قُلۡ تَرَبَّصُواْ فَإِنِّي مَعَكُم مِّنَ ٱلۡمُتَرَبِّصِينَ
Sema subirini basi hakika mimi pamoja nanyi ni miongoni mwa wenye kusubiri
Partager :
أَمۡ تَأۡمُرُهُمۡ أَحۡلَٰمُهُم بِهَٰذَآۚ أَمۡ هُمۡ قَوۡمٞ طَاغُونَ
Au zinawaamuru wao ndoto zao kwa hili au wao ni watu waovu
أَمۡ يَقُولُونَ تَقَوَّلَهُۥۚ بَل لَّا يُؤۡمِنُونَ
Au wanasema ameizua hiyo qurani bali hawaamini
فَلۡيَأۡتُواْ بِحَدِيثٖ مِّثۡلِهِۦٓ إِن كَانُواْ صَٰدِقِينَ
Basi walete mazungumzo (Quran) mfano wake kama watakua wakweli
أَمۡ خُلِقُواْ مِنۡ غَيۡرِ شَيۡءٍ أَمۡ هُمُ ٱلۡخَٰلِقُونَ
Au wameumbwa pasipo na kitu chochote (bila ya muumba) au wao ndio waumbaji?
أَمۡ خَلَقُواْ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَۚ بَل لَّا يُوقِنُونَ
Au wameumba mbingu na ardhi? Bali hawana yakini
أَمۡ عِندَهُمۡ خَزَآئِنُ رَبِّكَ أَمۡ هُمُ ٱلۡمُصَۜيۡطِرُونَ
Au wanazo hazina za Mola wako mlezi, au wao ndio wenye madaraka? (wenye kudhibiti)?
أَمۡ لَهُمۡ سُلَّمٞ يَسۡتَمِعُونَ فِيهِۖ فَلۡيَأۡتِ مُسۡتَمِعُهُم بِسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٍ
Au wanazo ngazi wanasikilizia kwa makini humo? Basi msikilizaji wao alete dalili bayana
أَمۡ لَهُ ٱلۡبَنَٰتُ وَلَكُمُ ٱلۡبَنُونَ
Au (Allah) Ana watoto wa kike, nanyi mna watoto wa kiume?
أَمۡ تَسۡـَٔلُهُمۡ أَجۡرٗا فَهُم مِّن مَّغۡرَمٖ مُّثۡقَلُونَ
Au unawaomba ujira kwa hiyo wameelemewa na uzito wa gharama?
أَمۡ عِندَهُمُ ٱلۡغَيۡبُ فَهُمۡ يَكۡتُبُونَ
Au wanayo elimu ya ghayb kisha wao wanaandika?
أَمۡ يُرِيدُونَ كَيۡدٗاۖ فَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ هُمُ ٱلۡمَكِيدُونَ
Au wanakusudia hila (shari)? Basi wale waliokufuru wao ndio watakaopangiwa hila
أَمۡ لَهُمۡ إِلَٰهٌ غَيۡرُ ٱللَّهِۚ سُبۡحَٰنَ ٱللَّهِ عَمَّا يُشۡرِكُونَ
Au wana wao mungu asiye Allah utakasifu ni wake allah na yote wanayomshirikisha nayo
وَإِن يَرَوۡاْ كِسۡفٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ سَاقِطٗا يَقُولُواْ سَحَابٞ مَّرۡكُومٞ
Na hata wangeliona pande la moto kutoka mbinguni linaanguka wangelisema: Mawingu tu yamerundikana
فَذَرۡهُمۡ حَتَّىٰ يُلَٰقُواْ يَوۡمَهُمُ ٱلَّذِي فِيهِ يُصۡعَقُونَ
Basi waachilie mbali mpaka wakutane na Siku yao ambayo humo wataangamizwa
يَوۡمَ لَا يُغۡنِي عَنۡهُمۡ كَيۡدُهُمۡ شَيۡـٔٗا وَلَا هُمۡ يُنصَرُونَ
Siku ambayo njama zao hazitowafaa kitu chochote, na wala wao hawatonusuriwa
وَإِنَّ لِلَّذِينَ ظَلَمُواْ عَذَابٗا دُونَ ذَٰلِكَ وَلَٰكِنَّ أَكۡثَرَهُمۡ لَا يَعۡلَمُونَ
Na hakika wale waliodhulumu watapata adhabu nyingine isiyokuwa hiyo, lakini wengi wao hawajui
وَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ فَإِنَّكَ بِأَعۡيُنِنَاۖ وَسَبِّحۡ بِحَمۡدِ رَبِّكَ حِينَ تَقُومُ
Na subiri hukumu ya mola wako mlezi na hakika wewe uko machoni kwetu (uangalizi wetu) na msabihi Mola wako mlezi pamoja na kusifu wakati unapoamka
وَمِنَ ٱلَّيۡلِ فَسَبِّحۡهُ وَإِدۡبَٰرَ ٱلنُّجُومِ
Na katika usiku Msabbih na zinapokuchwa nyota
وَٱلنَّجۡمِ إِذَا هَوَىٰ
Nina apa kwa nyota zinapozama
مَا ضَلَّ صَاحِبُكُمۡ وَمَا غَوَىٰ
Hakupotoka swahibu wenu na wala hakupotoka
وَمَا يَنطِقُ عَنِ ٱلۡهَوَىٰٓ
Na hasemi (neno lolote lile) kwa utashi wa nafsi (yake)
إِنۡ هُوَ إِلَّا وَحۡيٞ يُوحَىٰ
Hayakuwa hayo (anayaoyasema) isipokuwa tu ni Wahy unaofunuliwa
عَلَّمَهُۥ شَدِيدُ ٱلۡقُوَىٰ
Amemfundisha (Malaika Jibrili) Mwenye nguvu kubwa
ذُو مِرَّةٖ فَٱسۡتَوَىٰ
Mwenye nguvu na hekima na akakaa katika umbile lake halisi
وَهُوَ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡأَعۡلَىٰ
Naye yuko juu kabisa katika upeo wa macho
ثُمَّ دَنَا فَتَدَلَّىٰ
Kisha akakurubia na akashuka
فَكَانَ قَابَ قَوۡسَيۡنِ أَوۡ أَدۡنَىٰ
Kisha akawa kiasi cha umbali wa mipinde miwili au karibu zaidi
فَأَوۡحَىٰٓ إِلَىٰ عَبۡدِهِۦ مَآ أَوۡحَىٰ
(Allah) Akamfunulia Wahy mja Wake yale Aliyomfunulia Wahy
مَا كَذَبَ ٱلۡفُؤَادُ مَا رَأَىٰٓ
Moyo (wake) haukukadhibisha yale aliyoyaona