Sourate: ANNAJMI 

Verset : 31

وَلِلَّهِ مَا فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ وَمَا فِي ٱلۡأَرۡضِ لِيَجۡزِيَ ٱلَّذِينَ أَسَـٰٓـُٔواْ بِمَا عَمِلُواْ وَيَجۡزِيَ ٱلَّذِينَ أَحۡسَنُواْ بِٱلۡحُسۡنَى

Na ni vya Allah Pekee vilivyomo mbinguni na vilivyomo ardhini, ili Awalipe wale waliofanya uovu kwa yale waliyoyatenda, na Awalipe wale waliofanya mema kwa mema zaidi



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 32

ٱلَّذِينَ يَجۡتَنِبُونَ كَبَـٰٓئِرَ ٱلۡإِثۡمِ وَٱلۡفَوَٰحِشَ إِلَّا ٱللَّمَمَۚ إِنَّ رَبَّكَ وَٰسِعُ ٱلۡمَغۡفِرَةِۚ هُوَ أَعۡلَمُ بِكُمۡ إِذۡ أَنشَأَكُم مِّنَ ٱلۡأَرۡضِ وَإِذۡ أَنتُمۡ أَجِنَّةٞ فِي بُطُونِ أُمَّهَٰتِكُمۡۖ فَلَا تُزَكُّوٓاْ أَنفُسَكُمۡۖ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَنِ ٱتَّقَىٰٓ

Wale wanaojiepusha na madhambi makubwa na machafu isipokuwa makosa madogo-madogo. Hakika Bwana wako ni Mwingi wa msamaha. Yeye Anakujueni vyema, tangu Alipokuanzisheni kutoka katika ardhi, na pale mlipokuwa mimba changa matumboni mwa mama zenu. Basi msizitakase nafsi zenu. Yeye Anamjua zaidi aliyekuwa na taqwa



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 33

أَفَرَءَيۡتَ ٱلَّذِي تَوَلَّىٰ

Hivi umemuona yule ambaye amekengeuka



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 34

وَأَعۡطَىٰ قَلِيلٗا وَأَكۡدَىٰٓ

Na Akatoa kidogo, kisha akazuia.?



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 35

أَعِندَهُۥ عِلۡمُ ٱلۡغَيۡبِ فَهُوَ يَرَىٰٓ

hivi yeye ana elimu ya ghaibu basi kwa elimu hiyo yeye anaona?



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 36

أَمۡ لَمۡ يُنَبَّأۡ بِمَا فِي صُحُفِ مُوسَىٰ

Au hawajaambiwa kwa ambayo yamo kwenye kitabu cha Mussa?



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 37

وَإِبۡرَٰهِيمَ ٱلَّذِي وَفَّىٰٓ

Na Ibraahim aliyetimiza (ahadi)



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 38

أَلَّا تَزِرُ وَازِرَةٞ وِزۡرَ أُخۡرَىٰ

Na kwamba mbebaji dhambi hatobeba mzigo wa mwengine



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 39

وَأَن لَّيۡسَ لِلۡإِنسَٰنِ إِلَّا مَا سَعَىٰ

Na kwamba Mtu hatopata malipo isipokuwa yale aliyoyafanyia juhudi



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 40

وَأَنَّ سَعۡيَهُۥ سَوۡفَ يُرَىٰ

Na kwamba juhudi yake itakuja kuonekana



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 41

ثُمَّ يُجۡزَىٰهُ ٱلۡجَزَآءَ ٱلۡأَوۡفَىٰ

Kisha atalipwa malipo yake kamilifu



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 42

وَأَنَّ إِلَىٰ رَبِّكَ ٱلۡمُنتَهَىٰ

Na hakika kwa bwana wako ndio marejeo



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 43

وَأَنَّهُۥ هُوَ أَضۡحَكَ وَأَبۡكَىٰ

Na kwamba Yeye Ndiye Anayesababisha kwa Mtu kicheko (furaha) na kilio



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 44

وَأَنَّهُۥ هُوَ أَمَاتَ وَأَحۡيَا

Na hakika yeye ndiye anafisha na ndiye anayehuisha



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 45

وَأَنَّهُۥ خَلَقَ ٱلزَّوۡجَيۡنِ ٱلذَّكَرَ وَٱلۡأُنثَىٰ

Na hakika yeye ameumba aina mbili ya viumbe Dume Na Jike



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 46

مِن نُّطۡفَةٍ إِذَا تُمۡنَىٰ

Kutokana na tone la manii linapomiminwa



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 47

وَأَنَّ عَلَيۡهِ ٱلنَّشۡأَةَ ٱلۡأُخۡرَىٰ

Na kwamba ni juu Yake uanzishaji mwengine (kufufua)



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 48

وَأَنَّهُۥ هُوَ أَغۡنَىٰ وَأَقۡنَىٰ

Na kwamba Yeye Ndiye Atoshelezaye na Akinaishaye



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 49

وَأَنَّهُۥ هُوَ رَبُّ ٱلشِّعۡرَىٰ

Na kwamba Yeye ndiye Mola wa nyota ya Ash-Shi’-raa (inayoabudiwa).[1]


1- - Ash-Shi’-raa:- Hii ni Nyota maarufu, na Allah ameihusisha kuitaja hapa, ijapokuwa yeye ni Mola wa kila kitu kwasababu hii Nyota ni katika zilizokuwa zikiabudiwa katika zama za Kijaahiliyya, kwahiyo Allah akabainisha kila chochote wanacho kiabudu Washirikina basi hicho kimeumbwa na Allah, na hakistahiki kuabudiwa.


Sourate: ANNAJMI 

Verset : 50

وَأَنَّهُۥٓ أَهۡلَكَ عَادًا ٱلۡأُولَىٰ

Na kwamba Yeye Ndiye Aliyeangamiza kina ‘Aad Mwanzo



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 51

وَثَمُودَاْ فَمَآ أَبۡقَىٰ

Na Watu wa Thamuwd kisha Hakuwabakisha



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 52

وَقَوۡمَ نُوحٖ مِّن قَبۡلُۖ إِنَّهُمۡ كَانُواْ هُمۡ أَظۡلَمَ وَأَطۡغَىٰ

Na Watu wa Nuwh hapo kabla, hakika wao walikuwa madhalimu zaidi na wapindukaji mipaka zaidi wa kuasi



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 53

وَٱلۡمُؤۡتَفِكَةَ أَهۡوَىٰ

Na miji iliyopinduliwa ni yeye Allah aliyeipindulia mbali



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 54

فَغَشَّىٰهَا مَا غَشَّىٰ

Na ikawafunika ambacho kimewafunika



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 55

فَبِأَيِّ ءَالَآءِ رَبِّكَ تَتَمَارَىٰ

Basi neema gani za Bwana wako unazitilia shaka?



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 56

هَٰذَا نَذِيرٞ مِّنَ ٱلنُّذُرِ ٱلۡأُولَىٰٓ

Huyu (Mtume þ) ni muonyaji miongoni mwa waonyaji wa awali



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 57

أَزِفَتِ ٱلۡأٓزِفَةُ

Kimekaribia kinachokaribia



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 58

لَيۡسَ لَهَا مِن دُونِ ٱللَّهِ كَاشِفَةٌ

Hakuna asiyekuwa Allah mwenye uwezo wa kukibainisha



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 59

أَفَمِنۡ هَٰذَا ٱلۡحَدِيثِ تَعۡجَبُونَ

Je, mnastaajabu kwa Mazungumzo haya (ya Qur-aan)?



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 60

وَتَضۡحَكُونَ وَلَا تَبۡكُونَ

Na mnacheka na wala hamlii?