Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 61

عَلَىٰٓ أَن نُّبَدِّلَ أَمۡثَٰلَكُمۡ وَنُنشِئَكُمۡ فِي مَا لَا تَعۡلَمُونَ

Kwamba Tuwabadilishe wengine mfano wenu, na Tukuumbeni katika umbo msilolijua



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 62

وَلَقَدۡ عَلِمۡتُمُ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأُولَىٰ فَلَوۡلَا تَذَكَّرُونَ

Na bila shaka mmejua umbo la kwanza, basi kwanini hamkumbuki?



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 63

أَفَرَءَيۡتُم مَّا تَحۡرُثُونَ

Je, mnaona mbegu mnazo-zipanda?



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 64

ءَأَنتُمۡ تَزۡرَعُونَهُۥٓ أَمۡ نَحۡنُ ٱلزَّـٰرِعُونَ

Je, ni nyinyi ndio mnaziotesha, au Sisi ndio Wenye kuotesha mimea?



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 65

لَوۡ نَشَآءُ لَجَعَلۡنَٰهُ حُطَٰمٗا فَظَلۡتُمۡ تَفَكَّهُونَ

Lau Tungelitaka, Tungelifanya mabua yaliyonyauka na mkabaki mnashangaa na kusikitika



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 66

إِنَّا لَمُغۡرَمُونَ

(Mkisema): Hakika sisi tumegharimika



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 67

بَلۡ نَحۡنُ مَحۡرُومُونَ

Bali sisi tumenyimwa



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 68

أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلۡمَآءَ ٱلَّذِي تَشۡرَبُونَ

Je, mnaona maji ambayo mnakunywa?



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 69

ءَأَنتُمۡ أَنزَلۡتُمُوهُ مِنَ ٱلۡمُزۡنِ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنزِلُونَ

Je, ni nyinyi ndio mliyoyateremsha kutoka katika mawingu ya mvua au Sisi ndio Wateremshaji?



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 70

لَوۡ نَشَآءُ جَعَلۡنَٰهُ أُجَاجٗا فَلَوۡلَا تَشۡكُرُونَ

Lau Tungelitaka, Tungeliyafanya ya chumvi kali chungu basi kwa nini hamshukuru?



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 71

أَفَرَءَيۡتُمُ ٱلنَّارَ ٱلَّتِي تُورُونَ

Je, mnaona moto ambao mnauwasha?



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 72

ءَأَنتُمۡ أَنشَأۡتُمۡ شَجَرَتَهَآ أَمۡ نَحۡنُ ٱلۡمُنشِـُٔونَ

Je, ni nyinyi ndio mliouumba mti wake, au Sisi ndio Waumbaji wa mti huo?



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 73

نَحۡنُ جَعَلۡنَٰهَا تَذۡكِرَةٗ وَمَتَٰعٗا لِّلۡمُقۡوِينَ

Sisi Tumeufanya kuwa ni ukumbusho na manufaa kwa wasafiri



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 74

فَسَبِّحۡ بِٱسۡمِ رَبِّكَ ٱلۡعَظِيمِ

Basi litakase jina la Mola wako aliyetukuka



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 75

۞فَلَآ أُقۡسِمُ بِمَوَٰقِعِ ٱلنُّجُومِ

Basi Naapa kwa maangukio ya nyota



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 76

وَإِنَّهُۥ لَقَسَمٞ لَّوۡ تَعۡلَمُونَ عَظِيمٌ

Hakika hicho ni kiapo kikubwa lau mnaelewa



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 77

إِنَّهُۥ لَقُرۡءَانٞ كَرِيمٞ

Hakika ya hiyo ni Kurani tukufu



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 78

فِي كِتَٰبٖ مَّكۡنُونٖ

Katika Kitabu kilichohifadhiwa



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 79

لَّا يَمَسُّهُۥٓ إِلَّا ٱلۡمُطَهَّرُونَ

Haigusi isipokuwa waliotakaswa kabisa (Walio twahara)



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 80

تَنزِيلٞ مِّن رَّبِّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Ni uteremsho kutoka kwa Mola wa walimwengu wote



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 81

أَفَبِهَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ أَنتُم مُّدۡهِنُونَ

Hivi kwa maneno haya nyinyi mnapuuza na kuikanusha?



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 82

وَتَجۡعَلُونَ رِزۡقَكُمۡ أَنَّكُمۡ تُكَذِّبُونَ

Na mnafanya (badala ya kushu-kuru) kwa riziki mnayopata, nyinyi ndio mnakad hibisha



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 83

فَلَوۡلَآ إِذَا بَلَغَتِ ٱلۡحُلۡقُومَ

Itakuaje basi pale roho itaka-pofika kwenye koo



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 84

وَأَنتُمۡ حِينَئِذٖ تَنظُرُونَ

Na nyinyi wakati huo mnatazama tu



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 85

وَنَحۡنُ أَقۡرَبُ إِلَيۡهِ مِنكُمۡ وَلَٰكِن لَّا تُبۡصِرُونَ

Nasi Tuko karibu naye zaidi kuliko nyinyi, lakini nyinyi hamuoni



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 86

فَلَوۡلَآ إِن كُنتُمۡ غَيۡرَ مَدِينِينَ

Na lau kuwa nyinyi hammo katika mamlaka yangu.[1]


1- - Basi kama lau kusingekua na kufufuliwa.


Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 87

تَرۡجِعُونَهَآ إِن كُنتُمۡ صَٰدِقِينَ

Kwanini hamuirudishi hiyo roho (mwilini mwake), mkiwa ni wakweli?



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 88

فَأَمَّآ إِن كَانَ مِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ

Basi akiwa (mwenye roho hiyo) ni miongoni mwa waliokurubishwa



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 89

فَرَوۡحٞ وَرَيۡحَانٞ وَجَنَّتُ نَعِيمٖ

Basi ni raha, na manukato, na mabustani zenye kila aina ya neema



Sourate: AL-WAAQIA’H 

Verset : 90

وَأَمَّآ إِن كَانَ مِنۡ أَصۡحَٰبِ ٱلۡيَمِينِ

Ama ikiwa mwenye roho hiyo ni miongoni mwa watu wa kuliani