وَلَقَدۡ يَسَّرۡنَا ٱلۡقُرۡءَانَ لِلذِّكۡرِ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ
Na Hakika Tumeirahisisha Qur’ani kwaajili ya Ukumbusho Je Kuna Mwenye kukumbuka.?
Partager :
وَلَقَدۡ جَآءَ ءَالَ فِرۡعَوۡنَ ٱلنُّذُرُ
Hakika yaliwajia watu wafiraun maonyo
كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا كُلِّهَا فَأَخَذۡنَٰهُمۡ أَخۡذَ عَزِيزٖ مُّقۡتَدِرٍ
Na kwa yakini watu wa Fir’awn walifikiwa na waonyaji
أَكُفَّارُكُمۡ خَيۡرٞ مِّنۡ أُوْلَـٰٓئِكُمۡ أَمۡ لَكُم بَرَآءَةٞ فِي ٱلزُّبُرِ
Je, makafiri wenu (enyi Maquraysh) ni bora kuliko hao (ummah) wa awali? Au mna msamaha katika Maandiko Tukufu?
أَمۡ يَقُولُونَ نَحۡنُ جَمِيعٞ مُّنتَصِرٞ
Au wanasema: Sisi ni wengi (kundi) tutashinda tu.?
سَيُهۡزَمُ ٱلۡجَمۡعُ وَيُوَلُّونَ ٱلدُّبُرَ
Litashindwa kundi hilo na watakimbia
بَلِ ٱلسَّاعَةُ مَوۡعِدُهُمۡ وَٱلسَّاعَةُ أَدۡهَىٰ وَأَمَرُّ
Bali Kiyama Ndio Ahadi Yao Na Adhabu Ya Kiyama Kubwa Na Chungu Zaidi
إِنَّ ٱلۡمُجۡرِمِينَ فِي ضَلَٰلٖ وَسُعُرٖ
Hakika wahalifu wamo katika upotofu na wazimu
يَوۡمَ يُسۡحَبُونَ فِي ٱلنَّارِ عَلَىٰ وُجُوهِهِمۡ ذُوقُواْ مَسَّ سَقَرَ
Siku watakayoburutwa motoni kifudi fudi, Waambiwe: Onjeni mguso wa moto mkali mno
إِنَّا كُلَّ شَيۡءٍ خَلَقۡنَٰهُ بِقَدَرٖ
Hakika sisi Tumekiumba kila kitu kwa Qadar (makadirio)
وَمَآ أَمۡرُنَآ إِلَّا وَٰحِدَةٞ كَلَمۡحِۭ بِٱلۡبَصَرِ
Na amri Yetu haiwi ila ni moja tu, kama upepeso wa jicho
وَلَقَدۡ أَهۡلَكۡنَآ أَشۡيَاعَكُمۡ فَهَلۡ مِن مُّدَّكِرٖ
Na kwa yakini Tumewaangamiza wenzenu, je, basi yuko yeyote mwenye kuwaidhika?
وَكُلُّ شَيۡءٖ فَعَلُوهُ فِي ٱلزُّبُرِ
Na yote waliyoyafanya yamehi-fadhiwa kwenye vitabu
وَكُلُّ صَغِيرٖ وَكَبِيرٖ مُّسۡتَطَرٌ
Na kila kidogo na kikubwa kime-andikwa
إِنَّ ٱلۡمُتَّقِينَ فِي جَنَّـٰتٖ وَنَهَرٖ
Hakika Waliomcha Allah watakua kwenye mabustani Na Mito
فِي مَقۡعَدِ صِدۡقٍ عِندَ مَلِيكٖ مُّقۡتَدِرِۭ
Katika kizazi kilichoridhiwa mbele ya Mfalme aliye Muweza
ٱلرَّحۡمَٰنُ
(Allah) Mwingi wa rehma
عَلَّمَ ٱلۡقُرۡءَانَ
Amefundisha Qur’ani
خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ
Amemumba mwanadamu
عَلَّمَهُ ٱلۡبَيَانَ
Amemfundisha kusema (yaliyomo moyoni)
ٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُ بِحُسۡبَانٖ
Jua na mwezi (vinatembea) kwa hesabu (na mpangilio maalum)
وَٱلنَّجۡمُ وَٱلشَّجَرُ يَسۡجُدَانِ
Na nyota na miti vinasujudu
وَٱلسَّمَآءَ رَفَعَهَا وَوَضَعَ ٱلۡمِيزَانَ
Na mbingu ameinyanyua na ameweka mizani (kuthibitisha uadilifu na usawa)
أَلَّا تَطۡغَوۡاْ فِي ٱلۡمِيزَانِ
(Ameweka mizani) Ili msifanye dhulma katika upimaji
وَأَقِيمُواْ ٱلۡوَزۡنَ بِٱلۡقِسۡطِ وَلَا تُخۡسِرُواْ ٱلۡمِيزَانَ
Na simamisheni mzani kwa uadilifu na msipunguze mizani
وَٱلۡأَرۡضَ وَضَعَهَا لِلۡأَنَامِ
Na ardhi ameiweka kwa ajili ya viumbe
فِيهَا فَٰكِهَةٞ وَٱلنَّخۡلُ ذَاتُ ٱلۡأَكۡمَامِ
Humo mna matunda na mitende yenye makole
وَٱلۡحَبُّ ذُو ٱلۡعَصۡفِ وَٱلرَّيۡحَانُ
Na punje (nafaka ) zenye majani (makapi) na harufu nzuri
فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكُمَا تُكَذِّبَانِ
Basi ni zipi neema za Mola wenu mnazikanusha?
خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِن صَلۡصَٰلٖ كَٱلۡفَخَّارِ
Amemuumba mwanadamu kutokana na udongo utowao sauti kama vyombo vya udongo vilivyochomwa