Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 84

وَإِذۡ أَخَذۡنَا مِيثَٰقَكُمۡ لَا تَسۡفِكُونَ دِمَآءَكُمۡ وَلَا تُخۡرِجُونَ أَنفُسَكُم مِّن دِيَٰرِكُمۡ ثُمَّ أَقۡرَرۡتُمۡ وَأَنتُمۡ تَشۡهَدُونَ

Na (kumbukeni) tulipochukua ahadi kwenu kwamba msimwage damu zenu, wala msiwatoe watu wenu katika nyumba zenu, nanyi mkakubali ilhali mnashuhudia



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 85

ثُمَّ أَنتُمۡ هَـٰٓؤُلَآءِ تَقۡتُلُونَ أَنفُسَكُمۡ وَتُخۡرِجُونَ فَرِيقٗا مِّنكُم مِّن دِيَٰرِهِمۡ تَظَٰهَرُونَ عَلَيۡهِم بِٱلۡإِثۡمِ وَٱلۡعُدۡوَٰنِ وَإِن يَأۡتُوكُمۡ أُسَٰرَىٰ تُفَٰدُوهُمۡ وَهُوَ مُحَرَّمٌ عَلَيۡكُمۡ إِخۡرَاجُهُمۡۚ أَفَتُؤۡمِنُونَ بِبَعۡضِ ٱلۡكِتَٰبِ وَتَكۡفُرُونَ بِبَعۡضٖۚ فَمَا جَزَآءُ مَن يَفۡعَلُ ذَٰلِكَ مِنكُمۡ إِلَّا خِزۡيٞ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۖ وَيَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ يُرَدُّونَ إِلَىٰٓ أَشَدِّ ٱلۡعَذَابِۗ وَمَا ٱللَّهُ بِغَٰفِلٍ عَمَّا تَعۡمَلُونَ

Kisha nyinyi hao hao mnauana, na mnalitoa kundi kati yenu katika nyumba zao, mkisaidiana dhidi yao, kwa dhambi na uhasama. Na kama wakikujieni ilhali wakiwa mateka mnawakomboa wakati imeharamishwa kwenu kuwafukuza. Je, mnaamini baadhi ya maandiko na mengine mnayakataa? Basi hakuna malipo kwa mwenye kuyafanya hayo kati yenu isipokuwa tu hizaya katika maisha ya duniani, na Siku ya Kiyama watarejeshwa kwenye adhabu kali zaidi, na Allah si Mwenye kughafilika na yale mnayoyatenda



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 86

أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ ٱشۡتَرَوُاْ ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا بِٱلۡأٓخِرَةِۖ فَلَا يُخَفَّفُ عَنۡهُمُ ٱلۡعَذَابُ وَلَا هُمۡ يُنصَرُونَ

Hao ndio walionunua uhai wa dunia kwa Akhera, kwahiyo hawatapunguziwa adhabu na wala hawatanusuriwa



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 87

وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَا مُوسَى ٱلۡكِتَٰبَ وَقَفَّيۡنَا مِنۢ بَعۡدِهِۦ بِٱلرُّسُلِۖ وَءَاتَيۡنَا عِيسَى ٱبۡنَ مَرۡيَمَ ٱلۡبَيِّنَٰتِ وَأَيَّدۡنَٰهُ بِرُوحِ ٱلۡقُدُسِۗ أَفَكُلَّمَا جَآءَكُمۡ رَسُولُۢ بِمَا لَا تَهۡوَىٰٓ أَنفُسُكُمُ ٱسۡتَكۡبَرۡتُمۡ فَفَرِيقٗا كَذَّبۡتُمۡ وَفَرِيقٗا تَقۡتُلُونَ

Na kwa hakika tulimpa Musa Kitabu, na tukafuatishia baada yake kwa kupeleka Mitume, na tukampa Isa Mwana wa Mariamu miujiza iliyo wazi na tukampa nguvu kwa Roho Mtakatifu (Jibrili). Basi je, kila Mtume akikuleteeni yale yasiyopendwa na nafsi zenu mnafanya kiburi? (Mitume) Wengine mliwapinga na wengine mliwaua



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 88

وَقَالُواْ قُلُوبُنَا غُلۡفُۢۚ بَل لَّعَنَهُمُ ٱللَّهُ بِكُفۡرِهِمۡ فَقَلِيلٗا مَّا يُؤۡمِنُونَ

Na wakasema: Nyoyo zetu zimezibwa. Bali Allah amewalaani kwa kufuru zao, kwa hiyo imani yao ni kidogo mno



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 89

وَلَمَّا جَآءَهُمۡ كِتَٰبٞ مِّنۡ عِندِ ٱللَّهِ مُصَدِّقٞ لِّمَا مَعَهُمۡ وَكَانُواْ مِن قَبۡلُ يَسۡتَفۡتِحُونَ عَلَى ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فَلَمَّا جَآءَهُم مَّا عَرَفُواْ كَفَرُواْ بِهِۦۚ فَلَعۡنَةُ ٱللَّهِ عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ

Na kilipowafikia Kitabu kito-kacho kwa Allah, kinachothibitisha (yale) waliyokuwa nayo, na huko kabla walikuwa wakiomba nusra dhidi ya wale waliokufuru, basi alipowajia huyo waliye mjua, walimkataa. Basi laana ya Allah iwe juu ya makafiri



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 90

بِئۡسَمَا ٱشۡتَرَوۡاْ بِهِۦٓ أَنفُسَهُمۡ أَن يَكۡفُرُواْ بِمَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ بَغۡيًا أَن يُنَزِّلَ ٱللَّهُ مِن فَضۡلِهِۦ عَلَىٰ مَن يَشَآءُ مِنۡ عِبَادِهِۦۖ فَبَآءُو بِغَضَبٍ عَلَىٰ غَضَبٖۚ وَلِلۡكَٰفِرِينَ عَذَابٞ مُّهِينٞ

Ni kibaya mno walichojiuzia[1] cha kukataa yale aliyoyateremsha Allah kwa husuda ya kuwa Allah anamteremshia fadhila zake amtakaye miongoni mwa waja wake. Kwa sababu hiyo, walistahiki ghadhabu juu ya ghadhabu. Na makafiri watapata adhabu yenye kudhalilisha


1- - Walichojichagulia


Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 91

وَإِذَا قِيلَ لَهُمۡ ءَامِنُواْ بِمَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ قَالُواْ نُؤۡمِنُ بِمَآ أُنزِلَ عَلَيۡنَا وَيَكۡفُرُونَ بِمَا وَرَآءَهُۥ وَهُوَ ٱلۡحَقُّ مُصَدِّقٗا لِّمَا مَعَهُمۡۗ قُلۡ فَلِمَ تَقۡتُلُونَ أَنۢبِيَآءَ ٱللَّهِ مِن قَبۡلُ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ

Na wanapoambiwa: Yaaminini yale aliyoyateremsha Allah, husema: Tunaamini yale tulioteremshiwa na huyapinga yasiyokuwa hayo, nayo ndio haki yenye kuafiki waliyo nayo. Sema: Ni kwanini (mlikuwa) mnawaua Manabii wa Allah hapo zamani kama ninyi ni waumini?



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 92

۞وَلَقَدۡ جَآءَكُم مُّوسَىٰ بِٱلۡبَيِّنَٰتِ ثُمَّ ٱتَّخَذۡتُمُ ٱلۡعِجۡلَ مِنۢ بَعۡدِهِۦ وَأَنتُمۡ ظَٰلِمُونَ

Na kwa hakika kabisa, alikujieni Musa akiwa na miujiza ya wazi, kisha baada yake[1] mkamfanya Ndama (Mungu) na ilhali nyinyi ni wenye kudhulumu (nafsi zenu)


1- - Baada ya Musa kwenda kwenye kiaga cha kukutana na Mola wake


Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 93

وَإِذۡ أَخَذۡنَا مِيثَٰقَكُمۡ وَرَفَعۡنَا فَوۡقَكُمُ ٱلطُّورَ خُذُواْ مَآ ءَاتَيۡنَٰكُم بِقُوَّةٖ وَٱسۡمَعُواْۖ قَالُواْ سَمِعۡنَا وَعَصَيۡنَا وَأُشۡرِبُواْ فِي قُلُوبِهِمُ ٱلۡعِجۡلَ بِكُفۡرِهِمۡۚ قُلۡ بِئۡسَمَا يَأۡمُرُكُم بِهِۦٓ إِيمَٰنُكُمۡ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ

Na (kumbukeni) tulipochukua ahadi yenu na tukauinua (mlima) Turi juu yenu (tukakuambieni): Yashikeni kwa nguvu tuliyokupeni na sikilizeni. Wakasema: Tumesikia na tumeasi, na wakanyweshwa mioyoni mwao (kupenda) kuabudu ndama kwa sababu ya kufuru zao. Waambie: Ni jambo baya sana inavyokuamrisheni imani yenu, kama ninyi ni waumini



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 94

قُلۡ إِن كَانَتۡ لَكُمُ ٱلدَّارُ ٱلۡأٓخِرَةُ عِندَ ٱللَّهِ خَالِصَةٗ مِّن دُونِ ٱلنَّاسِ فَتَمَنَّوُاْ ٱلۡمَوۡتَ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Sema: Ikiwa makazi ya Akhera (yaliyopo) kwa Allah ni yenu tu kuliko watu wengine, basi tamanini kufa ikiwa nyinyi ni wakweli



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 95

وَلَن يَتَمَنَّوۡهُ أَبَدَۢا بِمَا قَدَّمَتۡ أَيۡدِيهِمۡۚ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِٱلظَّـٰلِمِينَ

Asilani, hawatalitamani hilo kwa sababu yale yaliyotangulizwa na mikono yao, na Allah anawajua sana wenye kudhulumu



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 96

وَلَتَجِدَنَّهُمۡ أَحۡرَصَ ٱلنَّاسِ عَلَىٰ حَيَوٰةٖ وَمِنَ ٱلَّذِينَ أَشۡرَكُواْۚ يَوَدُّ أَحَدُهُمۡ لَوۡ يُعَمَّرُ أَلۡفَ سَنَةٖ وَمَا هُوَ بِمُزَحۡزِحِهِۦ مِنَ ٱلۡعَذَابِ أَن يُعَمَّرَۗ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِمَا يَعۡمَلُونَ

Na kwa hakika kabisa, utawakuta wao (Wayahudi) ndio wanaojali mno uhai[1] kuliko watu wote, na miongoni mwa washirikishaji (pia utakuta nao wako hivyo); anatamani mmoja wao angalau apewe umri wa miaka elfu moja. Na kupewa kwake umri mrefu hakutamuepushia adhabu, na Allah ni Mwenye kuyaona wanayoyatenda


1- - Katika maisha ya duniani


Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 97

قُلۡ مَن كَانَ عَدُوّٗا لِّـجِبۡرِيلَ فَإِنَّهُۥ نَزَّلَهُۥ عَلَىٰ قَلۡبِكَ بِإِذۡنِ ٱللَّهِ مُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيۡهِ وَهُدٗى وَبُشۡرَىٰ لِلۡمُؤۡمِنِينَ

Sema: Mwenye kuwa adui wa Jibrili, basi (ajue kuwa) yeye ndiye aliyeuteremsha Wahyi (Qur’an) moyoni mwako kwa idhini ya Allah, unaosadikisha yale yaliyokuwa kabla yake na ni muongozo na bishara kwa waumini



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 98

مَن كَانَ عَدُوّٗا لِّلَّهِ وَمَلَـٰٓئِكَتِهِۦ وَرُسُلِهِۦ وَجِبۡرِيلَ وَمِيكَىٰلَ فَإِنَّ ٱللَّهَ عَدُوّٞ لِّلۡكَٰفِرِينَ

Mwenye kuwa adui wa Allah na Malaika wake na Mitume wake na Jibrilina Mikaili, basi hakika, Allah ni adui wa makafiri wote



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 99

وَلَقَدۡ أَنزَلۡنَآ إِلَيۡكَ ءَايَٰتِۭ بَيِّنَٰتٖۖ وَمَا يَكۡفُرُ بِهَآ إِلَّا ٱلۡفَٰسِقُونَ

Na kwa yakini kabisa, tume-kuteremshia hoja za wazi na hawazikanushi isipokuwa waovu tu



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 100

أَوَكُلَّمَا عَٰهَدُواْ عَهۡدٗا نَّبَذَهُۥ فَرِيقٞ مِّنۡهُمۚ بَلۡ أَكۡثَرُهُمۡ لَا يُؤۡمِنُونَ

Hivi ni kwanini kila watoapo ahadi, kuna kundi miongoni mwao linaivunja ahadi hiyo! Lakini (ukweli ni kwamba) wengi wao hawaamini



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 101

وَلَمَّا جَآءَهُمۡ رَسُولٞ مِّنۡ عِندِ ٱللَّهِ مُصَدِّقٞ لِّمَا مَعَهُمۡ نَبَذَ فَرِيقٞ مِّنَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡكِتَٰبَ كِتَٰبَ ٱللَّهِ وَرَآءَ ظُهُورِهِمۡ كَأَنَّهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ

Na alipowafikia Mtume kutoka kwa Allah mwenye kusadikisha yale waliyo nayo, kundi miongoni mwa wale waliopewa Kitabu walikitupa Kitabu cha Allah nyuma ya migongo yao kama kwamba hawajui



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 102

وَٱتَّبَعُواْ مَا تَتۡلُواْ ٱلشَّيَٰطِينُ عَلَىٰ مُلۡكِ سُلَيۡمَٰنَۖ وَمَا كَفَرَ سُلَيۡمَٰنُ وَلَٰكِنَّ ٱلشَّيَٰطِينَ كَفَرُواْ يُعَلِّمُونَ ٱلنَّاسَ ٱلسِّحۡرَ وَمَآ أُنزِلَ عَلَى ٱلۡمَلَكَيۡنِ بِبَابِلَ هَٰرُوتَ وَمَٰرُوتَۚ وَمَا يُعَلِّمَانِ مِنۡ أَحَدٍ حَتَّىٰ يَقُولَآ إِنَّمَا نَحۡنُ فِتۡنَةٞ فَلَا تَكۡفُرۡۖ فَيَتَعَلَّمُونَ مِنۡهُمَا مَا يُفَرِّقُونَ بِهِۦ بَيۡنَ ٱلۡمَرۡءِ وَزَوۡجِهِۦۚ وَمَا هُم بِضَآرِّينَ بِهِۦ مِنۡ أَحَدٍ إِلَّا بِإِذۡنِ ٱللَّهِۚ وَيَتَعَلَّمُونَ مَا يَضُرُّهُمۡ وَلَا يَنفَعُهُمۡۚ وَلَقَدۡ عَلِمُواْ لَمَنِ ٱشۡتَرَىٰهُ مَا لَهُۥ فِي ٱلۡأٓخِرَةِ مِنۡ خَلَٰقٖۚ وَلَبِئۡسَ مَا شَرَوۡاْ بِهِۦٓ أَنفُسَهُمۡۚ لَوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ

Na wamefuata yale yanayoso-mwa na Mashetani katika (wakati wa) ufalme wa Suleimani. Na Suleimani hakukufuru, lakini Mashetani ndio waliokufuru; (kwa sababu) wanawafundisha watu uchawi na yaliyoteremshwa kwa Malaika wawili Haruta na Maruta katika mji wa Babil. Na wala hawamfundishi yeyote mpaka wamwambie: Hakika sisi ni mtihani, basi usikufuru. Basi wakajifunza kwao yale yawezayo kumfarakanisha mtu na mkewe. Na wala wao hawana uwezo wa kumdhuru yeyote kwa hayo ila kwa idhini ya Allah tu. Na wanajifunza yale yanayowadhuru na wala hayawanufaishi. Na kwa yakini wamejua kwamba aliyechagua haya hatakuwa na fungu lolote Akhera. Na nikibaya mnokilewalichozichagulianafsizao laiti wangekuwa wanajua



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 103

وَلَوۡ أَنَّهُمۡ ءَامَنُواْ وَٱتَّقَوۡاْ لَمَثُوبَةٞ مِّنۡ عِندِ ٱللَّهِ خَيۡرٞۚ لَّوۡ كَانُواْ يَعۡلَمُونَ

Na lau wangeamini na kumcha Allah, bila ya shaka malipo yatokayo kwa Allah yangekuwa bora laiti wangelijua



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 104

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَقُولُواْ رَٰعِنَا وَقُولُواْ ٱنظُرۡنَا وَٱسۡمَعُواْۗ وَلِلۡكَٰفِرِينَ عَذَابٌ أَلِيمٞ

Enyi mlioamini! Msiseme: “Raainaa” na semeni “Undhurnaa”. Na sikieni. Na makafiri watapata adhabu iumizayo



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 105

مَّا يَوَدُّ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ مِنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ وَلَا ٱلۡمُشۡرِكِينَ أَن يُنَزَّلَ عَلَيۡكُم مِّنۡ خَيۡرٖ مِّن رَّبِّكُمۡۚ وَٱللَّهُ يَخۡتَصُّ بِرَحۡمَتِهِۦ مَن يَشَآءُۚ وَٱللَّهُ ذُو ٱلۡفَضۡلِ ٱلۡعَظِيمِ

Watu wa Kitabu waliokufuru na washirikishaji hawapendi mteremshiwe heri yoyote kutoka kwa Mola wenu. Na Allah humkusudia (kumpa) rehema zake amtakaye, na Allah ni Mwenye fadhila kubwa



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 106

۞مَا نَنسَخۡ مِنۡ ءَايَةٍ أَوۡ نُنسِهَا نَأۡتِ بِخَيۡرٖ مِّنۡهَآ أَوۡ مِثۡلِهَآۗ أَلَمۡ تَعۡلَمۡ أَنَّ ٱللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٌ

Hakuna Aya yoyote tunayoifuta au kuisahaulisha isipokuwa kwamba tunaleta iliyo bora zaidi kuliko ile au iliyo mfano wake. Je, hujui kwamba Allah ni Muweza wa kila jambo?



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 107

أَلَمۡ تَعۡلَمۡ أَنَّ ٱللَّهَ لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۗ وَمَا لَكُم مِّن دُونِ ٱللَّهِ مِن وَلِيّٖ وَلَا نَصِيرٍ

Je, hujui kwamba Allah ndiye Mwenye ufalme wa mbinguni na ardhini? Na nyinyi hamna mlinzi wala msaidizi mwingine badala ya Allah



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 108

أَمۡ تُرِيدُونَ أَن تَسۡـَٔلُواْ رَسُولَكُمۡ كَمَا سُئِلَ مُوسَىٰ مِن قَبۡلُۗ وَمَن يَتَبَدَّلِ ٱلۡكُفۡرَ بِٱلۡإِيمَٰنِ فَقَدۡ ضَلَّ سَوَآءَ ٱلسَّبِيلِ

Au mnataka kumuuliza Mtume wenu kama (Mtume) Musa alivyoulizwa hapo zamani? Na anayebadilisha imani kwa ukafiri, bila shaka ameipotea njia yasawa



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 109

وَدَّ كَثِيرٞ مِّنۡ أَهۡلِ ٱلۡكِتَٰبِ لَوۡ يَرُدُّونَكُم مِّنۢ بَعۡدِ إِيمَٰنِكُمۡ كُفَّارًا حَسَدٗا مِّنۡ عِندِ أَنفُسِهِم مِّنۢ بَعۡدِ مَا تَبَيَّنَ لَهُمُ ٱلۡحَقُّۖ فَٱعۡفُواْ وَٱصۡفَحُواْ حَتَّىٰ يَأۡتِيَ ٱللَّهُ بِأَمۡرِهِۦٓۗ إِنَّ ٱللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ

Watu wa Kitabu wengi wanapenda laiti wakurudisheni muwe makafiri baada ya kuamini kwenu, kwa sababu ya husuda iliyomo nyoyoni mwao baada ya kuwa haki imewapambanukia. Basi sameheni na puuzeni mpaka Allah alete amri yake. Hakika, Allah ni Muweza sana wa kila jambo



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 110

وَأَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَءَاتُواْ ٱلزَّكَوٰةَۚ وَمَا تُقَدِّمُواْ لِأَنفُسِكُم مِّنۡ خَيۡرٖ تَجِدُوهُ عِندَ ٱللَّهِۗ إِنَّ ٱللَّهَ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرٞ

Na simamisheni Swala na toeni Zaka, na heri yoyote muitanguliziayo kwa ajili yenu mtaikuta mbele ya Allah. Hakika, Allah anayaona mno mnayoyatenda



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 111

وَقَالُواْ لَن يَدۡخُلَ ٱلۡجَنَّةَ إِلَّا مَن كَانَ هُودًا أَوۡ نَصَٰرَىٰۗ تِلۡكَ أَمَانِيُّهُمۡۗ قُلۡ هَاتُواْ بُرۡهَٰنَكُمۡ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Na wamesema: Katu, hataingia Peponi isipokuwa tu Myahudi au Mnaswara! Hayo ndio matamanio yao. Sema: Leteni ushahidi wenu kama ninyi ni wa kweli



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 112

بَلَىٰۚ مَنۡ أَسۡلَمَ وَجۡهَهُۥ لِلَّهِ وَهُوَ مُحۡسِنٞ فَلَهُۥٓ أَجۡرُهُۥ عِندَ رَبِّهِۦ وَلَا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ

Naam, wenye kujisalimisha kwa Allah na ilhali wanatenda yaliyo mazuri, basi watapata malipo yao kwa Mola wao, na hawatakuwa na hofu na hawatahuzunika



Sourate: AL-BAQARAH 

Verset : 113

وَقَالَتِ ٱلۡيَهُودُ لَيۡسَتِ ٱلنَّصَٰرَىٰ عَلَىٰ شَيۡءٖ وَقَالَتِ ٱلنَّصَٰرَىٰ لَيۡسَتِ ٱلۡيَهُودُ عَلَىٰ شَيۡءٖ وَهُمۡ يَتۡلُونَ ٱلۡكِتَٰبَۗ كَذَٰلِكَ قَالَ ٱلَّذِينَ لَا يَعۡلَمُونَ مِثۡلَ قَوۡلِهِمۡۚ فَٱللَّهُ يَحۡكُمُ بَيۡنَهُمۡ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ فِيمَا كَانُواْ فِيهِ يَخۡتَلِفُونَ

Na Wayahudi wamesema: Manaswara hawa na kitu (chochote cha maana). Na Manaswara wame-sema: Wayahudi hawana kitu (chochote cha maana), na wao (wote) wanasoma Kitabu (kitakatifu kitokacho kwa Mola wao). Kama hivyo, wale ambao hawajui kitu wamesema mfano wa maneno yao. Basi Allah atahukumu baina yao Siku ya Kiyama katika yale waliyokuwa wakitafautiana