وَٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا وَٱسۡتَكۡبَرُواْ عَنۡهَآ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ
Na wale waliokadhibisha Aya zetu na kuzifanyia kiburi hao ni watu wa motoni, watakaa humo milele
فَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّنِ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبًا أَوۡ كَذَّبَ بِـَٔايَٰتِهِۦٓۚ أُوْلَـٰٓئِكَ يَنَالُهُمۡ نَصِيبُهُم مِّنَ ٱلۡكِتَٰبِۖ حَتَّىٰٓ إِذَا جَآءَتۡهُمۡ رُسُلُنَا يَتَوَفَّوۡنَهُمۡ قَالُوٓاْ أَيۡنَ مَا كُنتُمۡ تَدۡعُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِۖ قَالُواْ ضَلُّواْ عَنَّا وَشَهِدُواْ عَلَىٰٓ أَنفُسِهِمۡ أَنَّهُمۡ كَانُواْ كَٰفِرِينَ
Basi, ni nani dhalimu zaidi kuliko yule aliyemzushia uwongo Allah au kuzikadhibisha Aya zake? Hao itawapata sehemu ya maandiko (aliyowaandikia Allah) mpaka watakapowafikia Wajumbe wetu wakiwatoa roho watasema: Wako wapi mliokuwa mkiwaomba (mukiwaabudu) badala ya Allah watasema: “Wametupotea” na wamejishuhudia wenyewe kwamba walikuwa makafiri
قَالَ ٱدۡخُلُواْ فِيٓ أُمَمٖ قَدۡ خَلَتۡ مِن قَبۡلِكُم مِّنَ ٱلۡجِنِّ وَٱلۡإِنسِ فِي ٱلنَّارِۖ كُلَّمَا دَخَلَتۡ أُمَّةٞ لَّعَنَتۡ أُخۡتَهَاۖ حَتَّىٰٓ إِذَا ٱدَّارَكُواْ فِيهَا جَمِيعٗا قَالَتۡ أُخۡرَىٰهُمۡ لِأُولَىٰهُمۡ رَبَّنَا هَـٰٓؤُلَآءِ أَضَلُّونَا فَـَٔاتِهِمۡ عَذَابٗا ضِعۡفٗا مِّنَ ٱلنَّارِۖ قَالَ لِكُلّٖ ضِعۡفٞ وَلَٰكِن لَّا تَعۡلَمُونَ
(Allah) Atasema: Ingieni Motoni (nyinyi) pamoja na mataifa yaliyopita kabla yenu, ambao ni majini na watu. Kila umma unapoingia utawalaani (umma) ndugu yake (mwenzake) mpaka watakapokusanyika humo wote kwa pamoja, watasema wa mwisho wao (kuwashitaki) wa mwanzo wao (kwamba): “Ewe Mola wetu Mlezi, hawa ndio waliotupoteza, basi wape adhabu ya moto maradufu”. (Allah) Atasema: Kila mmoja wenu ana (adhabu) mara dufu na lakini hamjui
وَقَالَتۡ أُولَىٰهُمۡ لِأُخۡرَىٰهُمۡ فَمَا كَانَ لَكُمۡ عَلَيۡنَا مِن فَضۡلٖ فَذُوقُواْ ٱلۡعَذَابَ بِمَا كُنتُمۡ تَكۡسِبُونَ
Na watasema wa mwanzo wao kuwaambia wa mwisho wao (kwamba): Nyinyi hamkuwa na fadhila yoyote kwetu, basi onjeni adhabu kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyachuma
إِنَّ ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا وَٱسۡتَكۡبَرُواْ عَنۡهَا لَا تُفَتَّحُ لَهُمۡ أَبۡوَٰبُ ٱلسَّمَآءِ وَلَا يَدۡخُلُونَ ٱلۡجَنَّةَ حَتَّىٰ يَلِجَ ٱلۡجَمَلُ فِي سَمِّ ٱلۡخِيَاطِۚ وَكَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُجۡرِمِينَ
Hakika, wale wanaozikadhibisha aya zetu na kuzifanyia kiburi, hawatafunguliwa milango ya mbinguni na hawataingia Peponi isipokuwa kama ngamia ataingia (atapenya) katika tundu ya sindano. Na kama hivyo tunawalipa waovu
لَهُم مِّن جَهَنَّمَ مِهَادٞ وَمِن فَوۡقِهِمۡ غَوَاشٖۚ وَكَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلظَّـٰلِمِينَ
(Waovu) Jahanamu itakua kitanda chao na juu yao nguo za moto za kujifunika. Na hivyo ndivyo tunavowalipa madhalimu
وَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ لَا نُكَلِّفُ نَفۡسًا إِلَّا وُسۡعَهَآ أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡجَنَّةِۖ هُمۡ فِيهَا خَٰلِدُونَ
Na wale walioamini na wakatenda yaliyo mema hatutamkalifisha mtu yeyote (kufanya) isipokuwa tu aliwezalo. Hao ndio watu wa Peponi, wao humo watakaa milele
وَنَزَعۡنَا مَا فِي صُدُورِهِم مِّنۡ غِلّٖ تَجۡرِي مِن تَحۡتِهِمُ ٱلۡأَنۡهَٰرُۖ وَقَالُواْ ٱلۡحَمۡدُ لِلَّهِ ٱلَّذِي هَدَىٰنَا لِهَٰذَا وَمَا كُنَّا لِنَهۡتَدِيَ لَوۡلَآ أَنۡ هَدَىٰنَا ٱللَّهُۖ لَقَدۡ جَآءَتۡ رُسُلُ رَبِّنَا بِٱلۡحَقِّۖ وَنُودُوٓاْ أَن تِلۡكُمُ ٱلۡجَنَّةُ أُورِثۡتُمُوهَا بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ
Na tutaondoa husuda vifuani mwao, ikipita mito chini yao na watasema: “Kila sifa njema anaistahiki Allah ambaye ametuongoza kwenye hili na tusingeweza kuongoka kama Allah asingetuongoza”. Hakika kabisa, Mitume ya Allah imekuja kwa haki. Na (waumini huko peponi) wataitwa (na kuambiwa kwamba): Hii ndio pepo mliorithishwa kwa sababu ya yale mliyokuwa mkiyafanya
وَنَادَىٰٓ أَصۡحَٰبُ ٱلۡجَنَّةِ أَصۡحَٰبَ ٱلنَّارِ أَن قَدۡ وَجَدۡنَا مَا وَعَدَنَا رَبُّنَا حَقّٗا فَهَلۡ وَجَدتُّم مَّا وَعَدَ رَبُّكُمۡ حَقّٗاۖ قَالُواْ نَعَمۡۚ فَأَذَّنَ مُؤَذِّنُۢ بَيۡنَهُمۡ أَن لَّعۡنَةُ ٱللَّهِ عَلَى ٱلظَّـٰلِمِينَ
Na watu wa Peponi watawaita watu wa motoni (na kuwaambia): “Sisi kwa hakika tumekuta aliyotuahidi Mola wetu Mlezi ni kweli kabisa. Je, nyinyi mmekuta aliyowahidini Mola wenu ni kweli? (Watu wa Motoni) Watasema: Ndio. Basi atatangaza mtangazaji baina yao kwamba, laana ya Allah iwashukie madhalimu
ٱلَّذِينَ يَصُدُّونَ عَن سَبِيلِ ٱللَّهِ وَيَبۡغُونَهَا عِوَجٗا وَهُم بِٱلۡأٓخِرَةِ كَٰفِرُونَ
(Madhalimu) Ambao wanazuia (watu kufuata) njia ya Allah, na wanaitaka ipinde (iende vile wanavyotaka wao), na wao wanaikufuru Akhera
وَبَيۡنَهُمَا حِجَابٞۚ وَعَلَى ٱلۡأَعۡرَافِ رِجَالٞ يَعۡرِفُونَ كُلَّۢا بِسِيمَىٰهُمۡۚ وَنَادَوۡاْ أَصۡحَٰبَ ٱلۡجَنَّةِ أَن سَلَٰمٌ عَلَيۡكُمۡۚ لَمۡ يَدۡخُلُوهَا وَهُمۡ يَطۡمَعُونَ
Na baina yao (baina ya watu wa Peponi na watu wa Motoni) kuna kizuizi (cha muinuko/ukuta). Na juu ya muinuko (huo) kuna watu wanaowafahamu wote (watu wa Peponi na wa Motoni) kwa alama zao. Na watu wa muinuko (huo) watawaita watu wa Peponi (na kuwaambia): “Amani iwe kwenu” huku hawajaingia humo na wana tamaa (ya kuingia)
۞وَإِذَا صُرِفَتۡ أَبۡصَٰرُهُمۡ تِلۡقَآءَ أَصۡحَٰبِ ٱلنَّارِ قَالُواْ رَبَّنَا لَا تَجۡعَلۡنَا مَعَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلظَّـٰلِمِينَ
Na (watu walioko kwenye muinuko) macho yao yatakapogeuzwa yatazame upande wa watu wa Motoni, watasema: “Ewe Mola wetu, usituweke pamoja na watu madhalimu”
وَنَادَىٰٓ أَصۡحَٰبُ ٱلۡأَعۡرَافِ رِجَالٗا يَعۡرِفُونَهُم بِسِيمَىٰهُمۡ قَالُواْ مَآ أَغۡنَىٰ عَنكُمۡ جَمۡعُكُمۡ وَمَا كُنتُمۡ تَسۡتَكۡبِرُونَ
Na watu wa muinuko watawaita watu (wa Motoni) wanaowafahamu kwa alama zao na kuwaambia: “Haukukusaidieni wingi wenu wala hicho mlichokuwa mnafanyia kiburi
أَهَـٰٓؤُلَآءِ ٱلَّذِينَ أَقۡسَمۡتُمۡ لَا يَنَالُهُمُ ٱللَّهُ بِرَحۡمَةٍۚ ٱدۡخُلُواْ ٱلۡجَنَّةَ لَا خَوۡفٌ عَلَيۡكُمۡ وَلَآ أَنتُمۡ تَحۡزَنُونَ
Hivi hawa ndio wale (waumini waliokuwa wanyonge) mliokuwa mkiwaapia kwamba Allah hatawafikishia rehema? Ingieni Peponi, hamna hofu wala hamtahuzunika
وَنَادَىٰٓ أَصۡحَٰبُ ٱلنَّارِ أَصۡحَٰبَ ٱلۡجَنَّةِ أَنۡ أَفِيضُواْ عَلَيۡنَا مِنَ ٱلۡمَآءِ أَوۡ مِمَّا رَزَقَكُمُ ٱللَّهُۚ قَالُوٓاْ إِنَّ ٱللَّهَ حَرَّمَهُمَا عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ
Na watu motoni watawaita watu wa Peponi (na kuwaambia): Tumiminieni (kiasi japo kidogo cha) maji au katika vile (vitu vizuri) ambavyo Allah amekuruzukuni. (Watu wa Peponi) Watasema: Hakika, Allah ameviharamisha viwili hivyo kwa makafiri
ٱلَّذِينَ ٱتَّخَذُواْ دِينَهُمۡ لَهۡوٗا وَلَعِبٗا وَغَرَّتۡهُمُ ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَاۚ فَٱلۡيَوۡمَ نَنسَىٰهُمۡ كَمَا نَسُواْ لِقَآءَ يَوۡمِهِمۡ هَٰذَا وَمَا كَانُواْ بِـَٔايَٰتِنَا يَجۡحَدُونَ
Ambao wameifanya dini yao pumbao na mchezo, na maisha ya dunia yakawadanganya. Basi leo tunawasahau kama walivyosahau kukutana na siku yao hii, na kwa sababu walikuwa wanazipinga Aya zetu
وَلَقَدۡ جِئۡنَٰهُم بِكِتَٰبٖ فَصَّلۡنَٰهُ عَلَىٰ عِلۡمٍ هُدٗى وَرَحۡمَةٗ لِّقَوۡمٖ يُؤۡمِنُونَ
Na kwa hakika kabisa tumewa-letea kitabu tulichokifafanua kwa elimu, kikiwa ni muongozo na rehema kwa watu wanaoamini
هَلۡ يَنظُرُونَ إِلَّا تَأۡوِيلَهُۥۚ يَوۡمَ يَأۡتِي تَأۡوِيلُهُۥ يَقُولُ ٱلَّذِينَ نَسُوهُ مِن قَبۡلُ قَدۡ جَآءَتۡ رُسُلُ رَبِّنَا بِٱلۡحَقِّ فَهَل لَّنَا مِن شُفَعَآءَ فَيَشۡفَعُواْ لَنَآ أَوۡ نُرَدُّ فَنَعۡمَلَ غَيۡرَ ٱلَّذِي كُنَّا نَعۡمَلُۚ قَدۡ خَسِرُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ وَضَلَّ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَفۡتَرُونَ
Hawana wanachongoja isipokuwa tu matokeo yake. Siku yatakapokuja matokeo yake watasema wale waliokisahau (kitabu walicholetewa) kabla ya hapo kwamba: “Hakika, walikuja Mitume wa Mola wetu kwa haki. Basi je, kuna waombezi watuombee au turudishwe (duniani) na tufanye tofauti ya yale tuliyokuwa tunayafanya? Kwa hakika, wamezitia hasara nafsi zao, na yamewapotea yote waliyokuwa wakiyazusha
إِنَّ رَبَّكُمُ ٱللَّهُ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ فِي سِتَّةِ أَيَّامٖ ثُمَّ ٱسۡتَوَىٰ عَلَى ٱلۡعَرۡشِۖ يُغۡشِي ٱلَّيۡلَ ٱلنَّهَارَ يَطۡلُبُهُۥ حَثِيثٗا وَٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَ وَٱلنُّجُومَ مُسَخَّرَٰتِۭ بِأَمۡرِهِۦٓۗ أَلَا لَهُ ٱلۡخَلۡقُ وَٱلۡأَمۡرُۗ تَبَارَكَ ٱللَّهُ رَبُّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Hakika, Mola wenu Mlezi ni Allah ambaye ameziumba mbingu na ardhi katika siku sita, kisha akastawi juu ya Arshi. Anaufunika usiku kwa kuleta mchana, ukiufuata kwa haraka, na (ameumba) jua na mwezi na nyota vikiwa vimetiishwa (vimefanywa vitiifu kwa mwana-damu) kwa amri yake. Elewa (kwamba): kuumba na kuamrisha Ni kwake yeye tu. Ametukuka Allah, Mola Mlezi wa walimwengu wote
ٱدۡعُواْ رَبَّكُمۡ تَضَرُّعٗا وَخُفۡيَةًۚ إِنَّهُۥ لَا يُحِبُّ ٱلۡمُعۡتَدِينَ
Muombeni Mola wenu Mlezi kwa unyenyekevu na kificho (kimya kimya). Hakika, yeye (Allah) hawapendi wavukao mipaka (ya sheria zake)
وَلَا تُفۡسِدُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ بَعۡدَ إِصۡلَٰحِهَا وَٱدۡعُوهُ خَوۡفٗا وَطَمَعًاۚ إِنَّ رَحۡمَتَ ٱللَّهِ قَرِيبٞ مِّنَ ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Na msifanye uharibifu katika ardhi baada ya (ya Allah) kutengeneza na muombeni yeye (tu) kwa kuogopa (adhabu yake) na kutumai (rehema zake). Hakika, rehema za Allah zipo karibu na wenye kufanya mazuri
وَهُوَ ٱلَّذِي يُرۡسِلُ ٱلرِّيَٰحَ بُشۡرَۢا بَيۡنَ يَدَيۡ رَحۡمَتِهِۦۖ حَتَّىٰٓ إِذَآ أَقَلَّتۡ سَحَابٗا ثِقَالٗا سُقۡنَٰهُ لِبَلَدٖ مَّيِّتٖ فَأَنزَلۡنَا بِهِ ٱلۡمَآءَ فَأَخۡرَجۡنَا بِهِۦ مِن كُلِّ ٱلثَّمَرَٰتِۚ كَذَٰلِكَ نُخۡرِجُ ٱلۡمَوۡتَىٰ لَعَلَّكُمۡ تَذَكَّرُونَ
Na Yeye ndiye apelekae pepo zikiwa bishara ya kufika kwa rehema zake, hadi (pepo hizo) zinapobeba mawingu mazito tunayachunga (na kuyapeleka) kwenye mji uliokufa (kwa ukame) na tunateremsha hapo maji (mvua). Basi tukaotesha kwa mvua hizo kila aina ya matunda. Kama hivyo tunawafufua waliokufa, ili mpate kuonyeka
وَٱلۡبَلَدُ ٱلطَّيِّبُ يَخۡرُجُ نَبَاتُهُۥ بِإِذۡنِ رَبِّهِۦۖ وَٱلَّذِي خَبُثَ لَا يَخۡرُجُ إِلَّا نَكِدٗاۚ كَذَٰلِكَ نُصَرِّفُ ٱلۡأٓيَٰتِ لِقَوۡمٖ يَشۡكُرُونَ
Na nchi (ardhi) nzuri hutoa mimea yake kwa idhini ya Mola wake na nchi (ardhi) iliyokuwa mbaya haitoki (mimeya yake) ila kwa taabu mno. Kama hivyo tunazifafanua aya kwa watu wanaoshukuru
لَقَدۡ أَرۡسَلۡنَا نُوحًا إِلَىٰ قَوۡمِهِۦ فَقَالَ يَٰقَوۡمِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ مَا لَكُم مِّنۡ إِلَٰهٍ غَيۡرُهُۥٓ إِنِّيٓ أَخَافُ عَلَيۡكُمۡ عَذَابَ يَوۡمٍ عَظِيمٖ
Kwa hakika kabisa, tulimpeleka Nuhu kwa watu wake, akasema: Enyi watu wangu, muabuduni Allah (tu). Nyinyi hamna Mola mwingine zaidi yake. Hakika, mimi nakuhofieni (kupata) adhabu ya siku kubwa sana
قَالَ ٱلۡمَلَأُ مِن قَوۡمِهِۦٓ إِنَّا لَنَرَىٰكَ فِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٖ
Kundi la mamwinyi katika watu wake lilisema kuwa: Hakika, sisi tunakuona umo katika upotevu uliodhahiri sana
قَالَ يَٰقَوۡمِ لَيۡسَ بِي ضَلَٰلَةٞ وَلَٰكِنِّي رَسُولٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
(Mtume Nuhu) Akasema: Enyi watu wangu, mimi sina upotevu wowote, lakini mimi ni Mtume kutoka kwa Mola Mlezi wa wali-mwengu wote
أُبَلِّغُكُمۡ رِسَٰلَٰتِ رَبِّي وَأَنصَحُ لَكُمۡ وَأَعۡلَمُ مِنَ ٱللَّهِ مَا لَا تَعۡلَمُونَ
Ninakufikishieni ujumbe wa Mola wangu Mlezi na ninakupeni nasaha, na ninajua kwa Allah (mambo) msiyoyajua
أَوَعَجِبۡتُمۡ أَن جَآءَكُمۡ ذِكۡرٞ مِّن رَّبِّكُمۡ عَلَىٰ رَجُلٖ مِّنكُمۡ لِيُنذِرَكُمۡ وَلِتَتَّقُواْ وَلَعَلَّكُمۡ تُرۡحَمُونَ
Hivi mnastaajabu kwamba, umekufikieni ukumbusho kutoka kwa Mola wenu kupitia kwa mtu miongoni mwenu, ili akuonyeni na ili muwe wacha Mungu na ili mpate rehema?
فَكَذَّبُوهُ فَأَنجَيۡنَٰهُ وَٱلَّذِينَ مَعَهُۥ فِي ٱلۡفُلۡكِ وَأَغۡرَقۡنَا ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَآۚ إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَوۡمًا عَمِينَ
Basi wakamkadhibisha na tukamuokoa yeye na wale waliokuwa pamoja naye katika jahazi, na tukawazamisha baharini wale waliozikadhibisha aya zetu. Bila shaka, hao walikuwa watu vipofu (wana nyoyo)
۞وَإِلَىٰ عَادٍ أَخَاهُمۡ هُودٗاۚ قَالَ يَٰقَوۡمِ ٱعۡبُدُواْ ٱللَّهَ مَا لَكُم مِّنۡ إِلَٰهٍ غَيۡرُهُۥٓۚ أَفَلَا تَتَّقُونَ
Na kwa (kabila la) Aadi (tulimtuma) ndugu yao Hudi akasema: Enyi watu wangu, muabuduni Allah; hamna nyinyi Mola mwingine Mlezi zaidi yake. Basi hamuogopi (adhabu yake)?