Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 125

أَتَدۡعُونَ بَعۡلٗا وَتَذَرُونَ أَحۡسَنَ ٱلۡخَٰلِقِينَ

Mnamwomba Baali na mnamwacha Mbora wa waumbaji,



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 126

ٱللَّهَ رَبَّكُمۡ وَرَبَّ ءَابَآئِكُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Allah, Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa zamani?



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 127

فَكَذَّبُوهُ فَإِنَّهُمۡ لَمُحۡضَرُونَ

Wakamkadhibisha. Basi kwa hakika watahudhurishwa;



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 128

إِلَّا عِبَادَ ٱللَّهِ ٱلۡمُخۡلَصِينَ

Isipo kuwa waja wa Allah walio safishwa



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 129

وَتَرَكۡنَا عَلَيۡهِ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ

Na tumemwachia (sifa nzuri) kwa walio kuja baadaye



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 130

سَلَٰمٌ عَلَىٰٓ إِلۡ يَاسِينَ

Iwe salama kwa Ilyas



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 131

إِنَّا كَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Hakika hivyo ndivyo tunavyo walipa walio wema



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 132

إِنَّهُۥ مِنۡ عِبَادِنَا ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika yeye ni katika waja wetu walio amini



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 133

وَإِنَّ لُوطٗا لَّمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na hakika Lutwi bila ya shaka ni miongoni mwa Mitume



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 134

إِذۡ نَجَّيۡنَٰهُ وَأَهۡلَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ

Tulipo mwokoa yeye na watu wake wote,



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 135

إِلَّا عَجُوزٗا فِي ٱلۡغَٰبِرِينَ

Isipo kuwa mwanamke mkongwe katika wale walio bakia nyuma



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 136

ثُمَّ دَمَّرۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ

Kisha tukawaangamiza wale wengineo



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 137

وَإِنَّكُمۡ لَتَمُرُّونَ عَلَيۡهِم مُّصۡبِحِينَ

Na hakika nyinyi mnawapitia wakati wa asubuhi,



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 138

وَبِٱلَّيۡلِۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ

Na usiku. Basi je! Hamyatii akilini?



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 139

وَإِنَّ يُونُسَ لَمِنَ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na hakika Yunus alikuwa miongoni mwa Mitume



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 140

إِذۡ أَبَقَ إِلَى ٱلۡفُلۡكِ ٱلۡمَشۡحُونِ

Alipo kimbia katika jahazi lilio sheheni



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 141

فَسَاهَمَ فَكَانَ مِنَ ٱلۡمُدۡحَضِينَ

Akaingia katika kupigiwa kura, na akawa katika walio shindwa



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 142

فَٱلۡتَقَمَهُ ٱلۡحُوتُ وَهُوَ مُلِيمٞ

Samaki akammeza hali ya kuwa ni mwenye kulaumiwa



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 143

فَلَوۡلَآ أَنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلۡمُسَبِّحِينَ

Na ingeli kuwa hakuwa katika wanao mtakasa Allah,



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 144

لَلَبِثَ فِي بَطۡنِهِۦٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ

Bila ya shaka angeli kaa ndani yake mpaka siku ya kufufuliwa