Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 31

قُلۡ إِن كُنتُمۡ تُحِبُّونَ ٱللَّهَ فَٱتَّبِعُونِي يُحۡبِبۡكُمُ ٱللَّهُ وَيَغۡفِرۡ لَكُمۡ ذُنُوبَكُمۡۚ وَٱللَّهُ غَفُورٞ رَّحِيمٞ

Sema: Ikiwa nyinyi mnampenda Allah, basi nifuateni, Allah atakupendeni na atakusameheni madhambi yenu. Na Allah ni Mwingi wa kusamehe, Mwingi wa kurehemu



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 32

قُلۡ أَطِيعُواْ ٱللَّهَ وَٱلرَّسُولَۖ فَإِن تَوَلَّوۡاْ فَإِنَّ ٱللَّهَ لَا يُحِبُّ ٱلۡكَٰفِرِينَ

Sema: Mtiini Allah na Mtume. Kama mkikengeuka, basi kwa hakika Allah hawapendi makafiri



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 33

۞إِنَّ ٱللَّهَ ٱصۡطَفَىٰٓ ءَادَمَ وَنُوحٗا وَءَالَ إِبۡرَٰهِيمَ وَءَالَ عِمۡرَٰنَ عَلَى ٱلۡعَٰلَمِينَ

Hakika, Allah amemteua Adamu na Nuhu na familia ya Ibrahimu na familia ya Imrani kati ya walimwengu (wengine wa wakati wao)



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 34

ذُرِّيَّةَۢ بَعۡضُهَا مِنۢ بَعۡضٖۗ وَٱللَّهُ سَمِيعٌ عَلِيمٌ

Ni kizazi kinachotokana na wao kwa wao, na Allah ni Msikivu sana, Mjuzi mno



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 35

إِذۡ قَالَتِ ٱمۡرَأَتُ عِمۡرَٰنَ رَبِّ إِنِّي نَذَرۡتُ لَكَ مَا فِي بَطۡنِي مُحَرَّرٗا فَتَقَبَّلۡ مِنِّيٓۖ إِنَّكَ أَنتَ ٱلسَّمِيعُ ٱلۡعَلِيمُ

(Kumbuka) Aliposema mke wa Imrani (kwamba): Ewe Mola wangu, hakika mimi nimeweka nadhiri kwa aliyemo tumboni mwangu kwa ajili yako akiwa Wakfu, basi nikubalie. Hakika, wewe ni Msikiaji mno, Mjuzi sana



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 36

فَلَمَّا وَضَعَتۡهَا قَالَتۡ رَبِّ إِنِّي وَضَعۡتُهَآ أُنثَىٰ وَٱللَّهُ أَعۡلَمُ بِمَا وَضَعَتۡ وَلَيۡسَ ٱلذَّكَرُ كَٱلۡأُنثَىٰۖ وَإِنِّي سَمَّيۡتُهَا مَرۡيَمَ وَإِنِّيٓ أُعِيذُهَا بِكَ وَذُرِّيَّتَهَا مِنَ ٱلشَّيۡطَٰنِ ٱلرَّجِيمِ

Alipomzaa alisema: Ewe Mola wangu, hakika nimezaa (mtoto) mwanamke, na Allah anamjua zaidi (mtoto) aliyemzaa. Na (mtoto) mwanaume sio sawa na (mtoto) mwanamke. Na kwa hakika, mimi nimempa jina la Mariamu, na kwa hakika mimi nakuomba umkinge yeye na kizazi chake dhidi ya shetani aliyelaaniwa



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 37

فَتَقَبَّلَهَا رَبُّهَا بِقَبُولٍ حَسَنٖ وَأَنۢبَتَهَا نَبَاتًا حَسَنٗا وَكَفَّلَهَا زَكَرِيَّاۖ كُلَّمَا دَخَلَ عَلَيۡهَا زَكَرِيَّا ٱلۡمِحۡرَابَ وَجَدَ عِندَهَا رِزۡقٗاۖ قَالَ يَٰمَرۡيَمُ أَنَّىٰ لَكِ هَٰذَاۖ قَالَتۡ هُوَ مِنۡ عِندِ ٱللَّهِۖ إِنَّ ٱللَّهَ يَرۡزُقُ مَن يَشَآءُ بِغَيۡرِ حِسَابٍ

Basi Mola wake akampokea kwa mapokezi mazuri na akamkuza makuzi mazuri na akampa Zakaria jukumu la kumlea. Zakaria kila alipoingia kwa Mariamu katika Mihirabu[1] alikuta ana riziki (ya vyakula). Akasema: Ewe Mariamu, unavipata wapi (vyakula) hivi? Akasema: Vinatoka kwa Allah. Hakika Allah anampa riziki amtakaye bila ya hesabu


1- - Mihirabu ni chumba kinachokuwepo ndani ya msikiti kwa madhumuni ya kukaa faragha ili kumuabudu
Allah. Pia mihirabu ni sehemu anayosimama imamu katika kuongoza Swala msikitini.


Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 38

هُنَالِكَ دَعَا زَكَرِيَّا رَبَّهُۥۖ قَالَ رَبِّ هَبۡ لِي مِن لَّدُنكَ ذُرِّيَّةٗ طَيِّبَةًۖ إِنَّكَ سَمِيعُ ٱلدُّعَآءِ

Hapo, Zakaria alimuomba Mola wake. Alisema: “Ewe Mola wangu, nakuomba kizazi chema kutoka kwako, hakika wewe ni Mwingi wa kusikia maombi



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 39

فَنَادَتۡهُ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ وَهُوَ قَآئِمٞ يُصَلِّي فِي ٱلۡمِحۡرَابِ أَنَّ ٱللَّهَ يُبَشِّرُكَ بِيَحۡيَىٰ مُصَدِّقَۢا بِكَلِمَةٖ مِّنَ ٱللَّهِ وَسَيِّدٗا وَحَصُورٗا وَنَبِيّٗا مِّنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Malaika walimuita akiwa amesimama Mihirabuni akiswali (na kumwambia) kwamba: Allah anakupabishara (ya mtoto atakayeitwa) Yahya, Mwenye kusadikisha neno kutoka kwa Allah, na ni Bwana na ni Mtawa na Nabii atokanaye na watu wema



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 40

قَالَ رَبِّ أَنَّىٰ يَكُونُ لِي غُلَٰمٞ وَقَدۡ بَلَغَنِيَ ٱلۡكِبَرُ وَٱمۡرَأَتِي عَاقِرٞۖ قَالَ كَذَٰلِكَ ٱللَّهُ يَفۡعَلُ مَا يَشَآءُ

Akasema: Ewe Mola wangu, vipi nitapata mtoto ilhali ukongwe umenifikia na mke wangu ni tasa?Allah akasema: Hivyo ndivyo Allah hufanya apendavyo



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 41

قَالَ رَبِّ ٱجۡعَل لِّيٓ ءَايَةٗۖ قَالَ ءَايَتُكَ أَلَّا تُكَلِّمَ ٱلنَّاسَ ثَلَٰثَةَ أَيَّامٍ إِلَّا رَمۡزٗاۗ وَٱذۡكُر رَّبَّكَ كَثِيرٗا وَسَبِّحۡ بِٱلۡعَشِيِّ وَٱلۡإِبۡكَٰرِ

Akasema: Ewe Mola wangu, nakuomba nipe alama (dalili). Akasema: Alama yako ni kwamba hutazungumza na watu kwa siku tatu isipokuwa kwa ishara tu, na mtaje Mola wako kwa wingi, na umtakase katika nyakati za jioni na asubuhi



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 42

وَإِذۡ قَالَتِ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ يَٰمَرۡيَمُ إِنَّ ٱللَّهَ ٱصۡطَفَىٰكِ وَطَهَّرَكِ وَٱصۡطَفَىٰكِ عَلَىٰ نِسَآءِ ٱلۡعَٰلَمِينَ

Na (kumbuka) Malaika walipo-sema: Ewe Mariamu, hakika Allah amekuteua na amekutakasa, na amekuteua kuliko wanawake wa walimwengu wote



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 43

يَٰمَرۡيَمُ ٱقۡنُتِي لِرَبِّكِ وَٱسۡجُدِي وَٱرۡكَعِي مَعَ ٱلرَّـٰكِعِينَ

Ewe Mariamu, mnyenyekee Mola wako na sujudu na rukuu pamoja na wenye kurukuu



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 44

ذَٰلِكَ مِنۡ أَنۢبَآءِ ٱلۡغَيۡبِ نُوحِيهِ إِلَيۡكَۚ وَمَا كُنتَ لَدَيۡهِمۡ إِذۡ يُلۡقُونَ أَقۡلَٰمَهُمۡ أَيُّهُمۡ يَكۡفُلُ مَرۡيَمَ وَمَا كُنتَ لَدَيۡهِمۡ إِذۡ يَخۡتَصِمُونَ

Hizo ni baadhi tu ya habari za Ghaibu tunazokufunulia, na hukuwa nao wakati wakitupa kalamu zao (kwa kupiga kura); ni nani kati yao atamlea Mariamu. Na hukuwa nao walipokuwa wakigombana



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 45

إِذۡ قَالَتِ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةُ يَٰمَرۡيَمُ إِنَّ ٱللَّهَ يُبَشِّرُكِ بِكَلِمَةٖ مِّنۡهُ ٱسۡمُهُ ٱلۡمَسِيحُ عِيسَى ٱبۡنُ مَرۡيَمَ وَجِيهٗا فِي ٱلدُّنۡيَا وَٱلۡأٓخِرَةِ وَمِنَ ٱلۡمُقَرَّبِينَ

(Kumbuka) Malaika waliposema: Ewe Mariamu, hakika Allah anakubashiria (mtoto atakayepatikana) kwa neno kutoka kwake. Jina lake ni Masihi Isa bin Mariamu. Ni mwenye heshima duniani na akhera, na ni miongoni mwa watakaokurubishwa



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 46

وَيُكَلِّمُ ٱلنَّاسَ فِي ٱلۡمَهۡدِ وَكَهۡلٗا وَمِنَ ٱلصَّـٰلِحِينَ

Na atazungumza na watu akiwa mtoto mchanga na akiwa mtu mzima, na atakuwa miongoni mwa watu wema



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 47

قَالَتۡ رَبِّ أَنَّىٰ يَكُونُ لِي وَلَدٞ وَلَمۡ يَمۡسَسۡنِي بَشَرٞۖ قَالَ كَذَٰلِكِ ٱللَّهُ يَخۡلُقُ مَا يَشَآءُۚ إِذَا قَضَىٰٓ أَمۡرٗا فَإِنَّمَا يَقُولُ لَهُۥ كُن فَيَكُونُ

Mariamu akasema: Ewe Mola wangu, nitapataje mtoto na ilhali hajanigusa mtu yeyote na sikuwa mzinifu? Akasema: Hivyo ndivyo Allah anaumba atakavyo; pindi anapohukumu jambo huliambia: Kuwa na linakuwa



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 48

وَيُعَلِّمُهُ ٱلۡكِتَٰبَ وَٱلۡحِكۡمَةَ وَٱلتَّوۡرَىٰةَ وَٱلۡإِنجِيلَ

Na atamfundisha kitabu na hekima na Taurati na Injili



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 49

وَرَسُولًا إِلَىٰ بَنِيٓ إِسۡرَـٰٓءِيلَ أَنِّي قَدۡ جِئۡتُكُم بِـَٔايَةٖ مِّن رَّبِّكُمۡ أَنِّيٓ أَخۡلُقُ لَكُم مِّنَ ٱلطِّينِ كَهَيۡـَٔةِ ٱلطَّيۡرِ فَأَنفُخُ فِيهِ فَيَكُونُ طَيۡرَۢا بِإِذۡنِ ٱللَّهِۖ وَأُبۡرِئُ ٱلۡأَكۡمَهَ وَٱلۡأَبۡرَصَ وَأُحۡيِ ٱلۡمَوۡتَىٰ بِإِذۡنِ ٱللَّهِۖ وَأُنَبِّئُكُم بِمَا تَأۡكُلُونَ وَمَا تَدَّخِرُونَ فِي بُيُوتِكُمۡۚ إِنَّ فِي ذَٰلِكَ لَأٓيَةٗ لَّكُمۡ إِن كُنتُم مُّؤۡمِنِينَ

Na ni Mjumbe kwa Wana wa Israili (akiwa na ujumbe kwamba) hakika: Mimi nimekuleteeni muujiza kutoka kwa Mola wenu; hakika mimi nawaumbieni kutoka katika udongo umbile kama la ndege kisha na mpulizia na anakuwa ndege kwa idhini ya Allah. Na ninaponya kipofu na mwenye ukoma, na ninafufua wafu kwa idhini ya Allah, na nitawaambia kile mnachokula na mnachoweka akiba majumbani mwenu. Hakika, katika haya yote kuna ishara kwenu mkiwa ni wenye kuamini



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 50

وَمُصَدِّقٗا لِّمَا بَيۡنَ يَدَيَّ مِنَ ٱلتَّوۡرَىٰةِ وَلِأُحِلَّ لَكُم بَعۡضَ ٱلَّذِي حُرِّمَ عَلَيۡكُمۡۚ وَجِئۡتُكُم بِـَٔايَةٖ مِّن رَّبِّكُمۡ فَٱتَّقُواْ ٱللَّهَ وَأَطِيعُونِ

Na ni mwenye kusadiki Taurati iliyoteremshwa kabla yangu, na ili ni kuhalalishieni baadhi ya yale yaliyoharamishwa kwenu, na nimekujieni na ishara kutoka kwa Mola wenu. Basi mcheni Allah na mnitii



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 51

إِنَّ ٱللَّهَ رَبِّي وَرَبُّكُمۡ فَٱعۡبُدُوهُۚ هَٰذَا صِرَٰطٞ مُّسۡتَقِيمٞ

Hakika Allah ndiye Mola wangu na Mola wenu, basi muabuduni. Hii ndiyo njia iliyonyooka



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 52

۞فَلَمَّآ أَحَسَّ عِيسَىٰ مِنۡهُمُ ٱلۡكُفۡرَ قَالَ مَنۡ أَنصَارِيٓ إِلَى ٱللَّهِۖ قَالَ ٱلۡحَوَارِيُّونَ نَحۡنُ أَنصَارُ ٱللَّهِ ءَامَنَّا بِٱللَّهِ وَٱشۡهَدۡ بِأَنَّا مُسۡلِمُونَ

Isa alipohisi ukafiri kwao alisema: Ni nani watakaonisaidia katika kuelekea kwa Allah (kwa kuinusuru dini yake)? Wafuasi watiifu wakasema: Sisi niwatetezi wa (dini ya) Allah; tumemuamini Allah nashuhudia kwamba sisi ni Waislamu



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 53

رَبَّنَآ ءَامَنَّا بِمَآ أَنزَلۡتَ وَٱتَّبَعۡنَا ٱلرَّسُولَ فَٱكۡتُبۡنَا مَعَ ٱلشَّـٰهِدِينَ

Ewe Mola wetu, tumeyaamini yote uliyoyateremsha na tumemfuata Mtume, basi tuandike (kuwa) pamoja na Mashahidi



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 54

وَمَكَرُواْ وَمَكَرَ ٱللَّهُۖ وَٱللَّهُ خَيۡرُ ٱلۡمَٰكِرِينَ

Na wamepanga njama (dhidi ya Mtume wa Allah) na Allah amepanga njama (dhidi yao) na Allah ni zaidi ya wenye kupanga njama



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 55

إِذۡ قَالَ ٱللَّهُ يَٰعِيسَىٰٓ إِنِّي مُتَوَفِّيكَ وَرَافِعُكَ إِلَيَّ وَمُطَهِّرُكَ مِنَ ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ وَجَاعِلُ ٱلَّذِينَ ٱتَّبَعُوكَ فَوۡقَ ٱلَّذِينَ كَفَرُوٓاْ إِلَىٰ يَوۡمِ ٱلۡقِيَٰمَةِۖ ثُمَّ إِلَيَّ مَرۡجِعُكُمۡ فَأَحۡكُمُ بَيۡنَكُمۡ فِيمَا كُنتُمۡ فِيهِ تَخۡتَلِفُونَ

(Kumbuka) Allah aliposema: Ewe Isa, hakika mimi ni Mwenye kukufisha[1] na ni Mwenye kukupaisha kwangu na ni Mwenye kukutakasa dhidi ya waliokufuru, na ni Mwenye kuwafanya waliokufuata wawe juu ya waliokufuru mpaka Siku ya Kiama. Kisha, kwangu tu ndio marejeo yenu, na nitahukumu baina yenu katika yale ambayo mmetofautiana


1- - Wanazuoni katika kutafsiri neno “kufisha” katika Kurani wana kauli mbili. Shekh Twantwawiy amezieleza kauli hizi katika tafsiri yake ya Alwasiitw alipoizungumzia Aya hii kwa kusema kuwa:
Neno “Kufisha” limekuja kwa maana ya kufikwa na mauti, kwa maana kwamba kiumbe anavuliwa roho yake na kutenganishwa na kiwiliwili chake. Allah anasema kuwa: “Hakika wale ambao wamefishwa na Malaika (kwa kutenganishwa roho na viwili wili vyao) …”. Sura Annisaa (4), Aya ya 97.
Neno “kufisha” lina maana ya kulaza usingizini. Hii ina maana kwamba, Allah alimwambia Nabii Isa kuwa atamlaza usingizi na kumpaisha kwake mbimguni.
Hii ndio maana iliyokusudiwa kati Aya hii kwa kuzingatia ushahidi ufuatao:
Neno “kufisha” limetumika katika Kurani kwa maana ya kufa na kwa maana ya kulala katika maeneo tofauti. Kati ya maeneo hayo ni pale Allah aliposema katika Sura Azzumar (39), Aya ya 42 . Hapa kufisha kumetumika kwa maana mbili; ya kutoa uhai na ya kulaza
usingizini.


Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 56

فَأَمَّا ٱلَّذِينَ كَفَرُواْ فَأُعَذِّبُهُمۡ عَذَابٗا شَدِيدٗا فِي ٱلدُّنۡيَا وَٱلۡأٓخِرَةِ وَمَا لَهُم مِّن نَّـٰصِرِينَ

Ama waliokufuru nitawaadhibu adhabu kali duniani na Akhera, na hawatakuwa na yeyote wa kuwanusuru



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 57

وَأَمَّا ٱلَّذِينَ ءَامَنُواْ وَعَمِلُواْ ٱلصَّـٰلِحَٰتِ فَيُوَفِّيهِمۡ أُجُورَهُمۡۗ وَٱللَّهُ لَا يُحِبُّ ٱلظَّـٰلِمِينَ

Na ama walioamini na wakatenda mema, basi (Allah) atawalipa malipo yao kamili, na Allah hawapendi madhalimu



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 58

ذَٰلِكَ نَتۡلُوهُ عَلَيۡكَ مِنَ ٱلۡأٓيَٰتِ وَٱلذِّكۡرِ ٱلۡحَكِيمِ

Hayo tunayokusomea ni katika Aya na ukumbusho wenye hekima mno



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 59

إِنَّ مَثَلَ عِيسَىٰ عِندَ ٱللَّهِ كَمَثَلِ ءَادَمَۖ خَلَقَهُۥ مِن تُرَابٖ ثُمَّ قَالَ لَهُۥ كُن فَيَكُونُ

Hakika mfano (wa uumbwaji) wa Isa kwa Allah ni mfano wa (kuumbwa kwa) Adamu; (Allah) amemuumba kwa udongo, kisha akamwambia: Kuwa na akawa



Sourate: AL-IMRAN 

Verset : 60

ٱلۡحَقُّ مِن رَّبِّكَ فَلَا تَكُن مِّنَ ٱلۡمُمۡتَرِينَ

Haki inatoka kwa Mola wako tu, basi kamwe usiwe miongoni mwa wenye shaka