Sourate: AZZUKHRUF 

Verset : 84

وَهُوَ ٱلَّذِي فِي ٱلسَّمَآءِ إِلَٰهٞ وَفِي ٱلۡأَرۡضِ إِلَٰهٞۚ وَهُوَ ٱلۡحَكِيمُ ٱلۡعَلِيمُ

Na Yeye ndiye Allah mbinguni, na ndiye Allah katika ardhi. Naye ndiye Mwenye hekima, Mwenye ujuzi



Sourate: AZZUKHRUF 

Verset : 85

وَتَبَارَكَ ٱلَّذِي لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا وَعِندَهُۥ عِلۡمُ ٱلسَّاعَةِ وَإِلَيۡهِ تُرۡجَعُونَ

Na ametukuka Mwenye ufalme wa mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake. Na uko kwake ujuzi wa Saa ya Kiyama, na kwake Yeye mtarudishwa



Sourate: AZZUKHRUF 

Verset : 86

وَلَا يَمۡلِكُ ٱلَّذِينَ يَدۡعُونَ مِن دُونِهِ ٱلشَّفَٰعَةَ إِلَّا مَن شَهِدَ بِٱلۡحَقِّ وَهُمۡ يَعۡلَمُونَ

Wala hao mnao waomba badala yake hawana uwezo wa kumwombea mtu, isipo kuwa anayeshuhudia kwa haki, na wao wanajua



Sourate: AZZUKHRUF 

Verset : 87

وَلَئِن سَأَلۡتَهُم مَّنۡ خَلَقَهُمۡ لَيَقُولُنَّ ٱللَّهُۖ فَأَنَّىٰ يُؤۡفَكُونَ

Na ukiwauliza ni nani aliye waumba? Bila ya shaka watasema: ni Allah! Basi ni wapi wanako geuziwa?



Sourate: AZZUKHRUF 

Verset : 88

وَقِيلِهِۦ يَٰرَبِّ إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ قَوۡمٞ لَّا يُؤۡمِنُونَ

Na usemi wake (Mtume) ni: Ewe Mola wangu Mlezi! Hakika hawa ni watu wasio amini



Sourate: AZZUKHRUF 

Verset : 89

فَٱصۡفَحۡ عَنۡهُمۡ وَقُلۡ سَلَٰمٞۚ فَسَوۡفَ يَعۡلَمُونَ

Basi wasamehe, na uwambie maneno ya salama. Watakuja jua



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 1

حمٓ

Haamiim



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 2

وَٱلۡكِتَٰبِ ٱلۡمُبِينِ

Nina apa kwa Kitabu kinacho bainisha



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 3

إِنَّآ أَنزَلۡنَٰهُ فِي لَيۡلَةٖ مُّبَٰرَكَةٍۚ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ

Hakika, tumekiteremsha (kitabu hiki cha Qur’ani) katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi tumekuwa waonyaji



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 4

فِيهَا يُفۡرَقُ كُلُّ أَمۡرٍ حَكِيمٍ

Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hekima



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 5

أَمۡرٗا مِّنۡ عِندِنَآۚ إِنَّا كُنَّا مُرۡسِلِينَ

Jambo litokalo kwetu. Hakika Sisi ndio wenye kutuma



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 6

رَحۡمَةٗ مِّن رَّبِّكَۚ إِنَّهُۥ هُوَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ

Ni rehema kutoka kwa Mola wako Mlezi. Hakika Yeye ndiye tu Mwenye kusikia sana, Mwenye kujua



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 7

رَبِّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَآۖ إِن كُنتُم مُّوقِنِينَ

Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilivyopo baina yake, ikiwa nyinyi mna yakini



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 8

لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ يُحۡيِۦ وَيُمِيتُۖ رَبُّكُمۡ وَرَبُّ ءَابَآئِكُمُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Hakuna mungu ila Yeye; anahuisha na anafisha- Mola Mlezi wenu na Mola Mlezi wa baba zenu wa mwanzo



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 9

بَلۡ هُمۡ فِي شَكّٖ يَلۡعَبُونَ

Lakini wao wanacheza katika shaka



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 10

فَٱرۡتَقِبۡ يَوۡمَ تَأۡتِي ٱلسَّمَآءُ بِدُخَانٖ مُّبِينٖ

Basi ingoje siku ambayo mbingu zitakapoleta moshi ulio dhahiri



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 11

يَغۡشَى ٱلنَّاسَۖ هَٰذَا عَذَابٌ أَلِيمٞ

Utakaowafunika watu: Hii ni adhabu chungu!



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 12

رَّبَّنَا ٱكۡشِفۡ عَنَّا ٱلۡعَذَابَ إِنَّا مُؤۡمِنُونَ

Mola wetu Mlezi! Tuondolee adhabu hii. Hakika tutaamini



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 13

أَنَّىٰ لَهُمُ ٱلذِّكۡرَىٰ وَقَدۡ جَآءَهُمۡ رَسُولٞ مُّبِينٞ

Nini faida ya kukumbuka kwao? Na alikwishawafikia Mtume mwenye kubainisha



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 14

ثُمَّ تَوَلَّوۡاْ عَنۡهُ وَقَالُواْ مُعَلَّمٞ مَّجۡنُونٌ

Na wao wakamgeuzia uso, na wakasema: Huyu amefunzwa, naye ni mwendawazimu



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 15

إِنَّا كَاشِفُواْ ٱلۡعَذَابِ قَلِيلًاۚ إِنَّكُمۡ عَآئِدُونَ

Hakika sisi tutaiondoa adhabu kidogo, lakini nyinyi kwa yakini mtarejea vile vile!



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 16

يَوۡمَ نَبۡطِشُ ٱلۡبَطۡشَةَ ٱلۡكُبۡرَىٰٓ إِنَّا مُنتَقِمُونَ

Siku tutakayo yashambulia mashambulio makubwa, bila ya shaka Sisi ni wenye kutesa



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 17

۞وَلَقَدۡ فَتَنَّا قَبۡلَهُمۡ قَوۡمَ فِرۡعَوۡنَ وَجَآءَهُمۡ رَسُولٞ كَرِيمٌ

Na hakika kabla ya hawa tuliwafanyia mtihani watu wa Firauni, na aliwafikia Mtume Mtukufu



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 18

أَنۡ أَدُّوٓاْ إِلَيَّ عِبَادَ ٱللَّهِۖ إِنِّي لَكُمۡ رَسُولٌ أَمِينٞ

Akasema: Nipeni waja wa Allah; kwa hakika mimi kwenu ni Mtume Muaminifu



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 19

وَأَن لَّا تَعۡلُواْ عَلَى ٱللَّهِۖ إِنِّيٓ ءَاتِيكُم بِسُلۡطَٰنٖ مُّبِينٖ

Na msimfanyie kiburi Allah; hakika mimi nitakuleteeni uthibitisho ulio wazi



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 20

وَإِنِّي عُذۡتُ بِرَبِّي وَرَبِّكُمۡ أَن تَرۡجُمُونِ

Nami najikinga kwa Mola wangu Mlezi na ndiye Mola wenu Mlezi pia, ili msinipige mawe



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 21

وَإِن لَّمۡ تُؤۡمِنُواْ لِي فَٱعۡتَزِلُونِ

Na ikiwa hamniamini, basi jitengeni nami



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 22

فَدَعَا رَبَّهُۥٓ أَنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ قَوۡمٞ مُّجۡرِمُونَ

Ndipo akamwomba Mola wake Mlezi: Hakika watu hawa ni wakosefu



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 23

فَأَسۡرِ بِعِبَادِي لَيۡلًا إِنَّكُم مُّتَّبَعُونَ

Allah akasema: Basi nenda na waja wangu usiku. Kwa yakini mtafuatwa



Sourate: ADDUKHAAN 

Verset : 24

وَٱتۡرُكِ ٱلۡبَحۡرَ رَهۡوًاۖ إِنَّهُمۡ جُندٞ مُّغۡرَقُونَ

Na iache bahari vivyo hivyo imeachana, hakika wao hao ni jeshi litakalo zamishwa