وَكَذَّبَ بِهِۦ قَوۡمُكَ وَهُوَ ٱلۡحَقُّۚ قُل لَّسۡتُ عَلَيۡكُم بِوَكِيلٖ
Na watu wako wameikanusha (Qur’ani), na ilhali ndio haki. Sema: Mimi sio mtetezi wenu (lakini mimi ni muonyaji)
لِّكُلِّ نَبَإٖ مُّسۡتَقَرّٞۚ وَسَوۡفَ تَعۡلَمُونَ
Kila habari ina sehemu yake (maalumu), na punde tu mtajua
وَإِذَا رَأَيۡتَ ٱلَّذِينَ يَخُوضُونَ فِيٓ ءَايَٰتِنَا فَأَعۡرِضۡ عَنۡهُمۡ حَتَّىٰ يَخُوضُواْ فِي حَدِيثٍ غَيۡرِهِۦۚ وَإِمَّا يُنسِيَنَّكَ ٱلشَّيۡطَٰنُ فَلَا تَقۡعُدۡ بَعۡدَ ٱلذِّكۡرَىٰ مَعَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلظَّـٰلِمِينَ
Na utakapowaona wanaozizungumza vibaya Aya zetu, basi wapuuze (na jitenge nao) hadi waingie katika mazungumzo mengine. Na kama shetani atakusahaulisha, basi baada ya kukumbushwa usikae pamoja na watu madhalimu.[1]
1- - Aya hii inawataka Waislamu wahakikishe kuwa maandiko ya dini yao yanaheshimiwa. Pale watakapo ona yanakejiliwa, yanachezewa, yanabezwa au kupotoshwa wasikae kimya bali wakemee na ikibidi waondoke sehemu inapofanyika kejeli hiyo.
وَمَا عَلَى ٱلَّذِينَ يَتَّقُونَ مِنۡ حِسَابِهِم مِّن شَيۡءٖ وَلَٰكِن ذِكۡرَىٰ لَعَلَّهُمۡ يَتَّقُونَ
Na wale wanaomcha Allah hawana dhambi yoyote katika dhambi zao (watapojitenga nao), lakini (huu) ni ukumbusho tu, ili waogope
وَذَرِ ٱلَّذِينَ ٱتَّخَذُواْ دِينَهُمۡ لَعِبٗا وَلَهۡوٗا وَغَرَّتۡهُمُ ٱلۡحَيَوٰةُ ٱلدُّنۡيَاۚ وَذَكِّرۡ بِهِۦٓ أَن تُبۡسَلَ نَفۡسُۢ بِمَا كَسَبَتۡ لَيۡسَ لَهَا مِن دُونِ ٱللَّهِ وَلِيّٞ وَلَا شَفِيعٞ وَإِن تَعۡدِلۡ كُلَّ عَدۡلٖ لَّا يُؤۡخَذۡ مِنۡهَآۗ أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ أُبۡسِلُواْ بِمَا كَسَبُواْۖ لَهُمۡ شَرَابٞ مِّنۡ حَمِيمٖ وَعَذَابٌ أَلِيمُۢ بِمَا كَانُواْ يَكۡفُرُونَ
Na waache wale walioifanya dini yao mchezo na pumbao, na yamewahadaa maisha ya dunia. Na kumbusha kwayo (Qur’ani ili), isije nafsi ikaangamizwa kwasababu ya (madhambi) waliyoyachuma, haina mlinzi yeyote wala muombezi yeyote. Na hata kama (nafsi hiyo) itatoa fidia ya aina yoyote (ili isiadhibiwe) haitachukuliwa. Hao ndio wale walioangamizwa kwa (sababu ya madhambi) waliyoyachuma. Watapata kinywaji cha maji ya moto na adhabu iumizayo sana kwa (sababu) ya walivyokuwa wanakufuru
قُلۡ أَنَدۡعُواْ مِن دُونِ ٱللَّهِ مَا لَا يَنفَعُنَا وَلَا يَضُرُّنَا وَنُرَدُّ عَلَىٰٓ أَعۡقَابِنَا بَعۡدَ إِذۡ هَدَىٰنَا ٱللَّهُ كَٱلَّذِي ٱسۡتَهۡوَتۡهُ ٱلشَّيَٰطِينُ فِي ٱلۡأَرۡضِ حَيۡرَانَ لَهُۥٓ أَصۡحَٰبٞ يَدۡعُونَهُۥٓ إِلَى ٱلۡهُدَى ٱئۡتِنَاۗ قُلۡ إِنَّ هُدَى ٱللَّهِ هُوَ ٱلۡهُدَىٰۖ وَأُمِرۡنَا لِنُسۡلِمَ لِرَبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ
Sema: Hivi tuwaombe (tuwaa-budu) badala ya Allah (Miungu) ambao hawatunufaishi na hawatudhuru na turudishwe nyuma (kwenye itikadi potofu tulizokwisha ziacha) baada ya Allah kutuongoa kama yule ambaye mashetani wamempagawisha katika ardhi, akiduwaa, akiwa na marafiki wanaomuita aende katika uongofu (wakimwambia): Njoo kwetu?[1] Sema: Hakika, muongozo wa Allah ndio uongofu, na tumeamrishwa tujisalimishe kwa Mola Mlezi wa walimwengu wote
1- - Aya hapa inamtaka Muumini kuwa na msimamo imara na thabiti katika Imani na itikadi yake. Hatakiwi kuyumba au kuyumbishwa. Sio kila analolisikia au kuliona au kushawishiwa alifuate.
وَأَنۡ أَقِيمُواْ ٱلصَّلَوٰةَ وَٱتَّقُوهُۚ وَهُوَ ٱلَّذِيٓ إِلَيۡهِ تُحۡشَرُونَ
Na (tumeamrishwa kwamba): Simamisheni Swala, na mumche yeye (Allah), na yeye ndiye ambaye kwake tu ndiko mtakapokusanywa
وَهُوَ ٱلَّذِي خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ بِٱلۡحَقِّۖ وَيَوۡمَ يَقُولُ كُن فَيَكُونُۚ قَوۡلُهُ ٱلۡحَقُّۚ وَلَهُ ٱلۡمُلۡكُ يَوۡمَ يُنفَخُ فِي ٱلصُّورِۚ عَٰلِمُ ٱلۡغَيۡبِ وَٱلشَّهَٰدَةِۚ وَهُوَ ٱلۡحَكِيمُ ٱلۡخَبِيرُ
Na yeye ndiye aliyeumba mbingu na ardhi kwa haki. Na (kumbuka) siku (Allah) anaposema (kuliambia jambo): Kuwa, basi linakuwa. Kauli yake ni haki. Ni wake yeye tu ufalme siku litakapopulizwa baragumu. Ni mjuzi wa Ghaibu (yaliyofichika) na yaliyo bayana. Na yeye ni Mwenye hekima, Mjuzi wa habari (zote)
۞وَإِذۡ قَالَ إِبۡرَٰهِيمُ لِأَبِيهِ ءَازَرَ أَتَتَّخِذُ أَصۡنَامًا ءَالِهَةً إِنِّيٓ أَرَىٰكَ وَقَوۡمَكَ فِي ضَلَٰلٖ مُّبِينٖ
Na (kumbuka Mtume) Ibrahimu alipomwambia baba yake Azar (kwamba): Hivi unayafanya masanamu Miungu? Hakika, mimi ninakuona wewe na watu wako kwamba mmo katika upotevu ulio wazi
وَكَذَٰلِكَ نُرِيٓ إِبۡرَٰهِيمَ مَلَكُوتَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَلِيَكُونَ مِنَ ٱلۡمُوقِنِينَ
Na kama hivyo tunamuonyesha Ibrahimu ufalme wa mbinguni na ardhini, na ili awe miongoni mwa wenye yakini
فَلَمَّا جَنَّ عَلَيۡهِ ٱلَّيۡلُ رَءَا كَوۡكَبٗاۖ قَالَ هَٰذَا رَبِّيۖ فَلَمَّآ أَفَلَ قَالَ لَآ أُحِبُّ ٱلۡأٓفِلِينَ
Basi (Mtume Ibrahimu) ulipomjia usiku aliona nyota (na) akasema: Huyu ni Mola wangu Mlezi. (Nyota) Ilipozama alisema: Siwapendi wanaopotea
فَلَمَّا رَءَا ٱلۡقَمَرَ بَازِغٗا قَالَ هَٰذَا رَبِّيۖ فَلَمَّآ أَفَلَ قَالَ لَئِن لَّمۡ يَهۡدِنِي رَبِّي لَأَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡقَوۡمِ ٱلضَّآلِّينَ
Na alipoona mwezi umechomoza alisema: Huyu ni Mola wangu Mlezi. Na (mwezi) ulipozama alisema: Kama Mola wangu hataniongoza, kwa hakika kabisa nitakuwa miongoni mwa watu waliopotea
فَلَمَّا رَءَا ٱلشَّمۡسَ بَازِغَةٗ قَالَ هَٰذَا رَبِّي هَٰذَآ أَكۡبَرُۖ فَلَمَّآ أَفَلَتۡ قَالَ يَٰقَوۡمِ إِنِّي بَرِيٓءٞ مِّمَّا تُشۡرِكُونَ
Na alipoliona jua limechomoza alisema: Huyu ni Mola wangu. Huyu ni mkubwa zaidi (kuliko wote). Basi (jua) lilipozama, alisema: Enyi watu wangu, mimi najitenga mbali na (Miungu yote) mnayoshirikisha (na Allah).[1]
1- - Nabii Ibrahimu katika mdahalo huu aliofanya na watu wake hakumaanisha kwamba na yeye aliamini kuwa nyota, mwezi na jua ni Miungu kama walivyoamini. Alichofanya ni maelekezo aliyopewa na Allah kama ilivyoelezwa katika Aya ya 83 ya Sura hii. Pia hiyo ni aina fulani ya mbinu za ufundishaji ya kujifanya unayemfundisha uko pamoja naye ili ufike naye kwenye ukweli na autambue kwa kutumia hoja, akili na mazingira. Nabii Ibrahimu hakuwa Mshirikishaji bali alikuwa Muumini safi anayemuamini na kumuabudu Allah tu. Rejea Aya 120-123 ya Sura Annahli (16).
إِنِّي وَجَّهۡتُ وَجۡهِيَ لِلَّذِي فَطَرَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ حَنِيفٗاۖ وَمَآ أَنَا۠ مِنَ ٱلۡمُشۡرِكِينَ
Hakika, mimi nimeelekeza uso wangu kwa (Allah) aliyeumba mbingu na ardhi, nikiacha itikadi zote potofu, na mimi si miongoni mwa washirikina
وَحَآجَّهُۥ قَوۡمُهُۥۚ قَالَ أَتُحَـٰٓجُّوٓنِّي فِي ٱللَّهِ وَقَدۡ هَدَىٰنِۚ وَلَآ أَخَافُ مَا تُشۡرِكُونَ بِهِۦٓ إِلَّآ أَن يَشَآءَ رَبِّي شَيۡـٔٗاۚ وَسِعَ رَبِّي كُلَّ شَيۡءٍ عِلۡمًاۚ أَفَلَا تَتَذَكَّرُونَ
Na watu wake wakamuwekea mdahalo. Alisema: Hivi, mnanihoji kuhusu Allah, na ilhali ameniongoa? Na siwaogopi hao mnaowashirikisha naye, isipokuwa kama Mola wangu atapenda jambo lolote (linipate). Mola wangu anajua kila kitu kwa mapana na marefu. Hivi hamuonyeki (na haya ninayokuambieni)?
وَكَيۡفَ أَخَافُ مَآ أَشۡرَكۡتُمۡ وَلَا تَخَافُونَ أَنَّكُمۡ أَشۡرَكۡتُم بِٱللَّهِ مَا لَمۡ يُنَزِّلۡ بِهِۦ عَلَيۡكُمۡ سُلۡطَٰنٗاۚ فَأَيُّ ٱلۡفَرِيقَيۡنِ أَحَقُّ بِٱلۡأَمۡنِۖ إِن كُنتُمۡ تَعۡلَمُونَ
Na vipi niwaogope wale (Miungu bandia) mliowashirikisha (na Allah) na ilhali nyinyi hamuogopi kwamba mmemshirikisha Allah na vitu ambavyo hakukuteremshieni hoja (yoyote)? Basi ni kundi lipi lililo na haki zaidi ya kuwa katika amani kati ya makundi mawili (ya mimi na nyinyi) ikiwa (kweli) mnajua?
ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَلَمۡ يَلۡبِسُوٓاْ إِيمَٰنَهُم بِظُلۡمٍ أُوْلَـٰٓئِكَ لَهُمُ ٱلۡأَمۡنُ وَهُم مُّهۡتَدُونَ
Wale walioamini na imani zao hawakuzichanganya na dhuluma (ushirikina), hao ndio wenye amani na hao ndio waongofu
وَتِلۡكَ حُجَّتُنَآ ءَاتَيۡنَٰهَآ إِبۡرَٰهِيمَ عَلَىٰ قَوۡمِهِۦۚ نَرۡفَعُ دَرَجَٰتٖ مَّن نَّشَآءُۗ إِنَّ رَبَّكَ حَكِيمٌ عَلِيمٞ
Na hizo ndio hoja zetu tulizompa (Mtume) Ibrahimu ajadiliane na watu wake[1]. Tunampandisha vyeo tumtakae. Hakika, Mola wako ni Mwenye hekima sana, Mjuzi mno
1- - Hapa Aya inathibitisha kuwa, mdahalo wa Nabii Ibrahimu na watu ni maelekezo ya Allah na hoja zote na mpangilio mzima ameelekezwa na Mola wake.
وَوَهَبۡنَا لَهُۥٓ إِسۡحَٰقَ وَيَعۡقُوبَۚ كُلًّا هَدَيۡنَاۚ وَنُوحًا هَدَيۡنَا مِن قَبۡلُۖ وَمِن ذُرِّيَّتِهِۦ دَاوُۥدَ وَسُلَيۡمَٰنَ وَأَيُّوبَ وَيُوسُفَ وَمُوسَىٰ وَهَٰرُونَۚ وَكَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُحۡسِنِينَ
Na tulimtunuku (Mtume Ibrahimu) Isihaka na Yakubu. Wote tuliwaongoa. Na Nuhu tulimuongoa kabla (yao). Na katika kizazi chake tulimongoa Daudi na Suleimani na Ayubu na Yusufu na Mussa na Haruna. Na kama hivyo tunawalipa wafanyao mazuri
وَزَكَرِيَّا وَيَحۡيَىٰ وَعِيسَىٰ وَإِلۡيَاسَۖ كُلّٞ مِّنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ
Na Zakaria na Yahaya na Issa na Iliasa. Wote ni miongoni mwa watu wema
وَإِسۡمَٰعِيلَ وَٱلۡيَسَعَ وَيُونُسَ وَلُوطٗاۚ وَكُلّٗا فَضَّلۡنَا عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ
Na Ismaili na Alyasaa na Yunus na Lutwi. Na wote (hao) tumewafanya bora kuliko walimwengu (wengine wa zama zao)
وَمِنۡ ءَابَآئِهِمۡ وَذُرِّيَّـٰتِهِمۡ وَإِخۡوَٰنِهِمۡۖ وَٱجۡتَبَيۡنَٰهُمۡ وَهَدَيۡنَٰهُمۡ إِلَىٰ صِرَٰطٖ مُّسۡتَقِيمٖ
Na katika baba zao na watoto wao na ndugu zao. Na tuliwateua na tuliwaongoza njia iliyo nyooka
ذَٰلِكَ هُدَى ٱللَّهِ يَهۡدِي بِهِۦ مَن يَشَآءُ مِنۡ عِبَادِهِۦۚ وَلَوۡ أَشۡرَكُواْ لَحَبِطَ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ
Huo ndio muongozo wa Allah, anamuongoa amtakaye katika waja wake. Na lau kama (Mitume) wangefanya ushirikina (wa kumshi-rikisha Allah na vitu vingine), yangewaharibikia (matendo) waliyokuwa wanayafanya
أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ ءَاتَيۡنَٰهُمُ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡحُكۡمَ وَٱلنُّبُوَّةَۚ فَإِن يَكۡفُرۡ بِهَا هَـٰٓؤُلَآءِ فَقَدۡ وَكَّلۡنَا بِهَا قَوۡمٗا لَّيۡسُواْ بِهَا بِكَٰفِرِينَ
Hao ndio tuliowapa vitabu na utawala na Utume. Endepo hawa (watu wa Makkah) watayakataa hayo, basi tumesha yawakilisha kwa watu (wengine) wasioyakataa (ambao ni Muhajirina na Answari)
أُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ هَدَى ٱللَّهُۖ فَبِهُدَىٰهُمُ ٱقۡتَدِهۡۗ قُل لَّآ أَسۡـَٔلُكُمۡ عَلَيۡهِ أَجۡرًاۖ إِنۡ هُوَ إِلَّا ذِكۡرَىٰ لِلۡعَٰلَمِينَ
Hao ndio wale ambao Allah amewaongoa. Basi fuata muongozo wao[1]. Sema (uwaambie): Sikuombeni ujira wowote katika hilo (la kukufikishieni ujumbe wa Allah). Hayakuwa hayo (ninayokufikishieni) isipokuwa tu ni mawaidha kwa walimwengu wote
1- - Aya hapa inawaongoza Waumini kufuata muongozo wa viongozi wao. Iwapo kiongozi atakapotoka, utaachwa upotofu wake.
وَمَا قَدَرُواْ ٱللَّهَ حَقَّ قَدۡرِهِۦٓ إِذۡ قَالُواْ مَآ أَنزَلَ ٱللَّهُ عَلَىٰ بَشَرٖ مِّن شَيۡءٖۗ قُلۡ مَنۡ أَنزَلَ ٱلۡكِتَٰبَ ٱلَّذِي جَآءَ بِهِۦ مُوسَىٰ نُورٗا وَهُدٗى لِّلنَّاسِۖ تَجۡعَلُونَهُۥ قَرَاطِيسَ تُبۡدُونَهَا وَتُخۡفُونَ كَثِيرٗاۖ وَعُلِّمۡتُم مَّا لَمۡ تَعۡلَمُوٓاْ أَنتُمۡ وَلَآ ءَابَآؤُكُمۡۖ قُلِ ٱللَّهُۖ ثُمَّ ذَرۡهُمۡ فِي خَوۡضِهِمۡ يَلۡعَبُونَ
Na hawakumpa Allah heshima anayostahiki, pale waliposema: Allah hakuteremsha kitu chochote kwa mwanadamu. Sema: Ni nani aliyeteremsha kitabu alichokileta Mussa, kikiwa ni nuru na muongozo kwa watu? Mnakifanya ni makaratasi mnayoyaonyesha na mengi mnayaficha. Na mmefundishwa mliyokuwa hamyajui ninyi wala baba zenu. Sema: (Ni) Allah (ndiye aliyekiteremsha), kisha waache wacheze katika porojo zao
وَهَٰذَا كِتَٰبٌ أَنزَلۡنَٰهُ مُبَارَكٞ مُّصَدِّقُ ٱلَّذِي بَيۡنَ يَدَيۡهِ وَلِتُنذِرَ أُمَّ ٱلۡقُرَىٰ وَمَنۡ حَوۡلَهَاۚ وَٱلَّذِينَ يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ يُؤۡمِنُونَ بِهِۦۖ وَهُمۡ عَلَىٰ صَلَاتِهِمۡ يُحَافِظُونَ
Na hii (Qur’ani) ni kitabu tulichokiteremsha, kilochobarikiwa, kinachosadikisha (kitabu) kilichoko mbele yake na (tumekiteremsha) ili uwaonye (kwacho watu wa mji wa) Mama wa Miji (Makkah) na walioko (katika miji iliyopo) pembezoni mwake[1]. Na wale wanaoamini Akhera (kuwa ipo) wanakiamini kitabu hicho, nao wanadumisha Swala zao
1- - Kinachokusudiwa hapa ni maeneo mengine ya dunia. Qur’ani imeteremka kwa ajili ya watu wote duniani. Rejea Aya ya 41 ya sura Azzumar (39). Pia rejea Aya ya 51-52 ya Sura Alqalam (68).
وَمَنۡ أَظۡلَمُ مِمَّنِ ٱفۡتَرَىٰ عَلَى ٱللَّهِ كَذِبًا أَوۡ قَالَ أُوحِيَ إِلَيَّ وَلَمۡ يُوحَ إِلَيۡهِ شَيۡءٞ وَمَن قَالَ سَأُنزِلُ مِثۡلَ مَآ أَنزَلَ ٱللَّهُۗ وَلَوۡ تَرَىٰٓ إِذِ ٱلظَّـٰلِمُونَ فِي غَمَرَٰتِ ٱلۡمَوۡتِ وَٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ بَاسِطُوٓاْ أَيۡدِيهِمۡ أَخۡرِجُوٓاْ أَنفُسَكُمُۖ ٱلۡيَوۡمَ تُجۡزَوۡنَ عَذَابَ ٱلۡهُونِ بِمَا كُنتُمۡ تَقُولُونَ عَلَى ٱللَّهِ غَيۡرَ ٱلۡحَقِّ وَكُنتُمۡ عَنۡ ءَايَٰتِهِۦ تَسۡتَكۡبِرُونَ
Na ni nani dhalimu zaidi kuliko yule aliyemzushia Allah uongo (kuwa amempa Utume) au aliyesema kuwa: Nimeletewa Wahyi na ilhali hakuletewa Wahyi wowote? Na (ni nani dhalimu zaidi kuliko) yule aliyesema kuwa: Nitateremsha mfano wa aliyoteremsha Allah? Na lau ungeona wakati madhalimu wamo katika mahangaiko ya mauti na Malaika wamenyoosha mikono yao (wakiwa tayari kuchukua roho zao wakiwaambia): Zitoeni (ziokoeni) roho zenu (kutoka mikononi mwetu kama mnaweza kwa sababu) leo mtalipwa adhabu ya fedheha kwa sababu ya yale yasiyokuwa ya haki mliyomsingizia Allah, na mlikuwa mnazifanyia kiburi Aya zake
وَلَقَدۡ جِئۡتُمُونَا فُرَٰدَىٰ كَمَا خَلَقۡنَٰكُمۡ أَوَّلَ مَرَّةٖ وَتَرَكۡتُم مَّا خَوَّلۡنَٰكُمۡ وَرَآءَ ظُهُورِكُمۡۖ وَمَا نَرَىٰ مَعَكُمۡ شُفَعَآءَكُمُ ٱلَّذِينَ زَعَمۡتُمۡ أَنَّهُمۡ فِيكُمۡ شُرَكَـٰٓؤُاْۚ لَقَد تَّقَطَّعَ بَيۡنَكُمۡ وَضَلَّ عَنكُم مَّا كُنتُمۡ تَزۡعُمُونَ
Na kwa hakika kabisa, mmetujia (mkiwa) wapweke kama tulivyo kuumbeni mara ya kwanza, na mmeyaacha nyuma yenu yote tuliyokupeni, na hatuoni mkiwa pamoja nao (wale) waombezi wenu ambao mlidai kuwa mna ushirika nao. Kwa hakika kabisa, mafungamano kati yenu yamekatika, na yamekupoteeni mliyokuwa mnadai
۞إِنَّ ٱللَّهَ فَالِقُ ٱلۡحَبِّ وَٱلنَّوَىٰۖ يُخۡرِجُ ٱلۡحَيَّ مِنَ ٱلۡمَيِّتِ وَمُخۡرِجُ ٱلۡمَيِّتِ مِنَ ٱلۡحَيِّۚ ذَٰلِكُمُ ٱللَّهُۖ فَأَنَّىٰ تُؤۡفَكُونَ
Hakika Allah ndiye Mpasuaji punje na kokwa. Anatoa kilichoko hai kutoka katika kilichokufa na ni Mwenye kutoa kilichokufa kutoka katika kilichoko hai. Huyo kwenu ndiye Allah (Mwenye haki ya kuabudiwa). Basi vipi mnapotoshwa?