Sourate: AL-BALAD 

Verset : 1

لَآ أُقۡسِمُ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ

Naapa kwa Mji huu!



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 2

وَأَنتَ حِلُّۢ بِهَٰذَا ٱلۡبَلَدِ

Nawe unakaa Mji huu



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 3

وَوَالِدٖ وَمَا وَلَدَ

Na naapa kwa mzazi na alicho kizaa



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 4

لَقَدۡ خَلَقۡنَا ٱلۡإِنسَٰنَ فِي كَبَدٍ

Hakika tumemuumba mtu katika taabu



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 5

أَيَحۡسَبُ أَن لَّن يَقۡدِرَ عَلَيۡهِ أَحَدٞ

Ati anadhani hapana yeyote atakaye muweza?



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 6

يَقُولُ أَهۡلَكۡتُ مَالٗا لُّبَدًا

Anasema: Nimeteketeza mali chungu nzima



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 7

أَيَحۡسَبُ أَن لَّمۡ يَرَهُۥٓ أَحَدٌ

Ati anadhani ya kuwa hapana yeyote anaye mwona?



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 8

أَلَمۡ نَجۡعَل لَّهُۥ عَيۡنَيۡنِ

Kwani hatukumpa macho mawili?



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 9

وَلِسَانٗا وَشَفَتَيۡنِ

Na ulimi, na midomo miwili?



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 10

وَهَدَيۡنَٰهُ ٱلنَّجۡدَيۡنِ

Na tukambainishia njia zote mbili?



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 11

فَلَا ٱقۡتَحَمَ ٱلۡعَقَبَةَ

Lakini hakujitoma (hakuingia) kwenye njia ya vikwazo vya milimani



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 12

وَمَآ أَدۡرَىٰكَ مَا ٱلۡعَقَبَةُ

Na nini kitakujulisha ni nini njia ya vikwazo vya milimani?



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 13

فَكُّ رَقَبَةٍ

Kumkomboa mtumwa;



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 14

أَوۡ إِطۡعَٰمٞ فِي يَوۡمٖ ذِي مَسۡغَبَةٖ

Au kumlisha siku ya njaa



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 15

يَتِيمٗا ذَا مَقۡرَبَةٍ

Yatima aliye katika jamaa wa karibu (ndugu)



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 16

أَوۡ مِسۡكِينٗا ذَا مَتۡرَبَةٖ

Au masikini aliye vumbini



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 17

ثُمَّ كَانَ مِنَ ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلصَّبۡرِ وَتَوَاصَوۡاْ بِٱلۡمَرۡحَمَةِ

Tena awe miongoni mwa walio amini na wakausiana kusubiri na wakausiana kuhurumiana



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 18

أُوْلَـٰٓئِكَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَيۡمَنَةِ

Hao ndio watu wa kheri wa kuliani



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 19

وَٱلَّذِينَ كَفَرُواْ بِـَٔايَٰتِنَا هُمۡ أَصۡحَٰبُ ٱلۡمَشۡـَٔمَةِ

Lakini walio zikataa Ishara zetu, hao ndio watu wa shari wa kushotoni



Sourate: AL-BALAD 

Verset : 20

عَلَيۡهِمۡ نَارٞ مُّؤۡصَدَةُۢ

Juu yao utakuwa Moto ulio fungiwa kila upande