Sourate: IBRAHIM 

Verset : 49

وَتَرَى ٱلۡمُجۡرِمِينَ يَوۡمَئِذٖ مُّقَرَّنِينَ فِي ٱلۡأَصۡفَادِ

Na utawaona wahalifu siku hiyo wamefungwa katika minyororo



Sourate: IBRAHIM 

Verset : 50

سَرَابِيلُهُم مِّن قَطِرَانٖ وَتَغۡشَىٰ وُجُوهَهُمُ ٱلنَّارُ

Mavazi yao yatakuwa ya lami (nyeusi tii na yananuka), na nyuso zao zitagubikwa na Moto



Sourate: IBRAHIM 

Verset : 51

لِيَجۡزِيَ ٱللَّهُ كُلَّ نَفۡسٖ مَّا كَسَبَتۡۚ إِنَّ ٱللَّهَ سَرِيعُ ٱلۡحِسَابِ

(Watu watatoka makaburini) ili Allah ailipe kila nafsi kwa yale iliyo yachuma. Hakika Allah ni Mwepesi wa kuhesabu



Sourate: IBRAHIM 

Verset : 52

هَٰذَا بَلَٰغٞ لِّلنَّاسِ وَلِيُنذَرُواْ بِهِۦ وَلِيَعۡلَمُوٓاْ أَنَّمَا هُوَ إِلَٰهٞ وَٰحِدٞ وَلِيَذَّكَّرَ أُوْلُواْ ٱلۡأَلۡبَٰبِ

Hii (Qur’ani) ni ufikisho (wa ujumbe) kwa watu, na ili waonywe na ili wapate kujua kuwa, uhakika ni kwamba Yeye (Allah) ni Muabudiwa mmoja tu, na ili wenye akili wapate kuonyeka