Sourate: ANNAHLI 

Verset : 1

أَتَىٰٓ أَمۡرُ ٱللَّهِ فَلَا تَسۡتَعۡجِلُوهُۚ سُبۡحَٰنَهُۥ وَتَعَٰلَىٰ عَمَّا يُشۡرِكُونَ

Amri ya Allah imefika. Basi msiihimize. Utakasifu ni wake Allah, na ametukuka (juu) ya vyote wanavyovishirikisha naye



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 2

يُنَزِّلُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةَ بِٱلرُّوحِ مِنۡ أَمۡرِهِۦ عَلَىٰ مَن يَشَآءُ مِنۡ عِبَادِهِۦٓ أَنۡ أَنذِرُوٓاْ أَنَّهُۥ لَآ إِلَٰهَ إِلَّآ أَنَا۠ فَٱتَّقُونِ

Anateremsha Malaika (Jibrili) na wahyi kwa amri yake kwa amtakaye miongoni mwa waja wake (Mitume)(akiwaambia kuwa): Waonyeni watu, wajue kwamba: Hakika hakuna wa kuabudiwa kwa haki isipokuwa mimi tu; basi niogopeni



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 3

خَلَقَ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ بِٱلۡحَقِّۚ تَعَٰلَىٰ عَمَّا يُشۡرِكُونَ

Ameziumba mbingu na ardhi kwa haki. Ametukuka Allah na ametukuka (juu zaidi) ya vyote wanavyovishirikisha naye



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 4

خَلَقَ ٱلۡإِنسَٰنَ مِن نُّطۡفَةٖ فَإِذَا هُوَ خَصِيمٞ مُّبِينٞ

Amemuumba mwanadamu kutokana na tone la manii, ghafla amekuwa mshindani aliye dhahiri mno



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 5

وَٱلۡأَنۡعَٰمَ خَلَقَهَاۖ لَكُمۡ فِيهَا دِفۡءٞ وَمَنَٰفِعُ وَمِنۡهَا تَأۡكُلُونَ

Na wanyama amewaumba kwa ajili yenu, katika hao mnapata joto na manufaa (mbali mbali), na baadhi yao mnawala



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 6

وَلَكُمۡ فِيهَا جَمَالٌ حِينَ تُرِيحُونَ وَحِينَ تَسۡرَحُونَ

Na nipambo kwenu pale mnapowarudisha jioni na mnapowapeleka malishoni asubuhi



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 7

وَتَحۡمِلُ أَثۡقَالَكُمۡ إِلَىٰ بَلَدٖ لَّمۡ تَكُونُواْ بَٰلِغِيهِ إِلَّا بِشِقِّ ٱلۡأَنفُسِۚ إِنَّ رَبَّكُمۡ لَرَءُوفٞ رَّحِيمٞ

Na (baadhi ya wanyama hao) wanawabebea mizigo yenu kupeleka kwenye mji msikoweza kufika isipokuwa kwa juhudi na taabu kubwa. Hakika Mola wenu mlezi ni mpole sana, mwenye kurehemu



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 8

وَٱلۡخَيۡلَ وَٱلۡبِغَالَ وَٱلۡحَمِيرَ لِتَرۡكَبُوهَا وَزِينَةٗۚ وَيَخۡلُقُ مَا لَا تَعۡلَمُونَ

Na (amewaumba) farasi na nyumbu na punda ili muwapande (katika safari zenu) na mapambo, na anaumba msivyovijua



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 9

وَعَلَى ٱللَّهِ قَصۡدُ ٱلسَّبِيلِ وَمِنۡهَا جَآئِرٞۚ وَلَوۡ شَآءَ لَهَدَىٰكُمۡ أَجۡمَعِينَ

Na ni kwa Allah tu (kunako-bainishwa) njia iliyo sawa, na miongoni mwa njia zipo zisizo sawa. Na lau angependa (Mola wako mlezi), bila shaka angewaongozeni nyote



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 10

هُوَ ٱلَّذِيٓ أَنزَلَ مِنَ ٱلسَّمَآءِ مَآءٗۖ لَّكُم مِّنۡهُ شَرَابٞ وَمِنۡهُ شَجَرٞ فِيهِ تُسِيمُونَ

Ni yeye ambaye ameteremsha kwa ajili yenu maji (mvua) kutoka mawinguni; baadhi yake mna-kunywa na baadhi yake anaoteshea miti (mnachungia wanyama wenu)



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 11

يُنۢبِتُ لَكُم بِهِ ٱلزَّرۡعَ وَٱلزَّيۡتُونَ وَٱلنَّخِيلَ وَٱلۡأَعۡنَٰبَ وَمِن كُلِّ ٱلثَّمَرَٰتِۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗ لِّقَوۡمٖ يَتَفَكَّرُونَ

Anaotesha kwa ajili yenu kutokana na mvua mimea ya kila aina na mizaituni na mitende na mizabibu na kila matunda. Bila shaka katika hayo kuna ishara (kuhusu uweza wa Allah) kwa watu wenye kufikiri



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 12

وَسَخَّرَ لَكُمُ ٱلَّيۡلَ وَٱلنَّهَارَ وَٱلشَّمۡسَ وَٱلۡقَمَرَۖ وَٱلنُّجُومُ مُسَخَّرَٰتُۢ بِأَمۡرِهِۦٓۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّقَوۡمٖ يَعۡقِلُونَ

Na amewadhalilishia usiku na mchana, na jua na mwezi, na nyota zimetiishwa kwa amri yake. Hakika katika hayo kuna ishara (juu ya uwepo wa Allah) kwa watu wenye akili



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 13

وَمَا ذَرَأَ لَكُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ مُخۡتَلِفًا أَلۡوَٰنُهُۥٓۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗ لِّقَوۡمٖ يَذَّكَّرُونَ

Na vyote alivyowaumbieni katika ardhi vyenye rangi mbalimbali (vinawatiini). Hakika katika hayo kuna ishara (za kuwepo kwa uweza wake) kwa watu wanaokumbuka



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 14

وَهُوَ ٱلَّذِي سَخَّرَ ٱلۡبَحۡرَ لِتَأۡكُلُواْ مِنۡهُ لَحۡمٗا طَرِيّٗا وَتَسۡتَخۡرِجُواْ مِنۡهُ حِلۡيَةٗ تَلۡبَسُونَهَاۖ وَتَرَى ٱلۡفُلۡكَ مَوَاخِرَ فِيهِ وَلِتَبۡتَغُواْ مِن فَضۡلِهِۦ وَلَعَلَّكُمۡ تَشۡكُرُونَ

Na ni Yeye ambaye ameidhalilisha bahari ili (mvue) humo (samaki) mle nyama iliyombichi[1], na mtoe humo (lulu na marijani) mapambo mtakayovaa. Na utaona jahazi zikipasua humo (kuenda na kurudi), na ili mtafute fadhila zake na ili mpate kushukuru


1- - Maana ya mbichi hapa kinyume chake ni ukavu maana yake mle nyama ya samaki walio freshi na sio wabichi bila kupikwa.


Sourate: ANNAHLI 

Verset : 15

وَأَلۡقَىٰ فِي ٱلۡأَرۡضِ رَوَٰسِيَ أَن تَمِيدَ بِكُمۡ وَأَنۡهَٰرٗا وَسُبُلٗا لَّعَلَّكُمۡ تَهۡتَدُونَ

Na akaweka ardhini milima (majabali) madhubuti ili ituliye (isiiname upande mmoja) isiwamwage, na mito na njia ilimpate kuongoka (njia iliyo sawa)



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 16

وَعَلَٰمَٰتٖۚ وَبِٱلنَّجۡمِ هُمۡ يَهۡتَدُونَ

Na (ameweka ardhini) alama, (mnazotumia kujua njia) na kwa nyota wao wanajiongoza



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 17

أَفَمَن يَخۡلُقُ كَمَن لَّا يَخۡلُقُۚ أَفَلَا تَذَكَّرُونَ

Hivi, (mnamfanya) Allah anayeumba kuwa sawa na yule asiyeumba chochote?! Hivi, ham-kumbuki (hilo mkampwekesha)?



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 18

وَإِن تَعُدُّواْ نِعۡمَةَ ٱللَّهِ لَا تُحۡصُوهَآۗ إِنَّ ٱللَّهَ لَغَفُورٞ رَّحِيمٞ

Na kama mkihesabu neema za Allah (kwenu) hamtaweza kuzidhibiti. Hakika Allah ni msamehevu sana mwenye rehema



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 19

وَٱللَّهُ يَعۡلَمُ مَا تُسِرُّونَ وَمَا تُعۡلِنُونَ

Na Allah anayajua zaidi yale mnayoficha na mnayotangaza



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 20

وَٱلَّذِينَ يَدۡعُونَ مِن دُونِ ٱللَّهِ لَا يَخۡلُقُونَ شَيۡـٔٗا وَهُمۡ يُخۡلَقُونَ

Na wale wanaowaomba (Miungu wengine) badala ya Allah (Miungu hiyo) haina uwezo wakuumba chochote, bali wao ndio wameumbwa



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 21

أَمۡوَٰتٌ غَيۡرُ أَحۡيَآءٖۖ وَمَا يَشۡعُرُونَ أَيَّانَ يُبۡعَثُونَ

(Hivyo vyote) ni vitu visivyo na uhai, nahavijui lini Allah atawafufua wanaowaabudu (kisha kuwaingiza Motoni pamoja)



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 22

إِلَٰهُكُمۡ إِلَٰهٞ وَٰحِدٞۚ فَٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ قُلُوبُهُم مُّنكِرَةٞ وَهُم مُّسۡتَكۡبِرُونَ

Mungu wenu ni Mungu mmoja; Basi walewasioiamini Akhera nyoyo zao zinapinga tu ilhali wao wanafanya kiburi (kuikubali haki.)



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 23

لَا جَرَمَ أَنَّ ٱللَّهَ يَعۡلَمُ مَا يُسِرُّونَ وَمَا يُعۡلِنُونَۚ إِنَّهُۥ لَا يُحِبُّ ٱلۡمُسۡتَكۡبِرِينَ

Kweli kabisa kwa hakika Allah anajua wanayoficha na wanayotangaza. Kwa hakika yeye hawapendi wenye kiburi



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 24

وَإِذَا قِيلَ لَهُم مَّاذَآ أَنزَلَ رَبُّكُمۡ قَالُوٓاْ أَسَٰطِيرُ ٱلۡأَوَّلِينَ

Na pindi wanapoulizwa (Washirikina wa Makkah): Hivi nini ameteremsha Mola wenu mlezi (kwa Muhammad)? Wanasema: (Si chochote) ni hadithi tu za (watu) wa kale



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 25

لِيَحۡمِلُوٓاْ أَوۡزَارَهُمۡ كَامِلَةٗ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ وَمِنۡ أَوۡزَارِ ٱلَّذِينَ يُضِلُّونَهُم بِغَيۡرِ عِلۡمٍۗ أَلَا سَآءَ مَا يَزِرُونَ

Ili (mwisho) wabebe madhambi yaokamili Siku ya Kiyama, na sehemu ya madhambi ya wale wanaowapoteza bila ya kujua. Sikilizeni! Ni mabaya sana wanayobeba



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 26

قَدۡ مَكَرَ ٱلَّذِينَ مِن قَبۡلِهِمۡ فَأَتَى ٱللَّهُ بُنۡيَٰنَهُم مِّنَ ٱلۡقَوَاعِدِ فَخَرَّ عَلَيۡهِمُ ٱلسَّقۡفُ مِن فَوۡقِهِمۡ وَأَتَىٰهُمُ ٱلۡعَذَابُ مِنۡ حَيۡثُ لَا يَشۡعُرُونَ

Hakika walifanya vitimbi wale waliokuwa kabla yao, na Allah akawapelekea adhabu kuanzia katika misingi ya nyumba zao, basi dari zikawaangukia juu yao; na ikawafika adhabu bila wao kuhisi



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 27

ثُمَّ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ يُخۡزِيهِمۡ وَيَقُولُ أَيۡنَ شُرَكَآءِيَ ٱلَّذِينَ كُنتُمۡ تُشَـٰٓقُّونَ فِيهِمۡۚ قَالَ ٱلَّذِينَ أُوتُواْ ٱلۡعِلۡمَ إِنَّ ٱلۡخِزۡيَ ٱلۡيَوۡمَ وَٱلسُّوٓءَ عَلَى ٱلۡكَٰفِرِينَ

Kisha Siku ya Kiyama atawa-fedhehesha na atawauliza: Wako wapi washirika wangu ambao kwa ajili yao mlikuwa mkigombana (na Manabii)? Watasema wale waliopewa elimu: Hakika leo fed-heha na ubaya vitawafika makafiri,



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 28

ٱلَّذِينَ تَتَوَفَّىٰهُمُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ ظَالِمِيٓ أَنفُسِهِمۡۖ فَأَلۡقَوُاْ ٱلسَّلَمَ مَا كُنَّا نَعۡمَلُ مِن سُوٓءِۭۚ بَلَىٰٓۚ إِنَّ ٱللَّهَ عَلِيمُۢ بِمَا كُنتُمۡ تَعۡمَلُونَ

Wale ambao Malaika wame-wafisha ilhali wamedhulumu nafsi zao. Nawakajisalimisha kwa Allah (wakisema): hatukuwa tukifanya uovu wowote. Naam, hakika Allah anajua sana mliyokuwa mkiyatenda



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 29

فَٱدۡخُلُوٓاْ أَبۡوَٰبَ جَهَنَّمَ خَٰلِدِينَ فِيهَاۖ فَلَبِئۡسَ مَثۡوَى ٱلۡمُتَكَبِّرِينَ

Basi ingieni katika milango ya Jahannamu mtakaa humo milele. Na niubaya ulioje wamafikio kwa wafanyao kiburi



Sourate: ANNAHLI 

Verset : 30

۞وَقِيلَ لِلَّذِينَ ٱتَّقَوۡاْ مَاذَآ أَنزَلَ رَبُّكُمۡۚ قَالُواْ خَيۡرٗاۗ لِّلَّذِينَ أَحۡسَنُواْ فِي هَٰذِهِ ٱلدُّنۡيَا حَسَنَةٞۚ وَلَدَارُ ٱلۡأٓخِرَةِ خَيۡرٞۚ وَلَنِعۡمَ دَارُ ٱلۡمُتَّقِينَ

Na wakaaulizwa wale waliomcha (Allah): Hivi ni kipi ameteremsha Mola wenu mlezi? Watasema: Ni kheri tupu. Ama wale waliofanya wema katika hii dunia watapata wema, na hakika nyumba ya Akhera ni nzuri zaidi; na hakika ni nyumba bora ya Wacha Mungu