَ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na tulisema: Ewe Adamu, ishi wewe na mkeo Peponi na kuleni humo kwa uhuru popote mtakapo na msiusogelee mti huu ili msije mkawa miongoni mwa madhalimu



Capítulo: AL-BAQARAH 

Verso : 37

فَتَلَقَّىٰٓ ءَادَمُ مِن رَّبِّهِۦ كَلِمَٰتٖ فَتَابَ عَلَيۡهِۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلتَّوَّابُ ٱلرَّحِيمُ

Adamu akapokea maneno (ya toba) kutoka kwa Mola wake (akatubu) na (Allah) akamkubalia toba yake. Hakika yeye (Allah) ni Mwingi wa kupokea toba, Mwingi wa rehema



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 33

۞إِنَّ ٱللَّهَ ٱصۡطَفَىٰٓ ءَادَمَ وَنُوحٗا وَءَالَ إِبۡرَٰهِيمَ وَءَالَ عِمۡرَٰنَ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ

Hakika, Allah amemteua Adamu na Nuhu na familia ya Ibrahimu na familia ya Imrani kati ya walimwengu (wengine wa wakati wao)



Capítulo: AL-IMRAN 

Verso : 53

رَبَّنَآ ءَامَنَّا بِمَآ أَنزَلۡتَ وَٱتَّبَعۡنَا ٱلرَّسُولَ فَٱكۡتُبۡنَا مَعَ ٱلشَّـٰهِدِينَ

Ewe Mola wetu, tumeyaamini yote uliyoyateremsha na tumemfuata Mtume, basi tuandike (kuwa) pamoja na Mashahidi



Capítulo: AL-MAIDA 

Verso : 27

۞وَٱتۡلُ عَلَيۡهِمۡ نَبَأَ ٱبۡنَيۡ ءَادَمَ بِٱلۡحَقِّ إِذۡ قَرَّبَا قُرۡبَانٗا فَتُقُبِّلَ مِنۡ أَحَدِهِمَا وَلَمۡ يُتَقَبَّلۡ مِنَ ٱلۡأٓخَرِ قَالَ لَأَقۡتُلَنَّكَۖ قَالَ إِنَّمَا يَتَقَبَّلُ ٱللَّهُ مِنَ ٱلۡمُتَّقِينَ

Na wasomee, kwa haki, habari za wana wawili wa Adamu walipotoa sadaka, basi ikakubaliwa ya mmoja wao, na ya mwingine haikukubaliwa. (Aliyekataliwa sadaka yake) Aka-sema: Kwa Yakini kabisa, nitakuua. (Yule aliyekubaliwa sadaka yake) Akasema: Ilivyo ni kwamba, Allah anawakubalia wacha Mungu[1]


1- - Hapa hakuyasema haya kumwambia ndugu yake kwa lengo la majigambo na majivuno. Lakini aliyasema hayo kwa lengo la kumshawishi ndugu yake aache uovu na amuelekee Allah kwa unyenyekevu ili akubaliwe ibada zake.


Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 11

وَلَقَدۡ خَلَقۡنَٰكُمۡ ثُمَّ صَوَّرۡنَٰكُمۡ ثُمَّ قُلۡنَا لِلۡمَلَـٰٓئِكَةِ ٱسۡجُدُواْ لِأٓدَمَ فَسَجَدُوٓاْ إِلَّآ إِبۡلِيسَ لَمۡ يَكُن مِّنَ ٱلسَّـٰجِدِينَ

Na kwa hakika kabisa, tulikuumbeni, kisha tulikutieni sura, kisha tuliwaambia Malaika: Msujudieni Adamu. Walisujudu isipokuwa Ibilisi tu, hakuwa miongoni mwa waliosujudu



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 19

وَيَـٰٓـَٔادَمُ ٱسۡكُنۡ أَنتَ وَزَوۡجُكَ ٱلۡجَنَّةَ فَكُلَا مِنۡ حَيۡثُ شِئۡتُمَا وَلَا تَقۡرَبَا هَٰذِهِ ٱلشَّجَرَةَ فَتَكُونَا مِنَ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na ewe Adamu, kaa wewe na mkeo Peponi. Basi kuleni katika mpendavyo na msiusogelee mti huu, mtakuwa miongoni mwa madhalimu



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 26

يَٰبَنِيٓ ءَادَمَ قَدۡ أَنزَلۡنَا عَلَيۡكُمۡ لِبَاسٗا يُوَٰرِي سَوۡءَٰتِكُمۡ وَرِيشٗاۖ وَلِبَاسُ ٱلتَّقۡوَىٰ ذَٰلِكَ خَيۡرٞۚ ذَٰلِكَ مِنۡ ءَايَٰتِ ٱللَّهِ لَعَلَّهُمۡ يَذَّكَّرُونَ

Enyi wanadamu, hakika tumekuteremshieni vazi linaloficha tupu zenu na pambo. Na vazi la kumcha Allah ndio bora zaidi. Hizo ni baadhi ya ishara za Allah ili (wanadamu) wapate kukumbuka (neema za Mola wao Mlezi na kumshukuru)



Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 27

يَٰبَنِيٓ ءَادَمَ لَا يَفۡتِنَنَّكُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ كَمَآ أَخۡرَجَ أَبَوَيۡكُم مِّنَ ٱلۡجَنَّةِ يَنزِعُ عَنۡهُمَا لِبَاسَهُمَا لِيُرِيَهُمَا سَوۡءَٰتِهِمَآۚ إِنَّهُۥ يَرَىٰكُمۡ هُوَ وَقَبِيلُهُۥ مِنۡ حَيۡثُ لَا تَرَوۡنَهُمۡۗ إِنَّا جَعَلۡنَا ٱلشَّيَٰطِينَ أَوۡلِيَآءَ لِلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ

Enyi Wanadamu, kamwe shetani asikufitinisheni[1] kama alivyowatoa Peponi wazazi wenu, akiwavua nguo zao ili kuwawekea wazi tupu zao. Hakika yeye (shetani) anakuoneni yeye na jeshi lake katika namna ambayo nyinyi hamuwaoni. Hakika, sisi tumewafanya mashetani wandani wa (watu) wasioamini


1- - Shetani asikudanganyeni kwa kukupambieni maasi, kama ambavyo alimhadaa baba yenu Adamu na mkewe kwa kuwashawishi waonje mti. Matokeo yake walitolewa Peponi.


Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 31

۞يَٰبَنِيٓ ءَادَمَ خُذُواْ زِينَتَكُمۡ عِندَ كُلِّ مَسۡجِدٖ وَكُلُواْ وَٱشۡرَبُواْ وَلَا تُسۡرِفُوٓاْۚ إِنَّهُۥ لَا يُحِبُّ ٱلۡمُسۡرِفِينَ

Enyi wanadamu, chukueni mapambo yenu kila muendapo msikitini (kila mnaposwali)[1] na kuleni na kunyweni na msifanye ubadhirifu. Hakika, yeye (Allah) hawapendi wabadhirifu


1- - Aya hii ndio iliyoweka sharti la Muislamu kujisitiri kwa kuvaa nguo za heshima na sitara katika Swala. Na sio kuvaa nguo tu, lakini kuvaa nguo ya sitara, safi na inayopendeza. Kwa msingi huu, sio vyema kwa Muislamu kuswali akiwa amevaa nguo chafu au zenye michoro, picha na mandishi yasiyokuwa na lazima.


Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 35

يَٰبَنِيٓ ءَادَمَ إِمَّا يَأۡتِيَنَّكُمۡ رُسُلٞ مِّنكُمۡ يَقُصُّونَ عَلَيۡكُمۡ ءَايَٰتِي فَمَنِ ٱتَّقَىٰ وَأَصۡلَحَ فَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ

Enyi wanadamu, watakapo kufikieni Mitume watokanao na nyinyi wakikuhadithieni Aya zangu[1], basi yeyote atakayekuwa na uchaMungu na akafanya mema basi hawatakuwa na hofu yoyote, na hawatahuzunika


1- - Aya hii wanaitumia baadhi ya watu ili kupotosha. Wanadai kwamba, utume bado unaendelea. Itikadi ya Watu wa Sun ana Jama a ni kwamba, utume umekoma kwa Mtume Muhammad. Hakuna Mtume mwingine baada yake. Tujiulize swali la msingi. Aya hapa kama inasema kuwa Mitume wanaendelea kuja je, hizo Aya za Allah wanazotakiwa kutusomea ziko wapi? Rejea Aya ya 40, Sura Al-ahzab (33). Pia rejea Aya ya 158 ya Sura Al-aaraf (7).


Capítulo: AL-AARAAF 

Verso : 172

وَإِذۡ أَخَذَ رَبُّكَ مِنۢ بَنِيٓ ءَادَمَ مِن ظُهُورِهِمۡ ذُرِّيَّتَهُمۡ وَأَشۡهَدَهُمۡ عَلَىٰٓ أَنفُسِهِمۡ أَلَسۡتُ بِرَبِّكُمۡۖ قَالُواْ بَلَىٰ شَهِدۡنَآۚ أَن تَقُولُواْ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ إِنَّا كُنَّا عَنۡ هَٰذَا غَٰفِلِينَ

Na (kumbuka) wakati Mola wako alipochukua kwa wanadamu kizazi chao kutokea migongoni mwao na akawashuhudisha wen-yewe (kwa kuwauliza kwamba): Hivi mimi sio Mola wenu Mlezi? Wakasema: “Kwa nini (isiwe hivyo? Tumeshuhudia (kuwa wewe ni Mola wetu Mlezi”. (Tumefanya hivyo) Ili msije kusema Siku ya Kiyama kuwa: Sisi tulikuwa tumeghafilika na haya (tulikuwa hatuyajui)



Capítulo: AL-ISRAA 

Verso : 61

وَإِذۡ قُلۡنَا لِلۡمَلَـٰٓئِكَةِ ٱسۡجُدُواْ لِأٓدَمَ فَسَجَدُوٓاْ إِلَّآ إِبۡلِيسَ قَالَ ءَأَسۡجُدُ لِمَنۡ خَلَقۡتَ طِينٗا

Na pale tulipo waambia Malaika: Msujudieni Adam. Wakamsujudia isipo kuwa Iblisi. Akasema: Je! Nimsujudie uliye muumba kwa udongo?



Capítulo: AL-ISRAA 

Verso : 70

۞وَلَقَدۡ كَرَّمۡنَا بَنِيٓ ءَادَمَ وَحَمَلۡنَٰهُمۡ فِي ٱلۡبَرِّ وَٱلۡبَحۡرِ وَرَزَقۡنَٰهُم مِّنَ ٱلطَّيِّبَٰتِ وَفَضَّلۡنَٰهُمۡ عَلَىٰ كَثِيرٖ مِّمَّنۡ خَلَقۡنَا تَفۡضِيلٗا

Na hakika tumewatukuza wanaadamu, na tumewapa vya kupanda nchi kavu na baharini, na tumewaruzuku vitu vizuri vizuri, na tumewafadhilisha kwa fadhila kubwa kuliko wengi miongoni mwa tulio waumba



Capítulo: AL-KAHF 

Verso : 50

وَإِذۡ قُلۡنَا لِلۡمَلَـٰٓئِكَةِ ٱسۡجُدُواْ لِأٓدَمَ فَسَجَدُوٓاْ إِلَّآ إِبۡلِيسَ كَانَ مِنَ ٱلۡجِنِّ فَفَسَقَ عَنۡ أَمۡرِ رَبِّهِۦٓۗ أَفَتَتَّخِذُونَهُۥ وَذُرِّيَّتَهُۥٓ أَوۡلِيَآءَ مِن دُونِي وَهُمۡ لَكُمۡ عَدُوُّۢۚ بِئۡسَ لِلظَّـٰلِمِينَ بَدَلٗا

Na tulipo waambia Malaika: Msujudieni Adam! Walimsujudia isipo kuwa Iblisi. Yeye alikuwa miongoni mwa majini, na akavunja amri ya Mola wake Mlezi. Je! Mnamfanya yeye na kizazi chake kuwa marafiki badala yangu, hali wao ni adui zenu? Ni ubaya ulioje wa madhalimu kumtii Shetani badala ya kumtii Allah



Capítulo: MARYAM 

Verso : 58

أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ أَنۡعَمَ ٱللَّهُ عَلَيۡهِم مِّنَ ٱلنَّبِيِّـۧنَ مِن ذُرِّيَّةِ ءَادَمَ وَمِمَّنۡ حَمَلۡنَا مَعَ نُوحٖ وَمِن ذُرِّيَّةِ إِبۡرَٰهِيمَ وَإِسۡرَـٰٓءِيلَ وَمِمَّنۡ هَدَيۡنَا وَٱجۡتَبَيۡنَآۚ إِذَا تُتۡلَىٰ عَلَيۡهِمۡ ءَايَٰتُ ٱلرَّحۡمَٰنِ خَرُّواْۤ سُجَّدٗاۤ وَبُكِيّٗا۩

Hao ndio alio waneemesha Allah miongoni mwa Manabii katika uzao wa Adam, na katika uzao wa wale tulio wapandisha pamoja na Nuhu, na katika uzao wa Ibrahim na Israil, na katika wale tulio waongoa na tukawateuwa. Wanapo somewa Aya za Mwingi wa Rehema huanguka kusujudu na kulia



Capítulo: TWAHA 

Verso : 115

وَلَقَدۡ عَهِدۡنَآ إِلَىٰٓ ءَادَمَ مِن قَبۡلُ فَنَسِيَ وَلَمۡ نَجِدۡ لَهُۥ عَزۡمٗا

Na hapo zamani tuliagana na Adam, lakini alisahau, wala hatukuona kwake azma kubwa



Capítulo: TWAHA 

Verso : 116

وَإِذۡ قُلۡنَا لِلۡمَلَـٰٓئِكَةِ ٱسۡجُدُواْ لِأٓدَمَ فَسَجَدُوٓاْ إِلَّآ إِبۡلِيسَ أَبَىٰ

Na tulipo waambia Malaika: Msujudieni Adam! Wakasujudu, isipo kuwa Iblisi, alikataa



Capítulo: TWAHA 

Verso : 117

فَقُلۡنَا يَـٰٓـَٔادَمُ إِنَّ هَٰذَا عَدُوّٞ لَّكَ وَلِزَوۡجِكَ فَلَا يُخۡرِجَنَّكُمَا مِنَ ٱلۡجَنَّةِ فَتَشۡقَىٰٓ

Tukasema: Ewe Adam! Hakika huyu ni adui yako na wa mkeo. Basi asikutoeni katika Bustani hii, mkaingia mashakani



Capítulo: TWAHA 

Verso : 120

فَوَسۡوَسَ إِلَيۡهِ ٱلشَّيۡطَٰنُ قَالَ يَـٰٓـَٔادَمُ هَلۡ أَدُلُّكَ عَلَىٰ شَجَرَةِ ٱلۡخُلۡدِ وَمُلۡكٖ لَّا يَبۡلَىٰ

Lakini Shetani alimtia wasiwasi, akamwambia: Ewe Adam! Nikujuulishe mti wa kuishi milele na ufalme usio koma?



Capítulo: TWAHA 

Verso : 121

فَأَكَلَا مِنۡهَا فَبَدَتۡ لَهُمَا سَوۡءَٰتُهُمَا وَطَفِقَا يَخۡصِفَانِ عَلَيۡهِمَا مِن وَرَقِ ٱلۡجَنَّةِۚ وَعَصَىٰٓ ءَادَمُ رَبَّهُۥ فَغَوَىٰ

Basi wakaula wote wawili, na uchi wao ukawadhihirikia na wakaanza kujibandika majani ya Peponi. Na Adam akamuasi Mola wake Mlezi, na akapotea njia



Capítulo: YAASIIN 

Verso : 60

۞أَلَمۡ أَعۡهَدۡ إِلَيۡكُمۡ يَٰبَنِيٓ ءَادَمَ أَن لَّا تَعۡبُدُواْ ٱلشَّيۡطَٰنَۖ إِنَّهُۥ لَكُمۡ عَدُوّٞ مُّبِينٞ

Je! Sikuagana nanyi, enyi wanaadamu, kuwa msimuabudu Shet’ani? Hakika yeye ni adui dhaahiri kwenu



Capítulo: SWAAD 

Verso : 69

مَا كَانَ لِيَ مِنۡ عِلۡمِۭ بِٱلۡمَلَإِ ٱلۡأَعۡلَىٰٓ إِذۡ يَخۡتَصِمُونَ

Sikuwa na elimu ya mambo ya viumbe wakuu watukufu walipokuwa wakishindana