Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 151

قَالَ رَبِّ ٱغۡفِرۡ لِي وَلِأَخِي وَأَدۡخِلۡنَا فِي رَحۡمَتِكَۖ وَأَنتَ أَرۡحَمُ ٱلرَّـٰحِمِينَ

(Musa) Akasema: Ewe Mola wangu, nisamehe mimi na ndugu yangu na tuingize katika rehema zako, na wewe ni Rahimu zaidi ya warahimu (wote)



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 152

إِنَّ ٱلَّذِينَ ٱتَّخَذُواْ ٱلۡعِجۡلَ سَيَنَالُهُمۡ غَضَبٞ مِّن رَّبِّهِمۡ وَذِلَّةٞ فِي ٱلۡحَيَوٰةِ ٱلدُّنۡيَاۚ وَكَذَٰلِكَ نَجۡزِي ٱلۡمُفۡتَرِينَ

Hakika, wale waliomfanya ndama (Mungu) itawapata adhabu ya Mola wao Mlezi na madhila katika maisha ya duniani. Na kama hivyo ndivyo tunavyowalipa wazushi



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 153

وَٱلَّذِينَ عَمِلُواْ ٱلسَّيِّـَٔاتِ ثُمَّ تَابُواْ مِنۢ بَعۡدِهَا وَءَامَنُوٓاْ إِنَّ رَبَّكَ مِنۢ بَعۡدِهَا لَغَفُورٞ رَّحِيمٞ

Na wale waliotenda maovu, kisha wakatubu baada yake na wakaamini, hakika Mola wako baada ya hayo ni Msamehevu sana, Rahimu sana



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 154

وَلَمَّا سَكَتَ عَن مُّوسَى ٱلۡغَضَبُ أَخَذَ ٱلۡأَلۡوَاحَۖ وَفِي نُسۡخَتِهَا هُدٗى وَرَحۡمَةٞ لِّلَّذِينَ هُمۡ لِرَبِّهِمۡ يَرۡهَبُونَ

Na wakati ghadhabu ilipomtulia Musa alizichukua mbao zile na katika maandishi yake kuna muongozo na rehema kwa wanaomuogopa Mola wao



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 155

وَٱخۡتَارَ مُوسَىٰ قَوۡمَهُۥ سَبۡعِينَ رَجُلٗا لِّمِيقَٰتِنَاۖ فَلَمَّآ أَخَذَتۡهُمُ ٱلرَّجۡفَةُ قَالَ رَبِّ لَوۡ شِئۡتَ أَهۡلَكۡتَهُم مِّن قَبۡلُ وَإِيَّـٰيَۖ أَتُهۡلِكُنَا بِمَا فَعَلَ ٱلسُّفَهَآءُ مِنَّآۖ إِنۡ هِيَ إِلَّا فِتۡنَتُكَ تُضِلُّ بِهَا مَن تَشَآءُ وَتَهۡدِي مَن تَشَآءُۖ أَنتَ وَلِيُّنَا فَٱغۡفِرۡ لَنَا وَٱرۡحَمۡنَاۖ وَأَنتَ خَيۡرُ ٱلۡغَٰفِرِينَ

Na Musa aliteua katika watu wake wanaume sabini kwa ajili ya miadi yetu. Basi lilipowachukua tetemeko (la ardhi) alisema: Ewe Mola wangu Mlezi, lau kama ulitaka (kuwaangamiza) si ungewaangamiza wao na mimi kabla (ya leo)?[1] Hivi unatuangamiza kwa (sababu ya) waliyofanya wapuuzi miongoni mwetu? Haya si chochote isipokuwa tu ni mtihani wako. Kwa mtihani huo unamuacha umtakaye apotee na unamuongoza umtakaye. Wewe ndiye mwandani wetu. Basi tusamehe na turehemu, na wewe ni bora zaidi ya wenye kusamehe makosa


1- - Nabii Musa aliwachagua wanaume sabini katika watu bora miongoni mwa watu wake kwa ajili ya miadi na Mola wao. Walipofika katika eneo ambalo Musa aliahidiwa na Mola wake, wale watu sabini walimwambia Musa kuwa: Hatutakuamini wewe Musa hadi tumuone Allah bayana. Si unadai umeongea naye, basi tuoneshe sasa? likawakumba tetemeko la ardhi na kuwaangamiza. Nabii Musa alipozinduka akawa anamwambia Mola wake kuwa, atakwenda kusema nini akirudi kwa watu wake kwa kuwashirikisha viongozi wao bora? Ingekuwa vyema, kwa maoni yake, kwamba wangeangamizwa pale mwanzo walipoabudu ndama.


Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 156

۞وَٱكۡتُبۡ لَنَا فِي هَٰذِهِ ٱلدُّنۡيَا حَسَنَةٗ وَفِي ٱلۡأٓخِرَةِ إِنَّا هُدۡنَآ إِلَيۡكَۚ قَالَ عَذَابِيٓ أُصِيبُ بِهِۦ مَنۡ أَشَآءُۖ وَرَحۡمَتِي وَسِعَتۡ كُلَّ شَيۡءٖۚ فَسَأَكۡتُبُهَا لِلَّذِينَ يَتَّقُونَ وَيُؤۡتُونَ ٱلزَّكَوٰةَ وَٱلَّذِينَ هُم بِـَٔايَٰتِنَا يُؤۡمِنُونَ

Na tuandikie mazuri katika hii dunia na akhera (pia tuandikie mazuri). Hakika, sisi tumerejea kwako. (Allah) Akasema: Adhabu yangu ninamlenga nimtakaye, na rehema yangu imekienea kila kitu. Basi nitaiandika (hiyo rehema yangu) kwa ambao wanamcha Allah na wanaotoa Zaka na (kwa) wale ambao Aya zetu wanaziamini



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 157

ٱلَّذِينَ يَتَّبِعُونَ ٱلرَّسُولَ ٱلنَّبِيَّ ٱلۡأُمِّيَّ ٱلَّذِي يَجِدُونَهُۥ مَكۡتُوبًا عِندَهُمۡ فِي ٱلتَّوۡرَىٰةِ وَٱلۡإِنجِيلِ يَأۡمُرُهُم بِٱلۡمَعۡرُوفِ وَيَنۡهَىٰهُمۡ عَنِ ٱلۡمُنكَرِ وَيُحِلُّ لَهُمُ ٱلطَّيِّبَٰتِ وَيُحَرِّمُ عَلَيۡهِمُ ٱلۡخَبَـٰٓئِثَ وَيَضَعُ عَنۡهُمۡ إِصۡرَهُمۡ وَٱلۡأَغۡلَٰلَ ٱلَّتِي كَانَتۡ عَلَيۡهِمۡۚ فَٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ بِهِۦ وَعَزَّرُوهُ وَنَصَرُوهُ وَٱتَّبَعُواْ ٱلنُّورَ ٱلَّذِيٓ أُنزِلَ مَعَهُۥٓ أُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡمُفۡلِحُونَ

Ambao wanamfuata Mtume, Nabii, hasomi kilichoandikwa, ambaye kwao wanamkuta amean-dikwa katika Taurati na Injili, anawaamrisha mema na anawakataza maovu, na anawahalalishia vilivyo vizuri, na anawaharamishia vilivyo vibaya, na anawaondoshea mazito yao (sheria zao ngumu) na makongwa (minyororo ya dhambi) waliyokuwa nayo. Basi wale waliomuamini (Mtume huyo) na wakamheshimu na wakamsaidia na wakaifuata nuru aliyoteremshiwa, hao tu ndio waliofanikiwa



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 158

قُلۡ يَـٰٓأَيُّهَا ٱلنَّاسُ إِنِّي رَسُولُ ٱللَّهِ إِلَيۡكُمۡ جَمِيعًا ٱلَّذِي لَهُۥ مُلۡكُ ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضِۖ لَآ إِلَٰهَ إِلَّا هُوَ يُحۡيِۦ وَيُمِيتُۖ فَـَٔامِنُواْ بِٱللَّهِ وَرَسُولِهِ ٱلنَّبِيِّ ٱلۡأُمِّيِّ ٱلَّذِي يُؤۡمِنُ بِٱللَّهِ وَكَلِمَٰتِهِۦ وَٱتَّبِعُوهُ لَعَلَّكُمۡ تَهۡتَدُونَ

Sema: Enyi watu, hakika mimi ni Mtume wa Allah kwenu nyote[1]. (Allah) Ambaye ni wake pekee ufalme wa mbinguni na ardhini. Hapana mwenye haki ya kuabudiwa isipokuwa yeye tu. Anahuisha na anafisha. Basi muaminini Allah na Mtume wake, Nabii ambaye hasomi kilichoandikwa, ambaye anamuamini Allah na maneno yake, na mfuateni ili mpate kuongoka


1- - Aya hii ni tangazo rasmi kwamba, Uislamu ni dini ya ulimwengu wote na sio ya taifa fulani, kabila fulani au jamii fulani.


Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 159

وَمِن قَوۡمِ مُوسَىٰٓ أُمَّةٞ يَهۡدُونَ بِٱلۡحَقِّ وَبِهِۦ يَعۡدِلُونَ

Na katika watu wa Musa kuna kundi linalo ongoza kwa haki, na kwa haki hiyo wanafanya uadilifu



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 160

وَقَطَّعۡنَٰهُمُ ٱثۡنَتَيۡ عَشۡرَةَ أَسۡبَاطًا أُمَمٗاۚ وَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ إِذِ ٱسۡتَسۡقَىٰهُ قَوۡمُهُۥٓ أَنِ ٱضۡرِب بِّعَصَاكَ ٱلۡحَجَرَۖ فَٱنۢبَجَسَتۡ مِنۡهُ ٱثۡنَتَا عَشۡرَةَ عَيۡنٗاۖ قَدۡ عَلِمَ كُلُّ أُنَاسٖ مَّشۡرَبَهُمۡۚ وَظَلَّلۡنَا عَلَيۡهِمُ ٱلۡغَمَٰمَ وَأَنزَلۡنَا عَلَيۡهِمُ ٱلۡمَنَّ وَٱلسَّلۡوَىٰۖ كُلُواْ مِن طَيِّبَٰتِ مَا رَزَقۡنَٰكُمۡۚ وَمَا ظَلَمُونَا وَلَٰكِن كَانُوٓاْ أَنفُسَهُمۡ يَظۡلِمُونَ

Na tuliwakata kata (tuliwagawa makundi makundi) katika koo na mataifa kumi na mbili. Na tulimpa Musa Wahyi wakati watu wake walipomuomba maji (kwamba): Piga jiwe kwa fimbo yako, basi zikapasuka kutoka jiwe lile chemchem kumi na mbili. Kila watu walijua mahali pao pa (kupata huduma ya maji ya) kunywa. Na tuliwafunika kivuli cha mawingu na tukawateremshia Mana na Salwa (na tukawaambia): Kuleni katika vizuri vya vile tulivyokuruzukuni. Na hawakutudhulumu, na lakini walikuwa wanajidhulumu wao wenyewe



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 161

وَإِذۡ قِيلَ لَهُمُ ٱسۡكُنُواْ هَٰذِهِ ٱلۡقَرۡيَةَ وَكُلُواْ مِنۡهَا حَيۡثُ شِئۡتُمۡ وَقُولُواْ حِطَّةٞ وَٱدۡخُلُواْ ٱلۡبَابَ سُجَّدٗا نَّغۡفِرۡ لَكُمۡ خَطِيٓـَٰٔتِكُمۡۚ سَنَزِيدُ ٱلۡمُحۡسِنِينَ

Na (kumbuka) walipoambiwa: Kaeni katika mji huu na kuleni humo mpendavyo na semeni: “(Ewe Allah) Tufutie dhambi”, na ingieni katika lango (la mji huo) mkiwa wenye kusujudu (mkiwa wanyenyekevu). (Mkifanya hivyo), Tutakusameheni makosa yenu. Tutawazidishia wafanyao mazuri



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 162

فَبَدَّلَ ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ مِنۡهُمۡ قَوۡلًا غَيۡرَ ٱلَّذِي قِيلَ لَهُمۡ فَأَرۡسَلۡنَا عَلَيۡهِمۡ رِجۡزٗا مِّنَ ٱلسَّمَآءِ بِمَا كَانُواْ يَظۡلِمُونَ

Basi wale waliodhulumu miongoni mwao walibadili kauli isiyokuwa ile waliyoambiwa. Basi tukawapelekea adhabu kutoka mbinguni kwa sababu ya walivyokuwa wanadhulumu (nafsi zao)



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 163

وَسۡـَٔلۡهُمۡ عَنِ ٱلۡقَرۡيَةِ ٱلَّتِي كَانَتۡ حَاضِرَةَ ٱلۡبَحۡرِ إِذۡ يَعۡدُونَ فِي ٱلسَّبۡتِ إِذۡ تَأۡتِيهِمۡ حِيتَانُهُمۡ يَوۡمَ سَبۡتِهِمۡ شُرَّعٗا وَيَوۡمَ لَا يَسۡبِتُونَ لَا تَأۡتِيهِمۡۚ كَذَٰلِكَ نَبۡلُوهُم بِمَا كَانُواْ يَفۡسُقُونَ

Na waulize kuhusu mji uliokuwepo kando ya bahari walipokiuka (heshima ya siku ya) Jumamosi wakati samaki wao walipokuwa wanawajia nje nje siku yao ya mapumziko, na siku wasiyopumzika (samaki) hawawajii. Kama hivyo tunawajaribu (tunawapa mtihani) kwa vile walivyokuwa wakifanya uasi



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 164

وَإِذۡ قَالَتۡ أُمَّةٞ مِّنۡهُمۡ لِمَ تَعِظُونَ قَوۡمًا ٱللَّهُ مُهۡلِكُهُمۡ أَوۡ مُعَذِّبُهُمۡ عَذَابٗا شَدِيدٗاۖ قَالُواْ مَعۡذِرَةً إِلَىٰ رَبِّكُمۡ وَلَعَلَّهُمۡ يَتَّقُونَ

Na (kumbuka) wakati kundi miongoni mwao liliposema (kwamba): Kwa nini mnawapa mawaidha watu ambao Allah ni Mwenye kuwaangamiza au kuwaadhibu adhabu kali? Walisema: (Tunawapa mawaidha) Ili uwe udhuru kwa Mola wenu na huwenda nao wakawa wachaMungu



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 165

فَلَمَّا نَسُواْ مَا ذُكِّرُواْ بِهِۦٓ أَنجَيۡنَا ٱلَّذِينَ يَنۡهَوۡنَ عَنِ ٱلسُّوٓءِ وَأَخَذۡنَا ٱلَّذِينَ ظَلَمُواْ بِعَذَابِۭ بَـِٔيسِۭ بِمَا كَانُواْ يَفۡسُقُونَ

Basi walipoyasahau yale waliyokumbushwa tuliwaokoa waliokuwa wanakataza maovu na tuliwachukulia hatua ambao wamedhulumu (nafsi zao kwa kuasi) kwa (kuwapa) adhabu mbaya kwa walivyokuwa wanafanya uasi



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 166

فَلَمَّا عَتَوۡاْ عَن مَّا نُهُواْ عَنۡهُ قُلۡنَا لَهُمۡ كُونُواْ قِرَدَةً خَٰسِـِٔينَ

Basi walipoyapuuza yale waliyokatazwa tuliwaambia: Kuweni manyani dhalili



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 167

وَإِذۡ تَأَذَّنَ رَبُّكَ لَيَبۡعَثَنَّ عَلَيۡهِمۡ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِ مَن يَسُومُهُمۡ سُوٓءَ ٱلۡعَذَابِۗ إِنَّ رَبَّكَ لَسَرِيعُ ٱلۡعِقَابِ وَإِنَّهُۥ لَغَفُورٞ رَّحِيمٞ

Na (kumbuka) wakati Mola wako alipotangaza kuwa: Kwa hakika kabisa, atawapelekea watakaowaonjesha adhabu mbaya kabisa mpaka Siku ya Kiyama. Hakika kabisa, Mola wako ni Mwepesi mno wa kuadhibu na pia yeye ni Mwingi wa kusamehe, Rahimu sana



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 168

وَقَطَّعۡنَٰهُمۡ فِي ٱلۡأَرۡضِ أُمَمٗاۖ مِّنۡهُمُ ٱلصَّـٰلِحُونَ وَمِنۡهُمۡ دُونَ ذَٰلِكَۖ وَبَلَوۡنَٰهُم بِٱلۡحَسَنَٰتِ وَٱلسَّيِّـَٔاتِ لَعَلَّهُمۡ يَرۡجِعُونَ

Na tuliwakata kata mataifa mbali mbali duniani (tuliwafanya wafarakane makundi makundi). Miongoni mwao wapo walio wema na miongoni mwao wapo kinyume na hivyo. Na tuliwajaribu kwa (mambo) mazuri na mabaya ili wapate kurejea (kwa Mola wao)



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 169

فَخَلَفَ مِنۢ بَعۡدِهِمۡ خَلۡفٞ وَرِثُواْ ٱلۡكِتَٰبَ يَأۡخُذُونَ عَرَضَ هَٰذَا ٱلۡأَدۡنَىٰ وَيَقُولُونَ سَيُغۡفَرُ لَنَا وَإِن يَأۡتِهِمۡ عَرَضٞ مِّثۡلُهُۥ يَأۡخُذُوهُۚ أَلَمۡ يُؤۡخَذۡ عَلَيۡهِم مِّيثَٰقُ ٱلۡكِتَٰبِ أَن لَّا يَقُولُواْ عَلَى ٱللَّهِ إِلَّا ٱلۡحَقَّ وَدَرَسُواْ مَا فِيهِۗ وَٱلدَّارُ ٱلۡأٓخِرَةُ خَيۡرٞ لِّلَّذِينَ يَتَّقُونَۚ أَفَلَا تَعۡقِلُونَ

Basi kikafuatia baada yao kizazi kibaya kilichorithi kitabu (Taurati); wanashika anasa za haya maisha duni sana (ya duniani), na huku wanasema: Tutasamehewa (tu, acha tule maisha). Na ikiwajia tena anasa kama hiyo wanaichukua. Hivi haikuchukuliwa kwao ahadi nzito ya kitabu kwamba, wasimsemee Allah isipokuwa haki tu na ilhali wamesoma yaliyomo kwenye kitabu hicho? Na nyumba ya Akhera ni bora kwa wanaomcha Allah. Hivi hamtumii akili?



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 170

وَٱلَّذِينَ يُمَسِّكُونَ بِٱلۡكِتَٰبِ وَأَقَامُواْ ٱلصَّلَوٰةَ إِنَّا لَا نُضِيعُ أَجۡرَ ٱلۡمُصۡلِحِينَ

Na ambao wanakishika vilivyo kitabu (bila ya kukipuuza au kukifanyia mzaha) na wakadumisha Swala, hakika sisi hatupotezi ujira wa watengenezao (mambo ya kumridhisha Allah)



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 171

۞وَإِذۡ نَتَقۡنَا ٱلۡجَبَلَ فَوۡقَهُمۡ كَأَنَّهُۥ ظُلَّةٞ وَظَنُّوٓاْ أَنَّهُۥ وَاقِعُۢ بِهِمۡ خُذُواْ مَآ ءَاتَيۡنَٰكُم بِقُوَّةٖ وَٱذۡكُرُواْ مَا فِيهِ لَعَلَّكُمۡ تَتَّقُونَ

Na (kumbuka) wakati tulipou-nyanyua mlima juu yao ukawa kama kiwingu na wakadhani kuwa utawaangukia (na kuwaambia): Chukueni kwa nguvu yale tuliyo-kupeni, na yakumbukeni yaliomo ndani yake ili muwe wacha Mungu



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 172

وَإِذۡ أَخَذَ رَبُّكَ مِنۢ بَنِيٓ ءَادَمَ مِن ظُهُورِهِمۡ ذُرِّيَّتَهُمۡ وَأَشۡهَدَهُمۡ عَلَىٰٓ أَنفُسِهِمۡ أَلَسۡتُ بِرَبِّكُمۡۖ قَالُواْ بَلَىٰ شَهِدۡنَآۚ أَن تَقُولُواْ يَوۡمَ ٱلۡقِيَٰمَةِ إِنَّا كُنَّا عَنۡ هَٰذَا غَٰفِلِينَ

Na (kumbuka) wakati Mola wako alipochukua kwa wanadamu kizazi chao kutokea migongoni mwao na akawashuhudisha wen-yewe (kwa kuwauliza kwamba): Hivi mimi sio Mola wenu Mlezi? Wakasema: “Kwa nini (isiwe hivyo? Tumeshuhudia (kuwa wewe ni Mola wetu Mlezi”. (Tumefanya hivyo) Ili msije kusema Siku ya Kiyama kuwa: Sisi tulikuwa tumeghafilika na haya (tulikuwa hatuyajui)



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 173

أَوۡ تَقُولُوٓاْ إِنَّمَآ أَشۡرَكَ ءَابَآؤُنَا مِن قَبۡلُ وَكُنَّا ذُرِّيَّةٗ مِّنۢ بَعۡدِهِمۡۖ أَفَتُهۡلِكُنَا بِمَا فَعَلَ ٱلۡمُبۡطِلُونَ

Au (msije) mkasema: Hali ilivyo ni kwamba, baba zetu ndio waliofanya ushirikina kabla yetu, na sisi tulikuwa kizazi tu baada yao. Hivi basi unatuangamiza kwa sababu ya waliyoyafanya waharibifu?



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 174

وَكَذَٰلِكَ نُفَصِّلُ ٱلۡأٓيَٰتِ وَلَعَلَّهُمۡ يَرۡجِعُونَ

Na hivyo tunazifafanua Aya na huwenda watarejea (kwa Mola wao)



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 175

وَٱتۡلُ عَلَيۡهِمۡ نَبَأَ ٱلَّذِيٓ ءَاتَيۡنَٰهُ ءَايَٰتِنَا فَٱنسَلَخَ مِنۡهَا فَأَتۡبَعَهُ ٱلشَّيۡطَٰنُ فَكَانَ مِنَ ٱلۡغَاوِينَ

Na wasomee habari kubwa ya yule ambaye tulimpa Aya zetu na akajivua nazo (akazipuuza) na shetani akamfuatilia akawa miongoni mwa wapotevu



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 176

وَلَوۡ شِئۡنَا لَرَفَعۡنَٰهُ بِهَا وَلَٰكِنَّهُۥٓ أَخۡلَدَ إِلَى ٱلۡأَرۡضِ وَٱتَّبَعَ هَوَىٰهُۚ فَمَثَلُهُۥ كَمَثَلِ ٱلۡكَلۡبِ إِن تَحۡمِلۡ عَلَيۡهِ يَلۡهَثۡ أَوۡ تَتۡرُكۡهُ يَلۡهَثۚ ذَّـٰلِكَ مَثَلُ ٱلۡقَوۡمِ ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَاۚ فَٱقۡصُصِ ٱلۡقَصَصَ لَعَلَّهُمۡ يَتَفَكَّرُونَ

Na kwa hakika kabisa, lau kama tungetaka tungempandisha (daraja la juu kabisa) kwa Aya hizo, lakini yeye aliing’ang’ania dunia na akafuata utashi wa nafsi yake. Basi mfano wake ni kama mfano wa mbwa; ukimkurupusha anatoa ulimi kwa kuhema na ukimuacha anatoa ulimi kwa kuhema. Huo ni mfano wa watu waliozikadhibisha Aya zetu. Basi hadithia visa hivi ili (watu) watafakari



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 177

سَآءَ مَثَلًا ٱلۡقَوۡمُ ٱلَّذِينَ كَذَّبُواْ بِـَٔايَٰتِنَا وَأَنفُسَهُمۡ كَانُواْ يَظۡلِمُونَ

(Huo) Ni mfano mbaya kabisa (wa) watu waliokadhibisha Aya zetu na nafsi zao wakawa wanazidhulumu (kwa kutoamini)



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 178

مَن يَهۡدِ ٱللَّهُ فَهُوَ ٱلۡمُهۡتَدِيۖ وَمَن يُضۡلِلۡ فَأُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡخَٰسِرُونَ

Yeyote ambaye Allah amemuongoza, basi huyo tu ndiye aliyeongoka, na wale ambao amewaacha wapotee basi hao tu ndio waliopata hasara



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 179

وَلَقَدۡ ذَرَأۡنَا لِجَهَنَّمَ كَثِيرٗا مِّنَ ٱلۡجِنِّ وَٱلۡإِنسِۖ لَهُمۡ قُلُوبٞ لَّا يَفۡقَهُونَ بِهَا وَلَهُمۡ أَعۡيُنٞ لَّا يُبۡصِرُونَ بِهَا وَلَهُمۡ ءَاذَانٞ لَّا يَسۡمَعُونَ بِهَآۚ أُوْلَـٰٓئِكَ كَٱلۡأَنۡعَٰمِ بَلۡ هُمۡ أَضَلُّۚ أُوْلَـٰٓئِكَ هُمُ ٱلۡغَٰفِلُونَ

Na kwa hakika kabisa, tum-eiumbia Jahanamu majini na watu wengi. Wana nyoyo lakini hawafahamu kwa nyoyo hizo, na wana macho lakini hawaoni kwa macho hayo, na wana masikio lakini hawasikii kwa masikio hayo. Hao ni kama wanyama wafugwao, bali wao ni wapotevu zaidi (kuliko mifugo). Hao ndio hasa walioghafilika



Sourate: AL-AARAAF 

Verset : 180

وَلِلَّهِ ٱلۡأَسۡمَآءُ ٱلۡحُسۡنَىٰ فَٱدۡعُوهُ بِهَاۖ وَذَرُواْ ٱلَّذِينَ يُلۡحِدُونَ فِيٓ أَسۡمَـٰٓئِهِۦۚ سَيُجۡزَوۡنَ مَا كَانُواْ يَعۡمَلُونَ

Na Allah ana majina mazuri kabisa, basi muombeni kwa majina hayo. Na waacheni wale wanaoya-potosha majina yake; watalipwa yale waliyokuwa wakiyatenda