Sourate: ANNAJMI 

Verset : 1

وَٱلنَّجۡمِ إِذَا هَوَىٰ

Nina apa kwa nyota zinapozama



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 2

مَا ضَلَّ صَاحِبُكُمۡ وَمَا غَوَىٰ

Hakupotoka swahibu wenu na wala hakupotoka



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 3

وَمَا يَنطِقُ عَنِ ٱلۡهَوَىٰٓ

Na hasemi (neno lolote lile) kwa utashi wa nafsi (yake)



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 4

إِنۡ هُوَ إِلَّا وَحۡيٞ يُوحَىٰ

Hayakuwa hayo (anayaoyasema) isipokuwa tu ni Wahy unaofunuliwa



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 5

عَلَّمَهُۥ شَدِيدُ ٱلۡقُوَىٰ

Amemfundisha (Malaika Jibrili) Mwenye nguvu kubwa



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 6

ذُو مِرَّةٖ فَٱسۡتَوَىٰ

Mwenye nguvu na hekima na akakaa katika umbile lake halisi



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 7

وَهُوَ بِٱلۡأُفُقِ ٱلۡأَعۡلَىٰ

Naye yuko juu kabisa katika upeo wa macho



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 8

ثُمَّ دَنَا فَتَدَلَّىٰ

Kisha akakurubia na akashuka



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 9

فَكَانَ قَابَ قَوۡسَيۡنِ أَوۡ أَدۡنَىٰ

Kisha akawa kiasi cha umbali wa mipinde miwili au karibu zaidi



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 10

فَأَوۡحَىٰٓ إِلَىٰ عَبۡدِهِۦ مَآ أَوۡحَىٰ

(Allah) Akamfunulia Wahy mja Wake yale Aliyomfunulia Wahy



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 11

مَا كَذَبَ ٱلۡفُؤَادُ مَا رَأَىٰٓ

Moyo (wake) haukukadhibisha yale aliyoyaona



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 12

أَفَتُمَٰرُونَهُۥ عَلَىٰ مَا يَرَىٰ

Je, mnambishia kuhusu yale aliyoyaona?



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 13

وَلَقَدۡ رَءَاهُ نَزۡلَةً أُخۡرَىٰ

Na hakika alimuona (Jibriyl) kwa mara nyingine



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 14

عِندَ سِدۡرَةِ ٱلۡمُنتَهَىٰ

Kwenye mkunazi wa mpaka wa mwisho kabisa



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 15

عِندَهَا جَنَّةُ ٱلۡمَأۡوَىٰٓ

Karibu yake kuna Jannatu Al-Ma-waa



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 16

إِذۡ يَغۡشَى ٱلسِّدۡرَةَ مَا يَغۡشَىٰ

Ulipoufunika mkunazi huo hicho kilicho ufinika



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 17

مَا زَاغَ ٱلۡبَصَرُ وَمَا طَغَىٰ

Jicho lake halikukengeuka wala halikupindukia mipaka



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 18

لَقَدۡ رَأَىٰ مِنۡ ءَايَٰتِ رَبِّهِ ٱلۡكُبۡرَىٰٓ

Kwa yakini aliona miongoni mwa Aayaat (ishara, dalili) za Bwana wake kubwa kabisa



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 19

أَفَرَءَيۡتُمُ ٱللَّـٰتَ وَٱلۡعُزَّىٰ

Je, mmeona (masanamu) Laata na ‘Uzzaa?



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 20

وَمَنَوٰةَ ٱلثَّالِثَةَ ٱلۡأُخۡرَىٰٓ

Na Manaata mwengine wa tatu?



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 21

أَلَكُمُ ٱلذَّكَرُ وَلَهُ ٱلۡأُنثَىٰ

Je, nyinyi mna wana wa kiume Naye Ana wana wa kike?



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 22

تِلۡكَ إِذٗا قِسۡمَةٞ ضِيزَىٰٓ

Huo basi ni mgao wa dhulma!



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 23

إِنۡ هِيَ إِلَّآ أَسۡمَآءٞ سَمَّيۡتُمُوهَآ أَنتُمۡ وَءَابَآؤُكُم مَّآ أَنزَلَ ٱللَّهُ بِهَا مِن سُلۡطَٰنٍۚ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّ وَمَا تَهۡوَى ٱلۡأَنفُسُۖ وَلَقَدۡ جَآءَهُم مِّن رَّبِّهِمُ ٱلۡهُدَىٰٓ

Hayo si chochote isipokuwa ni majina mmeyaita nyinyi na baba zenu, wala Allah Hakuyateremshia dalili yoyote. Hawafuati isipokuwa dhana na yale yanayotamani nafsi (zao), na hali imekwishawajia kutoka kwa Bwana wao mwongozo



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 24

أَمۡ لِلۡإِنسَٰنِ مَا تَمَنَّىٰ

Kwani kila Mtu anapata kila anayoyatamani?



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 25

فَلِلَّهِ ٱلۡأٓخِرَةُ وَٱلۡأُولَىٰ

Na Allah ndiye mmiliki wa Akhera na Dunia



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 26

۞وَكَم مِّن مَّلَكٖ فِي ٱلسَّمَٰوَٰتِ لَا تُغۡنِي شَفَٰعَتُهُمۡ شَيۡـًٔا إِلَّا مِنۢ بَعۡدِ أَن يَأۡذَنَ ٱللَّهُ لِمَن يَشَآءُ وَيَرۡضَىٰٓ

Na kuna malaika wengi mbinguni hainufaishi chochote uombezi wao ila baada ya kupewa idhini na Allah kwa amtakaye na amridhie



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 27

إِنَّ ٱلَّذِينَ لَا يُؤۡمِنُونَ بِٱلۡأٓخِرَةِ لَيُسَمُّونَ ٱلۡمَلَـٰٓئِكَةَ تَسۡمِيَةَ ٱلۡأُنثَىٰ

Hakika wale wasioamini Aakhirah bila shaka wanawaita Malaika kwa majina ya kike



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 28

وَمَا لَهُم بِهِۦ مِنۡ عِلۡمٍۖ إِن يَتَّبِعُونَ إِلَّا ٱلظَّنَّۖ وَإِنَّ ٱلظَّنَّ لَا يُغۡنِي مِنَ ٱلۡحَقِّ شَيۡـٔٗا

Na wala hawana ujuzi wowote ule wa hayo; hawafuati isipokuwa dhana, na hakika dhana haifai kitu chochote mbele ya haki



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 29

فَأَعۡرِضۡ عَن مَّن تَوَلَّىٰ عَن ذِكۡرِنَا وَلَمۡ يُرِدۡ إِلَّا ٱلۡحَيَوٰةَ ٱلدُّنۡيَا

Basi achana naye ambaye ameupa mgongo ukumbusho Wetu na wala hataki isipokuwa maisha ya dunia



Sourate: ANNAJMI 

Verset : 30

ذَٰلِكَ مَبۡلَغُهُم مِّنَ ٱلۡعِلۡمِۚ إِنَّ رَبَّكَ هُوَ أَعۡلَمُ بِمَن ضَلَّ عَن سَبِيلِهِۦ وَهُوَ أَعۡلَمُ بِمَنِ ٱهۡتَدَىٰ

Huo ndio upeo wao wa elimu. Hakika Bwana wako ni Mjuzi zaidi wa ambaye amepotoka njia Yake, Naye Mjuzi zaidi wa ambaye ameongoka