Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 1

وَٱلصَّـٰٓفَّـٰتِ صَفّٗا

Nina apa kwa wanao jipanga kwa safu



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 2

فَٱلزَّـٰجِرَٰتِ زَجۡرٗا

Na wenye kukemea mabaya



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 3

فَٱلتَّـٰلِيَٰتِ ذِكۡرًا

Na wenye kusoma ukumbusho



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 4

إِنَّ إِلَٰهَكُمۡ لَوَٰحِدٞ

(Kwamba) Hakika kabisa, Mungu wenu ni Mmoja tu



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 5

رَّبُّ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِ وَمَا بَيۡنَهُمَا وَرَبُّ ٱلۡمَشَٰرِقِ

Mola Mlezi wa mbingu na ardhi na vilivyomo kati yao, na ni Mola Mlezi wa mashariki zote



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 6

إِنَّا زَيَّنَّا ٱلسَّمَآءَ ٱلدُّنۡيَا بِزِينَةٍ ٱلۡكَوَاكِبِ

Hakika Sisi tumeipamba mbingu ya karibu kwa pambo la nyota



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 7

وَحِفۡظٗا مِّن كُلِّ شَيۡطَٰنٖ مَّارِدٖ

Na kwa ajili ya ulinzi dhidi ya kila shetani muasi



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 8

لَّا يَسَّمَّعُونَ إِلَى ٱلۡمَلَإِ ٱلۡأَعۡلَىٰ وَيُقۡذَفُونَ مِن كُلِّ جَانِبٖ

Wasiweze kuwasikiliza viumbe watukufu. Na wanafukuzwa huko kila upande



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 9

دُحُورٗاۖ وَلَهُمۡ عَذَابٞ وَاصِبٌ

Wakifurushwa. Na wanayo adhabu ya kudumu



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 10

إِلَّا مَنۡ خَطِفَ ٱلۡخَطۡفَةَ فَأَتۡبَعَهُۥ شِهَابٞ ثَاقِبٞ

Isipo kuwa anayenyakua kitu kidogo, na mara humfuatia kimondo kinacho ng’ara



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 11

فَٱسۡتَفۡتِهِمۡ أَهُمۡ أَشَدُّ خَلۡقًا أَم مَّنۡ خَلَقۡنَآۚ إِنَّا خَلَقۡنَٰهُم مِّن طِينٖ لَّازِبِۭ

Hebu waulize: Je! Wao ni wenye umbo gumu zaidi au hao wengine tulio waumba? Hakika Sisi tuliwaumba wao kwa udongo unao nata



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 12

بَلۡ عَجِبۡتَ وَيَسۡخَرُونَ

Bali unastaajabu, na wao wanafanya maskhara



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 13

وَإِذَا ذُكِّرُواْ لَا يَذۡكُرُونَ

Na wanapo kumbushwa hawakumbuki



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 14

وَإِذَا رَأَوۡاْ ءَايَةٗ يَسۡتَسۡخِرُونَ

Na wanapo ona Ishara, wanafanya maskhara



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 15

وَقَالُوٓاْ إِنۡ هَٰذَآ إِلَّا سِحۡرٞ مُّبِينٌ

Na husema: Haya si chochote ila ni uchawi tu ulio dhaahiri



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 16

أَءِذَا مِتۡنَا وَكُنَّا تُرَابٗا وَعِظَٰمًا أَءِنَّا لَمَبۡعُوثُونَ

Ati tukisha kufa na tukawa udongo na mifupa ndio kweli tutafufuliwa?



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 17

أَوَءَابَآؤُنَا ٱلۡأَوَّلُونَ

Hata baba zetu wa zamani?



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 18

قُلۡ نَعَمۡ وَأَنتُمۡ دَٰخِرُونَ

Sema: Naam! (Mtafufuliwa) Hali nanyi ni madhalili



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 19

فَإِنَّمَا هِيَ زَجۡرَةٞ وَٰحِدَةٞ فَإِذَا هُمۡ يَنظُرُونَ

Huko utapigwa ukelele mmoja tu! Na hapo ndio wataona!



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 20

وَقَالُواْ يَٰوَيۡلَنَا هَٰذَا يَوۡمُ ٱلدِّينِ

Watasema: Ole wetu! Hii ndiyo Siku ya Malipo



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 21

هَٰذَا يَوۡمُ ٱلۡفَصۡلِ ٱلَّذِي كُنتُم بِهِۦ تُكَذِّبُونَ

Hii ndiyo Siku ya Hukumu mliyokuwa mnaikadhibisha



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 22

۞ٱحۡشُرُواْ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ وَأَزۡوَٰجَهُمۡ وَمَا كَانُواْ يَعۡبُدُونَ

Wakusanyeni walio dhulumu, na wake zao, na hao walio kuwa wakiwaabudu



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 23

مِن دُونِ ٱللَّهِ فَٱهۡدُوهُمۡ إِلَىٰ صِرَٰطِ ٱلۡجَحِيمِ

Badala ya Allah. Waongozeni njia ya Jahannamu!



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 24

وَقِفُوهُمۡۖ إِنَّهُم مَّسۡـُٔولُونَ

Na wasimamisheni. Hakika hao wataulizwa:



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 25

مَا لَكُمۡ لَا تَنَاصَرُونَ

Mna nini? Mbona hamsaidiani?



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 26

بَلۡ هُمُ ٱلۡيَوۡمَ مُسۡتَسۡلِمُونَ

Bali hii leo, watasalimu amri



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 27

وَأَقۡبَلَ بَعۡضُهُمۡ عَلَىٰ بَعۡضٖ يَتَسَآءَلُونَ

Watakabiliana wao kwa wao kuulizana



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 28

قَالُوٓاْ إِنَّكُمۡ كُنتُمۡ تَأۡتُونَنَا عَنِ ٱلۡيَمِينِ

Watasema: Kwa hakika nyinyi mlikuwa mkitujia upande wa kulia



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 29

قَالُواْ بَل لَّمۡ تَكُونُواْ مُؤۡمِنِينَ

Watasema (wakubwa): Bali nyinyi wenyewe hamkuwa Waumini



Sourate: ASSWAAFFAAT 

Verset : 30

وَمَا كَانَ لَنَا عَلَيۡكُم مِّن سُلۡطَٰنِۭۖ بَلۡ كُنتُمۡ قَوۡمٗا طَٰغِينَ

Sisi hatukuwa na mamlaka juu yenu, bali nyinyi wenyewe mlikuwa wapotovu