Sourate: AL-FAJRI 

Verset : 16

وَأَمَّآ إِذَا مَا ٱبۡتَلَىٰهُ فَقَدَرَ عَلَيۡهِ رِزۡقَهُۥ فَيَقُولُ رَبِّيٓ أَهَٰنَنِ

Na ama anapo mjaribu akampunguzia riziki yake, husema: Mola wangu Mlezi amenitia unyonge!



Sourate: AL-FAJRI 

Verset : 17

كَلَّاۖ بَل لَّا تُكۡرِمُونَ ٱلۡيَتِيمَ

Sivyo hivyo! Bali nyinyi hamuwakirimu mayatima,



Sourate: AL-FAJRI 

Verset : 18

وَلَا تَحَـٰٓضُّونَ عَلَىٰ طَعَامِ ٱلۡمِسۡكِينِ

Wala hamhimizani kulisha masikini;



Sourate: AL-FAJRI 

Verset : 19

وَتَأۡكُلُونَ ٱلتُّرَاثَ أَكۡلٗا لَّمّٗا

Na mnakula urithi kwa ulaji wa pupa,



Sourate: AL-FAJRI 

Verset : 20

وَتُحِبُّونَ ٱلۡمَالَ حُبّٗا جَمّٗا

Na mnapenda mali mapenzi ya kupita kiasi



Sourate: AL-FAJRI 

Verset : 21

كَلَّآۖ إِذَا دُكَّتِ ٱلۡأَرۡضُ دَكّٗا دَكّٗا

Sivyo hivyo! Itakapo vunjwa ardhi vipande vipande,



Sourate: AL-FAJRI 

Verset : 22

وَجَآءَ رَبُّكَ وَٱلۡمَلَكُ صَفّٗا صَفّٗا

Na akaja Mola wako Mlezi na Malaika safu safu,



Sourate: AL-FAJRI 

Verset : 23

وَجِاْيٓءَ يَوۡمَئِذِۭ بِجَهَنَّمَۚ يَوۡمَئِذٖ يَتَذَكَّرُ ٱلۡإِنسَٰنُ وَأَنَّىٰ لَهُ ٱلذِّكۡرَىٰ

Na ikaletwa Jahannamu siku hiyo, siku hiyo mtu atakumbuka! Lakini kukumbuka huko kutamfaa nini?



Sourate: AL-FAJRI 

Verset : 24

يَقُولُ يَٰلَيۡتَنِي قَدَّمۡتُ لِحَيَاتِي

Atasema: Laiti ningeli jitangulizia (mema) katika uhai wangu!



Sourate: AL-FAJRI 

Verset : 25

فَيَوۡمَئِذٖ لَّا يُعَذِّبُ عَذَابَهُۥٓ أَحَدٞ

Basi siku hiyo hataadhibu yeyote kama kuadhibu kwake



Sourate: AL-FAJRI 

Verset : 26

وَلَا يُوثِقُ وَثَاقَهُۥٓ أَحَدٞ

Wala hatafunga yeyote kama kufunga kwake



Sourate: AL-FAJRI 

Verset : 27

يَـٰٓأَيَّتُهَا ٱلنَّفۡسُ ٱلۡمُطۡمَئِنَّةُ

Ewe nafsi iliyo tua!



Sourate: AL-FAJRI 

Verset : 28

ٱرۡجِعِيٓ إِلَىٰ رَبِّكِ رَاضِيَةٗ مَّرۡضِيَّةٗ

Rejea kwa Mola wako Mlezi umeridhika, na umemridhisha



Sourate: AL-FAJRI 

Verset : 29

فَٱدۡخُلِي فِي عِبَٰدِي

Basi ingia miongoni mwa waja wangu,



Sourate: AL-FAJRI 

Verset : 30

وَٱدۡخُلِي جَنَّتِي

Na ingia katika Pepo yangu



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 1

لَآ أُقۡسِمُ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ

Naapa kwa Mji huu!



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 2

وَأَنتَ حِلُّۢ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ

Nawe unakaa Mji huu



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 3

وَوَالِدٖ وَمَا وَلَدَ

Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 4

لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِي كَبَدٍ

Hakika tumemuumba mtu katika taabu



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 5

أَيَحۡسَبُ أَن لَّن يَقۡدِرَ عَلَيۡهِ أَحَدٞ

Ati anadhani hapana yeyote atakaye muweza?



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 6

يَقُولُ أَهۡلَكۡتُ مَالٗا لُّبَدًا

Anasema: Nimeteketeza mali chungu nzima



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 7

أَيَحۡسَبُ أَن لَّمۡ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ

Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 8

أَلَمۡ نَجۡعَل لَّهُۥ عَيۡنَيۡنِ

Kwani hatukumpa macho mawili?



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 9

وَلِسَانٗا وَشَفَتَيۡنِ

Na ulimi, na midomo miwili?



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 10

وَهَدَيۡنَٰهُ ٱلنَّجۡدَيۡنِ

Na tukambainishia njia zote mbili?



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 11

فَلَا ٱقۡتَحَمَ ٱلۡعَقَبَةَ

Lakini hakujitoma (hakuingia) kwenye njia ya vikwazo vya milimani



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 12

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡعَقَبَةُ

Na nini kitakujulisha ni nini njia ya vikwazo vya milimani?



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 13

فَكُّ رَقَبَةٍ

Kumkomboa mtumwa;



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 14

أَوۡ إِطۡعَٰمٞ فِي يَوۡمٖ ذِي مَسۡغَبَةٖ

Au kumlisha siku ya njaa



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 15

يَتِيمٗا ذَا مَقۡرَبَةٍ

Yatima aliye katika jamaa wa karibu (ndugu)