Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 21

وَتَذَرُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ

Na mnaacha maisha ya Akhera, (kwa kutoijali Akhera)



Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 22

وُجُوهٞ يَوۡمَئِذٖ نَّاضِرَةٌ

Zipo Nyuso siku hiyo zitanawiri, (zitang’aa)



Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 23

إِلَىٰ رَبِّهَا نَاظِرَةٞ

Zikimtazama Mola wake



Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 24

وَوُجُوهٞ يَوۡمَئِذِۭ بَاسِرَةٞ

Na nyuso (nyenginezo) siku hiyo zitakunjana



Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 25

تَظُنُّ أَن يُفۡعَلَ بِهَا فَاقِرَةٞ

Zikiwa na yakini kuwa zitafikiwa na msiba unaovunja uti wa mgongo



Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 26

كَلَّآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلتَّرَاقِيَ

Sivyo! Itakapofika (roho) kwenye mafupa ya koo, (mitulinga)



Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 27

وَقِيلَ مَنۡۜ رَاقٖ

Na itasemwa: Ni nani tabibu wa kumponya?



Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 28

وَظَنَّ أَنَّهُ ٱلۡفِرَاقُ

Na mwenyewe akajua kwa hakika kuwa huko ndiko kufariki



Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 29

وَٱلۡتَفَّتِ ٱلسَّاقُ بِٱلسَّاقِ

Na utakapo ambatanishwa muundi kwa muundi



Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 30

إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمَسَاقُ

Siku hiyo ndiyo (ya) kuchungwa kupelekwa kwa Mola wako! (ama Peponi au Motoni)



Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 31

فَلَا صَدَّقَ وَلَا صَلَّىٰ

Kwa sababu hakusadiki, wala hakusali, (hakumsadiki Mtume wala Qur’ani)



Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 32

وَلَٰكِن كَذَّبَ وَتَوَلَّىٰ

Lakini alikadhibisha na akakengeuka



Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 33

ثُمَّ ذَهَبَ إِلَىٰٓ أَهۡلِهِۦ يَتَمَطَّىٰٓ

Kisha akaenda kwa watu wake wa nyumbani kwa maringo



Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 34

أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰ

Ole wako! Ole wako! (Ewe unaye kadhibisha, utaangamia!)



Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 35

ثُمَّ أَوۡلَىٰ لَكَ فَأَوۡلَىٰٓ

Kisha! Ole wako! Ole wako! (Ewe unaye kadhibisha, utaangamia!)



Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 36

أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَن يُتۡرَكَ سُدًى

Je, mwanadamu anadhani kuwa ataachwa bure tu?



Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 37

أَلَمۡ يَكُ نُطۡفَةٗ مِّن مَّنِيّٖ يُمۡنَىٰ

Kwani yeye hakuwa tone la manii lililotonwa?



Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 38

ثُمَّ كَانَ عَلَقَةٗ فَخَلَقَ فَسَوَّىٰ

Kisha akawa pande la damu, (Allaah) Akamuumba na Akamsawazisha?



Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 39

فَجَعَلَ مِنۡهُ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰٓ

Kisha akamfanya namna mbili, mwanamume na mwanamke



Sourate: ALQIYAAMA 

Verset : 40

أَلَيۡسَ ذَٰلِكَ بِقَٰدِرٍ عَلَىٰٓ أَن يُحۡـِۧيَ ٱلۡمَوۡتَىٰ

Je! Huyo (aliyefanya hivyo) hakuwa ni Muweza wa kufufua wafu?



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 1

هَلۡ أَتَىٰ عَلَى ٱلۡإِنسَٰنِ حِينٞ مِّنَ ٱلدَّهۡرِ لَمۡ يَكُن شَيۡـٔٗا مَّذۡكُورًا

Hakika, kilimpitia binaadamu kipindi katika zama kipindi (ambacho) hakuwa kitu kinachotajwa



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 2

إِنَّا خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ مِن نُّطۡفَةٍ أَمۡشَاجٖ نَّبۡتَلِيهِ فَجَعَلۡنَٰهُ سَمِيعَۢا بَصِيرًا

Hakika, sisi tumemuumba mwanadamu kutokana na mbegu ya uhai (Manii) iliyochanganyika ili tumfanyie mtihani. Kwa hivyo tumemfanya ni mwenye kusikia, mwenye kuona



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 3

إِنَّا هَدَيۡنَٰهُ ٱلسَّبِيلَ إِمَّا شَاكِرٗا وَإِمَّا كَفُورًا

Hakika, sisi tumemuongoza (tumempa mwongozo unaofikishwa na Mitume); ama awe mwenye kushukuru au mwenye kukufuru



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 4

إِنَّآ أَعۡتَدۡنَا لِلۡكَٰفِرِينَ سَلَٰسِلَاْ وَأَغۡلَٰلٗا وَسَعِيرًا

Hakika sisi tumewaandalia makafiri minyororo na pingu na moto mkali



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 5

إِنَّ ٱلۡأَبۡرَارَ يَشۡرَبُونَ مِن كَأۡسٖ كَانَ مِزَاجُهَا كَافُورًا

Hakika, watu wema watakunywa katika vinywaji vilivyo changanyika na kafuri



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 6

عَيۡنٗا يَشۡرَبُ بِهَا عِبَادُ ٱللَّهِ يُفَجِّرُونَهَا تَفۡجِيرٗا

Ni chemchem watakayoinywa waja wa Allah, wakiifanya imiminike kwa wingi



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 7

يُوفُونَ بِٱلنَّذۡرِ وَيَخَافُونَ يَوۡمٗا كَانَ شَرُّهُۥ مُسۡتَطِيرٗا

Wanatimiza ahadi, na wanaiogopa siku ambayo shari yake ni yenye kuenea sana



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 8

وَيُطۡعِمُونَ ٱلطَّعَامَ عَلَىٰ حُبِّهِۦ مِسۡكِينٗا وَيَتِيمٗا وَأَسِيرًا

Na wanalisha chakula, pamoja na kukipenda kwake, (wanawalisha) masikini na mayatima na mateka



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 9

إِنَّمَا نُطۡعِمُكُمۡ لِوَجۡهِ ٱللَّهِ لَا نُرِيدُ مِنكُمۡ جَزَآءٗ وَلَا شُكُورًا

Hakika sisi tunakulisheni kwa ajili ya kutaka radhi za Allah. Hatutaki kwenu malipo wala shukrani



Sourate: AL-INSAAN

Verset : 10

إِنَّا نَخَافُ مِن رَّبِّنَا يَوۡمًا عَبُوسٗا قَمۡطَرِيرٗا

Hakika sisi tunaiogopa kwa Mola wetu hiyo siku yenye shida na taabu