Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 61

فَلَمَّا تَرَـٰٓءَا ٱلۡجَمۡعَانِ قَالَ أَصۡحَٰبُ مُوسَىٰٓ إِنَّا لَمُدۡرَكُونَ

Na yalipoonana majeshi mawili haya, watu wa Mussa wakasema: Hakika sisi bila ya shaka tumepatikana!



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 62

قَالَ كَلَّآۖ إِنَّ مَعِيَ رَبِّي سَيَهۡدِينِ

(Mussa) akasema: Hasha! Hakika yu pamoja nami Mola wangu Mlezi. Yeye ataniongoa!



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 63

فَأَوۡحَيۡنَآ إِلَىٰ مُوسَىٰٓ أَنِ ٱضۡرِب بِّعَصَاكَ ٱلۡبَحۡرَۖ فَٱنفَلَقَ فَكَانَ كُلُّ فِرۡقٖ كَٱلطَّوۡدِ ٱلۡعَظِيمِ

Tulimletea wahyi Mussa tuka-mwambia: Piga bahari kwa fimbo yako. Basi ikatengana, na kila sehemu ikawa kama mlima mkubwa



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 64

وَأَزۡلَفۡنَا ثَمَّ ٱلۡأٓخَرِينَ

Na tukawajongeza hapo wale wengine



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 65

وَأَنجَيۡنَا مُوسَىٰ وَمَن مَّعَهُۥٓ أَجۡمَعِينَ

Tukawaokoa Musa na walio kuwa pamoja naye wote



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 66

ثُمَّ أَغۡرَقۡنَا ٱلۡأٓخَرِينَ

Kisha tukawazamisha hao wengine



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 67

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗۖ وَمَا كَانَ أَكۡثَرُهُم مُّؤۡمِنِينَ

Hakika bila ya shaka katika hayo ipo Ishara; lakini wengi wao si katika wenye kuamini



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 68

وَإِنَّ رَبَّكَ لَهُوَ ٱلۡعَزِيزُ ٱلرَّحِيمُ

Na kwa hakika Mola wako Mlezi ndiye Mwenye nguvu Mwenye kurehemu



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 69

وَٱتۡلُ عَلَيۡهِمۡ نَبَأَ إِبۡرَٰهِيمَ

Na wasomee khabari za Ibrahim



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 70

إِذۡ قَالَ لِأَبِيهِ وَقَوۡمِهِۦ مَا تَعۡبُدُونَ

Alipo mwambia baba yake na kaumu yake: Mnaabudu nini?



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 71

قَالُواْ نَعۡبُدُ أَصۡنَامٗا فَنَظَلُّ لَهَا عَٰكِفِينَ

Wakasema: Tunaabudu masa-namu, daima tunayanyenyekea



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 72

قَالَ هَلۡ يَسۡمَعُونَكُمۡ إِذۡ تَدۡعُونَ

Akasema: Je! Yanakusikieni mnapo yaita?



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 73

أَوۡ يَنفَعُونَكُمۡ أَوۡ يَضُرُّونَ

Au yanakufaeni, au yanaku-dhuruni?



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 74

قَالُواْ بَلۡ وَجَدۡنَآ ءَابَآءَنَا كَذَٰلِكَ يَفۡعَلُونَ

Wakasema: Bali tumewakuta baba zetu wakifanya hivyo hivyo



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 75

قَالَ أَفَرَءَيۡتُم مَّا كُنتُمۡ تَعۡبُدُونَ

Je! Mmewaona hawa mnao waabudu-



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 76

أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُمُ ٱلۡأَقۡدَمُونَ

Nyinyi na baba zenu wa zamani?



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 77

فَإِنَّهُمۡ عَدُوّٞ لِّيٓ إِلَّا رَبَّ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Kwani hakika hao ni adui zangu, isipokuwa Mola Mlezi wa walimwengu wote



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 78

ٱلَّذِي خَلَقَنِي فَهُوَ يَهۡدِينِ

Ambaye ndiye aliyeniumba, na Yeye ndiye ananiongoa



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 79

وَٱلَّذِي هُوَ يُطۡعِمُنِي وَيَسۡقِينِ

Na ambaye ndiye ananilisha na kuninywesha



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 80

وَإِذَا مَرِضۡتُ فَهُوَ يَشۡفِينِ

Na ninapo ugua ni Yeye ndiye anaye niponesha



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 81

وَٱلَّذِي يُمِيتُنِي ثُمَّ يُحۡيِينِ

Na ambaye atanifisha, na kisha atanihuisha



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 82

وَٱلَّذِيٓ أَطۡمَعُ أَن يَغۡفِرَ لِي خَطِيٓـَٔتِي يَوۡمَ ٱلدِّينِ

Na ambaye ndiye ninaye mtumai kunisamehe makosa yangu Siku ya Malipo



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 83

رَبِّ هَبۡ لِي حُكۡمٗا وَأَلۡحِقۡنِي بِٱلصَّـٰلِحِينَ

Mola wangu Mlezi! Nitunukie hukumu na uniunganishe na watendao mema



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 84

وَٱجۡعَل لِّي لِسَانَ صِدۡقٖ فِي ٱلۡأٓخِرِينَ

Na unijaalie nitajwe kwa wema na watu watakao kuja baadaye



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 85

وَٱجۡعَلۡنِي مِن وَرَثَةِ جَنَّةِ ٱلنَّعِيمِ

Na unijaalie katika warithi wa Bustani za neema



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 86

وَٱغۡفِرۡ لِأَبِيٓ إِنَّهُۥ كَانَ مِنَ ٱلضَّآلِّينَ

Na umsamehe baba yangu, kwani hakika alikuwa miongoni mwa wapotovu



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 87

وَلَا تُخۡزِنِي يَوۡمَ يُبۡعَثُونَ

Wala usinihizi (usinifedheheshe) Siku watapo fufuliwa



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 88

يَوۡمَ لَا يَنفَعُ مَالٞ وَلَا بَنُونَ

Siku ambayo kwamba mali hayatofaa kitu wala watoto



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 89

إِلَّا مَنۡ أَتَى ٱللَّهَ بِقَلۡبٖ سَلِيمٖ

Isipokuwa mwenye kumjia Allah na moyo safi



Sourate: ASH-SHUARAA 

Verset : 90

وَأُزۡلِفَتِ ٱلۡجَنَّةُ لِلۡمُتَّقِينَ

Na Pepo itasogezwa kwa wacha-mungu