وَظِلّٖ مِّن يَحۡمُومٖ
Na kivuli cha moshi mweusi mnene wa joto kali mno
Partager :
لَّا بَارِدٖ وَلَا كَرِيمٍ
Si cha baridi na wala si cha kunufaisha
إِنَّهُمۡ كَانُواْ قَبۡلَ ذَٰلِكَ مُتۡرَفِينَ
Hakika walikua kabla ya hapo kwenye maisha ya neema na anasa
وَكَانُواْ يُصِرُّونَ عَلَى ٱلۡحِنثِ ٱلۡعَظِيمِ
Na walikuwa wakishikilia kufanya dhambi kubwa mno
وَكَانُواْ يَقُولُونَ أَئِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ
Na walikuwa wakisema: Je, hivi tutakapo kufa na tukawa udongo na mifupa, je hivi sisi hakika tutafufuliwa?
أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ
Au na wazee wetu wa mwanzo?
قُلۡ إِنَّ ٱلۡأَوَّلِينَ وَٱلۡأٓخِرِينَ
Sema; Hakika wa mwanzo na wa mwisho,
لَمَجۡمُوعُونَ إِلَىٰ مِيقَٰتِ يَوۡمٖ مَّعۡلُومٖ
Hakika watakusanywa kwenye wakati na siku maalumu
ثُمَّ إِنَّكُمۡ أَيُّهَا ٱلضَّآلُّونَ ٱلۡمُكَذِّبُونَ
Kisha hakika nyinyi enyi wapotovu mnaokadhibisha
لَأٓكِلُونَ مِن شَجَرٖ مِّن زَقُّومٖ
Hakika mtakula chakula kitokanacho na mti wa mzakoum
فَمَالِـُٔونَ مِنۡهَا ٱلۡبُطُونَ
Basi mtajaza kutokana na mti huo matumbo yenu
فَشَٰرِبُونَ عَلَيۡهِ مِنَ ٱلۡحَمِيمِ
Na mtakunywa juu yake maji ya moto ya chemkayo
فَشَٰرِبُونَ شُرۡبَ ٱلۡهِيمِ
Tena mtakunywa unywaji wa ngamia mwenye kiu kubwa
هَٰذَا نُزُلُهُمۡ يَوۡمَ ٱلدِّينِ
Haya ndio mapokezi yao Siku ya Malipo! (Kiyama)
نَحۡنُ خَلَقۡنَٰكُمۡ فَلَوۡلَا تُصَدِّقُونَ
Sisi Tumekuumbeni, basi kwa nini hamsadikishi hilo?
أَفَرَءَيۡتُم مَّا تُمۡنُونَ
Je, mnaona mbegu ya uzazi mnayo imwagia kwa nguvu?
ءَأَنتُمۡ تَخۡلُقُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡخَٰلِقُونَ
Je, nyinyi ndio mnaiumba au sisi ndio Waumbaji?
نَحۡنُ قَدَّرۡنَا بَيۡنَكُمُ ٱلۡمَوۡتَ وَمَا نَحۡنُ بِمَسۡبُوقِينَ
Sisi tumekadiria kati yenu umauti na haikua sisi wenye kukimbiwa
عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ أَمۡثَٰلَكُمۡ وَنُنشِئَكُمۡ فِي مَا لَا تَعۡلَمُونَ
Kwamba Tuwabadilishe wengine mfano wenu, na Tukuumbeni katika umbo msilolijua
وَلَقَدۡ عَلِمۡتُمُ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأُولَىٰ فَلَوۡلَا تَذَكَّرُونَ
Na bila shaka mmejua umbo la kwanza, basi kwanini hamkumbuki?
أَفَرَءَيۡتُم مَّا تَحۡرُثُونَ
Je, mnaona mbegu mnazo-zipanda?
ءَأَنتُمۡ تَزۡرَعُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلزَّـٰرِعُونَ
Je, ni nyinyi ndio mnaziotesha, au Sisi ndio Wenye kuotesha mimea?
لَوۡ نَشَآءُ لَجَعَلۡنَٰهُ حُطَٰمٗا فَظَلۡتُمۡ تَفَكَّهُونَ
Lau Tungelitaka, Tungelifanya mabua yaliyonyauka na mkabaki mnashangaa na kusikitika
إِنَّا لَمُغۡرَمُونَ
(Mkisema): Hakika sisi tumegharimika
بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ
Bali sisi tumenyimwa
أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلۡمَآءَ ٱلَّذِي تَشۡرَبُونَ
Je, mnaona maji ambayo mnakunywa?
ءَأَنتُمۡ أَنزَلۡتُمُوهُ مِنَ ٱلۡمُزۡنِ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنزِلُونَ
Je, ni nyinyi ndio mliyoyateremsha kutoka katika mawingu ya mvua au Sisi ndio Wateremshaji?
لَوۡ نَشَآءُ جَعَلۡنَٰهُ أُجَاجٗا فَلَوۡلَا تَشۡكُرُونَ
Lau Tungelitaka, Tungeliyafanya ya chumvi kali chungu basi kwa nini hamshukuru?
أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلنَّارَ ٱلَّتِي تُورُونَ
Je, mnaona moto ambao mnauwasha?
ءَأَنتُمۡ أَنشَأۡتُمۡ شَجَرَتَهَآ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنشِـُٔونَ
Je, ni nyinyi ndio mliouumba mti wake, au Sisi ndio Waumbaji wa mti huo?