Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 1

الٓمٓصٓ

Allah ndiye Mjuzi zaidi wa alichokikusudia katika herufi hizi



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 2

كِتَٰبٌ أُنزِلَ إِلَيۡكَ فَلَا يَكُن فِي صَدۡرِكَ حَرَجٞ مِّنۡهُ لِتُنذِرَ بِهِۦ وَذِكۡرَىٰ لِلۡمُؤۡمِنِينَ

(Hii Qur’ani ni) Kitabu ulichoteremshiwa. Basi kusiwe na uzito wowote ndani ya kifua chako juu yake (usikose raha katika kukiamini na kukitangaza). (Umeteremshiwa kitabu hiki) Ili kwacho uwaonye (watu) na (ili kiwe) ukumbusho kwa waumini



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 3

ٱتَّبِعُواْ مَآ أُنزِلَ إِلَيۡكُم مِّن رَّبِّكُمۡ وَلَا تَتَّبِعُواْ مِن دُونِهِۦٓ أَوۡلِيَآءَۗ قَلِيلٗا مَّا تَذَكَّرُونَ

Fuateni yale yaliyoteremshwa kwenu kutoka kwa Mola wenu Mlezi na msifuate wapenzi wengine badala yake. Ni machache mno mnayowaidhika nayo



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 4

وَكَم مِّن قَرۡيَةٍ أَهۡلَكۡنَٰهَا فَجَآءَهَا بَأۡسُنَا بَيَٰتًا أَوۡ هُمۡ قَآئِلُونَ

Na ni miji mingi tumeiangamiza; iliwajia adhabu yetu wakiwa wamelala usiku au wakiwa wamejipumzisha mchana



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 5

فَمَا كَانَ دَعۡوَىٰهُمۡ إِذۡ جَآءَهُم بَأۡسُنَآ إِلَّآ أَن قَالُوٓاْ إِنَّا كُنَّا ظَٰلِمِينَ

Basi hayakuwa madai yao (majuto yao) pale adhabu yetu ilipowafika isipokuwa tu walisema: Hakika, sisi tulikuwa madhalimu



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 6

فَلَنَسۡـَٔلَنَّ ٱلَّذِينَ أُرۡسِلَ إِلَيۡهِمۡ وَلَنَسۡـَٔلَنَّ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Kwa hakika kabisa, tutawauliza wale waliopelekewa (Mitume) na kwa hakika kabisa tutawauliza tuliowapeleka (Mitume)



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 7

فَلَنَقُصَّنَّ عَلَيۡهِم بِعِلۡمٖۖ وَمَا كُنَّا غَآئِبِينَ

Tena, kwa yakini kabisa, tutawasimulia (walichokifanya) kwa kujua (kwa hoja), na hatukuwa mbali nao



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 8

وَٱلۡوَزۡنُ يَوۡمَئِذٍ ٱلۡحَقُّۚ فَمَن ثَقُلَتۡ مَوَٰزِينُهُۥ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ

Na mizani siku hiyo ni haki tu. Basi yeyote ambaye uzani wake (wa matendo yakheri) utakuwa mzito (na kuelemea) basi hao ndio tu wenye kufaulu



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 9

وَمَنۡ خَفَّتۡ مَوَٰزِينُهُۥ فَأُوْلَـٰٓئِكَ ٱلَّذِينَ خَسِرُوٓاْ أَنفُسَهُم بِمَا كَانُواْ بِـَٔايَٰتِنَا يَظۡلِمُونَ

Na yeyote ambaye uzani wake (wa matendo yake ya kheri) utakuwa hafifu, basi hao ndio waliozitia hasara nafsi zao kwa sababu ya walivyokuwa wanazifanyia dhulumu aya zetu (kwa kuzikataa na kuzipinga)



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 10

وَلَقَدۡ مَكَّنَّـٰكُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ وَجَعَلۡنَا لَكُمۡ فِيهَا مَعَٰيِشَۗ قَلِيلٗا مَّا تَشۡكُرُونَ

Na kwa hakika kabisa, tulikupeni nafasi ardhini (duniani), na tulikufanyieni humo njia za (kupata) maisha (yenu). Ni uchache mno mnavyoshukuru



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 11

وَلَقَدۡ خَلَقۡنَٰكُمۡ ثُمَّ صَوَّرۡنَٰكُمۡ ثُمَّ قُلۡنَا لِلۡمَلَـٰٓئِكَةِ ٱسۡجُدُواْ لِأٓدَمَ فَسَجَدُوٓاْ إِلَّآ إِبۡلِيسَ لَمۡ يَكُن مِّنَ ٱلسَّـٰجِدِينَ

Na kwa hakika kabisa, tulikuumbeni, kisha tulikutieni sura, kisha tuliwaambia Malaika: Msujudieni Adamu. Walisujudu isipokuwa Ibilisi tu, hakuwa miongoni mwa waliosujudu



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 12

قَالَ مَا مَنَعَكَ أَلَّا تَسۡجُدَ إِذۡ أَمَرۡتُكَۖ قَالَ أَنَا۠ خَيۡرٞ مِّنۡهُ خَلَقۡتَنِي مِن نَّارٖ وَخَلَقۡتَهُۥ مِن طِينٖ

(Allah) Alisema (akimuuliza Ibilisi): Kipi kilichokuzuia usisujudu pale nilipokuamrisha? (Ibilisi) Alisema: Mimi ni bora zaidi kuliko yeye; umeniumba kwa moto, na yeye umemuumba kwa udongo



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 13

قَالَ فَٱهۡبِطۡ مِنۡهَا فَمَا يَكُونُ لَكَ أَن تَتَكَبَّرَ فِيهَا فَٱخۡرُجۡ إِنَّكَ مِنَ ٱلصَّـٰغِرِينَ

(Allah) Akasema: Basi teremka humo. Haikustahiki kwako kufanya kiburi humo. Basi toka. Hakika, wewe ni miongoni mwa walio duni kabisa



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 14

قَالَ أَنظِرۡنِيٓ إِلَىٰ يَوۡمِ يُبۡعَثُونَ

(Ibilisi) Alisema: Nibakishe mpaka Siku (waja wako) wataka-pofufuliwa



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 15

قَالَ إِنَّكَ مِنَ ٱلۡمُنظَرِينَ

(Allah) Akasema: Hakika, wewe ni miongoni mwa watakaobakishwa



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 16

قَالَ فَبِمَآ أَغۡوَيۡتَنِي لَأَقۡعُدَنَّ لَهُمۡ صِرَٰطَكَ ٱلۡمُسۡتَقِيمَ

(Ibilisi) Akasema: Basi kwa sababu umenipotosha (umeniacha nipotoke), nina apa kwamba, nitawakalia (nitawawekea vikwazo) katika njia yako ya sawa



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 17

ثُمَّ لَأٓتِيَنَّهُم مِّنۢ بَيۡنِ أَيۡدِيهِمۡ وَمِنۡ خَلۡفِهِمۡ وَعَنۡ أَيۡمَٰنِهِمۡ وَعَن شَمَآئِلِهِمۡۖ وَلَا تَجِدُ أَكۡثَرَهُمۡ شَٰكِرِينَ

Kisha, kwa yakini kabisa, nitawaendea mbele yao na nyuma yao na kuliani kwao na kushotoni kwao[1]. Na hutapata wengi wao wenye kushukuru


1- - Hapa Ibilisi anakusudia kwamba, atamfuatilia mwanadamu kila alipo. Hii ni sawa na ule msemo wa Kiswahili wa mtaani usemao “Nitakula naye sahani moja”.


Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 18

قَالَ ٱخۡرُجۡ مِنۡهَا مَذۡءُومٗا مَّدۡحُورٗاۖ لَّمَن تَبِعَكَ مِنۡهُمۡ لَأَمۡلَأَنَّ جَهَنَّمَ مِنكُمۡ أَجۡمَعِينَ

(Allah) Akasema (kumwambia Ibilisi kwamba): Toka humo (Peponi) ukiwa umechukiwa, umelaaniwa. Kwa yakini kabisa, yeyote atakayekufuata wewe miongoni mwao hakika nitaijaza Jahanamu kwa (kukutumbukizeni humo) nyinyi nyote



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 19

وَيَـٰٓـَٔادَمُ ٱسۡكُنۡ أَنتَ وَزَوۡجُكَ ٱلۡجَنَّةَ فَكُلَا مِنۡ حَيۡثُ شِئۡتُمَا وَلَا تَقۡرَبَا هَٰذِهِ ٱلشَّجَرَةَ فَتَكُونَا مِنَ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na ewe Adamu, kaa wewe na mkeo Peponi. Basi kuleni katika mpendavyo na msiusogelee mti huu, mtakuwa miongoni mwa madhalimu



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 20

فَوَسۡوَسَ لَهُمَا ٱلشَّيۡطَٰنُ لِيُبۡدِيَ لَهُمَا مَا وُۥرِيَ عَنۡهُمَا مِن سَوۡءَٰتِهِمَا وَقَالَ مَا نَهَىٰكُمَا رَبُّكُمَا عَنۡ هَٰذِهِ ٱلشَّجَرَةِ إِلَّآ أَن تَكُونَا مَلَكَيۡنِ أَوۡ تَكُونَا مِنَ ٱلۡخَٰلِدِينَ

Basi shetani akawashawishi wawili hao ili awafunulie tupu zao zilizohifadhiwa na kusema (akiwaambia): Mola wenu hakukukatazeni mti huu isipokuwa tu msije mkawa Malaika wawili au mkawa miongoni mwa watakaoishi milele



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 21

وَقَاسَمَهُمَآ إِنِّي لَكُمَا لَمِنَ ٱلنَّـٰصِحِينَ

Na (shetani) akawaapia (kwamba): Kwa hakika kabisa, mimi kwenu ni miongoni mwa watoaji nasaha



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 22

فَدَلَّىٰهُمَا بِغُرُورٖۚ فَلَمَّا ذَاقَا ٱلشَّجَرَةَ بَدَتۡ لَهُمَا سَوۡءَٰتُهُمَا وَطَفِقَا يَخۡصِفَانِ عَلَيۡهِمَا مِن وَرَقِ ٱلۡجَنَّةِۖ وَنَادَىٰهُمَا رَبُّهُمَآ أَلَمۡ أَنۡهَكُمَا عَن تِلۡكُمَا ٱلشَّجَرَةِ وَأَقُل لَّكُمَآ إِنَّ ٱلشَّيۡطَٰنَ لَكُمَا عَدُوّٞ مُّبِينٞ

(Shetani) Akawashusha (Kutoka katika daraja la utiifu na kuwaweka katika uovu wa kukaidi amri ya Allah) kwa njia ya hadaa. Basi walipo uonja mti ule, zilidhihiri tupu zao na wakaanza kujibandika majani ya bustanini (ili kujisitiri). Na Mola wao aliwaita: Hivi sikukukatazeni mti ule na kukuambieni ya kwamba, hakika shetani kwenu ni adui aliye dhahiri sana?



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 23

قَالَا رَبَّنَا ظَلَمۡنَآ أَنفُسَنَا وَإِن لَّمۡ تَغۡفِرۡ لَنَا وَتَرۡحَمۡنَا لَنَكُونَنَّ مِنَ ٱلۡخَٰسِرِينَ

(Adamu na mkewe) Wakasema: Ewe Mola wetu Mlezi, sisi tumezidhulumu nafsi zetu, na kama hutatusamehe na kutuhurumia kwa hakika kabisa tutakuwa miongoni mwa wenye hasara



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 24

قَالَ ٱهۡبِطُواْ بَعۡضُكُمۡ لِبَعۡضٍ عَدُوّٞۖ وَلَكُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ مُسۡتَقَرّٞ وَمَتَٰعٌ إِلَىٰ حِينٖ

(Allah) Akasema: Teremkeni, nyinyi kwa nyinyi ni maadui, na nyinyi katika ardhi (duniani) mtakuwa na makazi na starehe (burudani) mpaka muda (maalumu)



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 25

قَالَ فِيهَا تَحۡيَوۡنَ وَفِيهَا تَمُوتُونَ وَمِنۡهَا تُخۡرَجُونَ

(Allah) Akasema: Humo (duniani) mtaishi na humo mtakufa na humo mtatolewa (mtafufuliwa)



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 26

يَٰبَنِيٓ ءَادَمَ قَدۡ أَنزَلۡنَا عَلَيۡكُمۡ لِبَاسٗا يُوَٰرِي سَوۡءَٰتِكُمۡ وَرِيشٗاۖ وَلِبَاسُ ٱلتَّقۡوَىٰ ذَٰلِكَ خَيۡرٞۚ ذَٰلِكَ مِنۡ ءَايَٰتِ ٱللَّهِ لَعَلَّهُمۡ يَذَّكَّرُونَ

Enyi wanadamu, hakika tumekuteremshieni vazi linaloficha tupu zenu na pambo. Na vazi la kumcha Allah ndio bora zaidi. Hizo ni baadhi ya ishara za Allah ili (wanadamu) wapate kukumbuka (neema za Mola wao Mlezi na kumshukuru)



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 27

يَٰبَنِيٓ ءَادَمَ لَا يَفۡتِنَنَّكُمُ ٱلشَّيۡطَٰنُ كَمَآ أَخۡرَجَ أَبَوَيۡكُم مِّنَ ٱلۡجَنَّةِ يَنزِعُ عَنۡهُمَا لِبَاسَهُمَا لِيُرِيَهُمَا سَوۡءَٰتِهِمَآۚ إِنَّهُۥ يَرَىٰكُمۡ هُوَ وَقَبِيلُهُۥ مِنۡ حَيۡثُ لَا تَرَوۡنَهُمۡۗ إِنَّا جَعَلۡنَا ٱلشَّيَٰطِينَ أَوۡلِيَآءَ لِلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ

Enyi Wanadamu, kamwe shetani asikufitinisheni[1] kama alivyowatoa Peponi wazazi wenu, akiwavua nguo zao ili kuwawekea wazi tupu zao. Hakika yeye (shetani) anakuoneni yeye na jeshi lake katika namna ambayo nyinyi hamuwaoni. Hakika, sisi tumewafanya mashetani wandani wa (watu) wasioamini


1- - Shetani asikudanganyeni kwa kukupambieni maasi, kama ambavyo alimhadaa baba yenu Adamu na mkewe kwa kuwashawishi waonje mti. Matokeo yake walitolewa Peponi.


Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 28

وَإِذَا فَعَلُواْ فَٰحِشَةٗ قَالُواْ وَجَدۡنَا عَلَيۡهَآ ءَابَآءَنَا وَٱللَّهُ أَمَرَنَا بِهَاۗ قُلۡ إِنَّ ٱللَّهَ لَا يَأۡمُرُ بِٱلۡفَحۡشَآءِۖ أَتَقُولُونَ عَلَى ٱللَّهِ مَا لَا تَعۡلَمُونَ

Na wafanyapo mambo machafu wanasema: (Haya tuyafanyayo) Tumewakuta nayo baba zetu na Allah ametuamuru hayo. Sema: Hakika, Allah haamrishi machafu. Hivi mnamzushia Allah msiyoyajua?



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 29

قُلۡ أَمَرَ رَبِّي بِٱلۡقِسۡطِۖ وَأَقِيمُواْ وُجُوهَكُمۡ عِندَ كُلِّ مَسۡجِدٖ وَٱدۡعُوهُ مُخۡلِصِينَ لَهُ ٱلدِّينَۚ كَمَا بَدَأَكُمۡ تَعُودُونَ

Sema: Mola wangu Mlezi ameamrisha (kufanya) uadilifu. Na elekezeni nyuso zenu kila mnaposwali (mkusudieni Allah kila mfanyapo ibada) na muabuduni yeye tu mkimtakasia dini. Kama (Allah) ambavyo amekuumbeni mwanzo ndivyo mtakavyorudi



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 30

فَرِيقًا هَدَىٰ وَفَرِيقًا حَقَّ عَلَيۡهِمُ ٱلضَّلَٰلَةُۚ إِنَّهُمُ ٱتَّخَذُواْ ٱلشَّيَٰطِينَ أَوۡلِيَآءَ مِن دُونِ ٱللَّهِ وَيَحۡسَبُونَ أَنَّهُم مُّهۡتَدُونَ

Kundi moja (Allah) ameliongoa na kundi (lingine) limestahiki kupotea. Hakika, wao wamewafanya mashetani wandani (wao) badala ya Allah na wanadhani kwamba wameongoka