Sourate: NUUH 

Verset : 3

أَنِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ وَٱتَّقُوهُ وَأَطِيعُونِ

(Nakuonyeni) Kwamba muabuduni Allah na mcheni (muogopeni) na mnitii



Sourate: NUUH 

Verset : 4

يَغۡفِرۡ لَكُم مِّن ذُنُوبِكُمۡ وَيُؤَخِّرۡكُمۡ إِلَىٰٓ أَجَلٖ مُّسَمًّىۚ إِنَّ أَجَلَ ٱللَّهِ إِذَا جَآءَ لَا يُؤَخَّرُۚ لَوۡ كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ

Atakusameheni madhambi yenu, na atakuahirisheni mpaka muda uliowekwa. Hakika muda wa Allah ukifika haucheleweshwi, lau kama mngekuwa mnajua



Sourate: NUUH 

Verset : 5

قَالَ رَبِّ إِنِّي دَعَوۡتُ قَوۡمِي لَيۡلٗا وَنَهَارٗا

(Nuhu) Akasema: Mola wangu! Hakika mimi nimewalingania watu wangu usiku na mchana



Sourate: NUUH 

Verset : 6

فَلَمۡ يَزِدۡهُمۡ دُعَآءِيٓ إِلَّا فِرَارٗا

Lakini haikuwazidishia wito wangu isipokuwa kukimbia



Sourate: NUUH 

Verset : 7

وَإِنِّي كُلَّمَا دَعَوۡتُهُمۡ لِتَغۡفِرَ لَهُمۡ جَعَلُوٓاْ أَصَٰبِعَهُمۡ فِيٓ ءَاذَانِهِمۡ وَٱسۡتَغۡشَوۡاْ ثِيَابَهُمۡ وَأَصَرُّواْ وَٱسۡتَكۡبَرُواْ ٱسۡتِكۡبَارٗا

Na hakika Mimi kila nilipowaita ili Uwasamehe; huweka vidole vyao masikioni mwao na wakajifunika nguo zao na wakashikilia (kukanusha) wakafanya kiburi kikubwa



Sourate: NUUH 

Verset : 8

ثُمَّ إِنِّي دَعَوۡتُهُمۡ جِهَارٗا

Kisha hakika mimi niliwalingania kwa waziwazi



Sourate: NUUH 

Verset : 9

ثُمَّ إِنِّيٓ أَعۡلَنتُ لَهُمۡ وَأَسۡرَرۡتُ لَهُمۡ إِسۡرَارٗا

Kisha nikawatangazia kwa sauti, halafu tena nikasema nao kwa siri



Sourate: NUUH 

Verset : 10

فَقُلۡتُ ٱسۡتَغۡفِرُواْ رَبَّكُمۡ إِنَّهُۥ كَانَ غَفَّارٗا

Nikasema: Ombeni msamaha kwa Mola wenu Mlezi; hakika Yeye ni Mwingi wa kusamehe



Sourate: NUUH 

Verset : 11

يُرۡسِلِ ٱلسَّمَآءَ عَلَيۡكُم مِّدۡرَارٗا

Atakuleteeni mvua inyeshe mfululizo (Yenye kuendelea)



Sourate: NUUH 

Verset : 12

وَيُمۡدِدۡكُم بِأَمۡوَٰلٖ وَبَنِينَ وَيَجۡعَل لَّكُمۡ جَنَّـٰتٖ وَيَجۡعَل لَّكُمۡ أَنۡهَٰرٗا

Na Atakuongezeeni mali na wana, na Atakupeni mabustani na Atakufanyieni mito



Sourate: NUUH 

Verset : 13

مَّا لَكُمۡ لَا تَرۡجُونَ لِلَّهِ وَقَارٗا

Mna nini hamweki heshima ya Allah?



Sourate: NUUH 

Verset : 14

وَقَدۡ خَلَقَكُمۡ أَطۡوَارًا

Na hali Amekuumbeni hatua baada ya hatua?



Sourate: NUUH 

Verset : 15

أَلَمۡ تَرَوۡاْ كَيۡفَ خَلَقَ ٱللَّهُ سَبۡعَ سَمَٰوَٰتٖ طِبَاقٗا

Kwani hamwoni jinsi Mwenyezi Mungu alivyo ziumba mbingu saba kwa matabaka?



Sourate: NUUH 

Verset : 16

وَجَعَلَ ٱلۡقَمَرَ فِيهِنَّ نُورٗا وَجَعَلَ ٱلشَّمۡسَ سِرَاجٗا

Na Akaufanya mwezi ndani yake uwe nuru, na Akalifanya jua ni taa yenye mwanga mkali?



Sourate: NUUH 

Verset : 17

وَٱللَّهُ أَنۢبَتَكُم مِّنَ ٱلۡأَرۡضِ نَبَاتٗا

Na Allah amekuotesheni (Amekuanzisheni vizuri katika udongo) wa ardhi kama mimea



Sourate: NUUH 

Verset : 18

ثُمَّ يُعِيدُكُمۡ فِيهَا وَيُخۡرِجُكُمۡ إِخۡرَاجٗا

Kisha Atakurudisheni humo na Atakutoeni tena mtoke (kuwa hai)



Sourate: NUUH 

Verset : 19

وَٱللَّهُ جَعَلَ لَكُمُ ٱلۡأَرۡضَ بِسَاطٗا

Na Allah Amekufanyieni ardhi kuwa (kama) busati



Sourate: NUUH 

Verset : 20

لِّتَسۡلُكُواْ مِنۡهَا سُبُلٗا فِجَاجٗا

Ili mtembee humo katika njia zilizo pana



Sourate: NUUH 

Verset : 21

قَالَ نُوحٞ رَّبِّ إِنَّهُمۡ عَصَوۡنِي وَٱتَّبَعُواْ مَن لَّمۡ يَزِدۡهُ مَالُهُۥ وَوَلَدُهُۥٓ إِلَّا خَسَارٗا

Nuhu akasema: Mola wangu! Hakika hao wameniasi, na wamemfuata yule ambaye mali yake na wanawe hawakumzidishia ila khasara tu



Sourate: NUUH 

Verset : 22

وَمَكَرُواْ مَكۡرٗا كُبَّارٗا

Na wakapanga vitimbi vikubwa



Sourate: NUUH 

Verset : 23

وَقَالُواْ لَا تَذَرُنَّ ءَالِهَتَكُمۡ وَلَا تَذَرُنَّ وَدّٗا وَلَا سُوَاعٗا وَلَا يَغُوثَ وَيَعُوقَ وَنَسۡرٗا

Na wakasema: Msiwaache miungu yenu, wala msimwache Wadda wala Suwaa’ wala Yaghutha, wala Yau’qa, wala Nasra.[1]


1- - Wadda, Su’waa’a, Yaghuwtha, Ya’uwqa, Nasraa: ni majina ya masanamu waliyokuwa wakiyaabudu watu wa Nabii Nuhu, haya masanamu yalikuwa makubwa na matukufu zaidi kwao, na kwaajili hiyo yalihusishwa kwa kutajwa hapa, na asili yake ni kama vile alivyosema U’rwah bin Zubeyri-


Sourate: NUUH 

Verset : 24

وَقَدۡ أَضَلُّواْ كَثِيرٗاۖ وَلَا تَزِدِ ٱلظَّـٰلِمِينَ إِلَّا ضَلَٰلٗا

Na hao walikwisha wapoteza wengi, wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea



Sourate: NUUH 

Verset : 25

مِّمَّا خَطِيٓـَٰٔتِهِمۡ أُغۡرِقُواْ فَأُدۡخِلُواْ نَارٗا فَلَمۡ يَجِدُواْ لَهُم مِّن دُونِ ٱللَّهِ أَنصَارٗا

Basi kwa ajili ya makosa yao waligharikishwa wakaingizwa Motoni, wala hawakuwapata wa kuwanusuru badala ya Allah



Sourate: NUUH 

Verset : 26

وَقَالَ نُوحٞ رَّبِّ لَا تَذَرۡ عَلَى ٱلۡأَرۡضِ مِنَ ٱلۡكَٰفِرِينَ دَيَّارًا

Na Nuh’u akasema: Mola wangu Mlezi! Usimwache juu ya ardhi mkaazi wake yeyote katika makafiri!



Sourate: NUUH 

Verset : 27

إِنَّكَ إِن تَذَرۡهُمۡ يُضِلُّواْ عِبَادَكَ وَلَا يَلِدُوٓاْ إِلَّا فَاجِرٗا كَفَّارٗا

Hakika Wewe Ukiwaacha, watawapoteza waja Wako, na wala hawatozaa isipokuwa mtendaji dhambi, kafiri mkanushaji mno



Sourate: NUUH 

Verset : 28

رَّبِّ ٱغۡفِرۡ لِي وَلِوَٰلِدَيَّ وَلِمَن دَخَلَ بَيۡتِيَ مُؤۡمِنٗا وَلِلۡمُؤۡمِنِينَ وَٱلۡمُؤۡمِنَٰتِۖ وَلَا تَزِدِ ٱلظَّـٰلِمِينَ إِلَّا تَبَارَۢا

Eee Mola wangu! Nisamehe Mimi na wazazi wangu, na kila aliye ingia nyumbani mwangu kuwa ni mwenye kuamini, na Waumini wote wanaume, na Waumini wote wanawake. Na wala usiwazidishie walio dhulumu ila kupotea, (na kuteketea kabisa)



Sourate: ALJINN 

Verset : 1

قُلۡ أُوحِيَ إِلَيَّ أَنَّهُ ٱسۡتَمَعَ نَفَرٞ مِّنَ ٱلۡجِنِّ فَقَالُوٓاْ إِنَّا سَمِعۡنَا قُرۡءَانًا عَجَبٗا

Sema: Nimefunuliwa Wahyi kwamba, kundi miongoni mwa majini lilisikiliza (Qur’ani) likasema: Hakika sisi tumeisikia Qurani ya ajabu sana



Sourate: ALJINN 

Verset : 2

يَهۡدِيٓ إِلَى ٱلرُّشۡدِ فَـَٔامَنَّا بِهِۦۖ وَلَن نُّشۡرِكَ بِرَبِّنَآ أَحَدٗا

Inaongoza kwenye uongofu, kwa hivyo tumeiamini, na wala hatutamshirikisha yeyote kwa Mola wetu Mlezi



Sourate: ALJINN 

Verset : 3

وَأَنَّهُۥ تَعَٰلَىٰ جَدُّ رَبِّنَا مَا ٱتَّخَذَ صَٰحِبَةٗ وَلَا وَلَدٗا

Na kwa hakika utukufu wa Mola wetu umetukuka kabisa; Hakujifanyia Mke wala Mtoto (hana mke wala mwana)



Sourate: ALJINN 

Verset : 4

وَأَنَّهُۥ كَانَ يَقُولُ سَفِيهُنَا عَلَى ٱللَّهِ شَطَطٗا

Na kwa hakika hali ilivyo, wapumbavu miongoni mwetu walikuwa wakisema juu ya Allah uongo uliopindukia mipaka