Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 153

۞إِذۡ تُصۡعِدُونَ وَلَا تَلۡوُۥنَ عَلَىٰٓ أَحَدٖ وَٱلرَّسُولُ يَدۡعُوكُمۡ فِيٓ أُخۡرَىٰكُمۡ فَأَثَٰبَكُمۡ غَمَّۢا بِغَمّٖ لِّكَيۡلَا تَحۡزَنُواْ عَلَىٰ مَا فَاتَكُمۡ وَلَا مَآ أَصَٰبَكُمۡۗ وَٱللَّهُ خَبِيرُۢ بِمَا تَعۡمَلُونَ

Kumbukeni mlipokuwa mkipanda Jabali kukimbia na hamumsikilizi yeyote, ilhali Mtume anawaiteni nyuma yenu. Basi Allah akakupeni huzuni juu ya huzuni, ili msisikitike kwa yaliyo kukoseni na kwa yaliyo kusibuni. Na Allah ni mwenye khabari juu ya yote myatendayo



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 154

ثُمَّ أَنزَلَ عَلَيۡكُم مِّنۢ بَعۡدِ ٱلۡغَمِّ أَمَنَةٗ نُّعَاسٗا يَغۡشَىٰ طَآئِفَةٗ مِّنكُمۡۖ وَطَآئِفَةٞ قَدۡ أَهَمَّتۡهُمۡ أَنفُسُهُمۡ يَظُنُّونَ بِٱللَّهِ غَيۡرَ ٱلۡحَقِّ ظَنَّ ٱلۡجَٰهِلِيَّةِۖ يَقُولُونَ هَل لَّنَا مِنَ ٱلۡأَمۡرِ مِن شَيۡءٖۗ قُلۡ إِنَّ ٱلۡأَمۡرَ كُلَّهُۥ لِلَّهِۗ يُخۡفُونَ فِيٓ أَنفُسِهِم مَّا لَا يُبۡدُونَ لَكَۖ يَقُولُونَ لَوۡ كَانَ لَنَا مِنَ ٱلۡأَمۡرِ شَيۡءٞ مَّا قُتِلۡنَا هَٰهُنَاۗ قُل لَّوۡ كُنتُمۡ فِي بُيُوتِكُمۡ لَبَرَزَ ٱلَّذِينَ كُتِبَ عَلَيۡهِمُ ٱلۡقَتۡلُ إِلَىٰ مَضَاجِعِهِمۡۖ وَلِيَبۡتَلِيَ ٱللَّهُ مَا فِي صُدُورِكُمۡ وَلِيُمَحِّصَ مَا فِي قُلُوبِكُمۡۚ وَٱللَّهُ عَلِيمُۢ بِذَاتِ ٱلصُّدُورِ

Kisha aliwateremshieni baada ya dhiki utulivu, usingizi ulifunika kundi moja kati yenu, na kundi lingine lilishughulishwa na nafsi zao hata wakamdhania Allah dhana isiyokuwa ya haki, dhana ya kijinga. Wakisema: Hivi sisi tuna jambo lolote katika hili? Sema: Mambo yote ni ya Allah. Wanaficha katika nafsi zao wasiyokubainishia. Wanasema: Lau ingelikuwa tuna lolote katika jambo hili tusingeuliwa hapa. Sema: Hata mngekuwa majumbani mwenu, basi wangetoka wale walioandikiwa kifo, wakaenda mahali pao pakuangukia wafe. Ili Allah ayajaribu yaliyomo vifuani mwenu, na asafishe yaliyomo nyoyoni mwenu. Na Allah anayajua yaliyomo vifuani



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 155

إِنَّ ٱلَّذِينَ تَوَلَّوۡاْ مِنكُمۡ يَوۡمَ ٱلۡتَقَى ٱلۡجَمۡعَانِ إِنَّمَا ٱسۡتَزَلَّهُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ بِبَعۡضِ مَا كَسَبُواْۖ وَلَقَدۡ عَفَا ٱللَّهُ عَنۡهُمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ غَفُورٌ حَلِيمٞ

Hakika Wale waliorudi miongoni mwenu siku ambayo majeshi mawili yalipokutana, hakika shetani (ndiye) aliyewatelezesha kwa sababu ya baadhi ya makosa waliyoyafanya, na kwa hakika Allah amewasamehe. Hakika Allah ni Msamehevu sana Mpole Mno



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 156

يَـٰٓأَيُّهَا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ لَا تَكُونُواْ كَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَقَالُواْ لِإِخۡوَٰنِهِمۡ إِذَا ضَرَبُواْ فِي ٱلۡأَرۡضِ أَوۡ كَانُواْ غُزّٗى لَّوۡ كَانُواْ عِندَنَا مَا مَاتُواْ وَمَا قُتِلُواْ لِيَجۡعَلَ ٱللَّهُ ذَٰلِكَ حَسۡرَةٗ فِي قُلُوبِهِمۡۗ وَٱللَّهُ يُحۡيِۦ وَيُمِيتُۗ وَٱللَّهُ بِمَا تَعۡمَلُونَ بَصِيرٞ

Enyi mlioamini msiwe kama wale waliokufuru na wakasema kuhusu ndugu zao waliposafiri ardhini au walipokuwa vitani; kama wangekuwa kwetu wasingekufa na wasingeuwawa ili Allah afanye hilo kuwa ni majuto katika nyoyo zao, na Allah anahuisha na anafisha na Allah kwa munayoyatenda ni Mwenye kuyaona mno



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 157

وَلَئِن قُتِلۡتُمۡ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ أَوۡ مُتُّمۡ لَمَغۡفِرَةٞ مِّنَ ٱللَّهِ وَرَحۡمَةٌ خَيۡرٞ مِّمَّا يَجۡمَعُونَ

Na ikiwa mtauliwa katika njia ya Allah au mkifa, hakika msamaha na rehema zitokazo kwa Allah ni bora kuliko yote wanayoyakusanya



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 158

وَلَئِن مُّتُّمۡ أَوۡ قُتِلۡتُمۡ لَإِلَى ٱللَّهِ تُحۡشَرُونَ

Na mkifa au mkiuliwa ni kwa Allah tu mtakusanywa



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 159

فَبِمَا رَحۡمَةٖ مِّنَ ٱللَّهِ لِنتَ لَهُمۡۖ وَلَوۡ كُنتَ فَظًّا غَلِيظَ ٱلۡقَلۡبِ لَٱنفَضُّواْ مِنۡ حَوۡلِكَۖ فَٱعۡفُ عَنۡهُمۡ وَٱسۡتَغۡفِرۡ لَهُمۡ وَشَاوِرۡهُمۡ فِي ٱلۡأَمۡرِۖ فَإِذَا عَزَمۡتَ فَتَوَكَّلۡ عَلَى ٱللَّهِۚ إِنَّ ٱللَّهَ يُحِبُّ ٱلۡمُتَوَكِّلِينَ

Basi ni kwa rehema za Allah umekuwa mpole kwao, na lau ungekuwa muovu wa tabia, mwenye moyo mgumu, bila ya shaka wangekukimbia, basi samehe na uwaombee msamaha na watake ushauri katika jambo, na ukitia azma ya jambo basi mtegemee Allah, hakika Allah anawapenda wenye kumtegemea



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 160

إِن يَنصُرۡكُمُ ٱللَّهُ فَلَا غَالِبَ لَكُمۡۖ وَإِن يَخۡذُلۡكُمۡ فَمَن ذَا ٱلَّذِي يَنصُرُكُم مِّنۢ بَعۡدِهِۦۗ وَعَلَى ٱللَّهِ فَلۡيَتَوَكَّلِ ٱلۡمُؤۡمِنُونَ

Iwapo Allah atawanusuru, basi hakuna wa kuwashinda na endapo atakuacheni basi ni nani mwingine baada ya Yeye atakunusuruni? Na Waumini wategemee kwa Allah tu



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 161

وَمَا كَانَ لِنَبِيٍّ أَن يَغُلَّۚ وَمَن يَغۡلُلۡ يَأۡتِ بِمَا غَلَّ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِۚ ثُمَّ تُوَفَّىٰ كُلُّ نَفۡسٖ مَّا كَسَبَتۡ وَهُمۡ لَا يُظۡلَمُونَ

Na haiwezekani kwa Nabii yeyote kufanya khiyana, na atakayefanya khiyana atayaleta aliyoyafanyia khiyana Siku ya Kiama kisha kila nafsi italipwa kwa iliyoyachuma kwa ukamilifu, nao hawatadhulumiwa



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 162

أَفَمَنِ ٱتَّبَعَ رِضۡوَٰنَ ٱللَّهِ كَمَنۢ بَآءَ بِسَخَطٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَمَأۡوَىٰهُ جَهَنَّمُۖ وَبِئۡسَ ٱلۡمَصِيرُ

Je aliyefuata yanayomridhisha Allah, ni kama yule aliyestahiki ghadhabu kutoka kwa Allah na makazi yake kuwa jahannamu? Na hayo nimarejeo mabaya mno



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 163

هُمۡ دَرَجَٰتٌ عِندَ ٱللَّهِۗ وَٱللَّهُ بَصِيرُۢ بِمَا يَعۡمَلُونَ

Hao wana vyeo mbalimbali kwa Allah, na Allah ni mwenye kuyaona yote wayatendayo



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 164

لَقَدۡ مَنَّ ٱللَّهُ عَلَى ٱلۡمُؤۡمِنِينَ إِذۡ بَعَثَ فِيهِمۡ رَسُولٗا مِّنۡ أَنفُسِهِمۡ يَتۡلُواْ عَلَيۡهِمۡ ءَايَٰتِهِۦ وَيُزَكِّيهِمۡ وَيُعَلِّمُهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡحِكۡمَةَ وَإِن كَانُواْ مِن قَبۡلُ لَفِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٍ

kwa hakika Allah amewaneemesha Waumini pale alipomtuma kwao Mtume anayetokana na wao wenyewe, anawasomea Aya zake, anawatakasa na anawafundisha kitabu na hekima japokuwa kabla ya hapo walikuwa katika uovu wa wazi



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 165

أَوَلَمَّآ أَصَٰبَتۡكُم مُّصِيبَةٞ قَدۡ أَصَبۡتُم مِّثۡلَيۡهَا قُلۡتُمۡ أَنَّىٰ هَٰذَاۖ قُلۡ هُوَ مِنۡ عِندِ أَنفُسِكُمۡۗ إِنَّ ٱللَّهَ عَلَىٰ كُلِّ شَيۡءٖ قَدِيرٞ

Hivi mlipopata msiba hakika mmekwishapatwa mara mbili ya huo, mlisema: umetoka wapi msiba huu? Sema huo umetoka kwenu wenyewe, hakika Allah juu ya kila kitu ni muweza



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 166

وَمَآ أَصَٰبَكُمۡ يَوۡمَ ٱلۡتَقَى ٱلۡجَمۡعَانِ فَبِإِذۡنِ ٱللَّهِ وَلِيَعۡلَمَ ٱلۡمُؤۡمِنِينَ

Na yale yaliyokupateni siku yalipopambana majeshi mawili yalikuwa kwa idhini ya Allah na ili awajue waumini



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 167

وَلِيَعۡلَمَ ٱلَّذِينَ نَافَقُواْۚ وَقِيلَ لَهُمۡ تَعَالَوۡاْ قَٰتِلُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ أَوِ ٱدۡفَعُواْۖ قَالُواْ لَوۡ نَعۡلَمُ قِتَالٗا لَّٱتَّبَعۡنَٰكُمۡۗ هُمۡ لِلۡكُفۡرِ يَوۡمَئِذٍ أَقۡرَبُ مِنۡهُمۡ لِلۡإِيمَٰنِۚ يَقُولُونَ بِأَفۡوَٰهِهِم مَّا لَيۡسَ فِي قُلُوبِهِمۡۚ وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا يَكۡتُمُونَ

Na ili awapambanue wanafiki, na wakaambiwa: njooni mpigane katika njia ya Allah au lindeni. Wakasema: lau tungejua kuwa kuna mapigano bila ya shaka tungelikufuateni. wao siku ile walikuwa wako karibu zaidi na ukafiri kuliko imani, wanasema kwa midomo yao yasiyokuwemo nyoyoni mwao, na Allah ni mjuzi zaidi kwa yale wanayoyaficha



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 168

ٱلَّذِينَ قَالُواْ لِإِخۡوَٰنِهِمۡ وَقَعَدُواْ لَوۡ أَطَاعُونَا مَا قُتِلُواْۗ قُلۡ فَٱدۡرَءُواْ عَنۡ أَنفُسِكُمُ ٱلۡمَوۡتَ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Hao ndio ambao walisema kuhusu ndugu zao na wao wakiwa wamekaa: Lau wangelitutii sisi wasingeuliwa sema: basi ziondoleeni nafsi zenu kifo ikiwa nyinyi ni wa kweli



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 169

وَلَا تَحۡسَبَنَّ ٱلَّذِينَ قُتِلُواْ فِي سَبِيلِ ٱللَّهِ أَمۡوَٰتَۢاۚ بَلۡ أَحۡيَآءٌ عِندَ رَبِّهِمۡ يُرۡزَقُونَ

Na kamwe msiwadhanie waliouliwa katika njia ya Allah kuwa ni wafu, bali wako hai kwa Mola wao wanaruzukiwa



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 170

فَرِحِينَ بِمَآ ءَاتَىٰهُمُ ٱللَّهُ مِن فَضۡلِهِۦ وَيَسۡتَبۡشِرُونَ بِٱلَّذِينَ لَمۡ يَلۡحَقُواْ بِهِم مِّنۡ خَلۡفِهِمۡ أَلَّا خَوۡفٌ عَلَيۡهِمۡ وَلَا هُمۡ يَحۡزَنُونَ

Wanafurahia waliyopewa na Allah miongoni mwa fadhila zake, na wanawabashiria walio nyuma yao ambao bado hawajajiunga nao, ya kwamba: Hakutakuwa na khofu yoyote juu yao, na wala hawatahuzunika