Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 61

فَلَمَّا جَآءَ ءَالَ لُوطٍ ٱلۡمُرۡسَلُونَ

Basi wale wajumbe (waliotumwa) walipofika kwa Lutwi



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 62

قَالَ إِنَّكُمۡ قَوۡمٞ مُّنكَرُونَ

(Lutwi) Alisema: Hakika nyinyi ni watu msiojulikana (hapa kwetu)



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 63

قَالُواْ بَلۡ جِئۡنَٰكَ بِمَا كَانُواْ فِيهِ يَمۡتَرُونَ

(Malaika) Walisema: Bali sisi tumekuletea (adhabu ya) yale waliyokuwa wakiyatilia shaka



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 64

وَأَتَيۡنَٰكَ بِٱلۡحَقِّ وَإِنَّا لَصَٰدِقُونَ

Na tumefika kwako kwa Haki, na hakika sisi tunasema kweli



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 65

فَأَسۡرِ بِأَهۡلِكَ بِقِطۡعٖ مِّنَ ٱلَّيۡلِ وَٱتَّبِعۡ أَدۡبَٰرَهُمۡ وَلَا يَلۡتَفِتۡ مِنكُمۡ أَحَدٞ وَٱمۡضُواْ حَيۡثُ تُؤۡمَرُونَ

Basi ondoka na ahli zako kwenye sehemu ya usiku, nawe ufuate nyuma yao (huku ukiwahimiza ili waharakishe kuondoka), wala yeyote kati yenu asigeuke nyuma. Na mwende mlikoamrishwa



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 66

وَقَضَيۡنَآ إِلَيۡهِ ذَٰلِكَ ٱلۡأَمۡرَ أَنَّ دَابِرَ هَـٰٓؤُلَآءِ مَقۡطُوعٞ مُّصۡبِحِينَ

Na tukamfunulia Lutwi wahyi huo kwamba, mwisho wa watu hawa ikifika (mapambazuko ya) asubuhi watakuwa wameshakatiliwa mbali



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 67

وَجَآءَ أَهۡلُ ٱلۡمَدِينَةِ يَسۡتَبۡشِرُونَ

Na walikuja watu wa mji ule (baada ya kusikia kwa Lutu kuna wageni wazuri) huku wakifurahi



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 68

قَالَ إِنَّ هَـٰٓؤُلَآءِ ضَيۡفِي فَلَا تَفۡضَحُونِ

(Lutwi) Alisema (kuwaambia): Hakika hawa wageni wangu (wanahitaji kuenziwa), tafadhalini msinifedheheshe



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 69

وَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَلَا تُخۡزُونِ

Na mcheni Allah, wala msinidhalilishe (mbele ya wageni)



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 70

قَالُوٓاْ أَوَلَمۡ نَنۡهَكَ عَنِ ٱلۡعَٰلَمِينَ

(Watu wa Lutwi) Walisema: Sisi situlikukataza usitie (neno tunapomtaka) yeyote katika walimwengu?



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 71

قَالَ هَـٰٓؤُلَآءِ بَنَاتِيٓ إِن كُنتُمۡ فَٰعِلِينَ

(Lutwi) Alisema (kuwaambia msinivunjie heshima): Hawa (hapa) binti zangu (waoeni), ikiwa nyinyi ni wafanyaji (mnaotaka kukata hamu zenu)



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 72

لَعَمۡرُكَ إِنَّهُمۡ لَفِي سَكۡرَتِهِمۡ يَعۡمَهُونَ

(Allah alisema) Naapia kwa umri wako! Hakika hao (watu wa Lutwi) wamepagawa katika ulevi wao, wanahangaika



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 73

فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّيۡحَةُ مُشۡرِقِينَ

Basi (ghafla) Ukelele mkali uliwachukua kipindi cha mapam-bazuko



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 74

فَجَعَلۡنَا عَٰلِيَهَا سَافِلَهَا وَأَمۡطَرۡنَا عَلَيۡهِمۡ حِجَارَةٗ مِّن سِجِّيلٍ

Na tukaigeuza nchi (yao) juu chini chini juu, na tukawanyeshea (mvua ya) mawe ya udongo wa Motoni



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 75

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَٰتٖ لِّلۡمُتَوَسِّمِينَ

Hakika katika hiyo (adhabu iliyowapata watu wa Lutwi) zipo ishara kwa wanaozingatia



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 76

وَإِنَّهَا لَبِسَبِيلٖ مُّقِيمٍ

Na (kitongoji cha watu wa Lutwi) kipo kwenye barabara ipitwayo (na watu wanaokwenda Sham)



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 77

إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗ لِّلۡمُؤۡمِنِينَ

Hakika katika hiyo (adhabu) ipo ishara (na mazingatio) kwa Waumini



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 78

وَإِن كَانَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡأَيۡكَةِ لَظَٰلِمِينَ

Japokuwa watu wa mji uliozingirwa na msitu (nao) walikuwa madhalimu[1]


1- - Hawa ni watu wa Nabii Shuaib, nao pia walikuwa wanamkufuru Allah.


Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 79

فَٱنتَقَمۡنَا مِنۡهُمۡ وَإِنَّهُمَا لَبِإِمَامٖ مُّبِينٖ

Kwa hivyo tuliwaadhibu. Na miji miwili hiyo ipo kwenye barabara iliyo wazi



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 80

وَلَقَدۡ كَذَّبَ أَصۡحَٰبُ ٱلۡحِجۡرِ ٱلۡمُرۡسَلِينَ

Na bila ya shaka wakazi wa Hijr[1] waliwapinga Mitume


1- - Hijri ni bonde linalopatikana kati ya mji wa Madina na ardhi ya Shamu


Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 81

وَءَاتَيۡنَٰهُمۡ ءَايَٰتِنَا فَكَانُواْ عَنۡهَا مُعۡرِضِينَ

Na tuliwapa (watu wa Thamud) ishara zetu, nao walizipuuza



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 82

وَكَانُواْ يَنۡحِتُونَ مِنَ ٱلۡجِبَالِ بُيُوتًا ءَامِنِينَ

Nao walikuwa wakichonga katika milima (na kuyafanya majumba) kwa amani



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 83

فَأَخَذَتۡهُمُ ٱلصَّيۡحَةُ مُصۡبِحِينَ

Basi ukelele ukawatwaa asubuhi



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 84

فَمَآ أَغۡنَىٰ عَنۡهُم مَّا كَانُواْ يَكۡسِبُونَ

Basi hayakuwafaa waliyokuwa wanayachuma



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 85

وَمَا خَلَقۡنَا ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَٱلۡأَرۡضَ وَمَا بَيۡنَهُمَآ إِلَّا بِٱلۡحَقِّۗ وَإِنَّ ٱلسَّاعَةَ لَأٓتِيَةٞۖ فَٱصۡفَحِ ٱلصَّفۡحَ ٱلۡجَمِيلَ

Na hatukuziumba mbingu na ardhi na vilivyomo ndani yake ila kwa ajili ya Haki. Na hakika Kiyama kitafika tu (wala hilo halina shaka). Basi (Ewe Mtume) samehe (watu wako) msamaha mzuri



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 86

إِنَّ رَبَّكَ هُوَ ٱلۡخَلَّـٰقُ ٱلۡعَلِيمُ

Hakika Mola wako Mlezi ndiye Muumbaji (wa kila kitu tena) Mjuzi sana



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 87

وَلَقَدۡ ءَاتَيۡنَٰكَ سَبۡعٗا مِّنَ ٱلۡمَثَانِي وَٱلۡقُرۡءَانَ ٱلۡعَظِيمَ

Na tumekupa Aya saba (za Sura Al-fatiha) zisomwazo mara kwa mara, na Qur’ani Tukufu



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 88

لَا تَمُدَّنَّ عَيۡنَيۡكَ إِلَىٰ مَا مَتَّعۡنَا بِهِۦٓ أَزۡوَٰجٗا مِّنۡهُمۡ وَلَا تَحۡزَنۡ عَلَيۡهِمۡ وَٱخۡفِضۡ جَنَاحَكَ لِلۡمُؤۡمِنِينَ

Usivikodolee macho yako vitu tulivyo waneemesha makundi fulani kati yao (hao makafiri), wala usiwahuzunikie (wasipoamaini). Na wainamishie bawa lako (la huruma) Waumini



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 89

وَقُلۡ إِنِّيٓ أَنَا ٱلنَّذِيرُ ٱلۡمُبِينُ

Na sema: Hakika mimi ni muonyaji mwenye kubainisha



Sourate: AL-HIJRI 

Verset : 90

كَمَآ أَنزَلۡنَا عَلَى ٱلۡمُقۡتَسِمِينَ

(Tumekuteremshia hii Qur’an) Kama tulivyowateremshia (Kitabu Mayahudi na Manaswara) walikigawanya (kwa kuamini baadhi na kukataa baadhi)