حَتَّىٰٓ أَتَىٰنَا ٱلۡيَقِينُ
Mpaka ikatufikia yakini (mauti)
Partager :
فَمَا تَنفَعُهُمۡ شَفَٰعَةُ ٱلشَّـٰفِعِينَ
Basi haitowafaa uombezi wowote wa waombezi
فَمَا لَهُمۡ عَنِ ٱلتَّذۡكِرَةِ مُعۡرِضِينَ
Basi wana nini hata wanapuuza ukumbusho huu!
كَأَنَّهُمۡ حُمُرٞ مُّسۡتَنفِرَةٞ
Kama kwamba ni punda milia wenye kutimuliwa, (wenye kushtuka)
فَرَّتۡ مِن قَسۡوَرَةِۭ
Wamekimbia mbio kutokana na kumkimbia simba
بَلۡ يُرِيدُ كُلُّ ٱمۡرِيٕٖ مِّنۡهُمۡ أَن يُؤۡتَىٰ صُحُفٗا مُّنَشَّرَةٗ
Bali anataka kila mtu miongoni mwao apewe nyaraka zilizofunuliwa
كَلَّاۖ بَل لَّا يَخَافُونَ ٱلۡأٓخِرَةَ
Si hivyo! hasha! Bali hawaiogopi Akhera
كَلَّآ إِنَّهُۥ تَذۡكِرَةٞ
Na sihivyo! Hakika hii (Qur’ani) ni mawaidha
فَمَن شَآءَ ذَكَرَهُۥ
Basi anayetaka atawaidhika
وَمَا يَذۡكُرُونَ إِلَّآ أَن يَشَآءَ ٱللَّهُۚ هُوَ أَهۡلُ ٱلتَّقۡوَىٰ وَأَهۡلُ ٱلۡمَغۡفِرَةِ
Na hawatowaidhika isipokuwa Akitaka Allah; Yeye Ndiye mwenye kustahiki kuogopwa, na mwenye kustahiki kusamehe (madhambi)
لَآ أُقۡسِمُ بِيَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ
Nina apa kwa Siku ya Kiyama
وَلَآ أُقۡسِمُ بِٱلنَّفۡسِ ٱللَّوَّامَةِ
Na nina apa kwa nafsi inayolaumu sana
أَيَحۡسَبُ ٱلۡإِنسَٰنُ أَلَّن نَّجۡمَعَ عِظَامَهُۥ
Je, mwanadamu anadhani kuwa Sisi hatutaikusanya mifupa yake?
بَلَىٰ قَٰدِرِينَ عَلَىٰٓ أَن نُّسَوِّيَ بَنَانَهُۥ
Ndio (tutaikusanya tu na) Tunao uwezo wa kuzifanya ziwe sawa sawa ncha za vidole vyake
بَلۡ يُرِيدُ ٱلۡإِنسَٰنُ لِيَفۡجُرَ أَمَامَهُۥ
Lakini mwanadamu anataka tu kuendelea na maasi kwa siku zilizoko mbele yake
يَسۡـَٔلُ أَيَّانَ يَوۡمُ ٱلۡقِيَٰمَةِ
Anauliza: Ni lini hiyo Siku ya Kiyama?
فَإِذَا بَرِقَ ٱلۡبَصَرُ
Basi jicho litakapoduwaa (kwa kupatwa na bumbuwazi na fadhaa)
وَخَسَفَ ٱلۡقَمَرُ
Na mwezi utakapo patwa,
وَجُمِعَ ٱلشَّمۡسُ وَٱلۡقَمَرُ
Na vikakusanywa jua na mwezi ((Katika Kupatwa),
يَقُولُ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذٍ أَيۡنَ ٱلۡمَفَرُّ
Atasema Mwanadamu siku hiyo: Wapi pa kukimbilia?
كَلَّا لَا وَزَرَ
La! Hapana mahala pa kukimbilia!
إِلَىٰ رَبِّكَ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡمُسۡتَقَرُّ
Kwa Mola wako siku hiyo ndio makazi ya (ya kutulia)
يُنَبَّؤُاْ ٱلۡإِنسَٰنُ يَوۡمَئِذِۭ بِمَا قَدَّمَ وَأَخَّرَ
Siku hiyo ataambiwa Mtu yale aliyo yatanguliza na aliyo yakawiza
بَلِ ٱلۡإِنسَٰنُ عَلَىٰ نَفۡسِهِۦ بَصِيرَةٞ
Bali Mtu anajijua Vizuri Sana yeye mwenyewe
وَلَوۡ أَلۡقَىٰ مَعَاذِيرَهُۥ
Ingawa atatoa nyudhuru chungu nzima
لَا تُحَرِّكۡ بِهِۦ لِسَانَكَ لِتَعۡجَلَ بِهِۦٓ
Usiutikisie ulimi wako huu wahyi (ufunuo) kwa kuufanyia haraka
إِنَّ عَلَيۡنَا جَمۡعَهُۥ وَقُرۡءَانَهُۥ
Hakika ni juu Yetu kuikusanya na kukuwezesha kuisoma kwake
فَإِذَا قَرَأۡنَٰهُ فَٱتَّبِعۡ قُرۡءَانَهُۥ
Basi Tunapoisoma (kupitia Jibrili), fuata kusomwa kwake
ثُمَّ إِنَّ عَلَيۡنَا بَيَانَهُۥ
Kisha ni juu yetu kuubainisha
كَلَّا بَلۡ تُحِبُّونَ ٱلۡعَاجِلَةَ
Sivyo hivyo! Bali nyinyi mnapenda maisha ya duniani,