Sourate: AL-INSAAN

Verset : 11

فَوَقَىٰهُمُ ٱللَّهُ شَرَّ ذَٰلِكَ ٱلۡيَوۡمِ وَلَقَّىٰهُمۡ نَضۡرَةٗ وَسُرُورٗا

Basi Allah Atawakinga na shari ya siku hiyo, na Atawapa nuru na kuwakutanisha na uchangamfu na furaha



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 12

وَجَزَىٰهُم بِمَا صَبَرُواْ جَنَّةٗ وَحَرِيرٗا

Na Atawalipa kwasababu ya kusubiri kwao, Pepo na nguo za hariri



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 13

مُّتَّكِـِٔينَ فِيهَا عَلَى ٱلۡأَرَآئِكِۖ لَا يَرَوۡنَ فِيهَا شَمۡسٗا وَلَا زَمۡهَرِيرٗا

Humo wataegemea juu ya viti vya enzi, hawataona (hawatahisi) humo jua kali wala baridi kali.[1]


1- - Aya ni dalili kuwa Akhera kuna adhabu ya Baridi. Kama alivyopokea Imamu Bukhariy na Muslim- kutoka kwa Abuu Hurairah (Allah amuwiye radhh) amesema; amesema Mtume wa Allah (Rehema na amani ziwe juu yake):-


Sourate: AL-INSAAN

Verset : 14

وَدَانِيَةً عَلَيۡهِمۡ ظِلَٰلُهَا وَذُلِّلَتۡ قُطُوفُهَا تَذۡلِيلٗا

Na vivuli vyake vitakuwa karibu yao, na mashada ya matunda yataning’inia mpaka chini



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 15

وَيُطَافُ عَلَيۡهِم بِـَٔانِيَةٖ مِّن فِضَّةٖ وَأَكۡوَابٖ كَانَتۡ قَوَارِيرَا۠

Na watazungushiwa vyombo vya fedha, na bilauri zilokuwa za vigae



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 16

قَوَارِيرَاْ مِن فِضَّةٖ قَدَّرُوهَا تَقۡدِيرٗا

Vigae safi kutokana na fedha wamezipima kwa kipimo



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 17

وَيُسۡقَوۡنَ فِيهَا كَأۡسٗا كَانَ مِزَاجُهَا زَنجَبِيلًا

Na humo watanyweshwa kinywaji kilicho changanyika na tangawizi



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 18

عَيۡنٗا فِيهَا تُسَمَّىٰ سَلۡسَبِيلٗا

Hiyo ni chemchem iliyo humo inaitwa Salsabil



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 19

۞وَيَطُوفُ عَلَيۡهِمۡ وِلۡدَٰنٞ مُّخَلَّدُونَ إِذَا رَأَيۡتَهُمۡ حَسِبۡتَهُمۡ لُؤۡلُؤٗا مَّنثُورٗا

Na watawazungukia wavulana wasio pevuka wakiwatumikia, ukiwaona utadhani ni lulu zilizo tawanywa



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 20

وَإِذَا رَأَيۡتَ ثَمَّ رَأَيۡتَ نَعِيمٗا وَمُلۡكٗا كَبِيرًا

Na utakapo yaona, utakuwa umeona neema na ufalme mkubwa



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 21

عَٰلِيَهُمۡ ثِيَابُ سُندُسٍ خُضۡرٞ وَإِسۡتَبۡرَقٞۖ وَحُلُّوٓاْ أَسَاوِرَ مِن فِضَّةٖ وَسَقَىٰهُمۡ رَبُّهُمۡ شَرَابٗا طَهُورًا

Juu yao zipo nguo za hariri laini za kijani kibichi, na hariri nzito ya atilasi. Na watavikwa vikuku vya fedha, na Mola wao atawanywesha kinywaji safi kabisa



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 22

إِنَّ هَٰذَا كَانَ لَكُمۡ جَزَآءٗ وَكَانَ سَعۡيُكُم مَّشۡكُورًا

(Wataambiwa) Hakika haya ni malipo yenu; na juhudi zenu zimekubaliwa



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 23

إِنَّا نَحۡنُ نَزَّلۡنَا عَلَيۡكَ ٱلۡقُرۡءَانَ تَنزِيلٗا

Hakika Sisi tumekuteremshia Qur’ani kidogo kidogo (hatua kwa hatua)



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 24

فَٱصۡبِرۡ لِحُكۡمِ رَبِّكَ وَلَا تُطِعۡ مِنۡهُمۡ ءَاثِمًا أَوۡ كَفُورٗا

Basi ngojea hukumu ya Mola wako wala usimtii miongoni mwao mwenye dhambi au mwenye kukufuru



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 25

وَٱذۡكُرِ ٱسۡمَ رَبِّكَ بُكۡرَةٗ وَأَصِيلٗا

Na litaje jina la Mola wako Mlezi asubuhi na jioni



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 26

وَمِنَ ٱلَّيۡلِ فَٱسۡجُدۡ لَهُۥ وَسَبِّحۡهُ لَيۡلٗا طَوِيلًا

Na usiku msujudie Yeye, na umtakase, (usali kwaajili yake) usiku, wakati mrefu



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 27

إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ يُحِبُّونَ ٱلۡعَاجِلَةَ وَيَذَرُونَ وَرَآءَهُمۡ يَوۡمٗا ثَقِيلٗا

Kwa hakika watu hawa wanapenda maisha ya kidunia, na wanaiacha nyuma yao siku nzito, (ya Kiyama)



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 28

نَّحۡنُ خَلَقۡنَٰهُمۡ وَشَدَدۡنَآ أَسۡرَهُمۡۖ وَإِذَا شِئۡنَا بَدَّلۡنَآ أَمۡثَٰلَهُمۡ تَبۡدِيلًا

Sisi tumewaumba, na tukavitia nguvu viungo vyao. Na tukitaka tutawabadilisha mfano wao wawe badala yao



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 29

إِنَّ هَٰذِهِۦ تَذۡكِرَةٞۖ فَمَن شَآءَ ٱتَّخَذَ إِلَىٰ رَبِّهِۦ سَبِيلٗا

Hakika haya ni mawaidha; basi anaye taka atashika Njia ya kwenda kwa Mola wake



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 30

وَمَا تَشَآءُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُۚ إِنَّ ٱللَّهَ كَانَ عَلِيمًا حَكِيمٗا

Wala hamuwezi kutaka ila atakapo Allah. Hakika Allah ni Mwenye elimu, Mwenye hekima



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 31

يُدۡخِلُ مَن يَشَآءُ فِي رَحۡمَتِهِۦۚ وَٱلظَّـٰلِمِينَ أَعَدَّ لَهُمۡ عَذَابًا أَلِيمَۢا

Humuingiza amtakaye katika rehema zake. Na wenye kudhulumu amewawekea adhabu iumizayo



Sourate: ALMURSALAAT 

Verset : 1

وَٱلۡمُرۡسَلَٰتِ عُرۡفٗا

Nina apa kwa pepo zitumwazo kwa mfuatano



Sourate: ALMURSALAAT 

Verset : 2

فَٱلۡعَٰصِفَٰتِ عَصۡفٗا

Kisha zinazovuma kwa kasi!



Sourate: ALMURSALAAT 

Verset : 3

وَٱلنَّـٰشِرَٰتِ نَشۡرٗا

Na kwa pepo zinazotawanya (mawingu na mvua)



Sourate: ALMURSALAAT 

Verset : 4

فَٱلۡفَٰرِقَٰتِ فَرۡقٗا

Kisha Nina apa kwa (Malaika) wanaopambanua haki na batili



Sourate: ALMURSALAAT 

Verset : 5

فَٱلۡمُلۡقِيَٰتِ ذِكۡرًا

Kisha kwa (Malaika) wanaopeleka Wahyi (kwa Mtume)



Sourate: ALMURSALAAT 

Verset : 6

عُذۡرًا أَوۡ نُذۡرًا

Kwa ajili ya kuondosha udhuru au kwa ajili ya kuonya



Sourate: ALMURSALAAT 

Verset : 7

إِنَّمَا تُوعَدُونَ لَوَٰقِعٞ

Hakika mnayo ahidiwa bila ya shaka yatatokea tu!



Sourate: ALMURSALAAT 

Verset : 8

فَإِذَا ٱلنُّجُومُ طُمِسَتۡ

Basi pale nyota zitakapofutiliwa mbali mwanga wake



Sourate: ALMURSALAAT 

Verset : 9

وَإِذَا ٱلسَّمَآءُ فُرِجَتۡ

Na mbingu zitakapo pasuliwa, (au zitakapo funguliwa)